Tafsiri na uchambuzi wa matokeo ya udiwani

Kuna Mr mmoja ameamua kubomoa UVCCM kwa mapesa yake kisa anataka kugombea urais 2015 kwa tiketi ya CCM, aelezwe mapema kuwa CDM ni moto wa kuotea mbali,chini ya katiba mpya asitegemee kuiba kura tena kama walivyozoea,kutakuwa na tume huru,sasa hayo mapesa ya ufisadi sijui atawahonga waTZ wote? anajaribu kupanga safu yake kuanzia sasa, na CDM mnatakiwa kuanza kuvunja nguvu zake za kifisadi kuanzia sasa kamwe nchi hii isinunuliwe na mtu kwa manufaa yake na ukoo wake.ishara au somo la kwanza iwe fundisho katika uchaguzi huu mdogo wa madiwani.
 
Mkuu Kitila,

Mimi nilitegemea CHADEMA kwa wakati huu na kwenye hizi chaguzi ndogo wawe wanashinda viti vingi kuliko ilivyotokea leo. Sababu kubwa ni kwamba tokea uchaguzi mkuu uishe 2010 CHADEMA imefanya kazi kubwa sana ya kuhamasisha wananchi na CCM imekuwa ikikumbwa na mabalaa mengi tu.

Ni vigumu sana kuongelea kumetokea swing ya asilimia ngapi kwasababu Tanzania ya leo bado vyama vya upinzani havijawa na base yake. Ndio kwanza vinaitengeneza sasa. Tunaweza kusema kwamba sasa positioning ndio kwanza inachukua nafasi. Wanachama wanajipanga huku na kule na kufikia 2015 vyama vitakuwa na base yake na baada ya hapo itakuwa rahisi kuongelea wanachama kiasi gani wamebadilisha position.

Ni rahisi sana kwenye hizi chaguzi ndogo kwa CHADEMA kutumia resources zote kuweza kuziendesha. Slaa na Mbowe wamekuwa wakizunguka kila sehemu pamoja na akina Zitto na wabunge wengine. Ikifika uchaguzi wa 2015 kila mtu atakuwa busy kwake na hivyo utakuwa mgumu hata zaidi.

Kwa haya matokeo ya leo sio siri CCM watafurahi sana. Kwa kuangalia uwingi wa watu wanaohudhuria mikutano ya CHADEMA, kulikuwa na uwezekano wa CCM kupoteza karibu kata zote hizi na hapo domino effect ingechukua nafasi yake. Lakini kwasababu ambazo wachunguzi wa mambo ya siasa wanaweza kuzitafuta, hilo halijatokea na kwa CCM wengi hili litawatia nguvu sana. Ni kama somehow wamefanikiwa kulisimamisha gurudumu la kuwaporomosha chini ya mwamba.

Siasa ni ngumu sana na bado tuna safari ndefu kabla ya kufikia mahali ambapo wananchi wetu watakuwa huru zaidi na kuweza kuchagua sera ambazo zina mshiko zaidi kwao na sio ushabiki wa kisiasa kama ilivyo sasa.

Jamani tukumbuke kitu kimoja kuwa wapiga kura ni walewale wa 2010,me nadhani daftari la wapiga kura likiandika wapya hapo cdm watakuwa na mtaji wa wapiga kura wapya
 
HOMOSAPIEN, kwanza kazi ya kuvunja huo mtandao wa huyo bwana si ya CDM kwa sasa, halaf Pili una uhakika kuwa kabla ya uchaguzi wa 2015 tutakuwa na katiba tuitakayo?
Unaamini kuwa CCM itakuwa tayari kujichimbia kaburi lake yenyewe? Kumbuka agenda yao kubwa ni Kushinda uchaguzi, japo mbinu hawaisemi.

Kwan kama kweli nia njema ipo, hili la tume huru ya uchaguzi linashindikana nini kwa sasa? Unakumbuka mapendekezo ya Tume ya Nyalali na Kisanga kuhusu tume huru ya Uchaguzi yalipopotelea!? Tangu wakati huo katiba imefanyiwa marekebisho mara ngapi? Na kwa nini hilo la tume huru halikufanyiwa kazi?

Haya mambo yapo by design ndugu yangu, na kwa maneno ya Mwanakijiji, SIYO jukumu la Chama tawala kuboresha upinzani ili upinzani uweze kushika madaraka badala yake. Ni jukumu la chama tawala kutumia mbinu mbalimbali za kisayansi kuudumaza upinzani na kuhakikisha hawapati nafasi ya
kutawala. Kwa maneno mengine
CCM haina jukumu la kuisaidia
CHADEMA iimarike. Jukumu la CCM
ni kuivuruga Chadema,
kuidhoofisha na kuhakikisha ukifika uchaguzi mkuu au
mwingine wowote inafanya
vibaya kuliko uchaguzi wa kabla
yake.

CCM wanalijua hilo na ndicho wanachokifanya, sasa ni kipi kinachokufanya wewe uamini kuwa watawatengenezea hayo mazingira mazuri kwenye katiba mpya? Kwanza kwa nchi inayoendeshwa kwa matukio kama Tanzania, si ajabu likatengenezwa tukio kubwa 2014 na akili za watu zikageukia huko. Just saying
 
Nadhani ni hesabu tu wanafanya ndugu yangu. Wenzio wanachukua zile kata 27 zlilizo kuwa za CCM kabla ya uchaguzi mdogo wanazifanya "denominator" ( kumbuka hesabu za sehemu). then zile ambazo CCM wamezipoteza ( yaani 3) wanazifanya "numerator" inakuwa 3/27 kisha wanazidisha kwa 100% ili kupata asilimia ya kushuka kwa CCM (11.1%). Kisha wanachukua zile walizopata CDM zote yaani (5) wanazifanya "denominator" na zile mpya za CDM zinakuwa "numerator" na inakuwa 3/5 kisha wanazidisha kwa 100%. hapo wanapata kuinuka kwa CDM kwa 60%. Yaani kwa kifupi hasa kwa sisi ambao hatupendi kusumbua vichwa kwa hesabu, ni kwamba CCM walitakiwa kutetea viti vyao vya udiwani vyote, kama walivyofanya CDM na ikibidi kukwapua vya mwenzio kama walivyofanya CDM. So ukiangalia kwa macho ya kawaida bila kujali uwingi wa idadi ya kata, SISI ( CCM) tumepoteza viti vyetu vitatu. Wenzetu (CDM) wameongeza viti vipya vitatu.UMEONA ndugu yangu KIGARAMA ?
Unadhani napingana na hizi kanuni za kihisabati!!? Ukisema CHADEMA imeongeza kata na kujimegea asilimia hizo kutoka kwenye idadi ya kata 29 zilizorudia uchaguzi hilo halina ubishani. Hoja yangu ukisema CHADEMA imepanda kwa alisilimia 60 siyo kweli hata kihisabati. Kama unataka kujua kama CHADEMA imepanda kwa kiwango gani basi unatakiwa ujue kata nchi nzima ziko ngapi na CHADEMA ilipata ngapi 2010 na CCM ilipata ngapi kwa hiyo unatoa hizo nne(?) ambazo CHADEMA na CUF wamezichukua toka CCM ndiyo utajua CCM imeshuka kwa kiwango gani na CHADEMA imepanda kwa kiwango gani. kushuka au kupanda hakuwezi kutokana na Kata 29 zilizofanya uchaguzi wa Marudio bali kata zote za nchi nzima!!

Kanuni za HIsabati zinataka hivyo!!
 
Unadhani napingana na hizi kanuni za kihisabati!!? Ukisema CHADEMA imeongeza kata na kujimegea asilimia hizo kutoka kwenye idadi ya kata 29 zilizorudia uchaguzi hilo halina ubishani. Hoja yangu ukisema CHADEMA imepanda kwa alisilimia 60 siyo kweli hata kihisabati. Kama unataka kujua kama CHADEMA imepanda kwa kiwango gani basi unatakiwa ujue kata nchi nzima ziko ngapi na CHADEMA ilipata ngapi 2010 na CCM ilipata ngapi kwa hiyo unatoa hizo nne(?) ambazo CHADEMA na CUF wamezichukua toka CCM ndiyo utajua CCM imeshuka kwa kiwango gani na CHADEMA imepanda kwa kiwango gani. kushuka au kupanda hakuwezi kutokana na Kata 29 zilizofanya uchaguzi wa Marudio bali kata zote za nchi nzima!!

Kanuni za HIsabati zinataka hivyo!!
we wa wapi ...!
nani kakufundisha hesabu za hivyo. Wastani unatafutwa kwa kilichopo hapo. yaani hata hesabu za kitoto tu unapata jibu
nikufundishe kidogo katika kata 29 mwanzoni CCM ilikuwa na kata ngapi ,na sasa baada ya uchaguzi imeambulia kata ngapi ....
 
we wa wapi ...!
nani kakufundisha hesabu za hivyo. Wastani unatafutwa kwa kilichopo hapo. yaani hata hesabu za kitoto tu unapata jibu
nikufundishe kidogo katika kata 29 mwanzoni CCM ilikuwa na kata ngapi ,na sasa baada ya uchaguzi imeambulia kata ngapi ....
Tatizo lenu vijana wa siku hizi hamuangalii kilichoandikwa bali mnabuni kilichoandikwa. Kanuni ya kihisabati ya kujua kama umepiga hatua ni kulinganisha ulipokuwa na ulipo sasa. Kwenye huu uchaguzi kulikuwa hakuna chama chenye kata kwenye hizo kata 29. Maana yake kila chama kilikuwa kina haki ya kushindana kuzichukua na ukisema zilikuwa kata za chama fulani basi ujue unazungumzia uchaguzi wa mwaka 2010.

Kwa mantiki hiyo kupanda au kushuka kwa chama hakupimwi kwa kutumia takwimu za uchaguzi huu wa marudio bali kwa uchaguzi wa mwaka 2010. Maana chama kinapanda kwenye takwimu zipi kama si zile zilizopo. Kwa ,mfano unaposema umeongeza mikoa ya Tanzania ni lazima useme kabla ya MKoa wa Katavi kuanzishwa kulikuwa na mikoa kadhaa na kuanzishwa kwa mikoa minne mipya ni sawa na ongezeko la asilimia kadhaa.

Nyie hizi kanuni zenu za Hisabati mmezitoa wapi!?
 
CHADEMA imepanda kwa 150% na CCM kushuka kwa 11%.(kwa nukuu ya takwimu tajwa za uzi huu)
hili ni pigo kubwa sana kwa CCM ukizingatia waliopiga kura ni walewale waliokuwa wameandikishwa kwa ajili ya uchaguzi wa 2010 na ukizingatia CHADEMA imepata mashabiki wengi vijana ambao hawajajiandikisha,kwahiyo ifikapo 2015 kundi ambalo litakuwa limeisaliti CCM linaweza kuifanya CHADEMA kupanda hadi kwa 600% ambapo ni kiama kamili cha CCM
 
No.
KATA
CCM
CDM
Jumla
Tofauti
Tofauti Asili mia
1
Magomeni (Pwani)
1,478.00
479.00
1,957.00
999.00
51.047522
2
Bangata
1,117.00
881.00
1,998.00
236.00
11.811812
3
Daraja mbili
1,324.00
2,193.00
3,517.00
(869.00)
-24.70856
4
Mahenge
710.00
444.00
1,154.00
266.00
23.05026
5
Mtibwa
1,372.00
3,096.00
4,468.00
(1,724.00)
-38.5855
6
Mtele
995.00
297.00
1,292.00
698.00
54.024768
7
Mpapai
1,443.00
280.00
1,723.00
1,163.00
67.498549
8
Luwumbu
565.00
25.00
590.00
540.00
91.525424
9
Malangali
1,247.00
1,418.00
2,665.00
(171.00)
-6.41651
10
Lwezera
1,317.00
925.00
2,242.00
392.00
17.484389
11
Makata
808.00
38.00
846.00
770.00
91.016548
12
Mlelomiembeni
818.00
138.00
956.00
680.00
71.129707
13
Minyenze
378.00
167.00
545.00
211.00
38.715596
14
Karitu
854.00
354.00
1,208.00
500.00
41.390728
15
Kiloleni
648.00
166.00
814.00
482.00
59.213759
16
Ipole
365.00
568.00
933.00
(203.00)
-21.75777
17
Bugarama
18
Mwananza
794.00
575.00
1,369.00
219.00
15.997078
19
Lubili
1,108.00
620.00
1,728.00
488.00
28.240741
20
Kitagiri
1,416.00
157.00
1,573.00
1,259.00
80.038144
21
Kikokona
1,149.00
367.00
1,516.00
782.00
51.583113
22
Nanjaraneha
1,128.00
2,370.00
3,498.00
(1,242.00)
-35.506
23
Kilema Kusini
784.00
734.00
1,518.00
50.00
3.2938076
24
Vugiri
1,460.00
337.00
1,797.00
1,123.00
62.493044
25
Tamota
1,060.00
772.00
1,832.00
288.00
15.720524
26
Msalato
869.00
450.00
1,319.00
419.00
31.76649
27
Mpwapwa
1,722.00
1,189.00
2,911.00
533.00
18.309859
28
Myovizi
1,726.00
1,498.00
3,224.00
228.00
7.0719603
29
Mpapa
903.00
310.00
1,213.00
593.00
48.887057
JUMLA
29,558.00
20,848.00
50,406.00
8,710.00
17.279689


Tujadili takwimu sasa; na hasa tofauti ya kura zote zilizopigwa. Kwa maoni yangu naziamini hizi takwimu. Nimekokotoa tofauti kwa tarakimu na asilimia ya tofauti. Nazungumzia tofauti ya asilimia ni 17.28. Kwangu mimi ili CCM ijidai kuwagalagaza CDM angalau tofauti ya asili mia ingekuwa zaidi ya asili mia 50. Kwa hiyo madai ya CCM ni uvuvuzela.

Ukitumia asilimia hiyo ya tofauti tofauti ya ubora wa CCM ni viti vitano tu. Yaani kwa ubora (quality) ya maamuzi ya wapiga kura 58.64 wameiamini na kuipigia kura CCM na 41.36 wameiamini na kuipigia kura CDM ukiacha za TLP na CUF kwa kuwa ni kidogo mno.

Ili kupata taswira ya utendaji kwenye kampeini ni vizuri tukalinganisha na asili mia iliyopo ya viti vya udiwani na idadi ya wapiga kura kulingana na uchaguzi uliopita. Kwa mtazamo wa CCM chama chao bado kinapendwa pamoja na kupoteza viti vitano kwa wapinzani.

Nahitimisha kwa kusema kwa takwimu za matokeo ya kuchakachuliwa ya uraisi CCM imeshuka toka juu ya asilimia 60 hadi chini ya asilimia hiyo.

Natazamisha kuwa uchaguzi haukujumuisha wapiga kura wote wanaostahili. Kwa hiyo dola inachakachua matokeo kwa kutumia mfumo na taratibu ambazo hazitoi majibu halali ya viwango vya demokrasia. Maana yake ni "mark time" ya maendeleo kwa kukosekana uwakilishi makini na wenye haki.
 
Tusimung'unye maneno hapa, kata ambazo cdm imeshinda zipo sehemu za miji! Vijijini bado m4c haijatia maguu. Kuna haja ya kuweka concentration kubwa sana vijijini, hawajajua mpaka sasa mabadiliko tunayoyataka yana maana gani kwao!
 
Kama ni kweli na wewe ni mhadhili basi nchi hii ina zaidi ya tatizo, sijawahi kukutana na Mhadhili mjinga kama wewe, pumba unazopost humu JF hazina hadhi ya kutoka kwa mtu mwenye status ya Uhadhili hata kama ni Pro CCM. Inawezekana wewe ndio Dr Msaki mfalme wa Vilaza.

Kwa bahati mbaya sana vigezo vya kazi yangu havipimwi na post ninazotuma kwenye vijiwe vya kahawa. Pia ninaweza kupambana kwa kila mtindo iwe matusi, kejeli, vijembe au busara ila na hoja tu sina nafasi ya kupambana na mtu ambaye hata simjui wala sina uhakika na umri wake wala elimu yake.
 
Hadi dakika hii matokeo yanaonyesha kwamba katika Kata 29, CHADEMA wameshinda katika kata 5 and TLP (1) na CCM kushinda katika kata zilizobaki.

Kwa muono wa karibu unaweza ukadhani kwamba CHADEMA wamepoteza sana katika uchaguzi huu. Hata hivyo ukiyachunguza matokeo haya kwa ukaribu utaona kwamba CHADEMA wamepata mafanikio makubwa na CCM wametelemka.

Tukumbuke kwamba CHADEMA walikuwa na kata mbili za kuzilinda katika uchaguzi huu ambazo ni Rombo na Mvomero. Kata hizi wamefanikiwa kuzilinda na kuongeza zingine tatu, ambazo ni Mlangila (Ludewa), Ipole na Daraja Mbili (zote hizi zilikuwa za CCM). Kwa hiyo wamelinda kata zao na kuzipokonya zingine tatu kutoka mikononi mwa CCM.

Na yote hii ni ndani ya miezi 24 tu tangu uchaguzi mkuu ufanyike. Kwa hiyo kimehesabu CCM wameshuka kwa 11.1% na CHADEMA wamepanda kwa 60%! So, CDM keep up the momentum!.....


Napenda sana watu kama nyie ambao mnatupa takwimu kama hizi. Wenye vichwa pazi watapinga hoja but time will tell.
Asante Mkuu

 
Kwa bahati mbaya sana vigezo vya kazi yangu havipimwi na post ninazotuma kwenye vijiwe vya kahawa. Pia ninaweza kupambana kwa kila mtindo iwe matusi, kejeli, vijembe au busara ila na hoja tu sina nafasi ya kupambana na mtu ambaye hata simjui wala sina uhakika na umri wake wala elimu yake.
Sikushangai kwa sababu hata Benson Bana ni PHD Holder. eti na wewe ni mhadhili!! bora mtoto wangu nimuanzishie ujasiriamali wa kufuga kuku mapema kuliko kuambukizwa ujinga na wahadhili wa type yako.
 
Sikushangai kwa sababu hata Benson Bana ni PHD Holder. eti na wewe ni mhadhili!! bora mtoto wangu nimuanzishie ujasiriamali wa kufuga kuku mapema kuliko kuambukizwa ujinga na wahadhili wa type yako.

Familia yenu yoooote mkiunganisha visetifiketi vyenu hamuwezi kuwa sawa na DR Bana, so uwe na heshima. Mtoto wako ataishia kuwa mpiga debe wa vyama vya siasa kama baba yake ulivyokuwa na nakuhakikishia kama alivyotumiwa mama na baba yako, siasa itaendelea kuwatumia ukooo wenu woote na hii ni kutokana umasikini wenu wa akili, fikra na mali.
 
Familia yenu yoooote mkiunganisha visetifiketi vyenu hamuwezi kuwa sawa na DR Bana, so uwe na heshima. Mtoto wako ataishia kuwa mpiga debe wa vyama vya siasa kama baba yake ulivyokuwa na nakuhakikishia kama alivyotumiwa mama na baba yako, siasa itaendelea kuwatumia ukooo wenu woote na hii ni kutokana umasikini wenu wa akili, fikra na mali.
Kwenye ukoo wetu wote mimi ndio msomi wao, ni Form Four Graduate. Lakini nina uwezo wa kumwajiri Benson Bana na wewe pia.
 
Back
Top Bottom