Tafakuri Yangu Ya Leo; Jenerali Ulimwengu Bakora Ya Watawala Acha Iwaadabishe Tu

KAMBOTA

Senior Member
Mar 21, 2011
176
103

……W’re polite and progressive by day, more tibalist than even the Kenyans by night…..

Ukweli kama huu anaoweza kuusema Jenerali Ulimwengu ndio umewafanya watawala wengi kumwogopa mwanaharakati huyu kushinda hata UKIMWI, nani nchi hii asiyemfahamu Jenerali Ulimwengu? Licha ya mwandishi huyu kukumbwa na misukosuko hata ya kutaka kunyang’anywa uraia aah wapi Bwana! Jenerali Ulimwengu hana mpinzani kwa jinsi anavyosimamia ukweli.
Pengine kwa waandishi wachanga wenye lengo la kufika alipofika Jenerali waanze mapema kukataa rushwa ambazo huwafanya kutumia kalamu zao kusifia uharamia kuliko kukosoa utawala mbovu, Alleluya Mungu Mwenyezi kwa kutupatia Jenerali Ulimwengu mwenye uwezo wa kuwasemea masikini wan chi hii, mwenye uwezo wa kukemea udini na ukabila , mwenye uwezo wa kumhoji hata rais bila uwoga nani kama Jenerali?
Naam Jenerali Ulimwengu ni bakora ya watawala acha iwachape tu!

Nani kama jenerali, Ulimwengu tumwone
Nani anayetujali, yu wapi tusemezane
Nani tumpe kibali, ukweli akawachane
Jenerali Ulimwengu, kiboko ya watawala.

Wamesuka njama nyingi, zote zimegonga mwamba
Jenerali ndio kingi, wanyonge tunampamba
Wanaoweka vigingi, hao wote ni mafamba
Jenerali Ulimwengu, bakora ya watawala


Nani asiyefahamu, Jenerali ni shujaa
Yu wapi tumuhukumu, kwa kuzidi kuzubaa
Jenerali ni muhimu, Arusha hata kondoa
Jenerali Ulimwengu, sindano ya mabwenyenye


Wakiwa maofisini, watawala wanalia
Wakisoma gazetini , hofu inawaingia
Kwa Jenerali makini, Mwema Raia sikia
Jenerali Ulimwengu, msome Raia Mwema


Beti tano nakomea, mengi nimeongelea
Ulimwengu endelea, uovu kuufunua
Ukweli tunaujua, wewe unatutetea
Jenerali Ulimwengu, mtetezi wa wanyonge.



Nova Kambota Mwanaharakati,
0717-709618 au 0766-730256
novakambota@gmail.com
www.novatzdream.blog.com
Tanzania, East Africa
Jumatano 29 March 2011.

 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom