Tafadhalini sana -huu ni wakati wa wana CHADEMA kuwa na mshikamano wa chama

nderingosha

JF-Expert Member
Mar 20, 2011
4,281
3,243
  • Ndio bandugu,nategemea mu wazima wa afya na kila mtu kwa nafasi yake anashiriki kwa njia moja au nyingine kuijenga nchi yetu iyojaa kila aina ya mapungu katika dhana nzima ya kimaendeleo.Leo nataka kugusia jambo la msingi sana linalohitajika katika kukiimarisha chama cha Chadema haswa ukizingatia ndicho chama kinachoelekea kuleta mapinduzi ya kweli katika jamii ya Mtanzania kifikra na kimaendeleo kwa ujumla.

  • Kuna dhana ambayo nimekuwa nikiipinga humu jukwaani(pamoja na kwamba post yangu iliondolewa na mod kabla ya kusomwa na wengi)ambayo imekuwa inahusisha watu kujadili watu/viongozi binafsi wa chadema badala ya kuwatakia mshikamano na hivyo hata kupelekea baadhi ya wachangiaji kuwaona baadhi ya viongozi wao kuwa hawafai(haswa pale wanapowahusisha na ushirikiano na chama cha ccm).Hoja hii imejitokeza sana pale ambapo kwa mfano mh.Zitto anapokuwa anajadiliwa kwa mtazamo hasi kwa kiwango kikubwa humu jukwaani pamoja na mchango wake mkubwa katika kukijenga chama cha chadema
  • Mimi binafsi hii dhana ya kujadili watu(kimajungu)badala ya issues zinazohusu maslahi ya nchi ninaipinga sana wajameni
  • Ni mategemeo yangu kuwa humu jukwaani michango inayohusisha mivurugano baina ya viongozi wa chadema na wanachama wao haitakuwapo tena badala yake tujadili issues za msingi za kimaendeleo na jinsi ya kupambana na mafisadi(majambazi)wa mali za umma kwani ndio wanaochangia kuturudisha nyuma
  • Tafadhalini tuache kuwasema vibaya viongozi wa chadema bali tuwape ushirikiano na ikiwezekana tips za jinsi ya kupambana na majambazi wa ccm au vyama vingine venye mitazamo hasi na juhudi za chadema kuikomboa nchi hii
  • Nategemea umoja huu utaimarika pia kati ya viongozi wa chadema,wabunge na wanachama wao haswa pale bungeni (na katika jamii) katika kuiweka kiti moto serikali hii ambayo kwa kiasi kikubwa imevunja matumaini ya Mtanzania kujikomboa kutokana na adui yetu mkubwa yaani: maradhi,ujinga,umaskini na ufisadi.
  • Ni katika mshikamano huu tu ndipo chadema wanaweza kuikamata dola na kuwafikisha Watanzania kwenye ndoto yao ya miaka mingi yaani: kupatikana kwa maendeleo endelevu yatakayotokana na kukua kwa pato la kila Mtanzania litakalotokana na matumizi endelevu ya raslimali zote za nchi hii na fursa sawa kwa kila Mtanzania
 
  • Ndio bandugu,nategemea mu wazima wa afya na kila mtu kwa nafasi yake anashiriki kwa njia moja au nyingine kuijenga nchi yetu iyojaa kila aina ya mapungu katika dhana nzima ya kimaendeleo.Leo nataka kugusia jambo la msingi sana linalohitajika katika kukiimarisha chama cha Chadema haswa ukizingatia ndicho chama kinachoelekea kuleta mapinduzi ya kweli katika jamii ya Mtanzania kifikra na kimaendeleo kwa ujumla.



  • Kuna dhana ambayo nimekuwa nikiipinga humu jukwaani(pamoja na kwamba post yangu iliondolewa na mod kabla ya kusomwa na wengi)ambayo imekuwa inahusisha watu kujadili watu/viongozi binafsi wa chadema badala ya kuwatakia mshikamano na hivyo hata kupelekea baadhi ya wachangiaji kuwaona baadhi ya viongozi wao kuwa hawafai(haswa pale wanapowahusisha na ushirikiano na chama cha ccm).Hoja hii imejitokeza sana pale ambapo kwa mfano mh.Zitto anapokuwa anajadiliwa kwa mtazamo hasi kwa kiwango kikubwa humu jukwaani pamoja na mchango wake mkubwa katika kukijenga chama cha chadema
  • Mimi binafsi hii dhana ya kujadili watu(kimajungu)badala ya issues zinazohusu maslahi ya nchi ninaipinga sana wajameni
  • Ni mategemeo yangu kuwa humu jukwaani michango inayohusisha mivurugano baina ya viongozi wa chadema na wanachama wao haitakuwapo tena badala yake tujadili issues za msingi za kimaendeleo na jinsi ya kupambana na mafisadi(majambazi)wa mali za umma kwani ndio wanaochangia kuturudisha nyuma
  • Tafadhalini tuache kuwasema vibaya viongozi wa chadema bali tuwape ushirikiano na ikiwezekana tips za jinsi ya kupambana na majambazi wa ccm au vyama vingine venye mitazamo hasi na juhudi za chadema kuikomboa nchi hii
  • Nategemea umoja huu utaimarika pia kati ya viongozi wa chadema,wabunge na wanachama wao haswa pale bungeni (na katika jamii) katika kuiweka kiti moto serikali hii ambayo kwa kiasi kikubwa imevunja matumaini ya Mtanzania kujikomboa kutokana na adui yetu mkubwa yaani: maradhi,ujinga,umaskini na ufisadi.
  • Ni katika mshikamano huu tu ndipo chadema wanaweza kuikamata dola na kuwafikisha Watanzania kwenye ndoto yao ya miaka mingi yaani: kupatikana kwa maendeleo endelevu yatakayotokana na kukua kwa pato la kila Mtanzania litakalotokana na matumizi endelevu ya raslimali zote za nchi hii na fursa sawa kwa kila Mtanzania



tick.gif





0a-900-dancing_cartoon.gif
 
Waberoya, mbona tena kuna rangi za kijani na njano huho kwenye hicho kibonzo?
 
Back
Top Bottom