Tafadhali Wabunge wetu, ACHENI KULALAMIKIA bajeti timizeni wajibu wenu!

Honey K

JF-Expert Member
Sep 14, 2008
629
72
HIVI KWANINI WABUNGE WETU WANALALAMIKA JUU YA BAJETI BADALA YA KUTIMIZA WAJIBU WAO?! WANAMLALAMIKIA NANI?

Kimsingi bajeti inapopelekwa Bungeni na serikali inakwenda kwa ajili ya mjadala na marekebisho palipo na mapungufu NA SI KUPITISHWA KAMA WAJIBU TU, tunategemea mjadala wenye lengo la kuboresha bajeti iliyowasilishwa bungeni kwa faida ya wananchi.

Sasa haya malalamiko ya baadhi ya wabunge barabarani, mara "niko tayari kufukuzwa"!! Nani anamfukuza nani?! Nani anayetishia uhuru, haki na wajibu wa kikatiba wa wabunge wetu mpaka wanalalamika barabarani?!!

Nashauri wabunge timizeni wajibu wenu, jadilini na kuishauri serikali ndani ya bunge juu ya maboresho ya bajeti iliyoletwa kwenu! Kulalamika barabarani kunaonyesha ama baadhi hawajui wajibu na haki zao kikatiba, au kuna watu wanatafuta umaarufu binafsi. Hivi kila mmoja akilalamika na nyie tuliowapa dhamana ya kuisimamia na kuishauri serikali maana yake nini? Nyie mlalamike na wananchi walalamike kuna sababu gani ya nyie kupewa dhamana hii kubwa mliopewa!!

With due respect TIMIZENI WAJIBU WENU BUNGENI NA SI BARABARANI KULALAMIKA KUTWA KUCHWA!
 
Nape, hii serikali mnayoiongoza mbona inaonyesha haijui wananchi wanachokitaka, inataka kushauriwa kwa kila kitu, kama vipi si muwaachie wanaoweza!!!!!!! anyway pole kwa kupigwa doro iringa!
 
anyway pole kwa kupigwa doro iringa!

Huna aibu sawa! Hata haya huna!??? Nenda kaulize nilichiwafanya Iringa!!! Ninaeleza maswala ya bajeti by the way, ukitaka mjadala wa Iringa anzisha thread!
 
Huna aibu sawa! Hata haya huna!??? Nenda kaulize nilichiwafanya Iringa!!! Ninaeleza maswala ya bajeti by the way, ukitaka mjadala wa Iringa anzisha thread!

hujaijibu hoja yangu ya msingi, mna-base kushauriwa tuuuuuu! mnaweza kufanya nini sasa! naona umejibu "asante" kwa tafsida.
 
For first time, nakubaliana na nawe Nape, wabunge wa magamba waache walalamike maana tayari wameshajiona ni chama cha upinzani, 2015 itadhibitisha hili.

Well wabunge wa CCM timizeni wajibu wenu kwa kuikataa bajeti, that is over, WAKIIKATAA WATAKUWA WAMETIMIZA WAJIBU WAO VIZURI, I support Nape.
 
Huna aibu sawa! Hata haya huna!??? Nenda kaulize nilichiwafanya Iringa!!! Ninaeleza maswala ya bajeti by the way, ukitaka mjadala wa Iringa anzisha thread!
We ndo unapaswa kuona aibu, manake walichokifanya ndugu zako wa CHADEMA hujafanikiwa kufika hata robo yake. Pamoja na kutumia mihela kibao wananchi hawakukubali kudanganyika kiviiiile.
attachment.php


Linganisha na:

IMG_3500.JPG

IMG_3504.JPG

IMG_3491.jpg
 
Wewe kumbe hujagundua, wanasiasa wa siku hizi wanafikiri kukosoa au kutoa maneno ya kupinga kila kitu kinachopangwa na serikali kutawafanya wakubalike kwa wananchi .kwa hiyo wanafanya sarakasi tu za kisiasa ili kujihakikishia maslahi yao.

Wananchi pia wameshaaminishwa kila mipango ya serikali ni mibovu kwahiyo lazima hao wambunge wataonekana mashujaa na watetezi wa watu.

Ni juu ya serikali kupanga mipango makini ili kurudisha imani za wananchi.

Mfano kama hi? bajeti kama kweli imetungwa ovyo kama wanavyodai wabunge basi itawacost na kama ni siasa tu tutajua tu pindi mjadala ukianza.
 
For first time, nakubaliana na nawe Nape, wabunge wa magamba waache walalamike maana tayari wameshajiona ni chama cha upinzani, 2015 itadhibitisha hili.

Well wabunge wa CCM timizeni wajibu wenu kwa kuikataa bajeti, that is over, WAKIIKATAA WATAKUWA WAMETIMIZA WAJIBU WAO VIZURI, I support Nape.
lengo la nape ni kuwa serikali ya CCM "ishauriwe" na wala si kukwamishwa!
 
Nashauri wabunge timizeni wajibu wenu, jadilini na kuishauri serikali ndani ya bunge juu ya maboresho ya bajeti iliyoletwa kwenu!
Kamanda Nape, kwenye RED kimsingi wanalalamika kwa sababu walishaishauri serikali lakini serikali inaleta USANII, walishasema hii bajeti haifai toka kwenye vikao vya kamati zao, serikali ikakubali USHAURI, chaajabu ikafanya usanii wa kuisoma ileile iliyokataliwa, kwa mtazamo wako Wafanye nini, that way wanakwenda said " barabarani" kwa sababu ndiko huko "barabarani" walizipata kura.
 
Huna aibu sawa! Hata haya huna!??? Nenda kaulize nilichiwafanya Iringa!!! Ninaeleza maswala ya bajeti by the way, ukitaka mjadala wa Iringa anzisha thread!
hahahahahaha,nape,pale sokoni ulwafanya kweli duh.hata mshipa wa aibu mafsadi wamekukata duh.
 
Sioni ajabu kwa tamko kama hili Ndugu yangu Nape, maana tukisema ugumu wa maisha wewe huwezi kujua kwa kuwa kila kitu kipo tayari kwenye stoo yako wewe ni kuchukua na kutumia.

Bajeti hii ya sasa ni bajeti jina na wewe unajua ila huwezi kutamka hadharani kuwa ni mbaya, sasa wabunge hawalalamiki barabarani wanawaambia wananchi waliowachagua juu ya kilichowasilishwa bungeni, huku wakiwajulisha kuwa ITAPITISHWA kwa wingi wa wabunge wa CCM pamoja na ubaya wake.
Wabunge hao hawalalamiki barabarani wanawaambia wananchi waliowachagua ili kuwajulisha kuwa siyo wale WALIOTEULIWA kiushuikaji ili kutetea wale waliowaweka walipo KAMA WEWE ULIYE MIONGONI MWA WATEULE.

Wabunge hawalalamiki barabarani ila wanawajulisha wananchi waliowachagua kuwa wote walioteuliwa wanatumia raslimali za Taifa bala kuwa na uchungu maana wanapita kila eneo nchini wakiwatukana wananchi wenzao kuwa ni VINYAGO, OIL CHAFU na mambo kama hayo huku wakisahau kuwa wanatumia kodi za watanzania wote.

Wabunge ni haki yao kuwajulisha wananchi maana ndio waliowatuma bungeni ila wakifanya hivyo vinatumwa vimemo, sms za vitisho kutoka kwa WATEULE kuwa wanakiuka maagizo ya CCM, basi kama hawatishwi mbona hakuna kukanusha habari wanazozitoa kutoka kwako Nape.

Msiwatishe wawakilishi wetu jamani ngoja watimize wajibu wao waliotumwa na waajiri wao WANANCHI.
 
Nape tueleze, ukiwa njiapanda kwenye jambo lolote hapo ndipo unahitaji ushauri, kwenye post yako umetaka serikali inayoundwa na chama chako ishauriwe na wabunge, UMESHAGUNDUA KUWA IKO NJIA PANDA KIASI KWAMBA HAIWEZI KUTOFAUTISHA Z NA 2 ???????
 
hujaijibu hoja yangu ya msingi, mna-base kushauriwa tuuuuuu! mnaweza kufanya nini sasa! naona umejibu "asante" kwa tafsida.

wewe sijui hasa hata unaongelea nini.au ndo unaamka nini....kushauriwa nini,wapi na lini?naona unaongea tu bila mpangilio.ama unataka tujuwe nawewe upo.
 
Malalamiko ya wabunge wa CCM yanatokana na msimamo mnaouweka kwenye party caucas.

Ndiyo maana mtasikia wabunge wa CCM wakiikosea bajeti lakini HITIMISHO lao linakuwa
ninaunga mkono BAJETI 100%
 
nape unatapatapa sana,mbona kama upo mwenyewe ccm au wamekususia chama,kaaaazi kweli kweli
 
lengo la nape ni kuwa serikali ya ccm "ishauriwe" na wala si kukwamishwa!
WALISHAISHAURI kwenye kamati ya kudumu ya bunge, fedha na uchumi. ilishaishauri na kusema hii bajeti haifai... serikali ikakubali then wameleta usanii wa kuirudisha the same, kushauri walishashauri...watimize wajibu wao.. kwa kuikaata
 
Mkuu Nape, pole kwa kazi..

Nadhani hata wewe unalalamika.. Kimsingi mjadala wa bajeti bado haujaanza na unategemewa kuanza leo. Kwa hiyo huwezi kusema kama wabunge wametimiza wajibu wao au hawajatimiza hadi hapo watakapoanza kujadili bajeti. Kuhusiana na suala la kuongelea bajeti wana haki ya kuizungumzia kulingana na jinsi wanavyoiona na kuitafakari. Tatizo litakuwa pale kama watalalamika nje na ndani ya bunge wakakaa kimya, hata hivyo hii ni kawaida sana kwa wabunge wa CCM. Najua una kiwewe cha M4C kwa sababu ni dhahiri imeingia kila mahali hata bungeni na wabunge wa CCM wanaonekana kuchanganyikiwa zaidi, wamesoma alama za nyakati na hawataki kuzikwa kaburi moja na chama chao!

Kazi unayo. Nakushauri mshauri bosi wako mtumie style ya BWM kuja Dodoma na kuwapiga mkwara wabunge wake. Kuhusu Iringa umenisikitisha sana kuanza style ya Lusinde.. Kwa nini utukane Nape? Wewe ni mtu mkubwa kama huelewi. You are a public figure! Maneno yako yanabeba taswira ya chama moja kwa moja! Jifunze nini cha kuongea na wapi kiongelewe! Hivi hujui kuwa hata Arumeru mitusi ya Lusinde ilichangia chama chako kushindwa! Grow up!
 
wewe sijui hasa hata unaongelea nini.au ndo unaamka nini....kushauriwa nini,wapi na lini?naona unaongea tu bila mpangilio.ama unataka tujuwe nawewe upo.

niliyemuuliza ni nape! uwepo wangu jf haufungamani na uwepo wa mwanajamii yeyote. ili kuwadhihirishia wasomaji kama wewe ni au si poyoyo, tuambie wewe ni nani kwa mistari isiyozidi mitatu!
 
Huna aibu sawa! Hata haya huna!??? Nenda kaulize nilichiwafanya Iringa!!! Ninaeleza maswala ya bajeti by the way, ukitaka mjadala wa Iringa anzisha thread!
Mkuu ni lini serikali yenu itaacha kutegemea kukusanya ushuru kwenye pombe na sigara?
 
Back
Top Bottom