Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Na. M. M. Mwanakijiji
Kuna msemo wa kiafrika unaosema, huwezi kuzuia masikio yako kusikia bali kuuzuia mdomo wako kuzungumza. Ndiyo siwezi kuzuia masikio yenu kusikia, lakini naweza kuziba mdomo wangu nisizungumze Rais Mstaafu Benjamin W. Mkapa
Kama kuna mtu katika Taifa letu ambaye anaamini kuwa Rais mstaafu na Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Mapinduzi Bw. Benjamin W. Mkapa alikuwa nikiongozi bora basi mtu huyo itampasa afungiwe jiwe la kusagia shingoni na kwenda kutupwa Baharini. Kama kuna yeyote ambaye anaamini kuwa mambo yanayosemwa juu ya uongozi wa Rais wetu huyo wa awamu iliyopita ni wivu, chuki, masimango binafsi dhidi yake basi na huyo naye tutamuongezea na jiwe la kukobolea! Na iwapo kuna kundi la watu ambao wanaamini kabisa kuwa Tanzania ilifanya vizuri wakati wa Rais Mkapa na hivyo tujipange kwa kupiga magoti na kutoa shukrani zetu kwake basi kundi hilo na watetezi wa uongozi wa awamu ya tatu ningelikuwa na uwezo ningehakikisha wanafutwa wote kwenye kitabu cha historia yetu.
Kuna msemo wa kiafrika unaosema, huwezi kuzuia masikio yako kusikia bali kuuzuia mdomo wako kuzungumza. Ndiyo siwezi kuzuia masikio yenu kusikia, lakini naweza kuziba mdomo wangu nisizungumze Rais Mstaafu Benjamin W. Mkapa
Kama kuna mtu katika Taifa letu ambaye anaamini kuwa Rais mstaafu na Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Mapinduzi Bw. Benjamin W. Mkapa alikuwa nikiongozi bora basi mtu huyo itampasa afungiwe jiwe la kusagia shingoni na kwenda kutupwa Baharini. Kama kuna yeyote ambaye anaamini kuwa mambo yanayosemwa juu ya uongozi wa Rais wetu huyo wa awamu iliyopita ni wivu, chuki, masimango binafsi dhidi yake basi na huyo naye tutamuongezea na jiwe la kukobolea! Na iwapo kuna kundi la watu ambao wanaamini kabisa kuwa Tanzania ilifanya vizuri wakati wa Rais Mkapa na hivyo tujipange kwa kupiga magoti na kutoa shukrani zetu kwake basi kundi hilo na watetezi wa uongozi wa awamu ya tatu ningelikuwa na uwezo ningehakikisha wanafutwa wote kwenye kitabu cha historia yetu.