Tafadhali Kikwete tangaza hali ya Dharura kwa Jiji la Dar; TUONGOZE KWENYE DHARURA HII!

MMM Viongozi wetu wanachangamkia pale tu pana presidential gain sasa JK Hana cha kupoteza . Hayupo kwa kuongoza nchi tena yeye kashapata alichokuwa anataka
 
Mwenzenu huwa najiuliza mara nyingi - hivi walipokuwa wanataka kuwa viongozi walikuwa wanafikiria wanatakiwa kuongoza nini magari? au kwa wingi wa saluti wanazopigiwa?

akili ya mtu huwa inakua kwa awamu, wengine akili zao hufika level miaka 24 kimtazamo wakati umri wao ni miaka 55 au zaidi, na wao hujidhania bado watoto na jamii huamini kuwa watu hao ni vijana.
Hivyo inawezekana kabisa kuwa wakati wanatafuta hizo nyazifa, walikuwa na mtazamo kuwa uongozi ni ufalme.
Inasikitisha sana, yaani tume imeundwa bila ya kusikia kauli ya rais wetu!!
Huu si wakati wa kutengeneza tume za uchunguzi, bali ni wakati wa kutangaza hali ya hatari na kufanya uokozi kabla utu wa watu kuanza kudharirika.
 
Umenena vyema mwanakijiji na nadhani wenye masikio wamekusikia ila wasiwasi wangu ni kuwa tunaweza tukasikia na wewe umepelekwa kisutu kwa sababu ya uchochezi! Nakumbuka wakati fulani miaka michache iliyopita nilipata kusoma andiko lako (sikumbuki kama ilikuwa ni makala au kijarida cha cheche) ambapo ulizungumzia kwa kina sana juu ya matatizo haya ya dar kwa maana ya ubovu wa miundo mbinu na madhara haya ambayo yamekuwa yakitokea na ndo haya tunayaona tena kwa mara nyingine wakati tu. Kama jinsi ambavyo hatua hazikuchukuliwa wakati wote huo na matatizo kutokea sasa, suala hili la mafuriko dar litatokea tena kwa kadri ambavyo tutaendelea kuwa na mazingira haya tuliyonayo sasa. Nafikiri hawakukusoma au walikusoma wakapuuzia ushauri wako. Usikate tamaa kuendelea kutimiza wajibu wako. Mungu awape heri wakazi wa dar na watanzania kwa ujumla wake na ninakubaliana na wewe kwamba ni kweli tunahitaji kiongozi katika hili ili atueleze nini tufanye ili kusaidia watanzania wenzetu.

Mkandara hapo juu amesema anataka kutoa msaada lakini ndo hivyo hajui hata wapi pa kuanzia!!! Kuna mambo mengine kwa kweli nadhani yanafanyika Tanzania tu.
 
Kwa hili kweli kunahitajika kufanyika kitu, mda mfupi uliopita wakati nakuja kibaruani kwangu nimekutana na malori ya Jeshi mengi sana (takriban 15) Mbozi road Chang'ombe sasa sijajua kama yanaelekea kuokoa watu ama yako kwenywe misele ya kawaida.
 
mara mia waziri wa makazi amejitaidi japo kwa kutuma salamu za pole ingawa yupo Uganda kikazi.
Mi nadhani amethubutu kuonyesha kujali kuliko kaka mkuu wa nchi.
 
Mama tumekusikia tangu wiki iliyopita huko Uganda ukitembelea na kujionea ulimaji wa migomba na utunzaji wa mimea.Tunachojiuliza coverage ya habari yako kwenye runinga ya TBC1 ni asilimia 30% na kuendelea kila siku, tumegundua huenda unayo ajenda yako ya urais 2015, lakini kumbuka kazi unayofanya ilipashwa kuwakilishwa na afisa kilimo ambaye ndiyo mtaalamu ndani ya jimbo lako na ndiye ataweza ku-implement strategies in place.

Lakini kikubwa zaidi mama huyu anatakiwa kurudi kuja kuwaongoza waathirika wa mafuriko kwani yeye ndiyo waziri mwenye dhamana ya nyumba na makazi, TUNAMTAKA AKATISHE ZIARA YAKE ARUDI KUWAJIBIKA

RUDI MJOMBA
 
mara mia waziri wa makazi amejitaidi japo kwa kutuma salamu za pole ingawa yupo Uganda kikazi.
Mi nadhani amethubutu kuonyesha kujali kuliko kaka mkuu wa nchi.

Kama ni salaam!!!! hata JK kamtumia mkuu wa mkoa, msipotoshe mada mama tibaijuka ni kiranja wa zamu kwa hili anapashwa kuwepo ili kuripoti matukio kwa kiranja mkuu
 
Mama tumekusikia tangu wiki iliyopita huko Uganda ukitembelea na kujionea ulimaji wa migomba na utunzaji wa mimea.Tunachojiuliza coverage ya habari yako kwenye runinga ya TBC1 ni asilimia 30% na kuendelea kila siku, tumegundua huenda unayo ajenda yako ya urais 2015, lakini kumbuka kazi unayofanya ilipashwa kuwakilishwa na afisa kilimo ambaye ndiyo mtaalamu ndani ya jimbo lako na ndiye ataweza ku-implement strategies in place.

Lakini kikubwa zaidi mama huyu anatakiwa kurudi kuja kuwaongoza waathirika wa mafuriko kwani yeye ndiyo waziri mwenye dhamana ya nyumba na makazi, TUNAMTAKA AKATISHE ZIARA YAKE ARUDI KUWAJIBIKA

RUDI MJOMBA

neno sahihi ni "ilipaswa"
 
Serikali ya JK iko active kuthibiti maandamano ya CDM si vinginevyo.
 
mara mia waziri wa makazi amejitaidi japo kwa kutuma salamu za pole ingawa yupo Uganda kikazi.
Mi nadhani amethubutu kuonyesha kujali kuliko kaka mkuu wa nchi.

Anamtumia nani salamu toka Uganda?
Anatakiwa avunje hiyo tour yake na arudi haraka sana nchini, yeye ndiyo anahitajika kutoa updates ya kila linaloendelea au hitajika.
Kwa hivyo hata hiyo tume iliyoundwa haina ushiriki wake kama waziri mwenye dhamana?
 
Huyu baba yetu nafikiri kichwani kwake kuna tatizo. Haiwezekani kabisa watoto wanaangamia, halfu baba yupo busy tu anaangalia TV! Shame on him!
 
Jamani inawezekana hali yake si nzuri si unajua huwa anatembea na ambulance sasa hiyo atakwendaje nayo huko kwenye maafa. Si wahanga wanaweza kumnyang'anya wakidai wao ndio wanaoistahili zaidi. Ndio maana akaona ni bora zaidi amtumie tu salamu shosti yake Sadick kwanza yeye mwenye hata hajaombwa msaada na shosti sa ajitie kiherehere cha nini??!!!
 
hivi yule mbunge anaitwa zungu au mzungu wa unga ni wa jimbo gani?
mkuu MMJ una uhakika Kikwete yupo Tanzania?yule jamaa kuna wakati anasafiri kwa siri,tunasubiri tuone
 
Back
Top Bottom