Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
- Wadai hauna nafasi katika jamiii ya Watanzania
- Wataka Pengo achunguzwe akibainika anachochea vurugu achukuliwe hatua
Rai hiyo wameitoa mwishoni mwa wiki walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Akitoa ufafanuzi juu ya waraka huo Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha TADEA, Bw. John Chipaka amesema kuwa kanisa katoliki kupitia wakala mkuu wa kanisa hilo nchini Mwadhama Polycarp Kanidali Pengo wamechukua waraka wa wanasiasa na kuuweka katika waraka wa kanisa.
Amesema kanisa hilo ujumbe mzima uliotumika katika waraka huo ulikuwa kwenye katiba ya vyama vya siasa ya mwaka 1992 na si wa kanisa katoliki.
Hivyo ilikuwa ni wajibu wa kanisa hilo kutoiga katiba hiyo na ilitakiwa kujipanga na kuandaa waraka stahiki mbali na huo wa kuigwa toka katika katiba ya wanasiasa ambao waliuandaa kudai demokrasia katika vyama vingi.
Waraka huo uliporwa toka kwa wapinzani wa vyama vya siasa wa madai ya kuboresha katiba ya nchi yetu na ulipelekwa mbele ya tume na kukataliwa na serikali ya chama tawala.
Anadai kinachoshangaza kuona kanisa hilo kukubaliana na wanataaluma wake kudai muafaka wakati kipindi hicho wakati vyama hivyo vilikuwa vinadai kuboresha katiba hiyo kanisa hilo lilikaa pembeni.
Amesema kanisa hilo kwa sasa lipo kwenye jitihada za kuwasafisha viongozi kupitia kanisa hilo kinyume na maadili ya kanisa hilo takatifu linavyohitajika litumike .
Pia vyama hivyo vilishangazwa na kitendo cha Kadinali Pengo kufoka na kughadhibika katika uma waliohudhuria mazishi ya Askofu Mkuu wa Jimbo la Mwanza Mhashamu Antony Mayala kuzungumzia mambo ya ufisadi kwenye mazishi hayo na ukomunisti kinyume na matakwa ya watu waliohudhuria mazishi hayo.
Wametaka Kadinali Pengo achunguzwe kiundani na akibainika kuwa anafanya uchochezi wa kuvuruga amani nchini akamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kama fujo zitaanzishwa na kanisa hilo zitahatarisha amani ndani ya nchi na hakuna atakayepona.
Hivyo walilitaka kanisa katoliki libadili msimamo wake na kurudisha na kusaka enzi za mungu kwa kuwafaidisha waumini wa kanisa hilo na kuacha kusaka utawala wa hapa duniani na bila kumwaga damu za wananchi wasio na hatia.
Chanzo: nifahamishe.com