Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kuna mjadala unaendelea wa kutafuta namna ya kumuenzi mzee Kawawa kwa kuliweka jina lake katika taasisi moja au zaidi ili kuakisi mchango wake katika historia ya ujenzi wa taifa letu. Hii inatokana na ukweli kwamba alitoa mchango mkubwa katika haki za wafanyakazi, sanaa, lugha na michezo na hata katika jeshi.
Alikuwa ni mwigizaji wa kwanza mzalendo
Muasisi wa shirikisho la wafanyakazi wa serikali
Mkuu wa nchi
Alitoa agizo la matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli za ofisi (agizo lake limerudiwa hivi karibuni)
Alishiriki katika uhamasishaji wa JWTZ wakati wa vita vya Kagera hadi kwenda mstari wa mbele kuwahamasisha wapiganaji
Alishiriki katika kandanda na hata kuwa mwamuzi
Ukiondoa barabara iliyopewa jina lake, ni taasisi gani nyingine ambazo zingeweza kupewa jina lake kwa heshima yake na mchango wake kwa taifa?
Alikuwa ni mwigizaji wa kwanza mzalendo
Muasisi wa shirikisho la wafanyakazi wa serikali
Mkuu wa nchi
Alitoa agizo la matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli za ofisi (agizo lake limerudiwa hivi karibuni)
Alishiriki katika uhamasishaji wa JWTZ wakati wa vita vya Kagera hadi kwenda mstari wa mbele kuwahamasisha wapiganaji
Alishiriki katika kandanda na hata kuwa mwamuzi
Ukiondoa barabara iliyopewa jina lake, ni taasisi gani nyingine ambazo zingeweza kupewa jina lake kwa heshima yake na mchango wake kwa taifa?