mkongojoli
Member
- Mar 8, 2009
- 20
- 6
Sio laana peke yake yaani mtakua mmetudisapoint sana watanzania kwa sababu hii ndo nafasi pekee ya kuiwajibisha serikali ya ccm, inawezekana 2010 tulichagua kwa kufuata mkumbo au uoga au kutojua au ahadi au kuhongwa nk. mambo ni mengi, kitu cha kujiuliza? kwa nini tusijifunze kutokana na makosa? namaanisha tulikosea kuichagua ccm,hilo sio kosa kwa nini turudie kosa tena? hata waswahili wanasema "kufanya kosa sio kosa ila kurudia kosa" mkichagua ccm mtakua mmerudia kosa na hapo hatutawasamehe, kwa hiyo please msirudie kosa, wote mnajua yaliyotokea na yanayoendelea kutokea ndani ya hii nchi, sina haja ya kuyataja yote kwani ni mengi ila tujikumbushe kidogo yaliyotokea baada ya ccm kuingia madarakani na hii hata mwaka haujaisha,mi nilifikiri watajifunza lakini wapi wote sisi ni mashahidi, walianza na
1. Malipo ya Dowans, wote mnakumbuka yaliyotokea
2. Wakaja akina Kombani na Werema kuhusu katiba,mnakumbuka walivyokuwa wanaongea
3. Ukaja muswada wa katiba, wote mnakumbuka pia ulivyokua mbovu
4. Ukaja mgao wa umeme, dah ndo balaa tupu mpaka sasa unaendelea
5. Kuna kupanda kwa gharama za maisha, hiki ni kilio cha kila mtu na hakuna walichofanya kututoa huko
Hivi karibuni pia mnakumbuka yaliyotokea
6. Wakati umeme bado ishu,likaingia la mafuta
7. Hatujasahau la mafuta mara akina Jairo hao
8. Hatujakaa vizuri suala la sukari limerudi tena
Haya ni kwa ufupi, tunajijua kua sisi ni waoga sana, hatuwezi hata kulalamika achilia mbali kuandamana kwa kisingizio kwamba tunadumisha amani,ok fine sasa hata hili la kutumia sanduku la kura nalo linatushinda? please tubadilike, kura yako ina thamani na inaweza kubadilisha hii hali, ifike wakati turelate umasikini wetu na uchaguzi wa viongozi tunaoufanya, hapo ndipo kura zitakapotuisaidia.
1. Malipo ya Dowans, wote mnakumbuka yaliyotokea
2. Wakaja akina Kombani na Werema kuhusu katiba,mnakumbuka walivyokuwa wanaongea
3. Ukaja muswada wa katiba, wote mnakumbuka pia ulivyokua mbovu
4. Ukaja mgao wa umeme, dah ndo balaa tupu mpaka sasa unaendelea
5. Kuna kupanda kwa gharama za maisha, hiki ni kilio cha kila mtu na hakuna walichofanya kututoa huko
Hivi karibuni pia mnakumbuka yaliyotokea
6. Wakati umeme bado ishu,likaingia la mafuta
7. Hatujasahau la mafuta mara akina Jairo hao
8. Hatujakaa vizuri suala la sukari limerudi tena
Haya ni kwa ufupi, tunajijua kua sisi ni waoga sana, hatuwezi hata kulalamika achilia mbali kuandamana kwa kisingizio kwamba tunadumisha amani,ok fine sasa hata hili la kutumia sanduku la kura nalo linatushinda? please tubadilike, kura yako ina thamani na inaweza kubadilisha hii hali, ifike wakati turelate umasikini wetu na uchaguzi wa viongozi tunaoufanya, hapo ndipo kura zitakapotuisaidia.