TIQO
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 13,787
- 2,078
TAARIFA YA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA FAMILIA YA WILLIAM SHELUKINDO KUHUSU UBUNGE JIMBO LA BUMBULI MKOANI TANGA
Kumezuka taarifa za uhakika kwamba tangu Mhe. Januari Makamba ashinde Ubonge katika Jimbo la Bumbuli hajawahi kukutana hata siku mmoja na mbunge wa zamani wa jimbo hilo Mzee William Shelukindo.
Katika hutuba yake alioitoa mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kura za maoni katika Chama cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Januari Makamba ailisema ataendelea kumuheshimu kama Mzee Shelukindo kama kiongozi wa muda mrefu kwenye Serikali.
Mheshimiwa Makamba aliendelea kusema Mzee Shelukindo ni hazina kubwa na uzoefu na busara zake bado zinahitajika katika jimbo la Bumbuli na kuahidi kuomba ushauri wake pindi atakapohitaji kufanya hivyo, wakati akiwatumikia wananchi wa Bumbuli kama mbunge wao.
Lakini kutokutana kwa viongozi hawa kutokutana tangu mheshimiwa Makamba achukue kumesababisha minong'ono na kuleta wasi wasi mkubwa kwa baadhi ya wanasiasa na wananchi wa Bumbuli.
Kumekuwa na upotoshwaji wa habari kwamba Mzee Shelukindo anawatayarisha watoto wake ili waweze kushindana na Mhe. Makamba katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.
Sisi kama watoto Mzee Shelukindo na tunawashutumu vikali baadhi ya wanasiasa wa Bumbuli ambao wamekuwa wakichochea maneno ili kuleta ugomvi na malumbano yasiokuwa ya msingi kati ya familia hizo mbili za Shelukindo na Makamba.
Watoto wa Mzee William Shelukindo, Bw. Samuel Shelukindo na Baraka Shelukindo wanawaasa wanasiasa wa Bumbuli kuacha uchochezi na kutotoa taarifa potufu na badala yake kumsaidia Mhe.Makamba ili kushughulikia changamoto zinazolikabili jimbo la Bumbuli.
Tunasema bado tuna mahusiano mazuri sana na Mhe. Makamba na tunamheshimu kama Mbunge wetu na hawatakubali kuona uhusiano huo unavurugwa na watu wachache wenye maslahi yao binafsi.
Sisi kama familia ya Shelukindo tunasema kwamba hakuna ndugu wala mtoto yoyote kutoka kwenye familia yetu mwenye nia ya kuingia kwenye siasa ili kupambana na Mhe. Makamba mwaka 2015.
Kama familia tupo kwenye mikakati ya kuwakutanisha Mhe. Makamba na Mzee Shelukindo ili kufuta fitna zilienezwa na kumuezesha Mhe. Makamba kuendelea kufanya kazi yake ya ubunge bila wasi wasi wowote kwa manufaa ya watu wote wa Bumbuli.
Asanteni
Bw. Samuel Shelukindo na Bw. Baraka Shelukindo
Cont:0784888765- Baraka Shelukindo
Kumezuka taarifa za uhakika kwamba tangu Mhe. Januari Makamba ashinde Ubonge katika Jimbo la Bumbuli hajawahi kukutana hata siku mmoja na mbunge wa zamani wa jimbo hilo Mzee William Shelukindo.
Katika hutuba yake alioitoa mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kura za maoni katika Chama cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Januari Makamba ailisema ataendelea kumuheshimu kama Mzee Shelukindo kama kiongozi wa muda mrefu kwenye Serikali.
Mheshimiwa Makamba aliendelea kusema Mzee Shelukindo ni hazina kubwa na uzoefu na busara zake bado zinahitajika katika jimbo la Bumbuli na kuahidi kuomba ushauri wake pindi atakapohitaji kufanya hivyo, wakati akiwatumikia wananchi wa Bumbuli kama mbunge wao.
Lakini kutokutana kwa viongozi hawa kutokutana tangu mheshimiwa Makamba achukue kumesababisha minong'ono na kuleta wasi wasi mkubwa kwa baadhi ya wanasiasa na wananchi wa Bumbuli.
Kumekuwa na upotoshwaji wa habari kwamba Mzee Shelukindo anawatayarisha watoto wake ili waweze kushindana na Mhe. Makamba katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.
Sisi kama watoto Mzee Shelukindo na tunawashutumu vikali baadhi ya wanasiasa wa Bumbuli ambao wamekuwa wakichochea maneno ili kuleta ugomvi na malumbano yasiokuwa ya msingi kati ya familia hizo mbili za Shelukindo na Makamba.
Watoto wa Mzee William Shelukindo, Bw. Samuel Shelukindo na Baraka Shelukindo wanawaasa wanasiasa wa Bumbuli kuacha uchochezi na kutotoa taarifa potufu na badala yake kumsaidia Mhe.Makamba ili kushughulikia changamoto zinazolikabili jimbo la Bumbuli.
Tunasema bado tuna mahusiano mazuri sana na Mhe. Makamba na tunamheshimu kama Mbunge wetu na hawatakubali kuona uhusiano huo unavurugwa na watu wachache wenye maslahi yao binafsi.
Sisi kama familia ya Shelukindo tunasema kwamba hakuna ndugu wala mtoto yoyote kutoka kwenye familia yetu mwenye nia ya kuingia kwenye siasa ili kupambana na Mhe. Makamba mwaka 2015.
Kama familia tupo kwenye mikakati ya kuwakutanisha Mhe. Makamba na Mzee Shelukindo ili kufuta fitna zilienezwa na kumuezesha Mhe. Makamba kuendelea kufanya kazi yake ya ubunge bila wasi wasi wowote kwa manufaa ya watu wote wa Bumbuli.
Asanteni
Bw. Samuel Shelukindo na Bw. Baraka Shelukindo
Cont:0784888765- Baraka Shelukindo