Taarifa ya serikali juu ya mgomo wa madaktari

Mkandara, kwenye taarifa ya bahari ITV 8pm yuko mzee mmoja (zaidi ya miaka 60) amevunjika mguu na alipoenda MOI hakupata matibabu kwa sababu ya mgomo. Lakini yule mzee alisema bila kumumunya maneno "madaktari wagome hadi wapate haki yao". Unaweza kuona ni jinsi gani wananchi wameamua kugharamia mabadiliko - life on the line kwa huyu mzee lakini aona bora iwe hivyo.

Na leo hii wabunge wa ccm hawako kwenye mood ya kujadili huu mgomo badala yake wamekazania kujadili JF! inasikitisha.
Huyu ni mzee mmoja kati ya wagonjwa wangapi wanaofikiria hivyo?. Ikiwa leo wapo Watanzania ambao wanafikiria kwa fikra zao mtu kama Lowassa ambaye miaka mitano tu iliyopita alikuwa adui mkubwa wa jamii na anayestahili kifungo cha Segelea, leo anahimizwa na kusifiwa il arudi madarakani unafikiri sisi wazima kweli?.
Kifupi mkuu wangu nimegundua jambo muhimu sana ambalo zamani nilijiaminisha kwamba vijana wasomi wa leo wanaweza kuleta mabadiliko kumbe nilikuwa najidanganya kama wadanganyika wengine. Inasikitika sana kuona Taifa langu linakoelekea lakini yanibidi kukubali matokeo kwa sababu UMOJA hautapatikana kutokana na sisi wenyewe kuupoteza UTU.
 
Hadi kufikia Jana, tarehe 01 February 2012, Rais wa sasa wa Tanzania, amesafiri mara 322 nje ya nchi. Ukizidisha hiyo idadi ya tripu/safari ( 322) kwa wastani wa siku 4 kwa kila tripu/safari. Utapata jumla ya siku 1288. Hizi siku 1288 ukizigawa kwa siku 365/366 ( siku za mwaka mmoja) utapata miaka 3.5 (yaani mika 3 na miezi 6) Rais amekaa nje ya mipaka ya Tanzania. Kwa kuwa Rais Jk aliingia madarakani mwaka 2005 na hadi sasa 2012 amekaa madarakani kwa miaka 6. Kwa hiyo, Rais amekaa nje ya nchi zaidi ya nusu ya muda wake wote aliokaa ktk nafasi ya urais (3.5 yrs out of 6 years) Je, Rais hajavunja rekodi ya kuingizwa ktk Guiness book of rekords ya dunia? Yaani Rais aliyekaa nje ya nchi yake kwa muda mrefu kuliko marais wote wa dunia? Rais gani amemezidi Rais wetu? Je, tumepata jibu la kwanini Rais mara nyingi husaini nyaraka feki kwa sababu ya ukosefu wa Muda wa kuzisoma? GHARAMA Safari ya mwisho ( safari ya 322) ya Davos 25 – 28 January 2012, iliigharimu Serikali Tsh mil 300. Nikiamu kuchukua theluthi mbili ya gharama hizo - yaani mil 200, kisha nikazidisha kwa idadi ya tripu 322. Jumla yake ni 64,400,000,000. Mabilioni haya ni mengi sana. Ukizigawa mil 50 ambazo ndio gharama ya kujenga zahanati mmoja kwa wastani, utapata jumla ya Zahanati 1288. Kwa kuwa Tanzania ina jumla ya Kata 2011, fedha hivi zingetosheleza kuweka zaidi ya 60%. Ikumbukwe kuwa Tz wanawake wajawazito kati 24 hadi 36 kwa siku wanakufa kwa sababu kadhaa ikiwepo kutokuwepo kwa zahanati au ziko mbali

upupu mtupu.
 
Hiyo taarifa ya Serikali uongo mtupu, kwanza nataka waziri wa afya achukuliwe hatua kwa kutoa tathmini ya uongo. Yani anasema hali ni shwari ma intern wamerudi kazini KCMC wakati nina habari za uhakika kabisa hawajarudi kazini. Anasema Muhimbili wale wanajeshi 15 wanahudumia wagonjwa na huduma ziko vizuri. Hivi Serikali ya aina gani inaweza kudiriki kudanganya ikiwa macho makavu hivyo?
 
Mbona kama haijakamilika hii????


Hivi ndivyo serikali ilivyouelezea mgomo wa Madaktari Bungeni

- Mgogoro ulianza baada ya madaktari wa mafunzo ya vitendo kugoma kwa jili ya kutaka malipo yao
- Serikali iliwapa malipo yao
- Lakini waliendelea na mgomo
- MAT iliingilia kati na kuendeleza mgomo
- MAT ikaunda kamati ya muda na kuendeleza mgomo

My Take
Taarifa imeegemea ktk kukandamiza madai ya msingi ya mgomo huo.
Serikali makini hujali watu wake na hutumia njia za hekima kutatua disputes zinazojitokeza kwenye jamii

 
Zote hizi sio "Professional BOards" kama NBAA, ERB. Hazikuanzishwa kwa "Act" yoyote ya Bunge. Hazina nguvu sana kisheria.


WildCard, inaonekana huwa hufuatilii sheria zitungwazo na Bunge. Hizo zote ni bodi za udhibiti na zimeanzishwa kwa sheria za bunge kama ifuatavyo:

  1. Optical Council of Tanganyika [Established by Opticians Act, 1965 (Act No. 6 of 1966)]
  2. Medical Council of Tanganyika [Established by Medical Practitioners and Dentists Ordinance, Cap. 409 as ammededed by Act No. 24 of 1968 ]
  3. Pharmacy Board or Pharmacy Council [Established by The Pharmacy Act No. 1 of 2011]
  4. Tanzania Nurses and Midwives Council [Established byThe Nurses and Midwives RegistrationACT, 1997, Act No. 12 of 1997]
  5. Private Health Laboratories Board [Established by Private Health Laboratories Regulation Act, 1997; Act No. 10 of 1997]
 
Back
Top Bottom