Taarifa ya matokeo ya sensa ya idadi ya tembo

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Kwa mujibu wa sensa iliyofanywa mwezi Oktoba na Wizara ya Maliasili na Utalii, kwa sasa Selous-Mikumi ina tembo wapatao 13,084 na Ruaha–Rungwa tembo wapatao 20,090. Takwimu hizi zinaonesha kupungua kwa idadi ya tembo na hasa Selous-Mikumi ikilinganishwa na Sensa za awali.

Mwaka 1976 Selous–Mikumi ilikuwa na tembo 109,419. Idadi hii ilipungua kufikia 22,208 mwaka 1991 kutokana na wimbi la ujangili uliokuwepo katika kipindi cha mwaka 1984 -1989.

Hata hivyo, idadi hiyo iliongezeka na kufikia 70,406 mwaka 2006 baada ya Operesheni Uhai iliyofanyika mwaka 1989 na 1990 na juhudi za kimataifa za uhifadhi ikiwemo kusitisha biashara ya meno ya tembo. Aidha, idadi ya tembo nchini ilipungua hadi kufikia jumla ya tembo 38,975 mwaka 2009 na kuendelea kupungua hadi kufikia tembo 13,084 hivi sasa.

Hali kama hiyo inaonekana pia Ruaha-Rungwa ambapo sensa ya mwaka 1990 ilionesha kuwa na tembo 11,712 kutokana na wimbi la ujangili. Idadi hii iliongezeka na kufikia 35,461 mwaka 2006. Hata hivyo, idadi hiyo imepungua na kubakia tembo 20,090 hivi sasa.

Kwa matokeo haya inaonyesha kuwa idadi ya tembo
Selous-Mikumi imepungua kwa asilimia 66 ikilinganishwa na idadi ya mwaka 2009 ambapo kulikuwa na jumla ya tembo 38,975. na huko Ruaha–Rungwa tembo wamepungua kwa asilimia 36.5 ikilinganishwa na idadi ya mwaka 2009 ambapo kulikuwa na jumla ya tembo wapatao 31,625.

Kupungua huku kunathibitishwa na idadi ya mizoga ya tembo iliyohesabiwa wakati wa zoezi la sensa. Jumla ya mizoga 6,516 na 3,496 ilihesabiwa katika mifumo ikolojia ya Selous-Mikumi na Ruaha–Rungwa. Katika zoezi hilo Wizara ilitumia vigezo vya uwiano wa mizoga na tembo hai waliohesabiwa (carcass ratio) kubaini vyanzo vya vifo hivyo. Katika hali ya kawaida, uwiano wa asilimia 7 – 8 unaashiria vifo vya asili kama vile ugonjwa na uzee.

Zaidi ya asilimia hiyo inaashiria vifo visivyo vya asili. Sensa iliyofanyika mwaka huu imeonesha uwiano wa asilimia 30 huko Selous-Mikumi na asilimia 14.6 kwa Ruaha–Rungwa. Kwa mujibu wa matokeo hayo, idadi kubwa ya vifo vya tembo vimetokana na vifo visivyo vya asili.

Chanzo: Kutoka Wizara husika.
 
Tungependa tupate taarifa za huo mtandao unaoua tembo kwa wingi kiasi hicho na waliokamatwa au walio na kesi za ujangili mahakamani
Kutuletea taarifa za takwimu bila kutupa wahusika wa huu ujangili hakutoshi EMT heri ya mwaka mpya mkuu na pia mwekundu
 
Last edited by a moderator:
Tungependa tupate taarifa za huo mtandao unaoua tembo kwa wingi kiasi hicho na waliokamatwa au walio na kesi za ujangili mahakamani. Kutuletea taarifa za takwimu bila kutupa wahusika wa huu ujangili hakutoshi EMT heri ya mwaka mpya mkuu na pia mwekundu

Kwa mujibu wa hiyo taarifa, "Uchambuzi wa kina umebainisha kuwa asilimia 95 na 85 ya mizoga iliyoonekana Selous-Mikumi na Ruaha–Rungwa ni ya zaidi ya miezi 18 iliyopita. Hii inaonesha kuwa juhudi za makusudi zilizofanywa na serikali ikiwa ni pamoja na kuimarisha doria na operesheni maalum mbalimbali za hivi karibuni zimesaidia kupunguza wimbi la ujangili kwa kiasi kikubwa."
 
majitu ni makatili kweli, yaani unaua tembo na unachukua pembe tu. Mung angekuwaga na hasira kama binadam hao wauaji wangepigwa kiberit cha gesi wakafa
 
Mkuu EMT tatizo kubwa hapa liko kwenye ngazi za utawala kwenyewe
Idadi ya Askasri walioajiriwa kupambana na ujangili kwa kweli ni kidogo sana na wanasimamia eneo kubwa sana na huku vitendea kazi vikiwa duni na mishahara isiyotosheleza na ambayo kwa kiasi kikubwa inachochea rushwa
Niliwahi kutembelea sehem mbali mbali za hifadhi na kuongea na askari kwa kweli hali zao ni mbaya sana na wanatembea na kulinda eneo kubwa bila tahadhari au gari la doria kuwa karibu kiasi kwamba kukitokea cha kutokea askari yule hana utetezi na kwake ni rahisi sana kuuwawa au kurubuniwa na majangili akaachia wafanye kazi zao
Mtandao wa ujangili haswa wale wanaokwenda field ni mpana sana na wana silaha nzito na risasi za kutosha na wamejihimili kwa lolote either wafe wao au waue askari wa wanyamapori ili mradi lengo lao lifanikiwe nalo ni kupata nyara
Tuseme wazi juhudi zinahitajika kwa kiasi kikubwa sana haswa kunyanyua ari ya askari hawa wanaopambana na majangili porini, kuwaongezea vifaa na maslahi yao na kuongeza pia idadi yao kwani wanafanya kazi kubwa sana
Huwezi tegemea askari kama wale wa Morogoro waliovamiwa na mmoja wao kuuwawa na majangili na wakakosa msaada wa polisi kuendelea kuwalinda tembo ni lazima wakiona majangili wao watakimbia na kuwaacha wafanye kazi yao
Maeneo mengine kama tukio moja lilitokea eneo la Maswa majangili walikuwa wamebeba risasi na ndoo na huku wakiwa na magazine kama nne zimejaa risasi huku askari wa wanyamapori ana risasi tatu apambane na watu kama hao
kazi ya ziada inahitajika
Sijui kama nimetoka nje ya mada mkuu
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
Ni vipi wanyama wakapewa hadhi kubwa kuliko binadamu? Kwa nini wanadamu wazuiliwe kutumia maliasili kama miti,madini na wanyama kwa manuafaa yao?
 
Mkuu EMT tatizo kubwa hapa liko kwenye ngazi za utawala kwenyewe
Idadi ya Askasri walioajiriwa kupambana na ujangili kwa kweli ni kidogo sana na wanasimamia eneo kubwa sana na huku vitendea kazi vikiwa duni na mishahara isiyotosheleza na ambayo kwa kiasi kikubwa inachochea rushwa
Niliwahi kutembelea sehem mbali mbali za hifadhi na kuongea na askari kwa kweli hali zao ni mbaya sana na wanatembea na kulinda eneo kubwa bila tahadhari au gari la doria kuwa karibu kiasi kwamba kukitokea cha kutokea askari yule hana utetezi na kwake ni rahisi sana kuuwawa au kurubuniwa na majangili akaachia wafanye kazi zao
Mtandao wa ujangili haswa wale wanaokwenda field ni mpana sana na wana silaha nzito na risasi za kutosha na wamejihimili kwa lolote either wafe wao au waue askari wa wanyamapori ili mradi lengo lao lifanikiwe nalo ni kupata nyara
Tuseme wazi juhudi zinahitajika kwa kiasi kikubwa sana haswa kunyanyua ari ya askari hawa wanaopambana na majangili porini, kuwaongezea vifaa na maslahi yao na kuongeza pia idadi yao kwani wanafanya kazi kubwa sana
Huwezi tegemea askari kama wale wa Morogoro waliovamiwa na mmoja wao kuuwawa na majangili na wakakosa msaada wa polisi kuendelea kuwalinda tembo ni lazima wakiona majangili wao watakimbia na kuwaacha wafanye kazi yao
Maeneo mengine kama tukio moja lilitokea eneo la Maswa majangili walikuwa wamebeba risasi na ndoo na huku wakiwa na magazine kama nne zimejaa risasi huku askari wa wanyamapori ana risasi tatu apambane na watu kama hao
kazi ya ziada inahitajika
Sijui kama nimetoka nje ya mada mkuu

Kuna mtu alipendekeza wanajeshi wawe wanafanya doria huko (siyo disaini ya operesheni tokomeza lakini).
 
Ni vipi wanyama wakapewa hadhi kubwa kuliko binadamu? Kwa nini wanadamu wazuiliwe kutumia maliasili kama miti,madini na wanyama kwa manuafaa yao?

Tukwangue mbuga zote tuzifanye mashamba? Maana kuna upungufu wa chakula cha binadamu.
 
Kuna mtu alipendekeza wanajeshi wawe wanafanya doria huko (siyo disaini ya operesheni tokomeza lakini).

Mkuu EMT hakuna wa kumwamini maana kuna na wanajeshi wanashiriki kwenye huo mtandao wa ujangili ila angalau itasaidia maana wanajeshi kama wa JKT badala ya kwenda kukaa uraiani wapewe kazi hiyo ya kulinda mapori haya
 
Last edited by a moderator:
kwa takwimu hizo kufikia mwakani 2015 mwaka wa uchaguzi mkuu mikumi itabaki na tembo wasiozidi 2000,
 
Kwa kuondoka KAGASHEKI tutarajie kubaki na Tembo 5000 hadi watakapoondoka hawa majangiri CCM hapo 2015.
 
Kuna mtu alipendekeza wanajeshi wawe wanafanya doria huko (siyo disaini ya operesheni tokomeza lakini).

Mkuu EMT hawa wanajeshi nao ndo majangili mara kibao wamekamatwa na nyara kwenye magari yao kwa ujumla mfumo mzima wa ulinzi umedorora hii nikutokana na kwamba ajira za hawa watu sikuhizi ni za kimzengwemzengwe nawengi wao hawajasoma(rejea uhakiki wa vyeti uliositishwa baada ya kuonekana idadi kubwa wanatumia vyeti vya watu wengine) .Watu wanamna hii unakuta ni wavuta Bangi,hawana maadili,hawajali kazi yao uzalendo kwao ni msamiati mgumu kwa hiyo kwa ujumla nchi inajikuta ina lundo la askari ambao badala ya kulinda usalama wa raia,nchi na mali zao wana uhatarisha kiasi cha kusababisha raia wajilinde dhidi ya skari na kujilinda kwa ajili ya usalama wa nchi,mali na maliasili.

Kinachotakiwa hapa ni kuponda kichwa cha huu mtandao na hicho kichwa hakipo huko operation zinakofanyika kipo huku Dar kwani Nyara zote zinakamatiwa huku na makontena yanapita Bandarini sasa wanachoshindwa kutress clue hapo nini? kweli kunahitajika Bunduki na lundo la Risasi kuchunguza waliokagua na kuidhinisha kontena kuvuka na kupakiwa kwenye meli au kuwahoji wachina kuhusu wanaowaletea na kama hawatoi majibu ya kuridhisha kwanini tusikimbie Bungeni na kutunga kasheria kaharakaharaka kanako aply retrospective kenye adhabu za kunyonga na kuanzisha Mahakama maalum ambayo hukumu ikitolewa basi mtu asikae zaidi ya wiki kabla ya kunyongwa hii tu ndiyo itakayowatisha hawa jamaa

Vinginevyo itaendelea kuwa hadithi ya Kuku na yai nani alitangulia!
 
Mkuu EMT hakuna wa kumwamini maana kuna na wanajeshi wanashiriki kwenye huo mtandao wa ujangili ila angalau itasaidia maana wanajeshi kama wa JKT badala ya kwenda kukaa uraiani wapewe kazi hiyo ya kulinda mapori haya
Kajunjumele BA kafafanua zaidi hapo juu.
 
Last edited by a moderator:
Tukwangue mbuga zote tuzifanye mashamba? Maana kuna upungufu wa chakula cha binadamu.
Mkuu wangu EMT, kwa vyovyote itakavyokuwa haiwezekani wanadamu wasinufaike na wanyama. Mi naona ilitakiwa kuwepo na taratibu rasmi za kuvuna hayo mazao yatokanayo na wanyama wetu wa asili la si hivyo ujangili hautakwisha! Ng'ombe wanaliwa na hawaishi....
 
Last edited by a moderator:
Mkuu EMT nimeuona ufafanuzi wa Kajunjumele ba na nakubaliana na yeye kwa kiasi kikubwa
Tatizo haliko kwa wananchi wanaozunguka hizi hifadhi liko kwenye mtandao ambao ni mkubwa sana na umesambaa kila sehem na unaoendesha ujangili huu kwa mbinu zote za kisayansi wanazozijua
Wananchi waliopigwa au kuteswa wengi wao ni wale wanaoingia kwenye hifadhi kutafuta kitoweo cha swala mmoja au digidigi kwa ajili ya mlo na walikutwa na ngozi za swala au digidigi
Mtandao upo kwa hao wanaopitisha nyara hizo meno ya tembo container kwa container ambao mtandao huo ni mkubwa
Dar haina tembo, temno wako mikumi au selous au ruaha au maswa au moyowosi na kizigo au serengeti ila container zenye pembe za ndovu zinakamatwa Dar na Zanzibar huko zilikopita na zilikopitiswa hakuna ajuae au je siku hiyo ukaguzi haukufanyika hakuna ajuaye na je container hizo hazina wenyewe hakuna ajuaye na je zilipopitishwa zilisajiliwa kwa jina gani hakuna ajuaye wala hatujawahi kuambiwa ni za nani ila zimekamatwa
Bila kuumaliza huo mtandao wa wanaozikusanya na wanaoenda kuwinda idadi kubwa hivyo ya tembo hatutakuwa na salama na bado ujangili utaendelea na hakuna mkuu yoyote wa pale Wizarani au bandarini atakayekuja hapa kutuambia kuwa ujangili umekwisha
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Back
Top Bottom