Nadhani huna sabau ya kunyanyapaa wanoumwa ukimwi. Magonjwa hayachagui wagonjwa; binadamu yeyote anaweza kuugua uganjwa wowote.
Tusifikishane huko!
Nadhani hujanielewa neno nililokuwa nataka kusema mie sikuwa na azma ya kumnyanyapaa mwenye ukimwi wala mafua ya kuku wote ni wagonjwa na kila mtu anaumwa ugonjwa huo na kama umenifahamu vizuri nimemuombea rais afya njema.
Kimsingi ishu ni kwamba miafrika especially sie watanzania hatupendi kuambiwa ukweli au tunapenda kutengeneza majungu na lawama zisizo na msingi. Daktari wa rais keshasema Muheshimiwa yuko fiti. Sasa wengine wanasema huo ni uongo au mara rais ana CD-4 (kama ndio inavyoandikwa) la msingi hizi zote ni fitna na chuki zilizomo ndani ya mioyo ya watu kwani inakukocost nini kumuombea afya njema mkuu wetu wanchi au just kwa vile huendani na policy zake. Vumilia atakuja utakayeendana nae na sio kupiga kelele mara ana umwa hivi mara vile alimradi tu kutia doa kwa kiongozi wa nchi.
Mie sio mpiga debe wala mpiga kampeni wa ccm but waswahili wanasema maskini mpeni haki yake. Mtu ameanguka kwa ajili ya uchovu na mzima basi mwacheni aendelee na shughuli ya kuongoza nchi na sio kukaa mkazungumza mie naona anaumwa hiki mara kile tuzungumze vitu vya msingi mfano BOT wanaunganisha vyeo viwili vya gavana na chairman wa board BOT serikali ndio juzi imeona umuhimu wa kuvitenganisha baada ya madudu haya je wale waliokwisha iba wafanyiwe nini!!! na sio kudiscuss afya ya rais