Taarifa ya daktari wa rais

Jamani ebu tutulize munkari kidogo.

Rais kapima vipimo vyote, vinaonyesha afya yake nzuri.
Lakini kila akisimama kuhutubia anazimika.
Madaktari wa hapa, Ulaya na Marekani wanasema hana tatizo.
Lakini kuzimika kunaendelea. Tufanyeje?

Kuna mkono wa mtu hapa. Lazima wataalam watafutwe. Na wapo ukienda Ikulu utawakuta siku hizi.
 
Nani aliyetaka afya ya Rais..wanajibu maswali ambayo haya kuulizwa na mtu yeyote..there is something fishy! ukute wakatoliki wanataka kumwua maana chuki zao hazina kipimo nadadisi tu!

What is this?
Is this what we call freedom of expression blaspheming others?
Hii thread imechukua a wrong turn.Ni udini sasa na porojo za kisiasa zimeanza!
 
Jamani ebu tutulize munkari kidogo.
Kuna mkono wa mtu hapa. Lazima wataalam watafutwe. Na wapo ukienda Ikulu utawakuta siku hizi.

Hizi Bangi! Unajichanganya changanya kama huna cha kuchangia kaa kimya
 
jamaa mtadhani kuku wamemwagiwa punga?duh kweli watz kwa porojo kazi kweeli kweeeli
 
Jamani ebu tutulize munkari kidogo.

Rais kapima vipimo vyote, vinaonyesha afya yake nzuri.
Lakini kila akisimama kuhutubia anazimika.
Madaktari wa hapa, Ulaya na Marekani wanasema hana tatizo.
Lakini kuzimika kunaendelea. Tufanyeje?

Kuna mkono wa mtu hapa. Lazima wataalam watafutwe. Na wapo ukienda Ikulu utawakuta siku hizi.

Kuzimika pia ni tatizo au sio?
 
Hata Mengi nilisikiaga ana mdudu tokea mwaka '94 lakini huyo bado anapeta tu...

Mijitu kwa ku speculate afya za watu tu...aaarrrggh

Julius,

Ni kweli kuna speculation katika afya ya Kikwete lakini pia kuna matukio ya wazi kama hili la Mwanza. Kama umeona zile picha zilizoweka utagundua kuwa Kikwete alizimika kabisa (yaani shingo ikalalia upande).

Watu wanataka kujua kuwa kuna matibabu yanaendelea. Kukataa flat out kuwa hakuna tatizo na wakati watu wameona wenyewe kilichotokea ndio issue hapa kwa baadhi ya watu (mimi mmoja wao).

BTW --- mimi sio mmoja wa wanaosema kuwa Kikwete ana ngoma.
 
Kama tatizo ni uchovu kwanini hamkumshauri mapema Rais?
Madakitari mmesubiri mpaka aanguke ndiyo mseme hayo yote?
Sijawaelewa madakitari. Kiini Machoooo...........

Rais mwenyewe baada ya tukio la Mwanza alisema kwamba alishauriwa na wasaidizi wake apumzike akawa MBISHI,sasa wewe sijui ulitaka wamshauri vp mkuu..Usiwalalamikie sana madaktari mkuu,walifanya kazi yao
 
Hata Mengi nilisikiaga ana mdudu tokea mwaka '94 lakini huyo bado anapeta tu...

Mijitu kwa ku speculate afya za watu tu...aaarrrggh

Tatizo Bongo ujuaji mwingi mkuu,kuna watu kibao wanawapima wenzao kwa kupitia vipimo vya macho yao
 
Hata Nyerere mlisubili afe ndo mjue chakuongea. Alafu huo uchovu uliokithili JK aliutoa wapi? Hizo safari alikuwa anakwenda kwa miguu, mbona anaosafiri nao huwa hawachoki kiasi cha kuanguka? Mara ya kwanza ilikuwa 2005, alianguka peke yake. Mbowe aliyefanya safari nyingi kuliko wote kwa helikopta hatukusikia ana uchovu na hata kuanguka. Leo ni 2009, JK kaanguka tena peke yake. Naona huyu rais ni mchovu kwa kila kitu, hata uongozi.
 
Ni kifafa tu ,akuna jingine ,kama aliishiwa nguvu na kupinda shingo bila ya shaka hapo hakuna mbadala na arudishwe uraiani apatiwe matibabu,kama hao madoctors wanaona clear katika vipimo vyao.
Na kuhusu infections za uti wa mgongo na shingo hilo si dogo ,ni jambo ambalo linaweza kuparalizisha sehemu fulani kwa wakati fulani ,kwa maana unakuwa unajikumbuka position zako za kuutegea mwili ,sasa kindende ukisahau na ukakosea na kuzisitua sehemu zenye athari hapo unaweza ukajikuta unapiga mweleka chali au pindu ,ila baada ya kukaa sawa na kujipiga na chini unakuwa upo makini na bila ya tabu yeyote ile unairudia hali yako ,japo utakuwa na maumivu ya ndani ,inaweza ikakuchukuwa muda kusahau tena na ndivyo inavyoonekana kwa Mheshimiwa ,labda mutafute dataza za siku ya matukio hayo ya kuanguka ,mutaona ni kila baada ya muda gani anakuwa anajisahau na kujiona yupo fiti kufanya manjonjo.
Dakitari amesema siku hizi hatikisi shingo na kichwa ,hii inamaana utingishaji wake unatokana na kuviweka sawa viungo vya sehemu hiyo. Athari hizi hutokea sehemu zinazokaribiana na mabega na ikiwa kuna kitu kitapata msituko katika sehemu hizo unaweza kuanguka au kujikuta unaelemea upande mmoja na tindi za mgongo za sehemu hiyo inasemekana huwa zinapata maumivu yanayoendelea kwa muda wa masiku ,japo utamuona mtu yupo makini lakini anakuwa hana nguvu na ugeukaji wake unakuwa wa kutegea tegea kama aneogopa kusituka shingo.
Sasa kidogo tumefarijika kwa kuijua hali ya Mheshimiwa Raisi na ugonjwa unaomsumbua ,anaweza kuparalize asifanye mchezo na mambo ya uti wa mgongo ni hatari sana ,na hili nimeliona pale dakitari walipomshauri na kumwambia afanye mazoezi tena mazoezi maalum , ni kweli kabisa nimeshawaona watu waliokuwa na kupata atahari hizo wakipewa aina ya mazoezi fulani tu.

Watupe na muhtasari wa afya ya Nkapa tuone ,jamaa anatumia vidonge vya kuzidisha unene ili kupambana na mdudu. Kama mnamkumbuka Mkapa na alivyo sasa mtajua unene unaomzidi si wa kawaida .tutampeleka Geneva hivyo hivyo.
 
nadhani tuna mambo mengi ya kujadili......kafa nyerere aje yeye?? Wengine si wapowatachukua madaraka??
 
Waungwana wanasema hasidi hawi bwana hata siku moja sasa wewe nikuulize ulitaka Daktari wa Rais asemeje ashakwambia hana tatizo lolote.

Mie binafsi nashukuru kwasababu urais ni taasisi hivyo kama mkuu wa taasisi anaumwa then nakuwa na wasiwasi na mwelekeo wa taasisi. Sasa wewe unasema uongo ulitaka wakwambia rais anaumwa kiharusi, sijui uzushi katazame gazeti la udaku kule Global Publishers, mwishoe mtadai rais anaumwa ukimwi (mmungu amuepushie nao mbali).

Acheni chuki zenu bwana kama hamkumchagua kikwete mie nilimchagua na nitampa kura mwakani mmungu akiniweka hai. But ukweli lazima usemwe na sio majungu tu yasiyo na mpango alaa!!!!

Nadhani huna sabau ya kunyanyapaa wanoumwa ukimwi. Magonjwa hayachagui wagonjwa; binadamu yeyote anaweza kuugua uganjwa wowote.
Tusifikishane huko!
 
Nimeisha kaa mara nyingi na Rais Kikwete, anapiga sana miayo!! huo si ugonjwa? au inatokana na nini?? sipendi kusikia Majibu ya juu juu kuwa miayo hiyo ina sababishwa na njaa. Siamini kuwa Rais wangu hupigwa na njaa mara nyingi hivyo !! Kama Dokta umeamua kusema kuhusu afya yake tueleweshe vizuri tuamini unachosema.
 
Sasa imewekwa wazi, na wananchi wameondolewa wasiwasi kuwa Rais wao ni mgonjwa baada ya kuwa anazidiwa mara kadhaa kila anapopatwa na kile kinachoelezwa kuwa uchovu wa kazi.
Leo Daktari wa Rais Jakaya Kikwete, Peter Mfisi ameibuka na kuqweka kila kitu hadharani kuhusu afya ya Rais wetu.
Daktari huyo akiwa Ikulu, akasema Rais Kikwete hana Ukimwi, hana kansa, hana dalili za kiharusi na kamwe hakuna kaugonjwa kokote kwenye damu yake wala nyama zake.
Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya Rais Kikwete kuishiwa nguvu wakati akihutubia katika Jubilee ya miaka 100 ya Kanisa la Africa Inland Tanzania (AICT) jijini Mwanza wiki iliyopita.
"Naelewa fika kutokana na kiapo cha udaktari na maadili yangu, siruhusiwi kutoa hadharani undani wa habari yoyote inayohusu mgonjwa ninayemtibu bila ridhaa yake...
... Kwa kuwa huyu ni Rais wa nchi, na suala la afya yake ni kwa maslahi ya Taifa na umma wa Watanzania kwa ujumla, na kwa kuwa yeye ameridhia kutolewa kwa habari za afya yake ili watu wajue ukweli na kuondoa hofu, nimeamua kufanya hivyo,"alisema Mfisi.

Alisema kila mara Kikwete amekuwa akipimwa na kufanyiwa uchunguzi wa afya yake na madaktari wa Tanzania na wale wa nje ambako huenda mara kwa mara na wote wamebaini kuwa hana kaugonjwa kokote kanakowez kufikiriwa na yeyote.
Mungu Mkubwa jamani, yote mabaya yaliyokuwa yakielezwa na wale wachokozi, kumbe hamna kitu na hiyo imethibitishwa na madaktari wake na wale wa nje, ambao nasikia hawana punje ya rushwa hata kusema uongo.
 
Eti anapunguza damu kila baada ya miezi 6!!! Si useme tu ukweli daktari. Au ndio kiapo hakiruhusu kusema?
 
eti anapunguza damu kila baada ya miezi 6!!! Si useme tu ukweli daktari. Au ndio kiapo hakiruhusu kusema?

tutumie muda zaidi kuitafakari hii taarifa yake kwa makini sana, hebu m.m.k.j tuambie umeelewa hapa anachokimaanisha daktari wa mkuu. Isije iwaka ni profile satatment kuficha ukweli kama ambavyo birthday yake ilivyoandaliwa kwa ajili ya kutufanya kusahau la kuishiwa nguvu mwanza
 
Eti anapunguza damu kila baada ya miezi 6!!! Si useme tu ukweli daktari. Au ndio kiapo hakiruhusu kusema?


i know this young man who is the predaa dr....kijana umekosea sana...kuiweka ripoti ya rais kwa urefu as if kuna kitu mnatetea hapo...psychology nyepesi hapo ni kuwa you have been toooo defensive which leaves quaetions as to what is the motive of being too elaborative....hata kama amekulazimisha utoe ripoti ungekuwa too brief...

....sasa ripoti yako ya kitaalamu umeiandika kisiasa ...itabidi uwe tayari kujibizana na wanasiasa.....

..huwa nafuatilia ripoti za marais mbalimbali duniani.....na ripoti za namna hii huwa brief short and clear......abide to your proffession ,....usimsikilize kikwete...ambaye yeye mwenyewe amekiri hapa kuwa ushauri wenu huwa anaukiuka......lakini kwenye ripoti yako umemsifu kwa kufuata ushauri....ianamaana kwa kumsifu kuwa aanafuata ushauri na amekiri hafuati..umesema uwongo...and this subject and jeoperdise all your report ...and it worth be called the scrap propaganda report!!!!

umeitukana fani yako mdogo wangu ..mfisi!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom