Taarifa toka NEC ya CCM - Yaridhia mabadiliko ya Katiba ya CCM

Hii ina faida kadhaa:

Muhimu ni kwamba itapunguza rushwa wakati wa uchaguzi wa NEC ambapo ilikuwa rahisi mno kuwahonga wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa ambao walikuwa wanakusanyika Dodoma Kupigia kura wajumbe 80 wa NEC. Kama tunavyofahamu, Ili mtu uwe na uhakika wa kura nyingi za NEC au Ushinde mchakato wa kugombea urais kupitia CCM, ni lazima ukamate wajumbe kutoka kanda ya Ziwa na Zanzibar, huku ukiokoteza okoteza kwenye mikoa iliyobakia. Kabla ya mabadiliko haya ya katiba ya CCM, ilikuwa rahisi sana zamani kubeba mamilioni yako na kwenda Mwanza ili ukapande treni na wajumbe kutoka mikoa ya Mara, Shinyanga, Kagera na Mwanza, kuelekea nao kwa treni Dodoma. Kazi yako kubwa humo njiani ilikuwa ni kuwanunulia Konyagi na Biskuti za kutosha pamoja na kuwapa posho za kujikimu wakifika Dodoma.

Kwa vile wajumbe kutoka Zanzibar huwa wanaenda Dodoma dakika za mwisho kutokana na ukaribu wa Zanzibar na DSM/Dodoma, chini ya utaratibu wa zamani, ukishamaliza mkakati wako wa kanda ya ziwa, unahamia kwa wajumbe wa Zanzibar ambapo wao pia unaandaa manoti yako na kwenda Zanzibar ili pia ukapande nao boti la kuja DSM, kisha kusafiri nao kwenye mabasi kuelekea Dodoma. Wajumbe waliobakia kutoka mikoa mingine, aidha wapambe wako (wabunge kutoka mikoa husika) wanakufanyia kazi ya kuokoteza wajumbe wa hapa na pale, au shughuli hiyo unaifanya mwenyewe ukifika Dodoma kwa kuwatembelea wajumbe hao kwenye gesti zao na vilabu vya pombe nyakati za usiku na kusambaza bahasha huku ukiwanunulia madumu tosha ya chibuku.

Chini ya utaratibu huu mpya, ina maana haya yote hayatawezekana tena, kwani tofauti na zamani, inabidi aidha ‘to risk' ugombee katika nafasi zile kumi za bara ambazo zina vigogo wa kila aina, pengine hamsini wenye majina mazito an wasio na kashfa, au ukagombee wilayani, lakini huko, chama tayari kimetoa indication kwamba hakitaki wabunge kujirundikia vyeo, hivyo wabunge wengi wa sasa hawatapita uchaguzi wa NEC huko wilayani kwani candidates wengi wilayani watatumia silaha hiyo kuwamaliza wabunge watakao jaribu gombea nafasi za NEC wilayani kwa kusema kwamba wanaenda kinyume na nia nzuri ya CCM kupunguza vyeo vingi kuwa chini ya mtu mmoja n.k. Wabunge wa CCM wana mtihani mgumu sana chini ya utaratibu huu mpya, kwani wengi wao walikuwa wanapata posho nyingi sana kutoka kwa wanasiasa wenye nia ya Urais 2015, kwasababu wabunge wengi walikuwa ni wajumbe wa NEC, na pia by default wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa.

Nadhani pia utaratibu wa kumpata mgombea urais kupitia CCM nao utabadilishwa siku za hapo mbeleni, ili wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa ambao ndio wapiga kura kwa nafasi hiyo, wasilazimike kukusanyika kwenye treni na mabasi kuelekea Dodoma kwa ajili ya shughuli hiyo, kwani kufanya hivyo kutawapa mwanya wagombea wenye pesa nyingi kufanya vitu vyao kwa urahisi. Nadhani wajumbe hawa watabakia katika mikoa yao na CCM itakuja na utaratibu ambapo wagombea Urais watatembezwa na chama katika mikoa yote ili kwenda kujieleza mbele ya wajumbe, mgombea mmoja baada ya mwingine, halafu CCM kutanganza siku maalum ya wajumbe mikoani kote kupigia kura moja tu kuchagua nani wanadhani anafaa kuwa mgombea wa kiti cha Urais.

Inawezekana wanasiasa wenye pesa ndani ya CCM wakafanikiwa ‘to bypass' vizingiti hivi vipya, lakini kwa hili CCM inastahili pongezi kwani ili wanasiasa wa aina hii wafanikiwe, itabidi wajipange kweli kweli, vinginevyo watabainika kwa urahisi sana na kamati mpya ya nidhamu, TAKUKURU n.k.
 
Kwa kuwa rais bado atakuwa m/kiti wa chama na mbunge na waziri lazima awe mbunge pamoja na kutoondolewa kwa nafasi za hovyo hovyo kama za wakuu wa wilaya na makatibu tarafa bado hawajanishawishi kuwaunga mkono.
 
Wakitenganisha mawaziri wactokane na vyama matumizi yatakuwa makubwa na tutaanza tena kulalamika na huo tena utakua ni mwanzao mwingine wa matumizi mabaya ya pesa za umma,,na kwa mfano wa ANC ikumbukwe South A,,,ni nchi yenye nguvu kubwa sana kiuchumi so hata bajet yake inaruhusu...sisi hatuwezi km walimu tu na ma docta imekua timbwili la asha ngedere je huko so ndo watatumaliza kabisa na hii nusu drip ya maji iliyobaki

Matumizi mabaya ya pesa za UMMA kivipi? Zaidi ya haya ya sasa? Ni vyema tukitofautisha katiia budget ya chama cha Siasa na Budget ya Serikali. Hebu fikiria waziri na msafara wake wa kiserikali wanaenda kwenye ziara za chama kwa gharama za walalahoi, NI SAWA. Hivi unadhani yule waziri wa mambo ya ndani alipopigwa mawe Tunduma ilikuwa ni kwa sababu gani? Na sio mawaziri tu hata Rais asiwe mwenyekiti wa chama
 
Kitendo cha CCM kupata katiba mpya ni ishara nzuri kuelekea kwenye Tanzania mpya 2014. Chama kipya, nchi mpya 2015..Nadhani vyama vingine ( hasa cdm, ambacho kwa mujibu wa matokeo ya uzini ndicho chama cha pili kwa ukubwa nchini) na vyenyewe viige mfano huu ili wasiingie kwenye nchi mpya ya Tanzania 2014 na ukiritimba wa mawazo ya mwenyekiti yaheshimiwe. Hongera CCM kwa kuonesha njia.
 
Yaani unataka na cdm wabadilihe katiba ili kumkomoa mtu kama CCM anavyofanya kumkpmoa EL kwa sababu inafahamika kuwa idadi kuba ya wabunge wanamuunga mkono ndio maana katiba imebadilishwa ili wasiweze kuwemo katika NEC mpya itakayotokana na uchaguzi wa CCM wa 2012 ambayo pia ndio itahusika na kupendekeza jina mgombea urais wa ccm 2015.
 
Mkuu RaiaMbishi kwa mtu anayefahamu mitandao ya kusaka madaraka ilivyo ndani ya CCM maelezo yako hayawezi mshawishi kwamba eti imepatikana dawa ya kuzuia rushwa na matendo mengine ya siasa za kihuni. Hii ni kitu imeletwa kujaribu kuzuia watu fulani wasipate madaraka na wala siyo kwa faida ya chama. Lakini yanaweza yakapatikana matokeo tofauti kabisa. Mchimba kisima anaweza akajikuta anatumbukia mwenyewe. Yataletwa mabadiliko mengi,itafika hatua watabadili hata jina la chama, lakini yote hayo hayataiokoa CCM kuondolewa madarakani.
 
Inasema rushwa ni adui wa haki, viongozi wala rushwa wasichaguliwe.

Hiyo ni ya zamani za jk mwalimu, na ili knock injini kwenye ka mwinuko ka kuelekea kwa mzee mwinyi,sasa hivi ndio tuna pambana kui-overhaul. We uko nchi gani wewe?
 
Taarifa kwa vyombo vya habari


Utangulizi:
Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi imefanya kikao chake maalum chini ya mwenyekiti wake wa taifa dr. Jakaya mrisho kikwete tarehe 12.02.2012. Katika kikao hicho halmashauri kuu ya taifa pamoja na mambo mengine imeamua;


Kufanya marekebisho ya katiba ya ccm ya 1977, toleo la 2010 na kanuni zake.


Halmashauri kuu ya taifa imeridhia marekebisho ya katiba ya CCM ya 1977, toleo la 2010 hivyo kubadili namna ambavyo wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM taifa inavyopatikana.


Kwa mujibu wa mabadiliko hayo wajumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya CCM watakuwa katika makundi yafuatayo:-
(a) ngazi ya taifa
wajumbe 10 kutoka tanzania bara
wajumbe 10 kutoka tanzania visiwani
(b) wajumbe 10 wa kuteuliwa na mwenyekiti wa CCM taifa
(c) wajumbe wanaoingia kwa nafasi zao.
(d). Wajumbe wanaotoka kwenye vyombo vya uwakilishi
i. Wanaochaguliwa na bunge 10 (bara 8, zanzibar 2)
ii. Wanaochaguliwa na blw 5 (zanzibar 5)
(e). Wajumbe wanaochaguliwa kutoka wilayani.-221
wajumbe wa halmashauri kuu ya taifa waliochaguliwa kupitia wilaya watakuwa ni viongozi wa kazi za muda wote ili kuweka wazi zaidi wajibu wa wajumbe hao wa kuwa karibu na wanachama na kushughulikia shida zao.
(f). Wajumbe toka kwenye jumuiya za chama
i. Wanaochaguliwa na uwt 15 (bara 9, zanzibar 6)
ii. Wanaochaguliwa na uvccm 10 (bara 6, zanzibar 4)
iii.wanaotokana na wazazi 5 (bara 3, zanzibar 2)


Aidha halmashauri kuu ya taifa imeamua kuwa viongozi wakuu wastaafu ngazi ya taifa waundiwe baraza la ushauri.
Baraza hilo litakuwa na wajumbe wafuatao:-
• marais wastaafu wa jamhuri ya muungano wa tanzania ambao walikuwa wenyeviti wa ccm taifa.
• marais wastaafu wa zanzibar ambao pia walikuwa makamu wenyeviti wa ccm taifa.
• makamu wa mwenyekiti wa ccm taifa wastaafu.


Baraza litakuwa na kazi ya kutoa ushauri kwa chama cha mapinduzi na serikali zinazoongozwa na ccm, kwa madhumuni hayo hayo katika jambo mahsusi. Wajumbe wa baraza hilo wanaweza pia kualikwa ama wote au mwakilishi wao kuhudhuria vikao vya chama ngazi ya taifa.
OTIS




 
Kumekucha. Yani mtu ashike nafasi ya juu ya dola kupitia chama lakini akimaliza uraisi uongozi wa chamani unakoma?
 
Back
Top Bottom