Taarifa Muhimu - Tafadhali Soma Hapa

hapa hakuna cha kukwazika. Ni uamuzi mzuri sana nami nauunga mkono asilimia mia moja
 
Ni uamuzi mzuri ambao labda utarudisha hadhi ya Jamii Forums iliyoanza kupotea na ambao utawavuta tena wakongwe wengi walioingia mitini.
 
Mods, mnaonaje mkianzisha kijukwaa cha ku-rant? Sehemu ambayo mtu anaweza kusema chochote hata bila ya kuanzisha thread?
 
Niko negatv kidooogo mkuu wangu ,nahisi hii itapunguza uhuru wa mchangiaji na kutokuwa tena sehemu ya new ideal ,kwanza ni criteria gani zinatumika kuijaji post kuwa ni upuuz inabidi mzidefine na ziwe specific,pili ukisha edit post ya mchangiaji nadhani ipost kwa jina lako kwa maana inakuwa yako si yake ni ya editor. USHAURI: Iwapo mtaset hizo criteria sasa then ikionekana haifai isipostiwe kabisa sio kuituma ukiiedit hiyo ni kuingilia right to identity ni crime
 
Niko negatv kidooogo mkuu wangu
Uko sawa mkuu ila uhuru bila moderation ni tohu wa bohu manake ni chaos tupu! Utashangaa hata mambo ya wakubwa yanaletwa hapa hata mada nyingine zisizoendana na Ugreat thinker bado zinaletwa hapa. I support!
 
Umefanya vyema ila pia wale wasiochangia k2 wanaingia kwa mada kisha et napita tu.
 
Niko negatv kidooogo mkuu wangu ,nahisi hii itapunguza uhuru wa mchangiaji na kutokuwa tena sehemu ya new ideal ,kwanza ni criteria gani zinatumika kuijaji post kuwa ni upuuz inabidi mzidefine na ziwe specific,pili ukisha edit post ya mchangiaji nadhani ipost kwa jina lako kwa maana inakuwa yako si yake ni ya editor. USHAURI: Iwapo mtaset hizo criteria sasa then ikionekana haifai isipostiwe kabisa sio kuituma ukiiedit hiyo ni kuingilia right to identity ni crime
Mkuu, MMU ina mambo mengi ikiwa ni pamoja na chit chat, majibu ya mzaha na raha ili mradi watu wana relax. Ina topic muhimu sana na za mchanganyiko.

Inapotokea mtu katuma thread ' Nisaidieni' halafu maudhui yake ' huwa nikifika kileleni nasikia raha sana'. Khaa! Ina maana gani kama si upuuzi.

Nanyi MMU ndio mnaendekeza low quality topic kwa kuchangia au kujibizana na mwanzisha thread zisizo na tija. Mkiuchuna atajionea haya kama si soni.

Naunga mkono hoja
 
Kutokana na hali ambayo imekuwa ikiendelea humu kwenye Jukwaa la MMU kwa muda mrefu napenda kuwafahamisha members wote kuwa kuanzia sasa thread zote ambazo zitakuwa posted hapa MMU zitakuwa under MODERATION kabla hazijawa approved tumeamua kufanya hivi kwa sababu kumekuwa na mlolongo wa TOPIC zisizokuwa na maana yoyote au TOPIC ambazo kimsingi hazina mantiki yoyote ndani ya Jukwaa hili.

Halikuwa lengo letu kufanya hivi ila kwasababu hali hii imeendelea kwa muda mrefu bila watu kujirekebisha hivyo basi tumeona itakuwa ni busara tukaliweka Jukwaa hili under MODERATION kama tulivyofanya kwenye Jukwaa la Siasa, topic ambazo tunaona zinafaa kukaa hapa zitawekwa hapa na ambazo tutaona hapa sio mahala pake zitahamishwa na kupelekwa Jukwaa husika. Lengo hasa ni kufanya maboresho kwenye Jukwaa hili na kuiweka JF katika hatua nyingine tofauti na sasa hivyo tunaomba sana ushirikiano wenu.

Poleni kwa usumbufu, na wale ambao watakwazika tunawataka radhi.


Uwamuzi mzuri, watu wajipange kabla ya kuleta topic wakati mwingine zinakuwa marudio na za kukosa busara kabisa kama mlevi fulani wa gongo.
 
Back
Top Bottom