Taarifa kwa Vyombo vya habari kutoka IKULU juu ya Katiba Mpya

Katiba hii inakithi viwango kabisa. Sema watu huwa hawaridhiki tu. Lakini katika hali halisi katiba tuipigieni kura ya ndiyo
 
shekinahpres naomba ibara zinazokufanya useme katiba ni mzur ipigiwe kura ya ndio… alafu ifananishe na ile ya tume na hiyo ya bmk...
 
Last edited by a moderator:
HISTORIA YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA
1. CCM hawakuwa na agenda ya Katiba mpya kwny Ilani yao.
2. Jk akaibuka na hiyo agenda mwenyewe ili aache cha kukumbukwa.
3. CCM wakachagua wajumbe wa BMK wenyewe
4. CCM wakajadil rasim wenyewe;
5. Wamepga kura wenyewe;
6.Wamesmamia kura wenyewe;
7. Wamehesab wenyewe;
8. Matokeo Wametangaza wenyewe;
9. Wameshinda wenyewe;
10. Wanashangilia wenyewe; na
11. Wamegeuza Bunge ukumb wa dans wenyewe!
12.Wamecheza dans maana katiba walotunga imewahakikshia kuendelea kuiba, kufisad ,kuwanyonya wanyonge, kuwadhulum Watanzania.!
Sema HAPANA kwa Katiba ya CCM! Tuma kwa watu wengi wajue kuikataa rasimu ya ccm!!
 
Ningekuwa nilitumia kura yangu kumchagua huyu jamaa ningehama nchi, sijawahi kuona raisi dhaifu kama huyu. Nadhani anatetea ulaji wa kuendelea kuchagua hawara zake kuwa mawaziri bila kuzuiwa na bunge. Pia anatetea kutoshtakiwa kwa wizi alioufanya kupitia kwa mwanae Riziwani. Katiba ya wananchi ilitaka raisi ashtakiwe na pia akifanya uteuzi lazima bunge lithibitishe na kuidhinisha kwanza. Anatetea kutokwenda jela au The Hague, ngoja ije huku tuwakomeshe.

Huna akili
 
Km raisi anawza kuongea ivo wakat kina mamilion ya watanzania wenye akili timam na wengine ni wasomi wanaojua kipi knafaa na kipi hakifai, basi didhan km ni mtu aliyestahili kua katka hyo nafasi. Katba kutaja makundi yote ya wananchi sio hoja ya msingi wala sio sababu ya kuwafanya watanzania wanaojielewa wardhke. Mbona marekani ni muungano wa nchi zaid ya 50 na wana serikali moja tu...na pia ni taifa lenye katba fubi zaid daunian, wana katba ina sura 6 tu..
Lakn mbna hatuskii wasanii wala aknamama au wakilima wakilalamika?? Inamaana hyo katiba imetaja makund yote ya wananch wa marekani?? Suala la msingi ambalo watanzania wanaojielewa wanalilalamikia ni suala la muundo wa serikali na jinsi wabunge wanavojipa uhuru zaidi. Hayo ndio mambo ya msingi ambayo yanajenga. Sasa mkikaa mnajadili mambo ya wanawake bungeni kua 50 kwa 50 na wanaume, wakat hata wanawke wenyew hawaamin km wanaweza kumudu hzo nafasi, km sio ushabik hao waliopendekeza katba wanafuta ni nn hasa??!! Watanzania tuamke.
 
Km raisi anawza kuongea ivo wakat kina mamilion ya watanzania wenye akili timam na wengine ni wasomi wanaojua kipi knafaa na kipi hakifai, basi didhan km ni mtu aliyestahili kua katka hyo nafasi. Katba kutaja makundi yote ya wananchi sio hoja ya msingi wala sio sababu ya kuwafanya watanzania wanaojielewa wardhke. Mbona marekani ni muungano wa nchi zaid ya 50 na wana serikali moja tu...na pia ni taifa lenye katba fubi zaid daunian, wana katba ina sura 6 tu..
Lakn mbna hatuskii wasanii wala aknamama au wakilima wakilalamika?? Inamaana hyo katiba imetaja makund yote ya wananch wa marekani?? Suala la msingi ambalo watanzania wanaojielewa wanalilalamikia ni suala la muundo wa serikali na jinsi wabunge wanavojipa uhuru zaidi. Hayo ndio mambo ya msingi ambayo yanajenga. Sasa mkikaa mnajadili mambo ya wanawake bungeni kua 50 kwa 50 na wanaume, wakat hata wanawke wenyew hawaamin km wanaweza kumudu hzo nafasi, km sio ushabik hao waliopendekeza katba wanafuta ni nn hasa??!! Watanzania tuamke.
Hiyo rasimu kwa upande wa pili ni ilani ya uchaguzi next yr
 
Katiba tuliyonayo sasa imejaa haki za binadamu lakini tunashuhudia watu hawazipati. Kutamka makundi katika katiba hakuifanyi I we bora ikiwa tu hakuna uhakikisho wa kupata haki makundi husika. Kuna vifungu tayari katika katiba vinazuia kudai haki Hizo za makundi! Je uzuri wake ni up?

Mkuu hilo neno. Inasema kila mtu ana haki ya kukusanyika lakini policcm wanazuia sasa sijui hiyo ijao ndio watatimiza kweli.
 
Jamani hii post ni feki imelenga kuichafua ikulu. Hata mtoto wa kindergarten hawezi kuandika hovyo hivi
 
Kwahiyo mnatulazimisha tupo tayari kwa lolote kuidai katiba mpya ilito tukana na maoni yetu sisi wananchi sio ya sitta na chenge
 
THEUNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATEOF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

TAARIFAKWA VYOMBO VYA HABARI

KamaKatiba Inayopendekezwa ni mbaya, hiyo nzuri ikoje?
auliza Rais Kikwete


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikweteamewashangaa watu wanaodai kuwa Katiba Inayopendekezwa ni mbaya,akiuliza kuwa kama Katiba hiyo ni mbaya basi hiyo nzuri ikoje?

Aidha,Rais Kikwete amesema kuwa Katiba inayojali makundi yote ndani yajamii, kama ilivyo Katiba Inayopendekezwa, kamwe haiwezi kuwa Katibambaya.

Rais Kikwete ameyasema hayo nyakati tofauti leo, Ijumaa, Oktoba 10, 2014,wakati alipozungumza na wananchi katika maeneo mbali mbali ya Mkoa waMwanza, ambako anafanya ziara ya siku tatu ya kikazi kukagua nakuzindua miradi ya maendeleo.

Akizungumza na mamia kwa mamia ya wananchi mjini Kisesa ambako ameweka jiwe lamsingi la ujenzi kwa kiwango cha lami na Barabara ya Usagara-Kisesa,Rais Kikwete amewataka wananchi kuwapuuza watu wachache wanaodai kuwaKatiba Inayopendekezwa ni mbaya na badala yake wajiandae kuipigiakura ya kuikubali wakati ukiwadia.

“Sijui katiba nyingine duniani ambayo inajadili makundi yote ndani ya jamiikama hii Katiba Inayopendekezwa. Hakuna aliyeachwa – wavuvi wamo,wajane wamo, wafanyabiashara ndogo ndogo wamo, akinamama lishe wamo,wakulima wamo, wafugaji wamo….kila mtu yumo. Akinamama ndio usisemekabisa wao wamepata hata asimilia 50 kwa 50 ndani ya Bunge.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Hivi katiba mbaya inakuwa kama inayopendekezwa nakama hii inayopendekezwa ni mbaya sasa hivi nzuri ikoje?

Rais Kikwete amewambia wananchi: “Watakuja watu kuwashawishi kuwa KatibaInayopendekezwa ni mbaya, wasikilizeni lakini tumieni akili yetu,kama ile hadithi ya mbayuwayu. Jiandaeni tu kupiga kura na kuungamkono Katiba Inayopendekezwa kwa sababu hii ni Katiba nzuri sana.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

10 Oktoba, 2014
Tusijadili katiba. Tujadili kwanza huu uandishi. Ni kweli ni wa ikulu?
 
Nasubiri ikulu ikanushe hii taarifa na kama ni wao wameandika basi hiki kitengo kinadhalilisha ikulu ya Tanzania. Huu ni upuuzi kutoka ikulu ya kikwete.
Why waandike namna hii?
TThese people,wanaweza kukanusha hata kama waliandika wao
 
Back
Top Bottom