Taarifa kwa Umma: VIPAUMBELE VYA KAMBI YA UPINZANI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013

n00b

JF-Expert Member
Apr 10, 2008
1,006
2,667
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: VIPAUMBELE VYA KAMBI YA UPINZANI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013




By Zitto Kabwe

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
06.06.2012
YAH: VIPAUMBELE VYA KAMBI YA UPINZANI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013


Ndg. Waandishi wa Habari

Mwaka 2011/2012 Kambi ya Upinzani Bungeni ilitangaza Vipaumbele vyake katika Bajeti Mbadala ambavyo vilikuwa:

1. Kupunguza misamaha ya kodi mpaka 1% ya pato la Taifa kutoka 3%

2. Kupunguza kodi kwenye bidhaa za mafuta ya petrol na dizeli ili kupunguza mfumuko wa bei

3. Kufuta mfumo wa posho za vikao (Sitting allowances).

4. Kupeleka sehemu ya tozo ya ujuzi (Skills Development levy-SDL) kwenye bodi ya mikopo ya elimu ya juu.

Masuala haya pamoja na mengine yalikuwa sehemu ya Bajeti kivuli iliyowasilishwa Bungeni na Kambi ya Upinzani.

Mapendekezo mawili,

(1) Kodi za mafuta ya Petrol na Diseli na
(2) Tozo ya SDL yalikubaliwa na kutekelezwa. Pendekezo la misamaha ya kodi lilikubaliwa lakini Serikali imeshindwa kulitekeleza na pendekezo la kufutilia mbali posho za vikao halikukubaliwa.

Kambi Rasmi ya Upinzani inataka maelezo ya kina ya kwa nini Serikali imeshindwa kutekeleza ahadi yake iliyoitoa Bungeni kwamba misamaha ya kodi itapungizwa mpaka kufikia 1% ya pato la Taifa. Halikadhalika Kambi ya Upinzani inarejea wito wake wa kufutwa kwa Mfumo wa posho za vikao (sitting allowances).
Serikali imependekeza Bajeti ya Tshs. 15trillioni kutoka Tshs. 13 trillion. Hata hivyo ni dhahiri kwamba Bajeti ya 2011/12 ilikuwa ina changamoto kubwa za utekelezaji. Serikali ieleze itawezaje kutekeleza Bajeti ya 15trillioni?
Katika Bajeti Mbadala ya 2012/2013 Kambi ya Upinzani itajikita katika maeneo yafuatayo na kuishinikiza Serikali kuyatekeleza.

1. Kuendelea kushinikiza kupunguzwa kwa misamaha ya kodi mpaka 1% ya Pato la Taifa. Hivi sasa misamaha ya kodi ni sawa na misaada yote kutoka nchi wahisani, Tshs 1.03 trillioni ni sawa na 3% ya Pato la Taifa.

2. Kuelekeza raslimali fedha kwenye maendeleo vijijini hasa kujenga miundombinu kama barabara za vijijini na umeme vijijini.

3. Kuelekeza fedha za kutosha kukarabati Reli ya Kati na kufufua njia za Reli za Tanga, Moshi na Arusha.

4. Kuongeza wigo wa kutoza tozo la ujuzi (Skills Development Levy) ambapo sasa waajiri wote walipe ikiwemo Serikali na mashirika ya umma. Pia kupunguza tozo hili mpaka 4% ambapo 1/3 itaenda VETA na vyuo vya Ufundi na 2/3 itaenda Bodi ya Mikopo ili kukabili changamoto ya mikopo kwa wanafunzi.

5. Kushusha kima cha chini cha kodi ya mapato (PAYE) mpaka 9% ili kuwezesha wananchi wa hali ya chini kubaki na fedha za kutumia na kukuza uchumi.

6. Kuongeza mapato ya ndani na kupunguza mikopo ya kibiashara kwa kuhakikisha mapato ya ndani yanafikia 20% ya pato la taifa, kuongeza nguvu za kisheria na udhibiti ili TRA ikusanye mapato zaidi kwenye kampuni za simu na kwenye shughuli za uchimbaji wa madini, mafuta na gesi.

7. Kutayarisha Taifa kuwa na uchumi wa Gesi.

8. Kupunguza /kufuta kodi kwenye bidhaaa za vyakula kwa muda maalum ili kushusha mfumuko wa bei.

9. Kuweka mfumo mpya wa elimu kwa kushirikisha sekta binafsi katika kutoa elimu kwa ubora zaidi, ikiwemo kuundwa kwa chombo cha Udhibiti wa Elimu(Regulatory authority)

10. Kutoa vipaumbele na unafuu vya kikodi kwa viwanda vya ndani vinavyotumia malighafi za nchni hasa za kilimo na zenye kuongeza ajira kama Korosho,Pamba na Mkonge.

Kambi ya Upinzani itaendelea kufuatilia kwa karibu sana suala la kukua kwa deni la Taifa amabalo limefikia hadi Tshs 22 trillioni na kutaka ukaguzi maalum kuhusu akaunti ya Deni la Taifa.

Kambi ya Upinzani itawekeza kusimamia kwa karibu suala la matumizi yasiyo na tija ya Serikali hasa kwenye magari na posho mbalimbali na Kwamba fedha nyingi zitumike kwa miradi mikubwa ya maendeleo ili kukuza ajira. Halikadhalika namna ya kupta fedha za kutekeleza mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano


Asanteni sana!


…………………………….
Zuberi Kabwe Zitto(Mb)

Waziri Kivuli-Fedha na Uchumi.
 
Heko Zitto, bajeti ya serikali imetupilia mbali elimu ya juu. Kama ukishindwa kuweka sekta ya elimu kuwa kipaumbele manake nini? Unatengeneza jamii ya mabumbumbu?. Kwa mfano mwaka 2012/13 serikali ni kama imeondoa udhamini wa wanafunzi elimu ya juu.
 
Mh. Zitto hongera kwa vipaumbele vinavyolenga kutukomboa kutoka katika hali hii ngumu ya maisha. Hata hivyo nina maswali machache:

  1. Nasikia Mtwara kulikuwa na reli je, kwanini bajeti yenu haikuigusa hiyo reli
  2. Kushinikiza kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma sio kipaumbele chenu? Hamuoni umuhimu wa hili?
  3. (Wadau) naombeni elimu kidogo ya kitu hiki tozo za development skills. Pia ni kwanini wakatwe watumishi wa serikali na mashirika ya umma tu?


Vinginevyo vimesimama imara kwa maoni yangu
 
Katika nchi yeyote inayopata maendeleo ya kweli ni kuwekeza ktk elimu serikali ya CCM mawazo yao ni mafinyo wamepunguza kipaumbele cha elimu hiyo inaonesha kuwa sasa elimu ya juu itabaki kuwa ya watu walio nacho kakini kwa mtoto wa mkulima hatanufaika na elimu ya juu kwa kuondoa mikopo kwa baadhi shahada, na serikali yetu inaonesha kufurahia matokeo yanayopatikana ya kidato cha IV mungu ibariki serikali ya CCM ili wapate mawazo mazuri ya kufikili.
 
Zitto atoa taarifa kwenye vyombo vya habari [url="www.zittokabwe.wordpress.com/2012/06/06/taarifa-kwa-vyombo-vya-habari-yah-vipaumbele-vya-kamba-ya-upinzani-kwa-mwaka-wa-fedha-20122013/]"Bonyeza Hapa [/url]
 
Mh. Zitto hongera kwa vipaumbele vinavyolenga kutukomboa kutoka katika hali hii ngumu ya maisha. Hata hivyo nina maswali machache:

  1. Nasikia Mtwara kulikuwa na reli je, kwanini bajeti yenu haikuigusa hiyo reli
  2. Kushinikiza kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma sio kipaumbele chenu? Hamuoni umuhimu wa hili?
  3. (Wadau) naombeni elimu kidogo ya kitu hiki tozo za development skills. Pia ni kwanini wakatwe watumishi wa serikali na mashirika ya umma tu?


Vinginevyo vimesimama imara kwa maoni yangu

Kwenye red naona umeelewa kinyume chake rudia kusoma vizuri.

Tatizo la TZ kwa sasa ni matumizi ya serikali ni makubwa ukilinganisha na mapato. Bajeti inatakiwa ilenge kuimarisha uchumi kwa maana ya mapato kuliko matumizi(mshahara kwa wafanyakazi haiwezi kuwa kipa umbele kwa bajeti ya aina hii)
 
Hapo kwenye kodi hadi 9% ni pazuri ila wafanyakazi tusahau serikali yetu iko radhi ipandishe hadi 40% kwa wafanyakazi na kumpunguzia mwekezaji kwa 1%
 
Kwenye red naona umeelewa kinyume chake rudia kusoma vizuri.

Tatizo la TZ kwa sasa ni matumizi ya serikali ni makubwa ukilinganisha na mapato. Bajeti inatakiwa ilenge kuimarisha uchumi kwa maana ya mapato kuliko matumizi(mshahara kwa wafanyakazi haiwezi kuwa kipa umbele kwa bajeti ya aina hii)

Nimekupata mkuu kweli sikuwa makini hapo. Ahsante.
 
Mh. Zitto hongera kwa vipaumbele vinavyolenga kutukomboa kutoka katika hali hii ngumu ya maisha. Hata hivyo nina maswali machache:

  1. Nasikia Mtwara kulikuwa na reli je, kwanini bajeti yenu haikuigusa hiyo reli
  2. Kushinikiza kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma sio kipaumbele chenu? Hamuoni umuhimu wa hili?
  3. (Wadau) naombeni elimu kidogo ya kitu hiki tozo za development skills. Pia ni kwanini wakatwe watumishi wa serikali na mashirika ya umma tu?


Vinginevyo vimesimama imara kwa maoni yangu

Skills and Dev Levy hulipwa na mwajiri na sio mfanyakazi kama ulivyoelewa, na kwa sasa wanalipa private sector tu. mantiki ya sasa ni kuwa kodi hii inasimama kama compensation kwa serikali kutokana na nguvukazi (rasilimali watu) ambayo imeelimishwa na serikali na sasa inatumiwa na private sector
Hii inakokotolewa kutoka kwenye total gross salary ambayo mwajiri analipa wafanyakazi wake na mfanyakazi halipi chochote kwenye hii.
Hoja ya upinzani ni kuwa sasa mashirika ya umma na taasisi za serikali walipe kwa kuwa nao wanatumia nguvu kazi hiyo, lakini pia itasaidia kuongeza wigo wa walipa kodi ya aina hii ambao sasa ni wachache (private sector only) na kiwango wanacholipa ni kikubwa, kipunguzwe
 
kima cha chini, hakijazunumziwa lakini nadhani lazima kiangaliwe upya. na kwa mawazo yangu, ili kupata kima cha chini, wenye salary ya 1,500,000/ kama basiki, waipandishiwe mshahara wao, bali pesa itakayopatikana utumike kupandisha mishara ya hawa watumishi wanaolipwa 80,000/- mishahara ya serikali hadi wale wanaolipwa chini ya 1,500,000/-
 
Vipaumbele vya sasa viko sawa,
1. Ila bado nasisitiza kodi kwenye mafuta(Diesel,Petrol na Mafuta ya Taa) waendelee kupigania ipunguzwe, maana sijaona nafuu ya huu uwagiziaji wa mafuta kwa pamoja imetusaidia nini sisi wananchi kwasababu hata dola imestabilize for a while now(Na kiwango cha ushujaji wa bei za mafuta kila mwezi na EWURA sasa hivi ni mdogo).

2. Na kwa upande wa kuamsha hizo reli zilizokuwa zimetelekezwa,nadhani hilo ile first priority kwa wizara ya uchukuzi,maana hata cost za usafirishaji wa bidhaa kwa kutumia reli zidakuwa chini na zitamnufaisha mwananchi kwa kweli.Na ziwekewe ulinzi wa kutosha kuepusha hujuma za kung'oa mataruma.
 
Believe me Serikali ya CCM ikikubali kufuta SITTING ALLOWANCE zote katika mfumo wake itaokoa pesa nyingi na kupunguza matumizi ya serikali.

Zitto vipi kuhusu UNUNUZI wa MASHANGINGI kwa viongozi wa serikali. Hili nalo ni eneo ambalo serikali ingeweza kupunguza matumizi yake kwa kiwango kikubwa. Mbona wenzetu Kenya tena wenye uchumi mzuri kuliko sisi wameweza?!.

Lakini haya yote ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu. The government of JK/CCM is ADDICTED IN SPENDING hakuna hata atakaye kusikiliza when it comes to serikali kubana matumizi.
 
yeah ni kweli kuna haja ya kufufua njia ya reli ya tanga,moshi mpaka arusha pamoja na kukarabati reli ya kati itasaidia sana barabara zetu ziweze kudumu,na kuboresha uchumi wetu kwa kasi.
 
Nafikiri pia PAYE inatakiwa kuangaliwa upya maana ndio inamaliza mishahara ya wafanyakazi, ni kubwa mno hii kitu
 
Jamani hapa nimekamatwa sana na pendekezo la kufufua reli ya kaskazini. We shall fight for it. Maendeleo huja kwa kuwa na miundombinu bora.
 
Skills and Dev Levy hulipwa na mwajiri na sio mfanyakazi kama ulivyoelewa, na kwa sasa wanalipa private sector tu. mantiki ya sasa ni kuwa kodi hii inasimama kama compensation kwa serikali kutokana na nguvukazi (rasilimali watu) ambayo imeelimishwa na serikali na sasa inatumiwa na private sector
Hii inakokotolewa kutoka kwenye total gross salary ambayo mwajiri analipa wafanyakazi wake na mfanyakazi halipi chochote kwenye hii.
Hoja ya upinzani ni kuwa sasa mashirika ya umma na taasisi za serikali walipe kwa kuwa nao wanatumia nguvu kazi hiyo, lakini pia itasaidia kuongeza wigo wa walipa kodi ya aina hii ambao sasa ni wachache (private sector only) na kiwango wanacholipa ni kikubwa, kipunguzwe

Ahsante mkuu ndio raha ya JF kuelimishana. Sikuwa na uelewa na iko kitu. Sasa tupo pamoja
 
Zitto naomba ufafanuzi budget ya 2011/2012 serikali ilipanga kutumia 13 tirillion. Lakini wote ni mashuhuda miradi mingi ya maendeleo imekwama kutokana na serikali kutokuwa na pesa. Je ktk budget ya 2011/2012 serikali iliweza kukusanya/ku-raise pesa kiasi gani? Je kulikuwa na deficit ya SH ngapi katika sh 13 trillion? Kama 2011/2012 tulishindwa ku raise 13 trillion. Je ni miujiza gani ambayo serikali imepata ya kuweza kukusanya/ku-raise 15 trillion ktk budget ya 2012/2013? Mimi sioni mantiki ya kupanga budget ya 15 trillion wakati tulishindwa kupata 13 trillion kwenye budget iliyopita.
 
Mimi naomba mambo makuu 2 tu muangalie kwa makini jamani

1. Miundombinu, Reli ya kati, TAZARA , barabara , bandari (DSM, Mtwara na Tanga)
Napendekeza serikali itoe incentives kwa watu watakaoshusha mizigo Tanga na Mtwara wapate unafuu mkubwa ili purukushani zipungue DSM mwisho wake tuwe na bandari 3 zinazofanyakazi sawa sawa.

Reli ya Kati atafutwe mwekezaji mwenye uwezo mkubwa apewe, na hii TAZARA iangaliwe mapema kabla haijafikia kama ile ya kati. Barabara za kuunganisha mikoa ya kusini zimaliziwe.

2. Kilimo ( training kwa wakulima wadogo, pembejeo, mbolea,maeneo,nk)

Ninahakika angalau tuki accomplish haya mawili 2012/2013 basi ifikapo 2015 nchi itakuwa na unafuu angalau na hata mfumuko wa bei utapungua.
 
ZITTO INGEPENDEZA PIA KAMA UNGEELEZA KWA KIFUPI UCHAMBUZI WA MAFANIKIO AU KUSHINDWA KWA BUDGET YA CCM 2011/2012 Maana hii wao waliishabikia mno kama mkombozi wao ili na sisi tuweze kutoa maoni
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom