Taarifa kwa umma toka kwa Lema (MB), apinga jeshi la polisi kutumiwa kisiasa

Nafarijika nikiwa Muasisi wa Chadema na Mwenyekiti Taifa wa kwanza, (mstaafu) kwamba Mhe. Godbless Lema ameonyesha ujasiri thabiti katika kupinga uonevu wa wanyonge na ukandamizaji wa demokrasia unaoonekana kuidhinishwa na Serikali ya nchi yetu. Mhe. Lema ameonyesha uzalendo uliotoka moyoni na kujitolea kwake kutumikia umma. Mungu atambariki na kumlinda.

Tamko lake kwa waandishi wa habari lime-cover kikamilifu misimamo ya CHADEMA kama ninavyoielewa na kuiamini, na nina hakika Kamati Kuu ya Chama itaridhia.

Hata hivyo, nionavyo mimi binafsi, Tanzania tunaelekea njia inayohatarisha amani na uhuru wa watu wetu; hasa pale Polisi wanapojiingiza kutekeleza maagizo ya chama tawala na kupindisha sheria na taratibu tulizojiwekea na zinazohakikisha kwamba Mahakama zinakuwa na uhuru kamili kuamua kesi zilizo mbele yao.

Kwa maoni yangu, vituko vya Arusha kuhusu Chadema na maagizo kwa Polisi yanayoashiria kwamba yana baraka za Serikali, yanastahili kujadiliwa na viongozi tuliwachagua, na tamko kutolewa kuhusu uhuru wa wanachama kuandamana na kukutana. 'ROLE' ya Polisi katika shughuli za vyama vya siasa ni lazima ifafanuliwe kama uongozi unadhamiria kwa dhati kudumisha amani.
Nimefarijika sana kwa maelezo yako yakumtia moyo kijana jasiri ,mwenyekudhubutu na mpambanaji LEMA.

Ni mfano wa vijana wachache ambao wana udhubutu wa namna ya Lema. Ikiwa vijana tukasimama tukapinga kwa nguvu udhalimu huu unaendelea kukuwa siku hadi siku wa ukandamizaji unaofanywa na polisi naamini tutashinda lakini muhimu zaidi tutakuwa tumetimiza wajibu wetu kama vijana wazalendo.

Big up Lema, Viva CDM.
 
haya sasa na hii serikali na viongizi wao ila chadema arusha imejikamilisha sana
 
Lema analilia kama mtoto wa chekechea maneno mengi..

Tanzania kuna wabunge zaidi ya 300 kila mmoja awe anatoa taarifa kwa umma si itawa nchi ya maigizo
 
Sasa wewe Lema unalilia kama mtoto wa chekechea unataka polisi wakuachie ufanye fujo tu..

Nchi yetu ni ya amani kama unataka kuleta fujo lazima polisi wafanye kazi yao..

Hongera sana kamanda wa polisi Arusha kwa kuleta amani
 
Kwa kweli nimejiandaa hata kupokea mauti* japo najua Mungu anapenda niishi muda mrefu ili kutimiza kusudi lake ,* sitarudi nyuma *katika harakati hizi* za kupinga uonevu , dhuluma na ukandamizaji wa haki za binadamu nasubiri kwa hamu sana kuona mikakati yote iliyopangwa kinyume nami na wafuasi wote wanaopinga uonevu. Hata hivyo Nimeiandaa* familia yangu *kuwa tiyari wakati wowote kwa jambo lolote na kwa taarifa yoyote dhidi ya ukweli tunaoupigania.

Mimi natambua kuwa faida ya kuishi* sio kuishi vizuri tu wewe na familia yako bali ni wewe kuwa sehemu ya mabadilikio ya watu wanaokuzunguka , katika kupigani UTU , HAKI ,* ustawi mzuri wa Jamii. Na kila mtu anayemuogopa Mwenyezi* Mungu ataishi kufanya hivyo kama* Mahatma Gadhi alivyopata kusema* "The best way to find yourself is to loose yourself in the service of others"*
Mara nyingii sana sipendi kutembelea jukwaa la siasa kwa sababu kila nipitapo kwenye jukwaa ili utoka nikiwa na msononeko wa moyo au jazba.....

Kwenye red mh. Lema amezungumza maneno ambayo ni viongozi wachache sana wanaweza kuzungumza maneno haya(Kwa bahati mbaya sana Tanzania tuna Watawala ). Lema yupo tayari kufa kwaajili ya kutetea haki ya wapiga kura wake je wapigakura wake wapo tayari kufa kwa kutetea haki zao?

Watanzania ni wanafiki sana, leo hii Lema anajitoa kutetea haki za wapiga kura wake na hata ikilazimu uhai wake kumtoka, wengi wetu hapa tutamsifu kwa ujasiri wake n'k ...

Hivi umnajua ni kwa nini watetea haki/wanamapinduzi ujakuishia kurubunika kirahisi na kutumbukia kwenye vile vitu walivyo kuwa wanavipinga na mwishoe kuwaita wasaliti?

Ni kwa sababu ya unafiki wetu watanzania leo mtu anajitoa kwa kila kitu kwetu kututetea sisi, na sisi tuna muachia kazi hii pasipo kushirikiana nae bega kwa bega badala yake wengi wetu tupo kwenye keyboard zetu tukimpa matumaini ya maandishi tu mwisho wasiku nae atachoka maana anaowatumikia hawana nia ya dhati ya kijikomboa...........

 
Lema analilia kama mtoto wa chekechea maneno mengi..

Tanzania kuna wabunge zaidi ya 300 kila mmoja awe anatoa taarifa kwa umma si itawa nchi ya maigizo

kwa lugha ya Chadema wanaita Matamko, so Lema ametoa tamko.
 
Sasa wewe Lema unalilia kama mtoto wa chekechea unataka polisi wakuachie ufanye fujo tu..

Nchi yetu ni ya amani kama unataka kuleta fujo lazima polisi wafanye kazi yao..

Hongera sana kamanda wa polisi Arusha kwa kuleta amani
Hili ndilo tatizo wanamagamba wengi, hawaumizi kichwa kukifikirisha, matokeo yake ndo haya
 
Wananchi wa Arusha kweli hawana akili, badala ya kufanya kazi mnaandamana hovyo mahakamani. Huyu jamaa siasa zake ni za sifa, hana lolote.

Mzee mpenda Amani.
Nilichogundua Arusha, vijana wengi hawana kazi nilikuwa huko wiki mbili zilizopita nimeona..

Wengi wao wanashinda kwenye vijiwe maeneo tofauti Unga Limited, standi ya vifodi, Sakina na kwenye vilabu vya mbege na komoni.

Wewe unadhani huo muda wanapoteza mahakamani wangeuelekeza kwenye ujenzi wa taifa viwandani au kwenye kilimo kwanza, au sekta binafsi wangekuwa mbali sana
 
Watanzania kama tutaendelea kuwa WAPUMBAVU kiasi hiki kwa kushabikia mtu au watu wakiitwa panya wakati ni watu,hapo tunatengeneza bomu litakalolipuka siku zijazo, na ni ujinga na upuuzi wa hatari kushabikia eti mbunge wa vurugu hivi wewe unaeshabikia eti polisi watammaliza na amini hazikutoshi.

Ila kama hujafanya tathimini nakuambieni hivi nchi hii inaenda kuingia katika machafuko ya hali ya juu,usidhani ukandamizaji huu unaofanywa na polisi na serikali kwa ujumla watu wote wanaushangilia kama baadhi yetu tulo laaniwa na vijipesa vya kuomba omba toka kwa mafisadi walioko ndani ya CCM.

Amini amini nawaambieni watanzania kuna kundi la watu ambao hawakubaliani hata kidogo na uonevu unaofanywa na jeshi la poslisi hasa wenye alkili na utashi kama wa OCD wa AR.uonevu huu upo tangu muda mrefu ambao umekuwa ukitekelezwa kwa namna nyingi tiofauti ikiwepo kuwabambikia raia kesi za ajabu ajabu.

Nawaambia hivi mimi ni mmoja wa watu ninaopinga vikali uonevu anaofanyiwa Mh Lema na wananchi wa arusha hasa waliompigia kura.najua haya ni maagizo ya CCM.Endeleeni kwa bidii na uonevu huo ila mkae mkijua wengine hatuna cha kupoteza,tuko tayari kufia haki na kupinga uonevu wa aina yoyote kwa wanyonge.

Hivi hamjiulizi ni kwa nini kuna wanadamu wanajiua,kuna wanadamu wanajilipua kwa mabomu? Jamani tujiangalie,ni kweli mnyinge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 
Pamoja mkuu! Wewe ni jemedari wetu. Mkuu nakuambia usiogope kitu kabisa siku ya ukombozi ipo karibu kufika na siku hiyo ikifika sijui huyo zuberi ataficha wapi hiyo pua yake. ole wake siku ikifika!!!!!!!!!! namalizia kwa kusema pole mkuu
 
Lema, alivyokuwa na upeo mdogo eti anataka wale wote walimpigia kura waende mahakamani, anajua kama hawana kazi ndio maana anasema hayo maneno
 
Hujui Polisi wanavyomhujumu Lema.
Wamuache na shughuli zake uone kama kuna tatizo!

Yaani watu wa arusha tutabakia na ushabiki tu kila siku maandamano au mahakamani shida ya mbunge wetu anapenda sifa sana na sifa zenyewe ni za kijinga mara gari aweke namba ni jina lake yani mambo ya ajabu si uwe kama mnyika au zitto wanahoja za msingi juu ya wapiga kura wao hata unaposema upo tayari kufa kwa ajili ya kutetea haki yako wewe na familia yako hivi hata leo hii ukifa kwasababu ya siasa unategemea utaiona hiyo paradiso kwasababu ya siasa never tena sahau habari hiyo kwanza chunguza uliletwa duniani kwa dhumuni lipi usidandie mambo ya mungu na siasa uchwara ambazo hazimtambui mungu
 
Sitashangaa siku moja kusikia OCD Zuberi amempiga risasi mh. Lema. Kama amefikia hatua ya kumpakazia kwamba anataka kumteka mwanae, huyo zuberi anaweza kufanya lolote baya dhidi ya Lema ama wananchi wa Arusha ili afikie malengo yake binafsi.

Kwa namna nchi hii vyeo vinatolewa kiholela holela, tusubiri kusikia zuberi kapandishwa cheo na ndicho anatafuta kwa nguvu zake zote.

Lakini asisahau kwamba malipo yote ni hapa hapa duniani, atalipwa haki yake siku moja.


Inaoneka huyo Zuberi ni mlevi tu, kama una ana hakika kuwa Lema ana mpango wa kumteka mwanaye kwa nini hasiende mahakamani kufungua shauri? Hii ni kutaka kuleta chuki tu dhidi ya polisi as taasisi na wananchi wa mkoa wa Arusha especially wa jimbo la Lema.
 
Sasa kama walikusanyika kama panya ulitaka waitwe nini? Hiyo kesi inamuhusu Lema basi kwanini ahamasishe wananchi wasio na uwezo wa kufikiri wakafanye zogo hapo mahakamani? Hizi ni njia za kushinikiza mahakama itoe maamuzi ya kumpendelea Lema kwa njia vitisho, ni watu wenye historia ya ujangiri ndio wanatumia mbinu hizi.

Mimi naona ni Bora aje Nape awashikishe ukuta nyie majobless wa Arusha.
 
Sitashangaa siku moja kusikia OCD Zuberi amempiga risasi mh. Lema. Kama amefikia hatua ya kumpakazia kwamba anataka kumteka mwanae, huyo zuberi anaweza kufanya lolote baya dhidi ya Lema ama wananchi wa Arusha ili afikie malengo yake binafsi.

Kwa namna nchi hii vyeo vinatolewa kiholela holela, tusubiri kusikia zuberi kapandishwa cheo na ndicho anatafuta kwa nguvu zake zote.

Lakini asisahau kwamba malipo yote ni hapa hapa duniani, atalipwa haki yake siku moja.


Umenikumbusha kupandishwa kwa Mahita aliyepewa kuwa IJP kwa kumdhibiti Mrema Augustino kipindi kile.

Kinachonisikitisha ni mtumishi wa umma anaposhindwa kufanya kazi yake na kugeuka kuwa mwanasiasa. Ni ukweli usiopingika kuwa kuwa "...human being are political animals...," kwamba siasa huwezi kuiepuka.

Lakini unapokuwa mtumishi wa umma, pamoja na kukipenda chama fulani, watumishi wote wa umma na polisi wakiwemo, hawatakiwi kuonesha wazi upendeleo wa chama fulani. Watumishi wa umma wanatakiwa kufanya kazi katika objectivity situation, bila kupendelea wala kukandamiza upande mmoja.

Sirro Mwanza, alisimama kama mtumishi wa umma, na aliondoka akiwa anahitajika na wengi bado. Mungu amjalie afya njema.

Na mwarobaini wa yote haya, ni pale tu mwanasiasa atakopokonywa mamlaka yake katika kugawa na kunyang'anya vyeo atakavyo. Katiba mpya tuitakayo, napenda ajibu hili vizuri.
 
Sasa kama walikusanyika kama panya ulitaka waitwe nini? Hiyo kesi inamuhusu Lema basi kwanini ahamasishe wananchi wasio na uwezo wa kufikiri wakafanye zogo hapo mahakamani? Hizi ni njia za kushinikiza mahakama itoe maamuzi ya kumpendelea Lema kwa njia vitisho, ni watu wenye historia ya ujangiri ndio wanatumia mbinu hizi.

Mimi naona ni Bora aje Nape awashikishe ukuta nyie majobless wa Arusha.

Ni kweli kesi inamhusu Lema. Lakini ni wananchi waliosababisha Lema awe na kesi hiyo. Mahakamani hazuiliwi mtu kusikiliza kesi, ni uhuru wa mtu kupata habari za mahakamani.

Je una ushahidi wowote kwamba Lema alipita mtaani kuwatangazia watu wahudhurie mahakani? Mbona hatujafahamishwa hilo? Kwani wananchi kwenda kusikiliza mwenendo wa kesi ya mtu waliyemchagua si kwa hila bali kwa upendo wao wenyewe wamevunja sheria gani?

Mahakama inatoa kikomo cha watu kuhudhuria mahakani? kama una idadi inayotakiwa kuwepo mahakani, tujuze sio uendelee na kulimbikiza ujinga kama Mr. Ebbo alivyosema katika wimbo wake wa MBADO
 
Sasa kama walikusanyika kama panya ulitaka waitwe nini? Hiyo kesi inamuhusu Lema basi kwanini ahamasishe wananchi wasio na uwezo wa kufikiri wakafanye zogo hapo mahakamani? Hizi ni njia za kushinikiza mahakama itoe maamuzi ya kumpendelea Lema kwa njia vitisho, ni watu wenye historia ya ujangiri ndio wanatumia mbinu hizi.

Mimi naona ni Bora aje Nape awashikishe ukuta nyie majobless wa Arusha.
Kesi haimhusu Lema peke yake ndiyo maana kati ya walioshitakiwa ni pamoja na mwanasheria wa Tanzania....na serikali imetenga bil 14 kwaajiri ya kesi za kupinga matokeo sasa niambie hizo bil 14 ni kodi za mama yako au kodi ya Lema....acha kukurupuka na isitoshe mwisho wa siku wananchi wa Arusha ndiyo watakao takiwa kutoa ushadi kama lema alituka ama alah sasa kama utakuwa unawazuia kuinga watafatiliaje.............au wafatilie kupitia magazeti ya Uhuru, Habari leo
 
Back
Top Bottom