Taarifa Kwa Umma Kutoka Benki Kuu Ya Tanzania kuhusu NBC

ukiona hivyo wanampango wa kuuza share za tz .........tumekwisha mie neenda toa pesa jamaa wengi wameshafukuzwa kwenye hii bank
 
[h=1][/h]


Katika Gazeti la Business Times toleo nambari 1248 la Ijumaa, tarehe 10 Agosti 2012, ziliandikwa habari zenye kichwa cha habari chenye maana kuwa “Operesheni za NBC zawekwa chini ya usimamizi wa Benki Kuu”.

Katika habari hiyo ilielezwa kuwa Benki Kuu imechukua hatua hiyo kufuatia ripoti za tuhuma kadhaa zihusuzo udhaifu katika uendeshaji wa benki na utawala bora.


Benki Kuu inapenda kuchukua fursa hii kuueleza umma kuwa haijaweka operesheni/shughuli za NBC chini yake. Benki hiyo inajiendesha yenyewe kwa kufuata utaratibu wa Sheria za Makampuni, 2002, Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha 2006 na miongozo itolewayo na Benki Kuu kama zilivyo benki zingine. Wateja wa NBC na Umma kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufanya biashara na benki hii kama kawaida.


IMETOLEWA NA BENKI KUU YA TANZANIA11AUGUST 2012

Big up Bot.
 
Kamshahara kangu kanapitia nbc, sasa ikifilisika cjui tu akiba twangu tutasalimika, lol hz fn thngz bana
 
Mkurugenzi alikuwa anatoa mikopo kama njugu kuna watu wengi sana wamechukuwa mikopo ya milioni 100 wametoa 10% hawa ndio wasomi wetu tunaojitapa nao kila siku humu JF.
 
Mkurugenzi alikuwa anatoa mikopo kama njugu kuna watu wengi sana wamechukuwa mikopo ya milioni 100 wametoa 10% hawa ndio wasomi wetu tunaojitapa nao kila siku humu JF.
Nasikia kuna jamaa walitoka Vodacom kuhamia hapo ndo wamepiga sana dili hapo NBC, ila inarudisha sana nyuma imani kwa vijana!
 
Huenda kuna shida huko
NBC. Masuala ya kibenki ni very sensitive hivyo BOT wanakanusha hata
kama kutakuwa na shida iwe kimya kimya kuepuka piblic punic.Nadhani
wangetuambia sababu ya Mafuru kusimamishwa na ni nani anaongoza NBC.
Uongozi katika masuala ya kibenki ni muhimu sana hivyo kuondolewa kwa
CEO kunaashiria kuwa mambo si shwari hapo NBC.
Ni kweli kusimamishwa kwa Mafuru kumetokana na matatuzo lakini hiyo haimaanishi kwa BoT imechukua operations xa hiyo benki. Inapofikia Central Bank kuweka operations za bank chini yake lazima hali ingejionyesha dhahiri na nadhani BoT huwa haifanyi taarifa hizo kuwa siri. Hao watu wa Business Times wanapaswa kuweka ushahidi wa taariya yao
 
this is too dangerous,hii ni bank kubwa sana wateja wakipanic na kuwithdraw their assets itakuwa tragic kwakweli
 
Mkuu Kiranga BOT wanasimamia mabenki yote. Akiondoka CEO lazima BOT wajue kaondoka kwa sababu gani na hata anayeingia lazima lazima apate baraka za BOT.Hivyo nadhani BOT wako well informed kuhusu matatizo ya NBC na hasa sababu ya kuondolewa kwa CEO. Hivyo basi hawatakiwi tu kukanusha wanatakiwa waende mbele kidogo na kutuambia kidogo kuhusu sababu ya CEO kuondolewa ili public isiwe na mashaka kuhusu akiba zao.
 
Last edited by a moderator:
Business Times inabidi ije na taarifa ya kukanusha, manake wanafanya sasa hata baadhi ya wateja hawaamini hiyo taarifa ya kutoka BOT, kwa habari ambazo sijazidhibitisha ni kuwa BOT wanafanya special review ya NBC ila hawataki wateja wajue, kuna shida sana ya hawa janaa wakaburu na repatriation of income katika services za ICT wanazotoa kwa NBC. Tusubiri tuone mwisho wa hii saga!
 
Ninachojua NBC ilinunuliwa na Baclays so haya yote ni njama za Baclays kuonyesha kuwa wazawa hatuwezi kumeneji na ndo maana wamempiga cHin mshikaj ili mzungu atake over. Sku c nyingi utackia mzungu ndo kachukua nafasi. NBC ilikua inafanya vizuri sana basi tu hawa wenzetu wana strategy za kufa mtu
 
Ninachojua NBC ilinunuliwa na Baclays so haya yote ni njama za Baclays kuonyesha kuwa wazawa hatuwezi kumeneji na ndo maana wamempiga cHin mshikaj ili mzungu atake over. Sku c nyingi utackia mzungu ndo kachukua nafasi. NBC ilikua inafanya vizuri sana basi tu hawa wenzetu wana strategy za kufa mtu

nahisi hujui unachokiongea,waulize staff wa nbc,watakuambia wether mbongo au mzungu anafaa nani!bora aongeze mzungu kuliko mtanzania anaekandamiza wafanyakaz tena watz,na kujichumia wenyewe wakubwa
 
Mkuu Kiranga BOT wanasimamia mabenki yote. Akiondoka CEO lazima BOT wajue kaondoka kwa sababu gani na hata anayeingia lazima lazima apate baraka za BOT.Hivyo nadhani BOT wako well informed kuhusu matatizo ya NBC na hasa sababu ya kuondolewa kwa CEO. Hivyo basi hawatakiwi tu kukanusha wanatakiwa waende mbele kidogo na kutuambia kidogo kuhusu sababu ya CEO kuondolewa ili public isiwe na mashaka kuhusu akiba zao.

Got you,

Between the lines.

Walichosema BOT hapo ni kwamba NBC haiko "under receivership" (I forgot the techno term). Kwa hiyo wao wanakanusha hiyo habari tu.

Mengine yote ni jukumu la NBC kuelezea.Hiyo communique ya BOT imekuwa deliberately short kwa sababu ya ku minimize any source of misinterpretations, contradictions and unintended leaks.Nia ni kukanusha habari za gazeti tu, wakaona wakianza sommersaults nyingine za kutetea NBC ndio wanaweza kuleta u Mwigulu Nchemba bin First Class Economist, katika kukanusha kwamba serikali haina forex za kutosha unajikuta unatoa info zinazohakikisha kwamba serikali haina forex za kutosha.Naona wamekuwa careful kutoingia katika details kwa sababu wakiingia katika details wataonyesha wazi kwamba kuna tatizo.

So why go into details and risk muddying the waters when they are not even obliged to?

Kama NBC ingekuwa under some sort of receivership kama ilivyokuwa "Greenland Bank" kwa wanaokumbuka miaka ile, then BOT ingekuwa obligated kutoa maelezo zaidi.

Kama ilivyosemwa juu, kuna matatizo ila wametoa hii statement kutuliza watu tu ili kusije kuwa na a "bank run". Na technically wako sawa kwa sababu hakuna any sort of receivership iliyopo sasa hivi.
 
Mkuu Kiranga kuna hii kitu inaitwa CAMEL ambayo hutumika katika ku assess banks. CAMEL -Capital, Assets, Management, Earnings and Liquidity. Hivyo vitu vinatakiwa vibalance kwa namna fulani. Sasa hapo NBC kuna tatizo la MAnagement basi hii inaonyesha kwamba hiyo CAMEL haiko vyema hata kidogo. Ni muhimu ikaangaliwa kwa jicho la tatu. Naamini kuwa kwa sasa BOT haiko Directly kwenye ku manage NBC lakini kukiwa na tatizo la kiuongozi katika commercial bank ama financial institution yoyote inayopokea amana za wananchi basi haraka Central Bank yoyote lazima iwe makini sana na mwenendo wa hiyo bank. Naamini pia kwamba BOT wako makini juu ya kadhia hii ya kiuongozi pale NBC
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kiranga kuna hii kitu inaitwa CAMEL ambayo hutumika katika ku assess banks. CAMEL -Capital, Assets, Management, Earnings and Liquidity. Hivyo vitu vinatakiwa vibalance kwa namna fulani. Sasa hapo NBC kuna tatizo la MAnagement basi hii inaonyesha kwamba hiyo CAMEL haiko vyema hata kidogo. Ni muhimu ikaangaliwa kwa jicho la tatu. Naamini kuwa kwa sasa BOT haiko Directly kwenye ku manage NBC lakini kukiwa na tatizo la kiuongozi katika commercial bank ama financial institution yoyote inayopokea amana za wananchi basi haraka Central Bank yoyote lazima iwe makini sana na mwenendo wa hiyo bank. Naamini pia kwamba BOT wako makini juu ya kadhia hii ya kiuongozi pale NBC


My sentiments exactly.
 
Unaweza ukaquantify hiyo akiba in numbers? Bank za US na Europe zilizocollapse unajua zilikuwa kubwa kiasi gani? Ebu tufikiri kwa kina!!!
 
Mkurugenzi alikuwa anatoa mikopo kama njugu kuna watu wengi sana wamechukuwa mikopo ya milioni 100 wametoa 10% hawa ndio wasomi wetu tunaojitapa nao kila siku humu JF.

Inasikitisha sana kuwa Watz tunapopewa fursa hua tunavuruga kwa kwenda mbele. Angalia huyu Mafuru alivyokuwa anasifiwa na kutumainiwa. Kaonesha kuwa hana tofauti na wengine

Angalia kule Mwananchi/ Citizen.Tangu aondoke Sholei wa Kenya, magazeti yameanza kujipendekeza kwa watawala mpaka inatia aibu. Hata yule Tito Muhando aliyetegemewa ni tofauti amekuwa kama waBongo wengine.

 
Huenda kuna shida huko NBC. Masuala ya kibenki ni very sensitive hivyo BOT wanakanusha hata kama kutakuwa na shida iwe kimya kimya kuepuka piblic punic.Nadhani wangetuambia sababu ya Mafuru kusimamishwa na ni nani anaongoza NBC. Uongozi katika masuala ya kibenki ni muhimu sana hivyo kuondolewa kwa CEO kunaashiria kuwa mambo si shwari hapo NBC.

Mkuu, upo sahihi kabisa. Kama ulifuatilia hata utendaji kazi wa benki hii umekuwa wa tabu kuanzia 2009 mpaka leo. Benki ambazo zilikuwa nyuma sana kama NMB sasa hivi inaiacha kwa mbali sana NBC kwa kila kitu.
 
Business Times inabidi ije na taarifa ya kukanusha, manake wanafanya sasa hata baadhi ya wateja hawaamini hiyo taarifa ya kutoka BOT, kwa habari ambazo sijazidhibitisha ni kuwa BOT wanafanya special review ya NBC ila hawataki wateja wajue, kuna shida sana ya hawa janaa wakaburu na repatriation of income katika services za ICT wanazotoa kwa NBC. Tusubiri tuone mwisho wa hii saga!

Mkuu NBC ilishauzwa kwa waingereza wa Barclays
 
Back
Top Bottom