Jasho la Damu
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 956
- 120
Leo nimemsikia Mhe Devotha Likokola Mbunge(VM) akishabikia Vyeo vya Wanawake hapa Duniani na Tanzania, wakati akichangia bajeti ya wizara ya maendeleo ya jamii. Mhe huyu alianza kwa kuwataja wanawake mbali mbali wenye nyadhifa huku akitamba wanawake hao kuwa wanaweza kuongoza kuliko wanaume. Huku akiwataja wakina Ana Makinda, Rose Migiro ya kuwa ndo mfano bora kwamba wanawake wanaweza kuongoza na kukubalika kuliko wanaume. Napenda nimfahamishe ya kwamba wanawake hao walipata nyadhifa hizo kwa kuzingatia jinsia zao na si kwamba walishindanishwa na wanaume na hata ukiangalia ufanisi wao leo hii huwezi kufananisha uwezo wa Sita alipokuwa Spika na Spika wa sasa Anne makinda. Anasimfia Rose Migiro kuna lipi la ajabu Migiro amefanya. Je kwa hizo nyadhifa walizopata walicompete kweli na wanaume au walipewa kwa kigezo cha kubebwa cha haki sawa kwa wote huku mwanaume akitengwa