Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Napenda kuchukua nafasi hii kukipongeza Chama Cha Madaktari,MAT(Medical Association of Tanzania) kwa kazi nzuri waliyoionyesha kwa kumjali na kumhudumia kiongozi wao Dr.Ulimboka tangu alipotekwa na kupigwa na kuteswa na hatimaye kusafirishwa mpaka Afrika Kusini kwa matibabu bora zaidi ambayo ndiyo yamemwezesha kurudi Tanzania akiwa na afya iliyoimarika barabara. Hongereni sana Madaktari na Mungu awabariki.
Hata hivyo nataka kutoa tahadhari kwa MAT na Madaktari wote kwa ujumla. Kwamba Dr. Ulimboka lazima apewe ulinzi imara na salama kwa masaa 24! Kama tu ambavyo MAT muliweza kuchangisha mamilioni ya Pesa kwa ajili ya matibabu ya kiongozi wa chama chenu basi ni wakti mwingine sasa kupanga mikakati ya ulinzi mkishirikiana na Familia namna ya kumpa ulinzi Dr. Ulimboka kwa wakti wote(24 hrs security). This will be another challenge to TMA. Jipangeni na mhakikishe hili la ulinzi linafanyika vinginevyo lolote laweza kutokea!
Kila Mtanzania anajua sakata la Dr.Ulimboka lilivyoanza na nina amini bado sakata hili litaendelea maadamu wale wabaya wa Dr.Ulimboka hawajawekwa wazi kwa maana ya kukamatwa, kuwekwa ndani na kufunguliwa mashtaka na hatimaye mkondo wa sheria kuchukua mkondo wake.Mengi yamesemwa kuhusu wahusika wa kazi hii chafu,yapo yenye ukweli na yapo yaliyojaaa uongo mtupu ili kupoteza ukweli wa tukio lenyewe. Nashawishika kusema kuwa kazi hii chafu ambayo kwa sehemu kubwa inaonekana kuratibiwa na Serikali ya CCM bado haikufikia malengo yaliyokusudiwa!(Mwenye masikio na asikie). Bado hawa wakora na wahuni watataka kukamilisha kazi yao chafu baada ya Dr.Ulimboka kurudi Tanzania ili wapoteze ushahidi wa kesi hii ambayo inaweza kufananishwa na "Watergate scandal".
Kumbukeni kuwa Dr.Ulimboka ndiye target na ndiye mwenye ushahidi wa kila kitu kama kesi itaanza kuunguruma. Dr. Ulimboka anawajua waliomteka kwa majina,sura na sauti na namba zao za simu.Hawa jamaa kwa namna yoyote ile watataka kufuta ushahidi huu kwa kumpoteza Dr.Ulimboka kwa gharama yoyote. They gonna strike back! Watatumia kila mbinu ili wamfikie au kumpata Dr.Ulimboka. It was confirmed by Dr. Uli himself that, they are trained soldires and killlers! Kwa hiyo watatumia mbinu zote walizofundishwa ili watimize adhima yao chafu. Kwa hiyo ulinzi ni jambo la msingi sana kwa usalama,uzima na uhai wa Dr. Ulimboka ili aendelee kutetea Afya bora kwa kila Mtanzania.
Naomba kuwasilisha.
Hata hivyo nataka kutoa tahadhari kwa MAT na Madaktari wote kwa ujumla. Kwamba Dr. Ulimboka lazima apewe ulinzi imara na salama kwa masaa 24! Kama tu ambavyo MAT muliweza kuchangisha mamilioni ya Pesa kwa ajili ya matibabu ya kiongozi wa chama chenu basi ni wakti mwingine sasa kupanga mikakati ya ulinzi mkishirikiana na Familia namna ya kumpa ulinzi Dr. Ulimboka kwa wakti wote(24 hrs security). This will be another challenge to TMA. Jipangeni na mhakikishe hili la ulinzi linafanyika vinginevyo lolote laweza kutokea!
Kila Mtanzania anajua sakata la Dr.Ulimboka lilivyoanza na nina amini bado sakata hili litaendelea maadamu wale wabaya wa Dr.Ulimboka hawajawekwa wazi kwa maana ya kukamatwa, kuwekwa ndani na kufunguliwa mashtaka na hatimaye mkondo wa sheria kuchukua mkondo wake.Mengi yamesemwa kuhusu wahusika wa kazi hii chafu,yapo yenye ukweli na yapo yaliyojaaa uongo mtupu ili kupoteza ukweli wa tukio lenyewe. Nashawishika kusema kuwa kazi hii chafu ambayo kwa sehemu kubwa inaonekana kuratibiwa na Serikali ya CCM bado haikufikia malengo yaliyokusudiwa!(Mwenye masikio na asikie). Bado hawa wakora na wahuni watataka kukamilisha kazi yao chafu baada ya Dr.Ulimboka kurudi Tanzania ili wapoteze ushahidi wa kesi hii ambayo inaweza kufananishwa na "Watergate scandal".
Kumbukeni kuwa Dr.Ulimboka ndiye target na ndiye mwenye ushahidi wa kila kitu kama kesi itaanza kuunguruma. Dr. Ulimboka anawajua waliomteka kwa majina,sura na sauti na namba zao za simu.Hawa jamaa kwa namna yoyote ile watataka kufuta ushahidi huu kwa kumpoteza Dr.Ulimboka kwa gharama yoyote. They gonna strike back! Watatumia kila mbinu ili wamfikie au kumpata Dr.Ulimboka. It was confirmed by Dr. Uli himself that, they are trained soldires and killlers! Kwa hiyo watatumia mbinu zote walizofundishwa ili watimize adhima yao chafu. Kwa hiyo ulinzi ni jambo la msingi sana kwa usalama,uzima na uhai wa Dr. Ulimboka ili aendelee kutetea Afya bora kwa kila Mtanzania.
Naomba kuwasilisha.