Taarifa juu ya kuibiwa mke

Billie

JF-Expert Member
Aug 13, 2011
12,720
19,860
Mambo jaman jana tarehe 27 nimeenda kumtembelea rafiki yangu Tukaongea mengi mno ila mwishon akanieleza kuwa kuna jambo linasumbua kichwa chake.Jambo lenyewe lipo hivi.

Yeye ana rafiki yake ambaye anafanya nae kazi muda mwingi hupenda kutumia muda wa wiki end kunywa nae vileo haswa wine nyumbani kwake Ila cha ajabu kuna mtu kampigia simu akimueleza kuwa rafiki yako na mkeo amewaona kama mara mbili wakiingia Lodge ambayo mtoa taarifa yupo jiran nayo iliyopo huko Yombo Buza(nimeisahau jina kidogo) jamaa hakutaja jina lake na akasisitiza alifuatilie hilo jambo yupo serious na baada ya hapo jamaa kazima simu yaan hapatikan.

Sasa jamaa anataka alipuuzie ili jambo ila bado linazunguka kichwani mwake cha ajabu anajiuliza mbona muda mwingi huwa yupo na rafiki yake isipokuwa wiki 1 iliyopita alienda Singida ki kazi na kuwaacha hao watuhumiwa Dar,Kingine ni kuwa rafiki yake bado hajaoa ila anae mpenzi ila hawaishi nae.

SASA ALINIOMBA NIMSAIDIE AANZIE WAPI KULICHUNGUZA ILI JAMBO MAANA LINAZIDI KUCHUKUA NAFASI KUBWA KICHWAN MWAKE HADI KUPELEKEA KUPOTEZA MAPENZI NA WOTE YAAN MKE WAKE NA RAFIKI YAKE.
 
refikii mkia wa fisiii ukiushirikiii atakufilisiiii....nadhani kuna kijiwimbo cha zamani kidogo kilikuwa kinaimba hivi
 
busara kubwa niliyopata ktk ulimwengu huu wa mapenzi kwanza usiogope kusalitiwa,mwenzako akiamua kaamua.kisha ukihisi,ukiona au kusikia unasalitiwa usilazimishe kutaka kugundua,we tega mitego yako kama ya ndezi porini,rudi nyumbani kalale kesho asubui rudi utamkuta mnyama wako kanasa!ukilazimisha sana unaweza kupewa hata ushahidi wa video ukiangalia unajiona ni wewe mwenyewe kuna siku ulizama na mpenzi wako huyo guest!stage one-mwambie atulie kwanza,kana kwamba hamna kitu kilichotokea,kisha ataendelea na uchunguzi wake taratibuuuuuu kama hataki vile!
 
Eneo ametajiwa akapandikize mtu wa kumpatia taarifa. as simple as that.

Bazazi na Bazazi!
 
Asifanye papara kufatilia jambo wala asionyeshe kua kunamabadiliko yoyote,ajifanye zuzu kama mwanzo ukweli ataupata...
 
Inategemea na mwanamke, kama ulioa mwanamke huna imani naye kama ni wako tu, atacheza game na wengine.

Watu kama mimi huwa hatuna wasi wasi na wake zetu, na ni bora uishi bila kuwa na mke kuliko kuwa na wasi wasi na mke wako, huo ni ugonjwa na hauna dawa.

Rafiki yako ni mlevi na siku zote mlevi huwa hana akili ndo mana alioa kabla ya kutumia akili, na mwanamke anaye olewa na mlevi mara nyingi naye huwa hazimtoshi ndo mana ukaona ni easy kugawa uhondo...hao ndo wale type nataka kuonja :biggrin:
 
Afuatilie kwa taratibu kama kuna jambo atagundua, lisemwalo lipo! Hata kama ni majungu ayafanyie kazi manake yanamuhusu mkewe!
 
Afuatilie kwa taratibu kama kuna jambo atagundua, lisemwalo lipo! Hata kama ni majungu ayafanyie kazi manake yanamuhusu mkewe!
Alaaa kwa hio nikisema wewe ni ki gf changu, basi umeisha kuwa gf wangu...I love you my gf :biggrin:
 
Asifanye papara kufatilia jambo wala asionyeshe kua kunamabadiliko yoyote,ajifanye zuzu kama mwanzo ukweli ataupata...

hadi muda huu hakumtaarifu yeyote kati ya hao watuhumiwa wawili ndiyo maana maswali mengi yana msumbua kichwani.
 
Inategemea na mwanamke, kama ulioa mwanamke huna imani naye kama ni wako tu, atacheza game na wengine.

Watu kama mimi huwa hatuna wasi wasi na wake zetu, na ni bora uishi bila kuwa na mke kuliko kuwa na wasi wasi na mke wako, huo ni ugonjwa na hauna dawa.

Rafiki yako ni mlevi na siku zote mlevi huwa hana akili ndo mana alioa kabla ya kutumia akili, na mwanamke anaye olewa na mlevi mara nyingi naye huwa hazimtoshi ndo mana ukaona ni easy kugawa uhondo...hao ndo wale type nataka kuonja :biggrin:

We huna hofu na mkeo labda kwa nini au humpendi au kuna kitu umemtega au nini?Mi ninachotambua kuwa hofu ya kuibiwa huja kwa kitu chako kizuri tena chenye dhaman Je hofu hiyo umewezaje kuiua?
 
Ni vzr kufuatilia kwa umakini. Hivi sasa kuna wimbi kubwa sana la kusalitiana ktk mapenzi na ndoa hivyo taarifa za namna si vibaya kuzifanyia uchunguzi. Anza taratibu kwa kufuatilia mienendo ya hao wawili bila kuwapa taarifa and with time iko siku utakuja kugundua ukweli uko wapi.
 
sweetlady mimi nakuja wewe vizuri jee umewacha tabia ya kuchukua ma bwana wezako
 
Hili ni gumu sana..lakini lazima awe amejiandaa kisaikolojia haswa.Je ameamua vipi akimkamata ugoni mkewe (atamwacha au atamsamehe?)....kama atamsamehe asiishi kwa mashaka makubwa atakufa kwa kihoro...ni ngumu lakini amweleze kwa umakini mkubwa kwamba katika mahusiano yao hali si shwari (na amtazame usoni wakati mwingine hao si rahisi kuficha hisia) halafu amwambie anahisi kusalitiwa na rafiki yake.Baada ya hapo kama mwanamke muungwana atakubali makosa ama kuonekana kujuta.Yakitokea hayo asamehe wala asijiulize maswali mengi sana kwa sababu siku hizi watu wanasalitiana wakati mwingine bila hata sababu za msingi (udogo wa mawazo-kudanganyika,fasheni).

Lakini kama akigundua atamwacha basi ni lazima awe na ushahidi concrete la sivyo ataonekana ana wivu wa kijinga na wagoni wake wataruka mtego.Kwa hili mtego unaweza kuhusisha namba ya mtoa taarifa..mtumie salio litakuja jina la mtoa taarifa na lazima utakuwa unamfahamu,muulize akupe data,au weka mtego Guest(wagoni huwa hawabadilishi).Na hutakiwi kuonyesha hisia zozote wakati wa hizo harakati.
 
We huna hofu na mkeo labda kwa nini au humpendi au kuna kitu umemtega au nini?Mi ninachotambua kuwa hofu ya kuibiwa huja kwa kitu chako kizuri tena chenye dhaman Je hofu hiyo umewezaje kuiua?
Swali lako la kwanza; Sina hofu na mke wangu kwa sababu namuamini 100%...sio yeye tu yani namini family yake wote wametulia sana.

Swali lako la pili; Ningekuwa simpendi nisinge muoa na hakuna kitu nimemtega niamini kabisa.

Point yako ingine kuhusu nimetoa vipi hofu!

Nimetoa hofu sababu mungu ndo kanijalia mke ambaye sina wasi wasi naye, afu nimeisha sema kuoa ni bahati, na bahati sio kila mmoja ana bahatika kuwa nayo...namshukuru mungu kwa kunipa mke mzuri kama wangu, katulizana kimyaa.

Yani huwezi kuamini mimi ndo shetani, lakini kuna siku mungu ataniokoa, tatulia tu na hivi wife dini nyingi dua yake itajibiwa tu :biggrin:
 
Inategemea na mwanamke, kama ulioa mwanamke huna imani naye kama ni wako tu, atacheza game na wengine.

Watu kama mimi huwa hatuna wasi wasi na wake zetu, na ni bora uishi bila kuwa na mke kuliko kuwa na wasi wasi na mke wako, huo ni ugonjwa na hauna dawa.

Rafiki yako ni mlevi na siku zote mlevi huwa hana akili ndo mana alioa kabla ya kutumia akili, na mwanamke anaye olewa na mlevi mara nyingi naye huwa hazimtoshi ndo mana ukaona ni easy kugawa uhondo...hao ndo wale type nataka kuonja :biggrin:

ameolewa na [mlevi walevi ndo awanaga akili] na yeye mwenyewe atakuwa mlevi,,wee usituletee ulokole wako wa***** apa mlevi anafananaje?jb swali
 
Si asafiri tena aende Singida! Atajua tu ka vyake vyaliwa! Kwani ticket ya Singida na mke kipi ghali mkwe!
 
Back
Top Bottom