Taarifa Fupi kuhusu Kazi za Maendeleo Jimboni Ubungo (AMUA)

Rais Kikwete aliahidi ajira milioni moja kila mwaka, lazima tuwaondoe

...ndiyohiyo

Alikwenda Gorani, Jimbo la Ubungo mwaka juzi, wananchi wakamwambia wanataka maji, akaahidi kuwa ataitisha kikao cha wadauwa maji ikulu. Akawataja. wananchi wakapiga kelele lazima mbunge awepo. Kikwete akalazimika kukubali kuwa mbunge awepo maana yeye ndiye mwakilishi wa wananchi na mpiganaji wa suala la maji ndani na nje ya bunge.

Hiyo ilikuwa mwaka 2013, siku chache baada ya hoja ya Mnyika kuhusu tatizo la maji kuzua zogo ndani ya ukumbi wa bunge. Watu wengi hawajui suala hili; kwamba vurugu ndani ya bunge kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu zilitokea siku hiyo ambapo, serikali bungeni, uongozi wa bunge na wabunge wa CCM walikuwa wanazuia hoja ya Mnyika kuhusu tatizo la maji Ubungo, Dar es Salaam na nchi nzima kwa ujumla isijadiliwe.

Eti ingewaumbua na kuanika ufisadi, uozo na udhaifu wa Serikali ya CCM katika tatizo hilo ambalo sasa linaanza kuwa sugu.

Hadi tunapoandika hapa ikulu haijawahi kuitisha kikao hicho kama ambavyo Rais Kikwete aliahidi tena akasema hadi siku/tarehe. Hadharani. Mbele ya wananchi. Leo ni miaka mitatu. Kikao tu....
 
Wewe mkigoma hujui ulisemalo. Wewe ndiye unayepiga domo. Sisi tunaoishi katika jimbo hili ndio tunaojua mwakilishi wetu Mnyika amefanya nini. Ni ukweli usiopingika kuwa Mnyika amejitahidi saaaana kutekeleza majukumu yake ya kibunge ukilinganisha na watangulizi wake wa chama cha madomo. Big up Mnyika. Kwanza ni wabunge wangapi wanaoweza kushirikisha wananchi wao kwa kutoa feedback kama anavyofanya Mnyika! Ni wazi ni wachache sana.

Nina wasiwasi na akili yako wewe sio mkazi wa ubungo na wakazi wa ubungo wakija wakisikia haya unayoyasema utatafuta pa kukimbilia
 
We jiandae kupigwa chini watu wa ubungo sio wana jf wengi wanaokupa pongezi ni watu wa hai hahaha kazi unayo

Mnyika kwa sasa ni Kama MBWA aliyepandishwa juu ya MTI na kubweka hovyo huku akiwa amesahau kazi yake ni kulinda lindo , sijui nan atamshusha huko aliko, tukutane OCTOBER
 
watu wa mjini bhana ukiwaona kama wana akili vile kumbe hamnazo kabisa sjui ninyi wemyewe na ubongo yenu mtakapolia kilio cha mbwa....
 
Kamanda,huna haja kueleza namna unavyofanya kazi zako,wewe ni jembe,tuko pamoja.Magamba wanabwabwaja tuu,hata CDM ikiweka jiwe hapo Ubungo litashinda.
 
Mkuu Mnyika, Mbunge wangu, naona umetuacha solemba wapiga kura wako. Tangia umetoa taarifa hii mwaka 2012 hujarudi tena kutoa mrejesho! Umekuwa huonekani jimboni, wananchi wa Bonyokwa, Golani, Kilungule, Makoka, Msewe, Kibangu, Kimara Temboni, Kimara mwisho, nk hawakuoni kuja kushiriki nao ama kuwahamasisha kujiletea maendeleo.

Barabara zimechoka ile mbaya, magari yanaumia kweli kweli na kila wiki wananchi wako wenye magari wanashinda garage. Ile Vitz yako haiwezi kufika kabisa maeneo hayo. Maji hakuna hata kidogo, visima vinatoa maji ya chumvi. Tunaoga maji ya chumvi hadi miili inakakamaa!

Mbunge wangu Mnyika umetuacha vibaya, hivi utarudi kuja kutuomba kura kweli au ndio umeingia anga za kitaifa kwenye unaibu Katibu Mkuu?
 
Wewe mkigoma hujui ulisemalo. Wewe ndiye unayepiga domo. Sisi tunaoishi katika jimbo hili ndio tunaojua mwakilishi wetu Mnyika amefanya nini. Ni ukweli usiopingika kuwa Mnyika amejitahidi saaaana kutekeleza majukumu yake ya kibunge ukilinganisha na watangulizi wake wa chama cha madomo. Big up Mnyika. Kwanza ni wabunge wangapi wanaoweza kushirikisha wananchi wao kwa kutoa feedback kama anavyofanya Mnyika! Ni wazi ni wachache sana.
Tangia atoe taarifa hii mwaka 2012, Mnyika hajarudi hapa kutupatia muendelezo wa utekelezaji wa majukumu yake.
 
Tangia atoe taarifa hii mwaka 2012, Mnyika hajarudi hapa kutupatia muendelezo wa utekelezaji wa majukumu yake.

Wewe unashinda JF wenzako mrejesho wanapeleka field, pole sana ukiwa na roho hii ungali kijana ukiwa mzee unakuwa mchawi.

Haya tueleze diwani wako anaitwa nani na ametekeleza nini? Na mwenyekiti wako wa mtaa ni nani na ametekeleza nini? Halafu tutamalizia na Mnyika.
 
Wewe unashinda JF wenzako mrejesho wanapeleka field, pole sana ukiwa na roho hii ungali kijana ukiwa mzee unakuwa mchawi.

Haya tueleze diwani wako anaitwa nani na ametekeleza nini? Na mwenyekiti wako wa mtaa ni nani na ametekeleza nini? Halafu tutamalizia na Mnyika.
Diwani wangu anaitwa Manota, anahangaika tu hana msaa wowote toka Kwa Mbunge.
Matola umri wangu umeenda sana kwa hiyo kama uzee ni uchawi basi mimi mchawi
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mnyika, Mbunge wangu, naona umetuacha solemba wapiga kura wako. Tangia umetoa taarifa hii mwaka 2012 hujarudi tena kutoa mrejesho! Umekuwa huonekani jimboni, wananchi wa Bonyokwa, Golani, Kilungule, Makoka, Msewe, Kibangu, Kimara Temboni, Kimara mwisho, nk hawakuoni kuja kushiriki nao ama kuwahamasisha kujiletea maendeleo.

Barabara zimechoka ile mbaya, magari yanaumia kweli kweli na kila wiki wananchi wako wenye magari wanashinda garage. Ile Vitz yako haiwezi kufika kabisa maeneo hayo. Maji hakuna hata kidogo, visima vinatoa maji ya chumvi. Tunaoga maji ya chumvi hadi miili inakakamaa!

Mbunge wangu Mnyika umetuacha vibaya, hivi utarudi kuja kutuomba kura kweli au ndio umeingia anga za kitaifa kwenye unaibu Katibu Mkuu?

Kwahiyo Kimbunga unahitaji mrejesho zaidi wa awamu ya pili alichofanya Mnyika katika kutimiza wajibu wake wa nafasi ya Ubunge, si ndiyo hoja yako hapa!
 
Last edited by a moderator:
Kwahiyo Kimbunga unahitaji mrejesho zaidi wa awamu ya pili alichofanya Mnyika katika kutimiza wajibu wake wa nafasi ya Ubunge, si ndiyo hoja yako hapa!

Naam, yaani tangia taarifa hii ya August 2012 hadi leo Utekelezaji ukoje? Tangia wakati huo nini kimefanyika.

Mimi ni mwana Ubungo kindakindaki
 
Diwani wangu anaitwa Manota, anahangaika tu hana msaa wowote toka Kwa Mbunge.
Matola umri wangu umeenda sana kwa hiyo kama uzee ni uchawi basi mimi mchawi
Wewe kweli kichwani mweupe, unayajuwa majukumu ya mbunge? Diwani wako huwa anakwenda council kufanya nini? Kutembea? Kazi ya meya wako ni ipi? Na Rais wako Kikwete ametimiza ahadi ngapi jimboni kwako?
 
Last edited by a moderator:
Wewe kweli kichwani mweupe, unayajuwa majukumu ya mbunge? Diwani wako huwa anakwenda council kufanya nini? Kutembea? Kazi ya meya wako ni ipi? Na Rais wako Kikwete ametimiza ahadi ngapi jimboni kwako?

Wewe ndio mweupe na lazima tung'oe Mnyika. Amemuita Rais dhaifu lazima asirudi tena Bungeni kuendelea kutukana viongozi

.....ndiyohiyo
 
Back
Top Bottom