Taarifa Fupi kuhusu Kazi za Maendeleo Jimboni Ubungo (AMUA)

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Napokea kwa unyenyekevu pongezi zilizotolewa na wachangiaji mbalimbali hapa JF lakini izingatiwe kuwa michango yangu bungeni ni matokeo ya heshima mliyonipa ya kuwawakilisha. Aidha yapo maoni machache ambayo yametoa tafsiri tenge kuhusu kazi ya mbunge na wengine mmetaka nieleze nimefanya kazi gani za maendeleo jimboni Ubungo.

Tarehe kama ya leo 21 Agosti 2005 nilianza mchakato wa kuwa kugombea ubunge nikiwa kwenye chakula na watoto yatima, tarehe kama hiyo mwaka 2010 nilianza kampeni za uchaguzi mitaani Ubungo, tarehe hii hii kwa mwaka huu wa 2012 naomba niitumie kutoa taarifa fupi ya utekelezaji kwa masuala ya maendeleo katika mwaka wa fedha 2011/2012 uliomalizika tarehe 30 Juni 2012;
http://mnyika.blogspot.com/2012/08/taarifa-fupi-kuhusu-kazi-za-maendeleo.html kuhusu elimu, ajira, miundombinu, maji, usalama, uwajibikaji, ardhi na afya; taarifa ya kina ya utekelezaji nitaitoa nitakapotimiza miaka miwili ya utendaji.

Hivyo, ufanisi wa ubunge wangu upimwe kwa kuzingatia msimamo huu kuhusu kazi nne za mbunge katika kuwezesha maendeleo:
http://mnyika.blogspot.com/2010/03/natangaza-rasmi-dhamira-ya-kugombea.html ambao niliwaeleza wananchi wakati wa uchaguzi hivyo nilichaguliwa ikifahamika wazi kuwa huo ndio wajibu ambao nitautekeleza katika kipindi cha miaka mitano.

Bado naendelea kuamini kwamba jimbo la Ubungo na taifa kwa ujumla tutapiga hatua ya haraka zaidi ya maendeleo kupitia mabadiliko katika mifumo yetu ya mgawanyo wa rasilimali na usimamizi wa matumizi ya fedha za umma na pia kwa kuweka mazingira bora ya kisera, kisheria na kiutendaji wa sekta binafsi.Tuliyoyafanya mpaka sasa ni sehemu tu katika mahitaji makubwa ya maendeleo kutokana na pengo la miaka 50 ukilinganisha na fursa ambazo taifa letu linazo; hata hivyo naamini miaka mitatu iliyobaki itafanya miaka mitano ya kuisimamia Serikali iliyopo madarakani hivi sasa pamoja na udhaifu wote uliokuwepo kuleta tofauti katika maendeleo majimboni.

Ni katika muktadha huo wakati mwingine tunazimika kuwakilisha na kuwasilisha matakwa ya wananchi namna hii:
http://www.youtube.com/watch?v=ES4OMOD_xME tukiamini kwamba watawala wenye dhamana kwa sasa ya kukusanya kodi watasikiliza na kuzingatia vipaumbele vya maendeleo vya wananchi.Aidha, baada ya kazi mkutano wa nane wa bunge naomba kutumia fursa mjadala utakaofuatia taarifa hii kupata maoni yenu kuhusu masuala ninayopaswa kuyapa kipaumbele katika kuwawakilisha na kuwatumikia jimboni katika kipindi cha mwezi Septemba mpaka Oktoba 2012 kabla ya kuanza kwa mkutano wa tisa wa bunge na pia kuhusu maandalizi ya mwaka 2013.

Kero nyingi zinazoendelea kuwepo kwa sasa ni neema iliyojificha (blessing in disguise) ili tuendelee kuunganisha nguvu ya umma kuendeleza wimbi la mabadiliko. Narudia tena kuwakumbusha kuwa nguvu ile ile tuliyoitumia kwenye kutafuta kura na kulinda kura ndio naiomba toka kwenu katika hatua hii ya kufanya kazi za kuwezesha maendeleo kwa kutimiza wajibu kila mmoja wetu kwa nafasi yake, kuisimamia serikali na kuunganisha rasilimali za wadau wengine; Maslahi ya Umma Kwanza.
 
Mh. Mnyika, kwanza natoa pongezi kwa kututoa dukuduku cc waumini wa siasa za Nchi hii kupitia hapa JF. Lakini pia kwa kua 90% ya waliokupa kura zao 2010 ni raia wa kawaida wasiojua au hawajapata fursa ya kujua kutumia mitandao ya kijamii nahitaji ujumbe huu uwafikie wao kwani ndio wanaojua utendaji wako hasa katika jimbo la Ubungo.

Ni mkakati gani ulionao ili taarifa kama hizi ziwe katika ncha za vidole vyao?
 
Bado naendelea kuamini kwamba jimbo la Ubungo na taifa kwa ujumla tutapiga hatua ya haraka zaidi ya maendeleo kupitia mabadiliko katika mifumo yetu ya mgawanyo wa rasilimali na usimamizi wa matumizi ya fedha za umma na pia kwa kuweka mazingira bora ya kisera, kisheria na kiutendaji wa sekta binafsi.Tuliyoyafanya mpaka sasa ni sehemu tu katika mahitaji makubwa ya maendeleo kutokana na pengo la miaka 50 ukilinganisha na fursa ambazo taifa letu linazo; hata hivyo naamini miaka mitatu iliyobaki itafanya miaka mitano ya kuisimamia Serikali iliyopo madarakani hivi sasa pamoja na udhaifu wote uliokuwepo kuleta tofauti katika maendeleo majimboni.

Mungu akusimamie na iwe kama unavyoamini......kila la kheri.

Ingekua vyema na wenzio wakajitoa na kuelezea nini walichofanya/wanayoendelea kufanya kwenye majimbo yao especially Halima Mdee.
 
Hongera sana John.Taarifa yako imenikumbusha kwanini wewe ni mbunge bora zaidi kwa kuwa na michango mingi bungeni.Lakini niwapongeze viongozi wetu wakuu Mbowe na Dr Slaa kwa kukupika na ukapikika.Hongera John vijana tunakujivunia....
 
watakuja na kejeri zao muda c mrefu!!!!!!!!!!!! hongera mhe.
 
Mh. Mnyika, kwanza natoa pongezi kwa kututoa dukuduku cc waumini wa siasa za Nchi hii kupitia hapa JF. Lakini pia kwa kua 90% ya waliokupa kura zao 2010 ni raia wa kawaida wasiojua au hawajapata fursa ya kujua kutumia mitandao ya kijamii nahitaji ujumbe huu uwafikie wao kwani ndio wanaojua utendaji wako hasa katika jimbo la Ubungo.

Ni mkakati gani ulionao ili taarifa kama hizi ziwe katika ncha za vidole vyao?

Naomba kuunga mkono hoja hii kwa nguvu sana.
Nashauri ripoti hii uichapishe na kuisambaza ktk jimbo lote. Viongozi wote wa chama ktk ngzi kata na tawi waipate ili wawaeleze wananchi.Ofisi zote za chama iwe na nakala.

Pili, Ni ukweli kwamba wagombea watarajiwa wa vyama vyote wanaeneza taarifa za uwongo huko mtaani kuwa wewe ni mbunge wa magazeti na mjengoni. Ukisambaza taarifa hii utakuwa umekata mzizi wa fitina.

Tatu, si vibaya kama utawaambia wengine kupitia vyombo vya habari. Well, wako watakaosema unatafuta cheap popularity, lakini ndivyo walivyomsema mbowe na helikopta yake 2005 lakini baadaye nao wakamwiga.

 
Wale wanafiki wanaokupinga wataishia kunawa tu....we maji ya moto na ni moto wa kifuu
 
safi sana mkuu tulianza na ww kwa kulinda kura na tutamaliza na ww katika kusaidiana kuleta maendeleo siyo ubungo tu bali tanzania kwa ujumla kwan ww ni mbuge wa kitaifa!
 
Napokea kwa unyenyekevu pongezi zilizotolewa na wachangiaji mbalimbali hapa JF lakini izingatiwe kuwa michango yangu bungeni ni matokeo ya heshima mliyonipa ya kuwawakilisha. Aidha yapo maoni machache ambayo yametoa tafsiri tenge kuhusu kazi ya mbunge na wengine mmetaka nieleze nimefanya kazi gani za maendeleo jimboni Ubungo.

Tarehe kama ya leo 21 Agosti 2005 nilianza mchakato wa kuwa kugombea ubunge nikiwa kwenye chakula na watoto yatima, tarehe kama hiyo mwaka 2010 nilianza kampeni za uchaguzi mitaani Ubungo, tarehe hii hii kwa mwaka huu wa 2012 naomba niitumie kutoa taarifa fupi ya utekelezaji kwa masuala ya maendeleo katika mwaka wa fedha 2011/2012 uliomalizika tarehe 30 Juni 2012;
http://mnyika.blogspot.com/2012/08/taarifa-fupi-kuhusu-kazi-za-maendeleo.html kuhusu elimu, ajira, miundombinu, maji, usalama, uwajibikaji, ardhi na afya; taarifa ya kina ya utekelezaji nitaitoa nitakapotimiza miaka miwili ya utendaji.

Hivyo, ufanisi wa ubunge wangu upimwe kwa kuzingatia msimamo huu kuhusu kazi nne za mbunge katika kuwezesha maendeleo:
http://mnyika.blogspot.com/2010/03/natangaza-rasmi-dhamira-ya-kugombea.html ambao niliwaeleza wananchi wakati wa uchaguzi hivyo nilichaguliwa ikifahamika wazi kuwa huo ndio wajibu ambao nitautekeleza katika kipindi cha miaka mitano.

Bado naendelea kuamini kwamba jimbo la Ubungo na taifa kwa ujumla tutapiga hatua ya haraka zaidi ya maendeleo kupitia mabadiliko katika mifumo yetu ya mgawanyo wa rasilimali na usimamizi wa matumizi ya fedha za umma na pia kwa kuweka mazingira bora ya kisera, kisheria na kiutendaji wa sekta binafsi.Tuliyoyafanya mpaka sasa ni sehemu tu katika mahitaji makubwa ya maendeleo kutokana na pengo la miaka 50 ukilinganisha na fursa ambazo taifa letu linazo; hata hivyo naamini miaka mitatu iliyobaki itafanya miaka mitano ya kuisimamia Serikali iliyopo madarakani hivi sasa pamoja na udhaifu wote uliokuwepo kuleta tofauti katika maendeleo majimboni.

Ni katika muktadha huo wakati mwingine tunazimika kuwakilisha na kuwasilisha matakwa ya wananchi namna hii:
http://www.youtube.com/watch?v=ES4OMOD_xME tukiamini kwamba watawala wenye dhamana kwa sasa ya kukusanya kodi watasikiliza na kuzingatia vipaumbele vya maendeleo vya wananchi.Aidha, baada ya kazi mkutano wa nane wa bunge naomba kutumia fursa mjadala utakaofuatia taarifa hii kupata maoni yenu kuhusu masuala ninayopaswa kuyapa kipaumbele katika kuwawakilisha na kuwatumikia jimboni katika kipindi cha mwezi Septemba mpaka Oktoba 2012 kabla ya kuanza kwa mkutano wa tisa wa bunge na pia kuhusu maandalizi ya mwaka 2013.

Kero nyingi zinazoendelea kuwepo kwa sasa ni neema iliyojificha (blessing in disguise) ili tuendelee kuunganisha nguvu ya umma kuendeleza wimbi la mabadiliko. Narudia tena kuwakumbusha kuwa nguvu ile ile tuliyoitumia kwenye kutafuta kura na kulinda kura ndio naiomba toka kwenu katika hatua hii ya kufanya kazi za kuwezesha maendeleo kwa kutimiza wajibu kila mmoja wetu kwa nafasi yake, kuisimamia serikali na kuunganisha rasilimali za wadau wengine; Maslahi ya Umma Kwanza.
Mkuu Mnyika,
Kazi yako ni hakika kila mtu anaikubali labda awe kuadi wa UFISADI. Tunashukuru leo upo nasi hapa kwenye forum. Nina ombi kwako mkuu wangu. Kwa niaba ya wapigakura wako wa Msakuzi/Makabe ninaomba kwa heshima na taadhima sasa ututembelee tusaidiane kutatua baadi ya changamoto ambazo zinatishia ustawi wa jamii yetu. Mambo ambayo tunataka utusaidie kusukuma ni;
1. UMEME: Mh. ni kwamba tunaishi msakuzi, njia ya kuelekea Mpiji magoe. Kitongoji chetu kina nyumba zaidi ya mia moja. Pia kuna nyumba/makazi ya watawa wa Katoliki pamoja na shule ya chekechea. TANESCO waliplan kuleta umeme maeneo hayo na tayari walileta na nguzo, cha ajabu nguzo zimeanza kuoza huu mwaka wa pili sasa umeme haupo. Cha ajabu maeneo ya jirani kuna umeme na tunazuiliwa kuunganisha umeme kutoka maeneo hayo kwa kisingizio cha kuw tuko kweye mradi mkubwa. Hivyo mkuu tunaomba ututembelee ili tupange pamoja nawewe namna ya kutusaidia.
2. Maji. Tunaomba ufatilie kwa kwa nini maji ya Ruvu juu yanatoka mbombani kwa wiki mara moja tuu na tena kwa mgao. Angalia isije ikawa ni hujuma dhidi yako ili wananchi wakuchukie kuwa huwatetei. Nadhani njia nzuri ni kututemeblea ili upate kero za wananchi

Ahsante

Mpigakura wako
 
Hivi wabunge wangapi wanaweza kujipima ubavu na utendaji wao kwako?....nadhani ni wachache sana wanaoweza kuvaa viatu vyako pamoja na kuwa mgeni kabisa ktk ulingo wa siasa
 
Mnyika yale yote ulioahidi hujatekeleza hata moja, ila kwa kupiga domo bungeni hilo umefanikiwa, nia yetu ya wakazi wa ubungo ni kutekeleza uliyotuahidi vinginevyo 2015 ukae mguu sawa ukalime.
 
nachukua fursa hii kukupongeza kwa kazi nzuri uayofanya pia nakuomba uongeze jitihada katika kuwateta wananchi wanyonge wanaoonewa na taasisi a kiserikali kama vile TANROAD. mwaka 2007 bunge lilipitisha sheria mpya ya barabara na kanuni zake mwaka 2009 ambazo zinztaja hifadhi ya barabara kuwa ni mita 30 badala ya 22.5 kwa barabar zote kuu kila upande toka katikati ya barabara, na Mita 60 badala MIta 120 kwa barabara ya kuu ya Morogoro.

Lakini hadi sasa watendaji wa TANROAD hawataka kukubali mabadiliko haya ya sheria waliyoyapitisha wenyewe na kupitishwa na bunge pia. Hali hii inawaathiri kiuchuni wananchi wanaoishi kandokndo ya barabara kuu ya Morogoro. hivyo unatakiwa kuwashinikza TANROAD waweke mipka mipya ya hifadhi ya barabarayaani Mita 60toka katikati ya barabara ili wananchi waweze kuitumia ardhi yao kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kukuza ajira
 
Back
Top Bottom