Maarifa
JF-Expert Member
- Nov 23, 2006
- 4,568
- 2,910
:A S embarassed:Jamani jana usiku nilikatiza katika kituo kipya cha mabasi kilichojengwa mbezi mwisho. Ilibidi nisimame kama dakika kumi hivi kutafakari kwa kile nilichokuwa nakiona. TAA zilizowekwa ni za barabarani NJANO ISIYONG'AAA!!! Mimi sio mhandisi lakini haichukui dakika moja kubaini uozo wa kupanga na luchagua. Iweje wahandisi waliosimamia ujenzi wa kituo kukubali kuwekwa taa hafiifu ili hali kituo cha mabasi kinafanya kwazi kuanzia alfajiri sana na usiku wa manane? Inatia aibu na kinyaa sana. Ni kwa nini wasiweke taa za kunga'aa tena siku hizi zipo poa za save energy. Jamani wadau pigieni kelele uozo huu!! Zile taa tunazihitaji barabarani na sio katika mkusanyiko wa watu wengi kama kiituo cha mabasi!! nawasilisha.