T.C.R.A Wanatumaliza; TiGO Nao Wanatunyofoa Ngozi, Chukua HATUA

Mimi nimeacha kupiga simu za tigo jioni maana nimeweka mia tano nimetumia sekunde 10, nimewapigia c.care hawapokei,
 
mie nilishasema huu mtandao unafuga wezi na hawana usajili wa kweli. wanafanya kiini macho. hata idadi ya wateja wao hawajui wanachojali pesa na promotion zao za kihuni huni. ukiibiwa kwa line zao hata ukienda Polisi hawatoi print out ya line unayolalamikia kwa sababu computer zao hazina KUMBUKUMBU. bado wako na ANOLOGY ile system ya MOBITEL hadi leo na ndio maana hukataa kutoa PRINT OUT za WEZI hata kwa POLISI na MAHAKAMA haraka iwezekanavyo. Nasikia wenye hiyo Kampuni ni MABOSI wa TCRA na MAWAZIRI fulani hivi.
 
TTCL wako wapi tuamie huko kizalendo?

TTCL ilishakufa. Naomba kama kuna mtu mwenye uwezo wa IT atusaidie kutengeneza SMS isambawe ili tutusie hii kampuni ya K.I.S.E.N.G.GE. Boyfriend wangu ananambia pia kwamba hii kampuni inamilikiwa na watu wa TCRA na Mafisadi flani flani
 
Mimi u$€n&€ wao unaoniboa ni ule wa kumpigia mtu yuko hewani then unaambiwa not reachable!!!
Kuna siku nlikua na shida ya muhimu sana,
Na mtu mwenye kuweza kunitatulia alikua ana laini ya tigo tu,
Ile shida ilini-cost sana kwa kweli, nikaishia kumtukana saviour wangu bure kumbe ni hawa wA$€n&€!!
 
Naivunjilia mbali line yao nabaki na hii ya voda
sikuizi wameanza upuuzi mtu hayupo hewani wanaanza maneno meeengi af ndo wanakwambia cm haipatikani! Hawajui kuwa umeme nao ni taabu sa wanatusikilizisha huo upupu wao weee hadi chaji ziishe,pamba.vu
 
Ni jana tu nimeweka kaela kangu ili niongee na mdogo wangu yuko Ug.cha ajabu simu inaita niko nasikiliza sikioni kumbe pesa inaliwa baadae naicheki nakuta dakik ya 2 na pesa inatembea kama kawa,na bado sm inaendelea kuita,nilitamani kuitupa laini,bado siku hizi usiku wanakata pesa unayolala nayo kwenye simu zaidi ya Tshs 50,na bado pesa siku hizi kabla haujamaliza salaamu tayari pesa imeisha,bado wanachajisha pesa kuongea na kastamu kea wakati wewe ni mteja wao na hiyo ni uduma ya wateja....Tgo =UOZO na tayari leo nimehamia Airtel0782177775....wanafunzi njooni Airtel
 
Kweli TIGO weshakuwa geedy for money sana,itakuwa bahati ya mtende kama utapiga simu yao ya huduma kwa wateja na ipokelewe,alafu huduma hiyo yalipiwa siku izi,uzuri nilishawahama.
 
Jana wamerusha kijimeseji cha kujikomba kwenye simu zetu eti MUHIMU, MCHANA KUTWA, USIKU KUCHA MASAA 20, UNAONGEA KWA SH.1/SEKUNDE 1, NA KILA BAADA YA DK3 KUANZIA SAA4 USIKU MPAKA SAA1 ASUBUHI UNAONGEA BURE. Mwanaume nikajitosa mida ya saa 11jioni nikaweka sh. 1,000/= nikijua nitaongea si chini ya dk15, ajabu na kweli niliongea dk4 wakakwangua hela yote!! Uroho+uongo ni vitu vibaya sana! Hii hali ya wizi itawacost! Binafsi utumiaji wangu wa line ya tigo umepungua almost to 10% from 100%. Mchakato ni kuachana nao forever!
 
Gharama za TiGo zimekuwa kubwa,
Mimi nimehama, Rafiki zangu wamehama
pia nakushauri na wewe uhame
Unangoja nini?


Sambaza ujumbe huu kwa ndugu na jamaa!
 
Tigo kwisha kabisa!. Riba daima hupelekea katika maangamizi.
 
Miezi ya hivi karibuni, kampuni ya simu ya Tigo imelalamikiwa sana kutokana na tabia zao za kihuni. Wamekuwa wakiwaibia wananchi mchana kweupe, na shirika letu la TCRA kushindwa kuchukua hatua yoyote licha ya malalamiko lukuki. Leo mchana, nimenunua vocha za Tsh 10,000 (yaani 5 mbli) nimehangaika sana kuziingiza bila ya mafanikio. Rafiki yangu ambaye nilienda kukutana naye pale Jacky’s akawa anajaribu kuweka naye kashindwa 5,000 nzima. Kwa pamoja tukajaribu sana kuwapigia kastama kea yao 0713-800-800 kwa takribani lisaa lizima, simu ikawa haipokelewi.

Wananchi, leo tunatangaza rasmi kuanza kuwasusia hawa majambazi. Tunajua serikali yetu imeoza na hakuna pa kupelekea malalamiko, TCRA yenyewe ndo hao wanaoenda shule na 2billion. Sasa kujikomboa dhidi ya hawa wezi ni kutupa smcard zao. Tunatangaza tarehe 08/11/2011 iwe ni siku ya kutokutumia laini za tigo. Zimekuwa ghali mno na ni wezi wa kutupwa. tafadhali sambaza ujumbe

mkuu ata kwenyekupiga wanakamua vibaya mno nipo kwenye mchakato wakuangalia mtandao unaofaa nihamie
 
TTCL wako wapi tuamie huko kizalendo?

TTCL ishakua kizee na wakati wake ushapita na ni njema kwangu 7bu waliringa sana enzi hizo kukuunganishia line ni kama tanesco sasa nao wakati wake ushapita
 
kuna theory kwenye Market inayoelezea Maisha ya bidhaa/huduma katika soko inajulikana kama PRODUCT LIFE CYCLE.Theory hii inaeleza namna product/service inavyozaliwa,inavyokuwa,inavyofikia ukomavu/uzee na hatimaye inavyoweza kupotea kwenye soko.Nahisi TiGO inaweza kujikuta inazeeka gafla na hatimaye kupotea ENDAPO Tu haitafanya jitihada mahususi kurudisha good image kwa customers wake.Nimeshuhudia malalamiko mengi sana katika huduma zake kwa wateja.Nimekwepo mikoa ya Mbeya,Iringa,Arusha na dar hapa malalamiko mengi yapo kwa wateja ambao ndiyo watumiaji wakubwa wa tigo na hasa wanachuo.Wengi sasa wanaline ya AIRTEL ukiwauliza kwanini unatumia line ya airtel atakwambia tigo w**zi.TIGO Mktng manager To loose one customer is likely to loose Millions of them.TAKE ACTION!
 
Mwenyewe since morning sijatumia line yao ya simu baada ya one day kulala nikiwa nimeacha sh 956 asubuhi nikakuta sh 232.wezi tu hawa,hawanaishu.
 
TCRA wako busy kufanya ufisadi kuwa mabillionea, tigo wanatunyofoa ngozi. jamani tuchukue hatua. Tunawaomba wataalam wa IT watengeneze email pamoja na mass SMS ili kususia huduma za tigo tarehe 15/11/2011. Hawa watu wezi sana. Sasa hivi ukiweka Tsh 10,000 kabla ya siku imeisha na hakuna simu yoyote ya maana unayopiga. Yaani hiyo ni tigo kwa tigo. Wazalendo wengine tusambaze huu ujumbe kwenye mitandao yote na social netowrks, tweeter na facebook. Siku moja tukiwaadhibu watasalimu amri.Tushirikiane. Ukiwa na namba yao, siku hiyo usijaze voucher wala kupiga simu kutumia TIGO. Next watakuwa ni Vodacom. Jamani sambazeni habari. Ukiwa na ndugu kijijini wataarifu, hawa ndo wasaliti wakubwa...hata JK wao ndo waliompigia Kura....Tarehe 15/11/2011 Sambaza ujumbe
 
tigo wanuzi sana-ukipiga hiyo namba 800800-hawapokei-na wanakata shs,50
yaani badala ya kukusaidia-wanazidi kukuongezea shida kwa kula salio lako pasipo msaada wowote
 
Back
Top Bottom