Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,268
- 33,041
Serikali ya Sweden imesaini mkataba wa kuipatia Serikali ya Tanzania Sh.bilioni 44 kwa ajili ya mradi wa usambazaji wa umeme vijijini.
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo jana na Serikali ya Sweden, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhani Khijjah, alisema msaada huo utasaidia kuondoa umaskini kwa wananchi vijijini pamoja na kuendeleza uchumi wao.
Alisema ni asilimia moja tu ya wananchi wa vijijini wanaofaidika na umeme unaozalishwa nchini.
Alisema lengo la msaada huo ambao umetolewa kupitia mfuko wa Uendelezaji wa Nishati ya Umeme Vijijini (Rea) ni kufanikisha Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini (Mkukuta) na kuendeleza Kilimo Kwanza sehemu za vijijini.
Khijjah alisema umeme huo utawezesha pia kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa ajili ya utengenezaji wa mazao ya wakulima vijijini pamoja na kuongeza ajira. Khijjah aliongeza kuwa uanzishwaji wa viwanda sehemu za vijijini utasaidia pia kuongeza thamani ya mazao.
Alisema malengo ya kufanikisha Kilimo Kwanza hayawezi kufikiwa endapo hakutakuwepo mpango madhubuti wa kufanikisha umeme vijijini na kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa wakulima. Aidha, alisema jambo kubwa ambalo limekuwa likichangia wakulima vijijini kutofikia maendeleo ni ukosefu wa umeme. Alisema mikoa 16 ya Tanzania bara ndio inatarajia kunufaika na mradi huo.
CHANZO: NIPASHE
Je Serikali itasambaza umeme vijijini? kama huo msaada Serikali ya Tanzania iliyopewa na Sweden? au ndio hizo pesa zitwafikia Mafisadi? Nawaombeni mnijibu Wakuu wenzangu.
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo jana na Serikali ya Sweden, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhani Khijjah, alisema msaada huo utasaidia kuondoa umaskini kwa wananchi vijijini pamoja na kuendeleza uchumi wao.
Alisema ni asilimia moja tu ya wananchi wa vijijini wanaofaidika na umeme unaozalishwa nchini.
Alisema lengo la msaada huo ambao umetolewa kupitia mfuko wa Uendelezaji wa Nishati ya Umeme Vijijini (Rea) ni kufanikisha Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini (Mkukuta) na kuendeleza Kilimo Kwanza sehemu za vijijini.
Khijjah alisema umeme huo utawezesha pia kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa ajili ya utengenezaji wa mazao ya wakulima vijijini pamoja na kuongeza ajira. Khijjah aliongeza kuwa uanzishwaji wa viwanda sehemu za vijijini utasaidia pia kuongeza thamani ya mazao.
Alisema malengo ya kufanikisha Kilimo Kwanza hayawezi kufikiwa endapo hakutakuwepo mpango madhubuti wa kufanikisha umeme vijijini na kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa wakulima. Aidha, alisema jambo kubwa ambalo limekuwa likichangia wakulima vijijini kutofikia maendeleo ni ukosefu wa umeme. Alisema mikoa 16 ya Tanzania bara ndio inatarajia kunufaika na mradi huo.
CHANZO: NIPASHE
Je Serikali itasambaza umeme vijijini? kama huo msaada Serikali ya Tanzania iliyopewa na Sweden? au ndio hizo pesa zitwafikia Mafisadi? Nawaombeni mnijibu Wakuu wenzangu.