Swali

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Wakuu mimi nina swali na nina uliza kwa kwa uzuri tu katika kufahamu zaidi nini kipo ndani ya mawazo, fikra na mioyo ya Watanzania. Chadema imetoka kupata washabiki wengi sana ndani na nje ya JF. Baadhi ya hawa mashabiki ni wanachama rasmi nikimaanisha wale wanao shikilia kadi za chama na kuna wale ambao wana support Chadema lakini si wanachama rasmi.

Swali langu haswa lina lengi supporters wa Chadema ambao si wanachama rasmi. Nieleweke kwamba sina neno na mtu kuwa mshabiki wa chama fulani bila kuwa mwanachama rasmi. Ni ukweli usiopingika kuwa nchi nyingi chaguzi hushindwa kwa kuvuta "independence" au wale wasio wanachama. Kwa maana mtu akishakua mwanachama huna haja ya kuuza sana sera za chama kwao kwani tayari wana zielewa na ni matumaini yangu wana ziishi.

Sasa swali langu ni je mashabiki wa Chadema ambao si wanachama bado wataendelea kuwa mashabiki pindi Chadema itakapo bahatika kushika madaraka? Je CCM ikisha anguka adui atakua nani? Je kama Chadema ikibahatika kushika madaraka na waka chemsha na wao kimbilio litakua lipi? Nauliza hivi kwa sababu kuna tofauti kati ya kuwa pro-Chadema na anti-CCM. Kuwa pro-Chadema ina maana wewe umeiva uana Chadema na upo nacho kwa hali yoyote. Kuwa anti-CCM ina maanisha wewe haufuati itikadi zozote bali lengo ni kuiona tu CCM ikiondoka na hata kesho kikitokea chama kingine cha upinzani chenye nguvu basi utahamia huko.

Nauliza swali kwa sababu ukweli utabaki pale pale kwamba katika vita yoyote kuna wale wanajeshi ambao unao tokea mwanzo na ambao wata pambana na wewe hata kama mnaelekea kushindwa vita. Na kuna wale watakao jiunga kwa kuangalia upande gani unashinda na wanakua na haraka sana kuhama pale vita inapoelekea kuelemea kwa upande wa pili.

Natambua wengi watashambulia hii mada kiunafiki kwa kutaka kuonekana kweli wana mapenzi ya dhati na Chadema na kwamba wao ni wana Chadema damu damu. Wapo wale wanachadema halisi ambao watakuja juu na nita waelewa. Lakini pia wapo wale ambao watakejeli mioyoni wakijua fika wao ni wanafiki wanaofuata tu upepo unapo kwenda. Nia ni kuamsha hisia za watu na kupima mawazo ya Watanzania wenzangu.
 
Mh very thought provoking. Naamini hapa utapata majibu mengi ya hasira japo ni kweli siyo kila anaesema ana mapenzi ya dhati ni kweli anayo mapenzi ya dhati. Haswa humu ndani ya JF ni rahisi sana mtu mwenye jina feki kujidai ni mshabiki lakini akitoka humu ndani anakua kimya.
 
As for me sina haja ya kuwa mwanachama wa chama chochote, kwanza haina maana ni kupoteza fedha yangu kulipia kadi wakati tayari wanakula ruzuku kutokana na kodi ninayokatwa. Na kwa hali ya sisi ni maana ya kuwa na wanachama? labda kama unataka kugombea uongozi kwenye hicho chama ni sawa lakini vingenevyo ni bora kukaa pembeni na kuwa mshabiki tu.

Watu wengi si kwamba wanaipenda sana Chadema, bali wamechoshwa na usanii wa CCM ndio wanaona labda Chadema inaweza wasogeza mbali. Hivyo kama Chadema nao wakiingia na kufanya kama wanavyofanya CCM dawa ni ile ile, piga chini angalia wengine wanaoweza kutupeleka and may be by that time CCM watakuwa wameshajifunza kinaweza tena kuwa chama kizuri!!
 
As for me sina haja ya kuwa mwanachama wa chama chochote, kwanza haina maana ni kupoteza fedha yangu kulipia kadi wakati tayari wanakula ruzuku kutokana na kodi ninayokatwa. Na kwa hali ya sisi ni maana ya kuwa na wanachama? labda kama unataka kugombea uongozi kwenye hicho chama ni sawa lakini vingenevyo ni bora kukaa pembeni na kuwa mshabiki tu.

Watu wengi si kwamba wanaipenda sana Chadema, bali wamechoshwa na usanii wa CCM ndio wanaona labda Chadema inaweza wasogeza mbali. Hivyo kama Chadema nao wakiingia na kufanya kama wanavyofanya CCM dawa ni ile ile, piga chini angalia wengine wanaoweza kutupeleka and may be by that time CCM watakuwa wameshajifunza kinaweza tena kuwa chama kizuri!!

Ni kweli mkuu si lazima uwe mwanachama. Ila unaweza ukawa mshabiki ila mwenye mapenzi ya kweli. Mfano ni mtu uwe shabiki wa Simba. Unaweza usiwe mwanachama ila unaipenda timu na siku zote upo nae aidha iwe juu au iwe chini. Ndicho haswa mimi ninacho ongelea.

Na unacho sema kwamba si kwamba wanaipenda Chadema bali wamechoshwa na CCM ina maana lengo kubwa haswa la watu ni CCM ijirekebisha kwa hiyo ikisha fanya hivyo Chadema itasahaulika?
 
hatushabikii uanachama wa chama flani bali tunakubali chama kinachotetea maslahi ya watanzania sio maslahi ya 10%...kwa sasa mimi naona cdm ndio chama pekee kinachojua watanzania maskini wanataka nini sio hawa mafisadi wa magamba..
 
hatushabikii uanachama wa chama flani bali tunakubali chama kinachotetea maslahi ya watanzania sio maslahi ya 10%...kwa sasa mimi naona cdm ndio chama pekee kinachojua watanzania maskini wanataka nini sio hawa mafisadi wa magamba..

Mkuu naona ni bora kuongea kwa niaba yako mwenyewe kuliko kuzungumzia wengine. Ukisema "hatu" ina maana una assume wote wengine wana mawazo kama yako kitu ambacho tuna weza kukubaliana siyo kweli.

Hapa mkuu nitakubaliana na wewe kwani umezungumza wewe kama wewe. Kama ndiyo nia yako ya kuipa support Chadema hapa lazima nikubaliana na wewe kwa asilimia mia. Siku zote maslahi ya Watanzania lazima yawekwe mbele ya makundi binafsi.
 
Ni kweli mkuu si lazima uwe mwanachama. Ila unaweza ukawa mshabiki ila mwenye mapenzi ya kweli. Mfano ni mtu uwe shabiki wa Simba. Unaweza usiwe mwanachama ila unaipenda timu na siku zote upo nae aidha iwe juu au iwe chini. Ndicho haswa mimi ninacho ongelea.

Na unacho sema kwamba si kwamba wanaipenda Chadema bali wamechoshwa na CCM ina maana lengo kubwa haswa la watu ni CCM ijirekebisha kwa hiyo ikisha fanya hivyo Chadema itasahaulika?

Lengo kubwa la watanzania ni kuboreshwa kwa maslahi ya maisha na maendeleo ya nchi yetu iwe kupitia Chadema, CCM, NCCR, PPPT n.k. Lakini kwa hali halisi ya sasa, CCM haiwezi kujirekebisha bila kwanza kupigwa chini vinginevyo ni kujidanganya. Maana mle wamejificha watu wenye "madhambi" na madudu kibao na ili waendelee kuwa salama ni lazima waendelee kufanya madhambi mengine waweze kujilinda.

Alisema mwalimu Nyerere CCM imekuwa chaka ambalo watu wenye madudu yao wanakimbilia kujificha ili mambo yao yaende sawa, na hawa watu hawatakubali watolewe peupe ili wahukumiwe, wenyewe mnaita magamba. Kiukweli zaidi ya asilimia 80 ya viongozi ndani ya CCM ni magamba, angalia mfano tu rahisi jinsi wabunge wa CCM wanavyosema Polisi kuuua raia Arusha, Tarime etc ni sawa!! Kweli mtu mwenye akili anaweza kushabikia kitu kama hiki?
 
Nimefuatilia post yako na naona umetaja tu Chadema..inamaana chadema ndicho chama pekee cha upinzani TZ?
Chadema hii hii nayoijua ya Ubinafsi, majigamo, utemi, ukabila, udini na utabaka,kwa mawazo yako chama kama hiki kitakaa kipate majority support na kiongoze nchi?
 
Lengo kubwa la watanzania ni kuboreshwa kwa maslahi ya maisha na maendeleo ya nchi yetu iwe kupitia Chadema, CCM, NCCR, PPPT n.k. Lakini kwa hali halisi ya sasa, CCM haiwezi kujirekebisha bila kwanza kupigwa chini vinginevyo ni kujidanganya. Maana mle wamejificha watu wenye "madhambi" na madudu kibao na ili waendelee kuwa salama ni lazima waendelee kufanya madhambi mengine waweze kujilinda.

Alisema mwalimu Nyerere CCM imekuwa chaka ambalo watu wenye madudu yao wanakimbilia kujificha ili mambo yao yaende sawa, na hawa watu hawatakubali watolewe peupe ili wahukumiwe, wenyewe mnaita magamba. Kiukweli zaidi ya asilimia 80 ya viongozi ndani ya CCM ni magamba, angalia mfano tu rahisi jinsi wabunge wa CCM wanavyosema Polisi kuuua raia Arusha, Tarime etc ni sawa!! Kweli mtu mwenye akili anaweza kushabikia kitu kama hiki?

Kweli mkuu nakubaliana na wewe. Ili Tanzania kuwa na demokrasia halisi ya vyama vingi ni lazima chama kilicho kaa madarakani tangia uhuru kianguke. Hii itajenga utamaduni wa kupokezana madaraka kati ya vyama na vyama na pia itajenga nidhamu ya vyama kuheshimu wananchi kwani wanajua hawawezi kufanya upumbavu wowote tu na waendelee kufaiidi madaraka. Kwa sasa kiburi kikubwa cha CCM ni kwamba bado hakuna ile kuamini kwamba ipo siku wanaweza angushwa.
 
nadhani nami pia naangukia kwenye kundi la wanaotaka mabadiliko.i admit few weeks ago nimechukua kadi ya chadema,lakini baada ya kufikiria kuwa maybe kuna siku nitaihitaji nitakapoamua ku-koki hii bunduki. japokuwa for the past 2 yrs nimekuwa niki-contribute here and there kwa chama. ninachotaka mimi ni badiliko na uwajibikaji. obviliously ccm imeshindwa kunipa ninachotaka, hopefully chadema can. ila na chadema pia ikishindwa, wala sitaona aibu kuitaliki! unakumbuka excitement iliyokuja na ccj? lakini baada ya kuonekana ccj haikidhi kiu ya wengi,well.. niseme kuwa chadema imeweza kuleta matumaini kiasi hichi hata kwa wanachama wa ccm pia. ndo maana hata kwenye uchaguzi kuna majimbo yalichagua mbunge wa chadema na rais wa ccm and vice versa. so kuwa mwanachama ama kutokuwa haina uhusiano directly na kuwa na imani na chadema.
 
Nimefuatilia post yako na naona umetaja tu Chadema..inamaana chadema ndicho chama pekee cha upinzani TZ?
Chadema hii hii nayoijua ya Ubinafsi, majigamo, utemi, ukabila, udini na utabaka,kwa mawazo yako chama kama hiki kitakaa kipate majority support na kiongoze nchi?

Mkuu ukisoma thread yangu vizuri utaona nimetumia neno "kama" kwa maana ni assumption ila hamna sehemu nilipo sema kwamba Chadema kitashika madaraka wala sehemu niliyo sema kwamba mimi binafsi naamini watakuja kushika madaraka.

Sababu ya kukitaja Chadema tu na siyo vyama vingine ni kwamba pamoja na ikitadi zangu za kisiasa na maoni yangu binafsi ni lazima nikubali kwamba Chadema ndicho chama pekee cha upinzani ambacho kina sikika kwa sasa. Nani anaongelea CUF (ukiacha linapo kuja swala la Zanzibar), nani anaongelea TLP, nani anaongelea UDP?

Nadhani ufafanuzi huu utakua umekusaidia kidogo kuelewa nini haswa madhumuni ya mimi kuandika kama nilivyo andika.
 
Kweli mkuu nakubaliana na wewe. Ili Tanzania kuwa na demokrasia halisi ya vyama vingi ni lazima chama kilicho kaa madarakani tangia uhuru kianguke. Hii itajenga utamaduni wa kupokezana madaraka kati ya vyama na vyama na pia itajenga nidhamu ya vyama kuheshimu wananchi kwani wanajua hawawezi kufanya upumbavu wowote tu na waendelee kufaiidi madaraka. Kwa sasa kiburi kikubwa cha CCM ni kwamba bado hakuna ile kuamini kwamba ipo siku wanaweza angushwa.

Inabidi ifike wakati tuwe kama Marekani au Uingereza, chama kinapewa nafasi ya kuongoza kutokana na sera zake then kikishindwa kutekeleza uchaguzi unaofuata kinawekwa pembeni wanapewa wengine. Lakini hii itahitaji tubadilishe Katiba yetu ile watu kama Wakuu wa Mikoa na Wilaya aidha waondolewe maana ni Makada wa vyama au wawe civil servants ambao hawaruhusiwi kuwa wanachama wa vyama vya siasa, maana hawa ndio wanatumika hasa na serikali ya CCM kuua demokrasia nchini.
 

Sasa swali langu ni je mashabiki wa Chadema ambao si wanachama bado wataendelea kuwa mashabiki pindi Chadema itakapo bahatika kushika madaraka? Je CCM ikisha anguka adui atakua nani?
kama mmoja wa wataka mabadilko ndani ya mwaka wakishika madaraka naweza kujua kama nao CDM watakuwa adui. na vigezo ni hivyo hivyo vinavyofanya CCM iwe adui leo.Binafsi sitegemei chama chochote kitachoiangusha CCM ifanye miujiza miaka ya mwanzo. Kazi kubwa itakuwa ni clear mess ya CCM kuweka mfumo na utaritibu itayochochea utawala wa sheria moja kwa wote. utengansha Utendajina siasa ( Eg TAKUKURU, Polisi)


Je kama Chadema ikibahatika kushika madaraka na waka chemsha na wao kimbilio litakua lipi?........
Enheee si unaona CCM inajipanga na kureform ikiwa madarakani. CCM itakuwa reformed vizuri na tarudi kuwa chama izuri kikikaa nje ya system japo kwa miaka mitano au kumi . Jibu hapa kimbilio laweza kuwa tena CCM au chama kingine chocote inategema na wakati hou hali itakuwaje. Haya mambo hayako static. But ni ukweli ulio wazi CCM ikiwekwa bench basi itazaliwa upya na itakuja ile CCM ya wananchi.


Nauliza hivi kwa sababu kuna tofauti kati ya kuwa pro-Chadema na anti-CCM. Kuwa pro-Chadema ina maana wewe umeiva uana Chadema na upo nacho kwa hali yoyote. Kuwa anti-CCM ina maanisha wewe haufuati itikadi zozote bali lengo ni kuiona tu CCM ikiondoka na hata kesho kikitokea chama kingine cha upinzani chenye nguvu basi utahamia huko........

Mimi kwa sasa ni Anti CCM na option ya kwanza mbadala ya kwa sasa ni CDM Kwa maana nyingine kwangu kama CDM isigeuwepo basi ningeunga mkono CUF, NCCR aau TLP . Ilimradi CCM ikae bench ijipange vizuri. Simply CCM imekimbia marathon muda mrefu inahitaji kupumzika.
 
nadhani nami pia naangukia kwenye kundi la wanaotaka mabadiliko.i admit few weeks ago nimechukua kadi ya chadema,lakini baada ya kufikiria kuwa maybe kuna siku nitaihitaji nitakapoamua ku-koki hii bunduki. japokuwa for the past 2 yrs nimekuwa niki-contribute here and there kwa chama. ninachotaka mimi ni badiliko na uwajibikaji. obviliously ccm imeshindwa kunipa ninachotaka, hopefully chadema can. ila na chadema pia ikishindwa, wala sitaona aibu kuitaliki! unakumbuka excitement iliyokuja na ccj? lakini baada ya kuonekana ccj haikidhi kiu ya wengi,well.. niseme kuwa chadema imeweza kuleta matumaini kiasi hichi hata kwa wanachama wa ccm pia. ndo maana hata kwenye uchaguzi kuna majimbo yalichagua mbunge wa chadema na rais wa ccm and vice versa. so kuwa mwanachama ama kutokuwa haina uhusiano directly na kuwa na imani na chadema.

Ila mkuu mabadiliko ya kweli huoni yataletwa na chama kitakacho leta changamoto haswa na si nguvu ya soda tu? Tuliona NCCR mwaka 1995, tukaona na CUF mwaka 2000 kisha ikaja zamu ya Chadema 2010. Historia inaonyesha kwamba kwenye siasa za Tanzania vyama vya upinzani vina muda mfupi sana wa umaarufu na katika muda huo hamna mabadiliko ya kweli yaliyo letwa.

Sisemi Chadema nayo itaangukia kwenye kundi hilo hilo la historia la hasha. Ila Watanzania wana hitaji chama kitakacho kuwa a force to be reckoned with na siyo mbu atakae nga'ta kidogo na kusababisha muasho lakini mwisho wa siku hamna kikubwa kilicho tendeka. Kama CCM bado inashinda uraisi ni kiashiria kwamba bado wananchi hawapo tayari kuona serikali inayo ongozwa na upinzani. Au could I be wrong?
 
Inabidi ifike wakati tuwe kama Marekani au Uingereza, chama kinapewa nafasi ya kuongoza kutokana na sera zake then kikishindwa kutekeleza uchaguzi unaofuata kinawekwa pembeni wanapewa wengine. Lakini hii itahitaji tubadilishe Katiba yetu ile watu kama Wakuu wa Mikoa na Wilaya aidha waondolewe maana ni Makada wa vyama au wawe civil servants ambao hawaruhusiwi kuwa wanachama wa vyama vya siasa, maana hawa ndio wanatumika hasa na serikali ya CCM kuua demokrasia nchini.

Ila katiba mpya itaandikwa na nani mkuu kama siyo na chama chenye wabunge wengi bungeni? Je tunaweza kutegemea hiyo katiba mpya kweli iwe tofauti na ya sasa? Nani haswa akabidhiwe hili jukumu la kuandika katiba mpya?
 
Mkuu Mtazamaji,

Binafsi nilikua na mwalimu aliyekua ananiambia siku zote kwamba "If plan A comes come up with a plan B but ensure first that plan B is better than plan A". Sisemi mwalimu wangu alikua sahihi unaweza ukapingana nae. Ila alicho kua ana maanisha ni kwamba tusikimbilia kuchukua option ya pili kabla hatuja tafakari na kuona ni bora zaidi. Je Watanzania wame tafakari na kujiaminisha kwamba kweli Chadema ni tofauti na CCM na kweli kikipata madaraka kuna nafasi ya kuwa tofauti (siyo lazima kuleta mabadiliko makubwa) na CCM?

Cha pili ni kwamba muda si mrefu wazee wa CCM wenye makamo ya JK na kwenda juu karibia wata staafu au kuwa wachache. Je vijana wanao chipukia CCM wanaweza kutoa changamoto kwa kujionesha kuwa wao ni tofauti na "the old guard"?
 
Issue ni kwamba sasa tunataka mabadiliko. Everything too much is harmful. Sasa hivi wana magamba wanajiona ndio wana hati miliki na nchi hii. Wapishe hata wengine. Tumechoka na mawazo mgando
 
Mimi binafsi nina/tasapoti chochote kitakachoonyesha kuitoa ccm madarakani. Siyo tu Chadema, nccr, cuf, upd au tlp. Mimi hata jeshi likipindua serikali ya ccm nitaliunga mkono 100%.... Sababu yangu ni moja, TUKIWEZA KUITOA ccm MADARAKANI YEYOTE ATAKAYEKUJA AKIWA HOVYO TUTAKUWA NA UJASIRI WA KUMTOA.. So, mimi sina kadi ya chama chochote lakini nasaidia kile nachoona kwa wakati husika kina mwelekeo wa kuitoa au kuidhoofisha ccm. Na wakipotoka hawanioni.
 
Kaka MIMI ni Ant- Goverment sikuzote hata wakiwa CHADEMA/CUF/TLP n.k ,
Bado nitaendelea kuwa CRITIC wa Serekali kwanihakuna Serekali inayotenda haki duniani.
 
Mkuu Mtazamaji,

..............Ila alicho kua ana maanisha ni kwamba tusikimbilia kuchukua option ya pili kabla hatuja tafakari na kuona ni bora zaidi. Je Watanzania wame tafakari na kujiaminisha kwamba kweli Chadema ni tofauti na CCM na kweli kikipata madaraka kuna nafasi ya kuwa tofauti (siyo lazima kuleta mabadiliko makubwa) na CCM?


Inawezekana CDM wasiwe tofauti kiutendaji na na CCM lakini hatuwezi kujua mpaka CDM nao wawe kwenye nafasi ya maamuzi. Pil . Hiii CCM unaiyoiona sasa itakuwa bora zaidi hata ya CDM kama ikiwekwa pembeni. Kuhusu CDM au chama chochote kuleta mabadiliko wakipewa nafasi hilo sina shaka. Yanaweza kuwa mabadiliko mazuri sana au mabaya sana. Tatizo nadhani ni kipimo cha wananchi cha mabadiliko ni nini. Hii ni mada nyingine. Maana CDM inaweza isijenge hata KM moja ya rami lakini ikakomesha RUSHWa na ufisadi. Haya kwangu ni mafanikio na mabadiliko.

Wanaweza wasijenge shule za kata nyingi kama alizojenga CCM (Lowasa).lakini tukasikia hizo shule zilizojengwa na CCM wameziongezea ubora ( eg mitaala maabara, nk..)

CDM nikiona wanasema viongozi wao wote watatumia Saloon car kwa safafri za kikazo wawapo jijini kwangu ni mabadiliko.


Cha pili ni kwamba muda si mrefu wazee wa CCM wenye makamo ya JK na kwenda juu karibia wata staafu au kuwa wachache. Je vijana wanao chipukia CCM wanaweza kutoa changamoto kwa kujionesha kuwa wao ni tofauti na "the old guard"?

Mfano kijana gani ? watatoa changamoto gani? Kama una ijanana mwana CCM mwenye uweo wa kuleta mabadilio ya kweli basi kwa sasa yupo CDM NCCR au CUF . Huwezi ukamuona kijana wa CCM tofauti akiwa CCM. Kijana wa CCM akioneana ana changamoto basi changamoto yake ni kwa mtu fulani na sio mfumo.

Kuna vijana wa CCM wanatia moyo( Siwataji majina ) lakini tatizo lao hawaonekani kukoosa mfumo. wanawalenga watu fulani fulani. Sijaona kijana ambaye ana msukumo wa kutoa changamoto za kizalendo. Wengi wanacheza karata za Kisiasa.
 
Back
Top Bottom