Ni kweli makundi ya damu hubadilika?

lolypop

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
2,430
1,681
Wanajamii forum wenzangu naomba mnisaidie nipate kuelewa juu ya blood groups, kwamba.

(1) Mtoto anaweza kufanana blood group na wazazi wake au mtoto huzaliwa na group lake la damu tofauti na wazazi wake.

(2) Je blood group hubadilika?

Nauliza hili swali kwa sababu yupo sister mmoja ni mjamzito alipoenda clinic kupima damu aliambiwa apime tena blood group mana huwa zinabadilika.

Je hili ni kweli?Doctors msaada hapo.
 
Wanajamii forum wenzangu naomba mnisaidie nipate kuelewa juu ya blood groups, kwamba
(1) Mtoto anaweza kufanana blood group na wazazi wake au mtoto huzaliwa na group lake la damu tofauti na wazazi wake
(2) Je blood group hubadilika? nauliza hili swali kwa sababu yupo sister mmoja ni mjamzito alipoenda clinic kupima damu aliambiwa apime tena blood group mana huwa zinabadilika je hili ni kweli?
Doctors msaada hapo
 
ok, ok ok
mtu mwenye group A
maana yake anaweza akatoa O na A
mtu mwenye group B anaweza akatoa O na B
mtu mwenye AB anaweza akatoa B na A
mtu mwenye O anaweza akatoa O tu peke yake
sasa kwenye kuzaa mtoto
kila mzazi ana donate nusu kwa nusu
mfano baba ana group A mama ana group A pia
baba anaweza akatoa sperm yenye A au O
na mama anaweza akatoa yai lenye A au O
baba akitoa sperm A na mama akatoa yai A mtoto atakua na group A
baba akitoa sperm O na mama akatoa yai A mtoto atakua na A pia
baba akitoa O na mama akitoa O mtoto atakua O
cha muhimu hapa kujua ni kua wazazi wote wanachangia nusu kwa nusu kwenye blood group ya mtoto, na O ni wa kutawaliwa endapo ataungana na either B au A then unaaanza kuzichanganya ili kupata possible blood groups ya mtoto
so mtoto anaweza akawa na blood group tofauti na wazazi wake kutegemeana na combination iliyofanyika

blood group hazibadiliki, zipo kwenye genes kwa hiyo kubadilika kwa mtu huyo haiwezekani

hope umenielewa, kama una swali tena uliza
 
Mtoto akizaliwa hufanana blood group na wazaz wake mfano baba ni o na mama ni b yule Mtoto atachukua blood group moja kat ya o au b...
Blood group haibadilik kamwe.
 
Kuna types za Blood group A, B, AB, O.."Hazibadiliki"
Each biological parent donates one of their two ABO alleles to their child. A mother who is blood type O can only pass an O allele to her son or daughter. A father who is blood type AB could pass either an A or a B allele to his son or daughter.
 
ok, ok ok
mtu mwenye group A
maana yake anaweza akatoa O na A
mtu mwenye group B anaweza akatoa O na B
mtu mwenye AB anaweza akatoa B na A
mtu mwenye O anaweza akatoa O tu peke yake
sasa kwenye kuzaa mtoto
kila mzazi ana donate nusu kwa nusu
mfano baba ana group A mama ana group A pia
baba anaweza akatoa sperm yenye A au O
na mama anaweza akatoa yai lenye A au O
baba akitoa sperm A na mama akatoa yai A mtoto atakua na group A
baba akitoa sperm O na mama akatoa yai A mtoto atakua na A pia
baba akitoa O na mama akitoa O mtoto atakua O
cha muhimu hapa kujua ni kua wazazi wote wanachangia nusu kwa nusu kwenye blood group ya mtoto, na O ni wa kutawaliwa endapo ataungana na either B au A then unaaanza kuzichanganya ili kupata possible blood groups ya mtoto
so mtoto anaweza akawa na blood group tofauti na wazazi wake kutegemeana na combination iliyofanyika

blood group hazibadiliki, zipo kwenye genes kwa hiyo kubadilika kwa mtu huyo haiwezekani

hope umenielewa, kama una swali tena uliza
Asante sana real G, bado nina swali moja tu
(1) baba ana A naye mama ana AB lakini wamezaa mtoto mwenye blood group O+.
naumesema hapo A hutoa A na O, AB hutoa A na B.
Kama nimekuelewa O hutoka kwa baba na mama, sasa hapa inakuaje?
 
Asante sana real G, bado nina swali moja tu
(1) baba ana A naye mama ana AB lakini wamezaa mtoto mwenye blood group O+.
naumesema hapo A hutoa A na O, AB hutoa A na B.
Kama nimekuelewa O hutoka kwa baba na mama, sasa hapa inakuaje?
Kuna kitu kinachunguzwa hapa i guessss!
 
Asante sana real G, bado nina swali moja tu
(1) baba ana A naye mama ana AB lakini wamezaa mtoto mwenye blood group O+.
naumesema hapo A hutoa A na O, AB hutoa A na B.
Kama nimekuelewa O hutoka kwa baba na mama, sasa hapa inakuaje?
hapo kama nimekuelewa unamaanisha baba ana group A na mama ana AB halafu wakatoa mtoto mwenye O+ (ambayo ni aina ya O)
hapa naona haiwezekani,
kwa kua baba atachanga sperm yenye A au O na mama mwenye AB atatoa yai lenye A au B so tukichanganya hapa kupata possible blood groups za mtoto tutapata A, B na AB tu, hapa naona watakua wamekosea vipimo vya blood group ya mama au mtoto, maana hata mama angechepuka kwa sababu tayari ana AB asingeweza kutoa mtoto mwenye O kamwe
 
hapo kama nimekuelewa unamaanisha baba ana group A na mama ana AB halafu wakatoa mtoto mwenye O+ (ambayo ni aina ya O)
hapa naona haiwezekani,
kwa kua baba atachanga sperm yenye A au O na mama mwenye AB atatoa yai lenye A au B so tukichanganya hapa kupata possible blood groups za mtoto tutapata A, B na AB tu, hapa naona watakua wamekosea vipimo vya blood group ya mama au mtoto, maana hata mama angechepuka kwa sababu tayari ana AB asingeweza kutoa mtoto mwenye O kamwe
Asante sana kwa maelezo haya nimekuelewa ila kuna jambo limenisononesha sana...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom