Swali la Ugomvi: Serikali isiyo na "fedha" inaweza vipi kwenda vitani?

Mzee Mwanakijiji umesoma kitabu gani kuweza kucome up na hii argument. serious.
 
Mimi nadhani, Sakata la Malawi sijalielewa vema ndiyomaana nasita kidogo kuwalaumu, Kwasababu viongozi wetu wanatoa matamshi mazito yanayotisha.
 
Noana watu ameshindwa kuelewa, wamesema ikibidi tutaenda vitani. Mnajua maana ya ikibidi? Na kama unavamiwa na na eti huna pesa na inadidi uende vitani utakataa, acheni kupotosha kwani njia za majadiliano bado zinaendelea!
 
hawakutakiwa kuzungumzia masuala ya vita at all. Siyo katika hatua hii hata kikao cha kwanza cha "njia nyingine" hakijafanyika! Si wamepanga kukutana Augusti 20? so haraka yao ya nini?

RIGHT. Alafu kwa nini kauli nzito namna hii itolewe na mawiziri, eti hadi lowasa na yeye anajichomeka na kuelezea uwezo wa majeshi yetu? au mimi ndio sielewi chain of Command ilivyo. wen't MR President supposed to say if there were in need a need to say anything about our readness to deproy the armied forces? au wametake advantage ya Udhaifu wa rais?
 
Hilo andiko limekaa ki-fifth columnist.
No proud Tanzania will swallow that!
You may be.

Kaka nakubaliana na wewe 100%. Ki ukweli pamoja na heshima zoote za MMM, hili andiko lake halina mashiko kabisa, labda mtu ambae hawezi kung'amua kwa jicho la tatu. Siyo kila kitu arukie tu na kutoa maoni yake, hili andiko lake liko shallow sana, na halima mwangaza wowote kwa Taifa zaidi ya kupinga pinga tu!
 
Tujiulize Maswali Kabla Hatujasogea Mbele zaidi!! Hawa waliotangaza Vita wananafasi Yoyote Katika katiba hii ya zamani / soryy iliyopo sasa kutangaza Hayo? Au ndio Ile kusema kwa sasa Nchi haina Msemaji? / Amiri Jeshi Mkuu? Hadi watu wanamsemea tu?

mkuu hakuna aliye tangaza vita hata yule mwenye mamlaka ya kufanya hivyo,hakuna aliyetoa amri ya kwenda vitani,kwakua kuna amri ya kwenda vitani inatolewa kwa utaratibu wake,na kuna tangazo la vita dhidi ya nchi na adui wake nalo hutolewa kwa wakati wake,yote haya yana wakati na watu husika wayatoa.Kilichofanyika ni matamko tu ya nia ya kweli kama msimamo wa serikali dhid ya wavamizi.Hapa mvamizi inatakiwa apigwe kwanza then ndio mkakae mezani kusuruhishwa au mvamizi inatakiwa apigwe ndipo aende kushtak.unaposema sitaki mtu aingie shamban kwangu na ntalinda shamba langu kwa gharama yoyote haimanisha kuwa umetangaza vita,maana yake utampiga ikiwezekana kumkamata yule ambaye amekuvamia,ikitokea mkajibizana mapigano sasa ndio unatangaza rasmi vita,wakati unatangaza tayari kuna mambo kadha yameshafanyika ikiwa ni pamoja na amri ya kuingia vitani then unawatangazia wananchi kuwa unapigana kwa sababu fulan na lengo ni furan,
 
Kaka nakubaliana na wewe 100%. Ki ukweli pamoja na heshima zoote za MMM, hili andiko lake halina mashiko kabisa, labda mtu ambae hawezi kung'amua kwa jicho la tatu. Siyo kila kitu arukie tu na kutoa maoni yake, hili andiko lake liko shallow sana, na halima mwangaza wowote kwa Taifa zaidi ya kupinga pinga tu!

huyu mzee kachanganyikiwa,siunajua tena tembo akisifiwa sana!....kwanza mpaka sasa sijaamini kama yeye ndio kaandika haya
 
RIGHT. Alafu kwa nini kauli nzito namna hii itolewe na mawiziri, eti hadi lowasa na yeye anajichomeka na kuelezea uwezo wa majeshi yetu? au mimi ndio sielewi chain of Command ilivyo. wen't MR President supposed to say if there were in need a need to say anything about our readness to deproy the armied forces? au wametake advantage ya Udhaifu wa rais?

mkuu kueleza uwezo wa jeshi si kosa,wala aimanishi lowasa katangaza vita,wala haimanishi mawaziri wametoa amri ya vita,narudia hata wewe unaweza kusema lolote kwa kusifia jesh la nchi yako,ni kama yanga watambe kwa simba.walichokifanya bungeni ni hamasa na kutoa tamko la serikali juu ya msimamo na nia ya nchi bas.mpaka sasa hakuna aliyetoa amri walata tangazo la vita hata yule mwenye mamlaka ya kufanya hivyo.kifup MM kachemka
 
KT0183.jpg


Mara zote wakiulizwa kuhusu mambo mbalimbali wanasema 'hawana fedha' na kuwa serikali ni maskini. Tumeona migomo ya madaktari, walimu na tishio la migomo ya wafanyakazi. Tumeona jinsi ambavyo wamekuwa wakilalamika kila kukicha kuwa "serikali haina fedha" -sikiliza kwa makini majibu ya mawaziri Bungeni wanavyorudia suala hili. Wanasema "serikali ikiwa na uwezo" au "tunaendelea kutafua fedha kwa ajili ya mradi huo; tena za ndani na za 'washirika wa maendeleo'".

Kila ukiwauliza mengi ambayo hayaendi vizuri jibu lao ni "serikali yetu haina fedha" au "hali ngumu". Sasa leo hii serikali hii hii ambayo "haina uwezo" inadai ati iko tayari kwenda vitani. Wale ambao tulikuwepo wakati wa vita vya Uganda tunakumbuka gharama kubwa (great toll) ya vita ile kwa maisha ya wananchi hadi vijijini. Hakuna ambaye kwa namna yake hakusikia maumivu (pinch) ya vita. Na vita ilipokwisha gharama yake kwenye uchumi wetu na maendeleo ya watu wetu haikuweza kurudishwa kwa urahisi. Kwa karibu miaka minne (miwili ya vita na ile ya reconstruction) ilisababisha nchi yetu kurudi nyuma zaidi ya ilipokuwepo. Ni kweli tulishinda vita lakini kwa gharama kubwa sana siyo tu ya fedha bali pia ya watu.

Kwa wanaokumbuka historia ya Uganda mojawapo ya matukio ya vita ni vita ya kuichukua Lukuya (Battle of Lukuya) ni hapa kiasi cha wanajeshi wetu kiliposhtukizwa na wanajeshi mamluki wa Libya na kujikuta kinarudishwa nyuma kabla ya Brigedi ya 201 na 208 kujipanga upya na kuwashambulia mamluki hao na kuwashinda na kusafisha njia ya kwenda Kampala (baada ya kuchukua Entebbe na Jinja). Gharama ya fedha tu serikali ya Museveni ndio iliweza kuilipa Tanzania mwaka 2007! Ikumbukwe kuwa vita ya Uganda inakadiriwa kuigharimu Tanzania dola milioni 1 kwa siku na hizo zilitoka mifukoni mwetu (hatukuwa na wajomba). Leo hii tumepiga kelele kulipa dola laki moja kwa Symbion kwa siku. Fikiria Wamarekani kwenye vita ya Iraq walikuwa wanaunguza dola bilioni 1 kwa siku!

Nikiangalia hali hiyo najiuliza; hivi kweli kina Lowassa na wengine wanaoshabikia vita wanafikiria kweli gharama yake? Hivi kuna mtu amewahi kuuliza Tanzania ilipoteza askari wangapi vita ya Uganda? Hivi watu wanajua kuwa ili jeshi letu liende vitani ni lazima wale wote waliokuwa reserve nao wawe reactivated? Yaani kabla ya kwenda Vitani itabidi kwanza tuongeze askari wote kutoka kama 30,000 waliopo sasa hivi na kufikia angalau 150,000 hivi kuweza kushinda vita. Hawa tutakaowachukua wengi ndio wasomi wenyewe na wafanyakazi maofisini watabadilishwa na nani? Ikumbukwe kwenye vita ya Uganda hawakwenda JWTZ tu bali Mgambo, Polisi, Magereza na wale waliopewa mafunzo ya haraka haraka. Je tuko tayari kuleta "draft" ya kulazimisha wanaume wote wenye miaka 18 na zaidi kuingia kambini? au watu wanafikiria ni "JWTZ" ndio litaenda vitani wakati wengine tunacheza ping pong na kuchat kwenye JF juu ya maendeleo ya vita?

Ninachopinga kabisa na ninaona ni mambo ya hatari ni kuzungumzia masuala ya vita bila kuonesha fikara na hekima. Kabla haujaamua kwenda vitani jipe nguvu kwanza. Na hakuna nguvu kubwa zaidi kama nguvu ya kiuchumi. Lakini jambo jingine ambalo labda wengine wameshafikiria ni vikosi vyetu vitakula nini? Au watu wanafikiria wanajeshi wakienda vitani wanapewa zile ration tu? Pamoja na gharama nyingine zote je bado tutaweza kulilisha taifa letu wakati wa vita? Wapo ambao hawajui kuwa njaa ya mwanzoni mwa miaka ya 1980 sehemu kubwa pia ni matokeo ya vita ya Uganda? Je tuko tayari kula dona na yanga tena na kurudishwa kwenye ration kwa taifa zima na mambo yale ya duka la kaya? au watu wanafikiria wataendelea kula nyama choma jioni wakati vita inaendelea?

Tusianze kupiga ngoma za vita (we shouldn't beat the drums of war) kama hatuko tayari kuingia vitani. Ni uzembe na reckless na binafsi naamini viongozi wote watatu (Lowassa, Membe na Sitta) wanatia shaka kama wana hekima na busara ya kuwa viongozi wa taifa letu. Kiongozi hata mwenye uwezo kiasi gani ni lazima asite linapokuja suala la vita na siyo kusita kwa sababu ya woga lakini kusita kwa sababu ya kujua analiita taifa lake kufanya nini. Na anapozungumza vita awe na uhakika kabisa (absolute confidence) kuwa hakukuwa na njia nyingine yoyote ya kuepuka vita hiyo.

Kwa mara nyingine nawasihi watu wanaoshabikia vita kama njia ya "kulinda mipaka yetu" wafikirie kwa hekima kuwa zipo njia nyingine nyingi zaidi za kufanya hivyo ikiwemo mazungumzo na mashtaka kwenye mahakama ya kimataifa. NI LAZIMA TUMALIZE NJIA ZOTE ZA AMANI (siyo mazungumzo tu) kabla hatujasema "we have had enough, we are preparing for war) na binafsi naamini kama tutaonesha hekima ya kutumia njia zote na busara ya kuepuka vita siku ikiitwa vita kweli kabisa tunaweza kwenda siyo kujihami tu bali kuiona Malawi kama tishio na kuanzisha an offensive assault ili kuliondoa tishio hilo mara moja na daima.

Nashauri vichwa vilivyotulia vizungumza lugha ya amani sasa hivi na kutuliza hizi ngoma za vita na mbiu za mapigano. Maana kama sasa hivi tu wanahangaika kulipa mishahara na kulisha taifa letu, sijui itakuwaje WAKATI WA VITA!


MMM


Umeshamsikia Mr. Lowassa akisema tutakopa per our GAS deposits kwasababu Mpaka sasa ni sawa na

$ trillioni 240.00 na bado zinapatikana zaidi...

Wewe Mpaka IMF imaidhinisha mkopo kwa Tanzania wa $ 230.00 uko kabatini wakati wowote serikali ya

Tanzania ikataka inaupata; wakati Spaina, Greece, Malawi, Italy lazima waende kwenye chungu kinachouma sana

cha Austerity. Tanzinaania sasa hivi ni Uongozi Mbovu iko juu haswa... na pembeni ina URANIUM kibao sio Masikini

Masikini ni haoooo itakopigana nao MALAWI... Jeshi zima la MALAWI ni 5,600 la Tanzania 27,000...
 
Nadhani hukuwasikia vizuri viongozi we2. Wamesema kama itabidi kufika huko itabidi kuingia vitani. Sasa jiulize kama hizo njia zingine zimeshindikana unatemegea tukae kimya? Kuwa Mzalendo wewe.

Hao wazalendo unaowaona wewe ndo hao wanaotangaza vita vya kumpiga Malawi kwa sababu ya ziwa?? mbona hao hao wameshindwa vita vya ufisadi wanajiumauma tu na kuinamisha nyuso chini kila wakiguswa??? mabilioni ya uswisi yaliyosemwa juzi kati ulimuona kidume gani ambaye alionesha DHATI kuyafuatilia???? Jamani watanzania tuweni makini na hawa kina EL, kwanza basi tu kwa sababu watanzania tumefungwa na blanket fulani hivi machoni na nyoyoni kiasi tunashinwa hata kuona na kufikiria mambo ya msingi mchana kweupe.

Ilitakiwa mpaka sasa tuwe tumeshaanza kuchapana VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE HAPA NCHINI KATI YA WANANCHI NA MAFISADI. POTELEA MBALI. LIWALO NA LIWE
 
Akamatwe kwa kosa lipi? Wa kututangazia nchi iko tayari kwa lolote ni Sitta au Lowasa? Waambie wanaSIASA wetu wasilikuze suala hili kwa malengo yao kijinga.

Mimi ni kunguru mwoga, ningependa kukimbiza mabawa yangu. Mimi kwa hii issue kimyaa,.... nawasikiliza wenyewe watakavyoamua, ila si kuendelea kujadili katika forum kama hii!
 
Noana watu ameshindwa kuelewa, wamesema ikibidi tutaenda vitani. Mnajua maana ya ikibidi? Na kama unavamiwa na na eti huna pesa na inadidi uende vitani utakataa, acheni kupotosha kwani njia za majadiliano bado zinaendelea!

yule mama anapigwa ndani ya masaa kadhaa na hata pata nafasi ya kutoroka tutamshika kama kuku na kuwaletea hapa nyumban
 
Mimi ni kunguru mwoga, ningependa kukimbiza mabawa yangu. Mimi kwa hii issue kimyaa,.... nawasikiliza wenyewe watakavyoamua, ila si kuendelea kujadili katika forum kama hii!

kunawatu wanapiga kelele hapa wala hawajui lolote
 
mkuu mmm definetly uko sahihi,kwa uchumi wa sasa wa tz wa kila kiongozi anawaza kujichotea kila
anachoona kiko karibu yake,na kupiga kelele kuwa serikali haina pesa kwa kila jambo la muhimu, je
tunawezaje kuingiza nchi vitani ktk mazingira ya ufisadi uliokithiri?kitakachotokea hata pesa itakayotengwa
kwa ajili ya hiyo vita itachakachuliwa.ilivyo ni kwamba joyce banda amesoma udhaifu wa serikali yetu na
uongozi uliopo sasa.ili kuiponya nchi yetu tusithubutu kuingia vitani tuwaachie malawi ziwa lao.

nina mashaka kama wewe ni mtanzania.
 
Thaks mwanakijiji umetupa darasa tosha japo hawa malawi now wanazingua;binafsi siamin hata tukishinda hizo gas na oil zitanufaisha majority au tunaenda kupigania masrahi ya wachache?
 
Hao wazalendo unaowaona wewe ndo hao wanaotangaza vita vya kumpiga Malawi kwa sababu ya ziwa?? mbona hao hao wameshindwa vita vya ufisadi wanajiumauma tu na kuinamisha nyuso chini kila wakiguswa??? mabilioni ya uswisi yaliyosemwa juzi kati ulimuona kidume gani ambaye alionesha DHATI kuyafuatilia???? Jamani watanzania tuweni makini na hawa kina EL, kwanza basi tu kwa sababu watanzania tumefungwa na blanket fulani hivi machoni na nyoyoni kiasi tunashinwa hata kuona na kufikiria mambo ya msingi mchana kweupe.

Ilitakiwa mpaka sasa tuwe tumeshaanza kuchapana VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE HAPA NCHINI KATI YA WANANCHI NA MAFISADI. POTELEA MBALI. LIWALO NA LIWE

Ha ha haaa, ngoja nicheke kidogo, so, kwa sababu wameshindwa vita ya ufisadi ndo kama ni "lazina" kwenda kupigania 'ziwa' ndo tusipigane au kuwapinga Wamalawi? Jipambanue mzee!
 
Wa kwanza kukamatwa unatakiwa kuwa wewe,unaejifanya huujui au unataka kuficha ukweli ambao uko wazi
kwani inapotikea migomo ya madaktari na walimu na hali duni ya maisha ya watanzania Tanzania inakuwa yai
kwamba taarifa hazitfiki nje ya mipaka yetu? Na je udhaifu wa hii serikali ni siri kweli? Tuache kujifariji kwenye
ukweli tuambizane bwana.

Ni sawa, tuambizane ukweli wetu sisi, na si kila mtu dunia nzima. Asiye na ulazima wa kuyafahamu haya hakuna haja ya kumfahamisha! Si kila kinachojiri Tanzania kila mtu anatakiwa akijue
 
Kaka nakubaliana na wewe 100%. Ki ukweli pamoja na heshima zoote za MMM, hili andiko lake halina mashiko kabisa, labda mtu ambae hawezi kung'amua kwa jicho la tatu. Siyo kila kitu arukie tu na kutoa maoni yake, hili andiko lake liko shallow sana, na halima mwangaza wowote kwa Taifa zaidi ya kupinga pinga tu!
Kweli kabisa mkuu!
When it comes to national pride, waandishi should be careful, they might be asked to fall on their own pen-swords!
 
Mzee Mwanakijiji,hawa watakopeshwa ama watapewa "msaada" wa silaha na fedha,military training etc.Inaingizwa kwenye bill tu,final payer ni mwananchi.Hivyo ni haki ya mwananchi kuuliza hiyo pesa itatoka wapi kwasababu ni yeye ama vizazi vijavyo watakaolipa.Na mara nyingi matatizo kama hayo ndo hupelekea kutubana wakati wa kusaini mikataba ya rasilimali za Taifa.
 
Back
Top Bottom