Swali la Ugomvi: Serikali isiyo na "fedha" inaweza vipi kwenda vitani?

Tanzania mpya yenye national spirit itapatikana kupitia Vita, cha kusikitisha ni kuwa Vita haitatokea sababu hao viongozi wenyewe hawapo tayari, maana ni wakati vita inaendelea huenda ukatokea uasi na vita nyingine ya ndani walengwa wakiwa ni wao na wote waliofaidika kupitia wao na mifumo yao mibovu waliyoiweka kwa makusudi.
Believe me, wanaimba ngonjera za vita lakini wao hawapo tayari kabisa, as you said si JWTZ pekee watakaopigana vita hii bali kila mtanzania kijana atahusika, hapo ndipo panawaumiza vichwa...maana kila penye keki ya taifa walitanguliza familia zao, marafiki, ndugu, mahawala mbele na maslahi binafsi yao binafsi....Je undhani watakuwa tayari kuwatanguliza mbele kwenda vitani?? Forget kabisa???
Nadhani turudi sasa kwenye ile mijadala mingine kama ile ya wanakamati wa kamati za bunge kujihusisha kuchukua rushwa n.k hili halijafika wala halitafika kwenye conclusions wanazoziimba....Malawi wenyewe mkononi wameshika Heligoland Treaty, wakati sisi tunahangaika kutafuta silaha zilipo...very funny.
 
Nikiangalia hali hiyo najiuliza; hivi kweli kina Lowassa na wengine wanaoshabikia vita wanafikiria kweli gharama yake? Hivi kuna mtu amewahi kuuliza Tanzania ilipoteza askari wangapi vita ya Uganda? Hivi watu wanajua kuwa ili jeshi letu liende vitani ni lazima wale wote waliokuwa reserve nao wawe reactivated? Yaani kabla ya kwenda Vitani itabidi kwanza tuongeze askari wote kutoka kama 30,000 waliopo sasa hivi na kufikia angalau 150,000 hivi kuweza kushinda vita. Hawa tutakaowachukua wengi ndio wasomi wenyewe na wafanyakazi maofisini watabadilishwa na nani? Ikumbukwe kwenye vita ya Uganda hawakwenda JWTZ tu bali Mgambo, Polisi, Magereza na wale waliopewa mafunzo ya haraka haraka. Je tuko tayari kuleta "draft" ya kulazimisha wanaume wote wenye miaka 18 na zaidi kuingia kambini? au watu wanafikiria ni "JWTZ" ndio litaenda vitani wakati wengine tunacheza ping pong na kuchat kwenye JF juu ya maendeleo ya vita?

Ninachopinga kabisa na ninaona ni mambo ya hatari ni kuzungumzia masuala ya vita bila kuonesha fikara na hekima. Kabla haujaamua kwenda vitani jipe nguvu kwanza. Na hakuna nguvu kubwa zaidi kama nguvu ya kiuchumi.

...................

Tusianze kupiga ngoma za vita (we shouldn't beat the drums of war) kama hatuko tayari kuingia vitani. Ni uzembe na reckless na binafsi naamini viongozi wote watatu (Lowassa, Membe na Sitta) wanatia shaka kama wana hekima na busara ya kuwa viongozi wa taifa letu. Kiongozi hata mwenye uwezo kiasi gani ni lazima asite linapokuja suala la vita na siyo kusita kwa sababu ya woga lakini kusita kwa sababu ya kujua analiita taifa lake kufanya nini. Na anapozungumza vita awe na uhakika kabisa (absolute confidence) kuwa hakukuwa na njia nyingine yoyote ya kuepuka vita hiyo.

Mkuu Mwanakijiji, nakubaliana na wewe kuwa vita wakati wowote ule ni mbaya kwa jamii.
Ni mbaya kwa elimu, mbaya kwa hospitali, mbaya kwa maendeleo, ni mbaya mbaya mbaya!

Lakini inabidi tujiulize kitu kimoja , mtu akikukalia utosini utamwacha kwa vile hupendi kupigana?
Uchezewe chezewe tu kwa vile we mpole na hutaki vita?

Gharama ya kudharauliwa ni mbaya zaidi kimataifa na inabidimajirani waelewe hivyo.
Tuna miaka mingi sana kuanzia Kenya,Uganda,Burundi,Congo,Zambia, hiyo Malawi na hata Msumbiji.

Hili swala la mpaka wa Malawi halikuanza leo, bali mara tu baada ya uhuru, na utata wake si mgeni.
Mwalimu alipeleka vikosi huko ku-assert position ya Tanzania miaka ya nyuma, na Malawi wanaliewa hilo.

Sitta, Membe na Lowassa wamefanya vema kuikumbusha Malawi kwamba Tanzania tupo na wasijichukulie sheria mkononi katika suala ambalo hatujakubaliana.

Kwamba Malawi wameuza vitalu vya ku explore mafuta/gesi katika sehemu ambayo ndiyo tunagombea ni dalili ya DHARAU.

Nchi haidharauliwi kirahisi namna hiyo.
 
Kingine kilichonitatiza mimi ni pale kila mtu alionekana kama vile ni AMIRI JESHI MKUU wa majeshi yetu:-
-Alianza Samwel Sitta alipokuwa akikaimu kama kiongozi wa shughuli za serikali Bungeni;
-Akaja Membe, Waziri wa Mambo ya Nje;
-Lowasa ndiye akafunga kazi kabisa. Akasema Jeshi liko tayari kiakili, kivifaa,...
Hawa wote watatu ndio tunaoambiwa wanauwania huu uamirijeshi mwaka 2015. Wangesubiri waupate kwanza kuliko kumdhalilisha Amiri Jeshi Mkuu aliyepo sasa. Vita ya Kagera aliitangaza Mwalimu mwenyewe ingawa walikuwepo watu kwenye nafasi hizo walipo akina Sitta, Membe na Lowasa. Huu pia ni uvunjaji wa makusudi wa katiba yetu ya JMT.
 
Mzee Mwanakijiji huwa nakueshimu sana lakini leo umeongea pumba.Taaluma yako ya uandishi wa makala huishie huko huko.Wala hujui lolote juu ya Jeshi na hasa JWTZ,wala hujui hasa chanzo kilichokuwepo cha vita kati ya TZ na UGANDA,sanasana utaeleza ni mipaka lakini chanzo hadi kuwa mipaka ilikua nini hujui unaishia kubwabwaja.Labda ni kwambie jambo la msingi,kama mnatuchokoza mkazania hatutaweza kufanya lolote eti hatuna hela,tayari mmefeli vita,kwa taalifa tutawapiga ndani ya dk 30,naongea kama mmoja wa JWTZ,we kaongelee kwenxe magazeti mi ntaongea kwa vitendo,subiri utaniambia
 
Last edited by a moderator:
KT0183.jpg


Mara zote wakiulizwa kuhusu mambo mbalimbali wanasema 'hawana fedha' na kuwa serikali ni maskini. Tumeona migomo ya madaktari, walimu na tishio la migomo ya wafanyakazi. Tumeona jinsi ambavyo wamekuwa wakilalamika kila kukicha kuwa "serikali haina fedha" -sikiliza kwa makini majibu ya mawaziri Bungeni wanavyorudia suala hili. Wanasema "serikali ikiwa na uwezo" au "tunaendelea kutafua fedha kwa ajili ya mradi huo; tena za ndani na za 'washirika wa maendeleo'".

Kila ukiwauliza mengi ambayo hayaendi vizuri jibu lao ni "serikali yetu haina fedha" au "hali ngumu". Sasa leo hii serikali hii hii ambayo "haina uwezo" inadai ati iko tayari kwenda vitani. Wale ambao tulikuwepo wakati wa vita vya Uganda tunakumbuka gharama kubwa (great toll) ya vita ile kwa maisha ya wananchi hadi vijijini. Hakuna ambaye kwa namna yake hakusikia maumivu (pinch) ya vita. Na vita ilipokwisha gharama yake kwenye uchumi wetu na maendeleo ya watu wetu haikuweza kurudishwa kwa urahisi. Kwa karibu miaka minne (miwili ya vita na ile ya reconstruction) ilisababisha nchi yetu kurudi nyuma zaidi ya ilipokuwepo. Ni kweli tulishinda vita lakini kwa gharama kubwa sana siyo tu ya fedha bali pia ya watu.

Kwa wanaokumbuka historia ya Uganda mojawapo ya matukio ya vita ni vita ya kuichukua Lukuya (Battle of Lukuya) ni hapa kiasi cha wanajeshi wetu kiliposhtukizwa na wanajeshi mamluki wa Libya na kujikuta kinarudishwa nyuma kabla ya Brigedi ya 201 na 208 kujipanga upya na kuwashambulia mamluki hao na kuwashinda na kusafisha njia ya kwenda Kampala (baada ya kuchukua Entebbe na Jinja). Gharama ya fedha tu serikali ya Museveni ndio iliweza kuilipa Tanzania mwaka 2007! Ikumbukwe kuwa vita ya Uganda inakadiriwa kuigharimu Tanzania dola milioni 1 kwa siku na hizo zilitoka mifukoni mwetu (hatukuwa na wajomba). Leo hii tumepiga kelele kulipa dola laki moja kwa Symbion kwa siku. Fikiria Wamarekani kwenye vita ya Iraq walikuwa wanaunguza dola bilioni 1 kwa siku!

Nikiangalia hali hiyo najiuliza; hivi kweli kina Lowassa na wengine wanaoshabikia vita wanafikiria kweli gharama yake? Hivi kuna mtu amewahi kuuliza Tanzania ilipoteza askari wangapi vita ya Uganda? Hivi watu wanajua kuwa ili jeshi letu liende vitani ni lazima wale wote waliokuwa reserve nao wawe reactivated? Yaani kabla ya kwenda Vitani itabidi kwanza tuongeze askari wote kutoka kama 30,000 waliopo sasa hivi na kufikia angalau 150,000 hivi kuweza kushinda vita. Hawa tutakaowachukua wengi ndio wasomi wenyewe na wafanyakazi maofisini watabadilishwa na nani? Ikumbukwe kwenye vita ya Uganda hawakwenda JWTZ tu bali Mgambo, Polisi, Magereza na wale waliopewa mafunzo ya haraka haraka. Je tuko tayari kuleta "draft" ya kulazimisha wanaume wote wenye miaka 18 na zaidi kuingia kambini? au watu wanafikiria ni "JWTZ" ndio litaenda vitani wakati wengine tunacheza ping pong na kuchat kwenye JF juu ya maendeleo ya vita?

Ninachopinga kabisa na ninaona ni mambo ya hatari ni kuzungumzia masuala ya vita bila kuonesha fikara na hekima. Kabla haujaamua kwenda vitani jipe nguvu kwanza. Na hakuna nguvu kubwa zaidi kama nguvu ya kiuchumi. Lakini jambo jingine ambalo labda wengine wameshafikiria ni vikosi vyetu vitakula nini? Au watu wanafikiria wanajeshi wakienda vitani wanapewa zile ration tu? Pamoja na gharama nyingine zote je bado tutaweza kulilisha taifa letu wakati wa vita? Wapo ambao hawajui kuwa njaa ya mwanzoni mwa miaka ya 1980 sehemu kubwa pia ni matokeo ya vita ya Uganda? Je tuko tayari kula dona na yanga tena na kurudishwa kwenye ration kwa taifa zima na mambo yale ya duka la kaya? au watu wanafikiria wataendelea kula nyama choma jioni wakati vita inaendelea?

Tusianze kupiga ngoma za vita (we shouldn't beat the drums of war) kama hatuko tayari kuingia vitani. Ni uzembe na reckless na binafsi naamini viongozi wote watatu (Lowassa, Membe na Sitta) wanatia shaka kama wana hekima na busara ya kuwa viongozi wa taifa letu. Kiongozi hata mwenye uwezo kiasi gani ni lazima asite linapokuja suala la vita na siyo kusita kwa sababu ya woga lakini kusita kwa sababu ya kujua analiita taifa lake kufanya nini. Na anapozungumza vita awe na uhakika kabisa (absolute confidence) kuwa hakukuwa na njia nyingine yoyote ya kuepuka vita hiyo.

Kwa mara nyingine nawasihi watu wanaoshabikia vita kama njia ya "kulinda mipaka yetu" wafikirie kwa hekima kuwa zipo njia nyingine nyingi zaidi za kufanya hivyo ikiwemo mazungumzo na mashtaka kwenye mahakama ya kimataifa. NI LAZIMA TUMALIZE NJIA ZOTE ZA AMANI (siyo mazungumzo tu) kabla hatujasema "we have had enough, we are preparing for war) na binafsi naamini kama tutaonesha hekima ya kutumia njia zote na busara ya kuepuka vita siku ikiitwa vita kweli kabisa tunaweza kwenda siyo kujihami tu bali kuiona Malawi kama tishio na kuanzisha an offensive assault ili kuliondoa tishio hilo mara moja na daima.

Nashauri vichwa vilivyotulia vizungumza lugha ya amani sasa hivi na kutuliza hizi ngoma za vita na mbiu za mapigano. Maana kama sasa hivi tu wanahangaika kulipa mishahara na kulisha taifa letu, sijui itakuwaje WAKATI WA VITA!


MMM
MM,
Ningekuwa na madaraka ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ningeagiza ukamatwe mara moja na ufunguliwe kesi ya uhaini. Nchi inapokuwa kwenye hali tete namna hii hutakiwi kutoa habari yenye heading ya namna hii, bila kujali ina ukweli ama la.

Na, ashuming kweli hatuna hela, unataka adui sasa atuvamie akijua kuwa hatuna hela? Ningeomba hii mada ifutwe na tuendelee na mijadala mingine, na pia watu wawe waangalifu na watu popular ndani ya forum hii kwa sababu wakati mwingine huwa wanachemsha saaaana ila tunashindwa kuona sababu ya popularity iliyowafunika.
Kwa hili MM ningekuomba usiongee sana hapa, kama una nafasi ongea na hao viongozi na wana siasa ana kwa ana, au hata kwa simu, uwape duku duku lako na si kukaa unamwaga mwaga mambo yako hapa hadharani. Hili swala ni tete na tusilijadili sana hapa, tuviachieni vyombo vinavyohusika vitali-handle. This case is a unique one and very different fron RICHMOND, KAGODA or whichever. Tuliache tusikae tunapayuka payuka hapa. Mwenye hoja, akaongee na viongozi wetu wapo watamsikiliza, na siyo ku-publicize, tuna jeopardize usalama wa nchi yetu na tukiendelea hivi ipo siku itakuja kutugharimu, japo siyo sasa!
 
Kama tutakwenda vitani vijana woote mi siendi mpaka nimuone Ritz yupo pembeni yangu Mbambaa bay tunaelekea Malawi

mambo ya kina Ritz,lowasa,membe,na nani na nan pamoja na mpuuzi Mzee Mwanakijiji sisi hatuyaangalii wakati tunaenda ulingoni,kwenda ulingoni wengine ndio kazi yetu kwanza tunahamu,sisi tutawaface maadui tu mambo mengine ni baada ya ushindi,we baki jf lakn sis tutaenda kupigana kwa ajili ya nchi yetu na watu wake
 
Last edited by a moderator:
KT0183.jpg


Mara zote wakiulizwa kuhusu mambo mbalimbali wanasema 'hawana fedha' na kuwa serikali ni maskini. Tumeona migomo ya madaktari, walimu na tishio la migomo ya wafanyakazi. Tumeona jinsi ambavyo wamekuwa wakilalamika kila kukicha kuwa "serikali haina fedha" -sikiliza kwa makini majibu ya mawaziri Bungeni wanavyorudia suala hili. Wanasema "serikali ikiwa na uwezo" au "tunaendelea kutafua fedha kwa ajili ya mradi huo; tena za ndani na za 'washirika wa maendeleo'".

Kila ukiwauliza mengi ambayo hayaendi vizuri jibu lao ni "serikali yetu haina fedha" au "hali ngumu". Sasa leo hii serikali hii hii ambayo "haina uwezo" inadai ati iko tayari kwenda vitani. Wale ambao tulikuwepo wakati wa vita vya Uganda tunakumbuka gharama kubwa (great toll) ya vita ile kwa maisha ya wananchi hadi vijijini. Hakuna ambaye kwa namna yake hakusikia maumivu (pinch) ya vita. Na vita ilipokwisha gharama yake kwenye uchumi wetu na maendeleo ya watu wetu haikuweza kurudishwa kwa urahisi. Kwa karibu miaka minne (miwili ya vita na ile ya reconstruction) ilisababisha nchi yetu kurudi nyuma zaidi ya ilipokuwepo. Ni kweli tulishinda vita lakini kwa gharama kubwa sana siyo tu ya fedha bali pia ya watu.

Kwa wanaokumbuka historia ya Uganda mojawapo ya matukio ya vita ni vita ya kuichukua Lukuya (Battle of Lukuya) ni hapa kiasi cha wanajeshi wetu kiliposhtukizwa na wanajeshi mamluki wa Libya na kujikuta kinarudishwa nyuma kabla ya Brigedi ya 201 na 208 kujipanga upya na kuwashambulia mamluki hao na kuwashinda na kusafisha njia ya kwenda Kampala (baada ya kuchukua Entebbe na Jinja). Gharama ya fedha tu serikali ya Museveni ndio iliweza kuilipa Tanzania mwaka 2007! Ikumbukwe kuwa vita ya Uganda inakadiriwa kuigharimu Tanzania dola milioni 1 kwa siku na hizo zilitoka mifukoni mwetu (hatukuwa na wajomba). Leo hii tumepiga kelele kulipa dola laki moja kwa Symbion kwa siku. Fikiria Wamarekani kwenye vita ya Iraq walikuwa wanaunguza dola bilioni 1 kwa siku!

Nikiangalia hali hiyo najiuliza; hivi kweli kina Lowassa na wengine wanaoshabikia vita wanafikiria kweli gharama yake? Hivi kuna mtu amewahi kuuliza Tanzania ilipoteza askari wangapi vita ya Uganda? Hivi watu wanajua kuwa ili jeshi letu liende vitani ni lazima wale wote waliokuwa reserve nao wawe reactivated? Yaani kabla ya kwenda Vitani itabidi kwanza tuongeze askari wote kutoka kama 30,000 waliopo sasa hivi na kufikia angalau 150,000 hivi kuweza kushinda vita. Hawa tutakaowachukua wengi ndio wasomi wenyewe na wafanyakazi maofisini watabadilishwa na nani? Ikumbukwe kwenye vita ya Uganda hawakwenda JWTZ tu bali Mgambo, Polisi, Magereza na wale waliopewa mafunzo ya haraka haraka. Je tuko tayari kuleta "draft" ya kulazimisha wanaume wote wenye miaka 18 na zaidi kuingia kambini? au watu wanafikiria ni "JWTZ" ndio litaenda vitani wakati wengine tunacheza ping pong na kuchat kwenye JF juu ya maendeleo ya vita?

Ninachopinga kabisa na ninaona ni mambo ya hatari ni kuzungumzia masuala ya vita bila kuonesha fikara na hekima. Kabla haujaamua kwenda vitani jipe nguvu kwanza. Na hakuna nguvu kubwa zaidi kama nguvu ya kiuchumi. Lakini jambo jingine ambalo labda wengine wameshafikiria ni vikosi vyetu vitakula nini? Au watu wanafikiria wanajeshi wakienda vitani wanapewa zile ration tu? Pamoja na gharama nyingine zote je bado tutaweza kulilisha taifa letu wakati wa vita? Wapo ambao hawajui kuwa njaa ya mwanzoni mwa miaka ya 1980 sehemu kubwa pia ni matokeo ya vita ya Uganda? Je tuko tayari kula dona na yanga tena na kurudishwa kwenye ration kwa taifa zima na mambo yale ya duka la kaya? au watu wanafikiria wataendelea kula nyama choma jioni wakati vita inaendelea?

Tusianze kupiga ngoma za vita (we shouldn't beat the drums of war) kama hatuko tayari kuingia vitani. Ni uzembe na reckless na binafsi naamini viongozi wote watatu (Lowassa, Membe na Sitta) wanatia shaka kama wana hekima na busara ya kuwa viongozi wa taifa letu. Kiongozi hata mwenye uwezo kiasi gani ni lazima asite linapokuja suala la vita na siyo kusita kwa sababu ya woga lakini kusita kwa sababu ya kujua analiita taifa lake kufanya nini. Na anapozungumza vita awe na uhakika kabisa (absolute confidence) kuwa hakukuwa na njia nyingine yoyote ya kuepuka vita hiyo.

Kwa mara nyingine nawasihi watu wanaoshabikia vita kama njia ya "kulinda mipaka yetu" wafikirie kwa hekima kuwa zipo njia nyingine nyingi zaidi za kufanya hivyo ikiwemo mazungumzo na mashtaka kwenye mahakama ya kimataifa. NI LAZIMA TUMALIZE NJIA ZOTE ZA AMANI (siyo mazungumzo tu) kabla hatujasema "we have had enough, we are preparing for war) na binafsi naamini kama tutaonesha hekima ya kutumia njia zote na busara ya kuepuka vita siku ikiitwa vita kweli kabisa tunaweza kwenda siyo kujihami tu bali kuiona Malawi kama tishio na kuanzisha an offensive assault ili kuliondoa tishio hilo mara moja na daima.

Nashauri vichwa vilivyotulia vizungumza lugha ya amani sasa hivi na kutuliza hizi ngoma za vita na mbiu za mapigano. Maana kama sasa hivi tu wanahangaika kulipa mishahara na kulisha taifa letu, sijui itakuwaje WAKATI WA VITA!


MMM

i wish every Tanzanian would know, understand and contemplate this...well said MM.
 
Wakati ndio huu, acha ushamba,unaandika usichokijua na pengine JWTZ ulikwenda kwa intake ya upishi au kucheza ngoma.Vita haipiganwi bila fedha na ndio maana logisitics kama mafuta na vyakula vitapatikanaje.?Mwanakijiji amehit point sanasana wewe pengine ni ufinyu wa elimu yako haivuki zaidi ya kivuli chako.
 
Last edited by a moderator:
MM,
Ningekuwa na madaraka ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ningeagiza ukamatwe mara moja na ufunguliwe kesi ya uhaini. Nchi inapokuwa kwenye hali tete namna hii hutakiwi kutoa habari yenye heading ya namna hii, bila kujali ina ukweli ama la.

Na, ashuming kweli hatuna hela, unataka adui sasa atuvamie akijua kuwa hatuna hela? Ningeomba hii mada ifutwe na tuendelee na mijadala mingine, na pia watu wawe waangalifu na watu popular ndani ya forum hii kwa sababu wakati mwingine huwa wanachemsha saaaana ila tunashindwa kuona sababu ya popularity iliyowafunika.
Kwa hili MM ningekuomba usiongee sana hapa, kama una nafasi ongea na hao viongozi na wana siasa ana kwa ana, au hata kwa simu, uwape duku duku lako na si kukaa unamwaga mwaga mambo yako hapa hadharani. Hili swala ni tete na tusilijadili sana hapa, tuviachieni vyombo vinavyohusika vitali-handle. This case is a unique one and very different fron RICHMOND, KAGODA or whichever. Tuliache tusikae tunapayuka payuka hapa. Mwenye hoja, akaongee na viongozi wetu wapo watamsikiliza, na siyo ku-publicize, tuna jeopardize usalama wa nchi yetu na tukiendelea hivi ipo siku itakuja kutugharimu, japo siyo sasa!
Akamatwe kwa kosa lipi? Wa kututangazia nchi iko tayari kwa lolote ni Sitta au Lowasa? Waambie wanaSIASA wetu wasilikuze suala hili kwa malengo yao kijinga.
 
Makanyaga leo nimemshanga sana MM, huyu jamaa sikujui kuwa ni mpuuzi kiasi hiki,Namwambia tena kupitia kwako,Sisi(wapigangaji) hatuangalii matakataka ndani ya serikali kipindi hiki,tunachoangalia ni adui tu,Tutawapiga malawi kwa muda wa dk 30 na hapo ndipo mtakapo tuheshimu
 
Last edited by a moderator:
Makanyaga leo nimemshanga sana MM, huyu jamaa sikujui kuwa ni mpuuzi kiasi hiki,Namwambia tena kupitia kwako,Sisi(wapigangaji) hatuangalii matakataka ndani ya serikali kipindi hiki,tunachoangalia ni adui tu,Tutawapiga malawi kwa muda wa dk 30 na hapo ndipo mtakapo tuheshimu
Uanajeshi wako una walakini. Amiri Jeshi Mkuu wako ni Sitta? Ni Membe? Ni Lowasa? Unapokea amri kutoka kwa yeyote tu!
 
MM,
Ningekuwa na madaraka ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ningeagiza ukamatwe mara moja na ufunguliwe kesi ya uhaini. Nchi inapokuwa kwenye hali tete namna hii hutakiwi kutoa habari yenye heading ya namna hii, bila kujali ina ukweli ama la.

Na, ashuming kweli hatuna hela, unataka adui sasa atuvamie akijua kuwa hatuna hela? Ningeomba hii mada ifutwe na tuendelee na mijadala mingine, na pia watu wawe waangalifu na watu popular ndani ya forum hii kwa sababu wakati mwingine huwa wanachemsha saaaana ila tunashindwa kuona sababu ya popularity iliyowafunika.
Kwa hili MM ningekuomba usiongee sana hapa, kama una nafasi ongea na hao viongozi na wana siasa ana kwa ana, au hata kwa simu, uwape duku duku lako na si kukaa unamwaga mwaga mambo yako hapa hadharani. Hili swala ni tete na tusilijadili sana hapa, tuviachieni vyombo vinavyohusika vitali-handle. This case is a unique one and very different fron RICHMOND, KAGODA or whichever. Tuliache tusikae tunapayuka payuka hapa. Mwenye hoja, akaongee na viongozi wetu wapo watamsikiliza, na siyo ku-publicize, tuna jeopardize usalama wa nchi yetu na tukiendelea hivi ipo siku itakuja kutugharimu, japo siyo sasa!

na ndio maana huna hayo madaraka.keep on wishing.
 
Mzee Mwanakijiji huwa nakueshimu sana lakini leo umeongea pumba.Taaluma yako ya uandishi wa makala huishie huko huko.Wala hujui lolote juu ya Jeshi na hasa JWTZ,wala hujui hasa chanzo kilichokuwepo cha vita kati ya TZ na UGANDA,sanasana utaeleza ni mipaka lakini chanzo hadi kuwa mipaka ilikua nini hujui unaishia kubwabwaja.Labda ni kwambie jambo la msingi,kama mnatuchokoza mkazania hatutaweza kufanya lolote eti hatuna hela,tayari mmefeli vita,kwa taalifa tutawapiga ndani ya dk 30,naongea kama mmoja wa JWTZ,we kaongelee kwenxe magazeti mi ntaongea kwa vitendo,subiri utaniambia
Nakuunga mkono mpiganaji!!
 
Wakati ndio huu, acha ushamba,unaandika usichokijua na pengine JWTZ ulikwenda kwa intake ya upishi au kucheza ngoma.Vita haipiganwi bila fedha na ndio maana logisitics kama mafuta na vyakula vitapatikanaje.?Mwanakijiji amehit point sanasana wewe pengine ni ufinyu wa elimu yako haivuki zaidi ya kivuli chako.

sikulaumu elimu yako/ufahamu wako na ndio umeishia hapo,kaa ukijua hatujiandai mara tukisikia kuna vita,huwa tupo kamili wakati wote na siku zote.Mi sigombani na wewe kwa ujinga na upuuzi uliojazwa na MM,bwabwaja na maneno yanayotoka kwenye stock ya ubwege,lakn nakuapia tupo tayari,neno TAYARI namaanisha tayari kinamna yoyote ile,na huyo mama yenu tunawaletea hapa tena akiwa uchi,ngoja nikuache
 
Last edited by a moderator:
Dear Mwanakijiji,

As much as you have a point to say it is just a matter of the government to adjust itself. Unapolinganisha suala la vita na mishahara ya wananchi nadhani you are missing a point somewhere. Kwasababu gani mishahara ya wafanyakazi wa serikali au taasisi za serikali ni kuongeza mzigo wa gharama za uendeshaji wa serikali. Tofauti na inapotokea emergency kama hii ya vita ambapo tunaweza kujipanga gharama za serikali zikaongezeka kwa muda fulani tukiona hatutaweza kuendelea basi tunaweza kumaliza vita tukarudi kujipanga. Mwanakijiji huwezi ukafuta suala la vita kwani mipaka ya nchi ni mali ya nchi husika lazima ilindwe kwa gharama yeyote. Sasa kama wamekutuma wamarekani kuja kuwachanganya watu hapa na spin off zako waambie watanzania wako makini diplomatic discussions zina nafasi yake but hatuwezi kusema eti turule off war option hilo si suala la kubeza.

Nilikuwapo!
 
MM,
Ningekuwa na madaraka ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ningeagiza ukamatwe mara moja na ufunguliwe kesi ya uhaini. Nchi inapokuwa kwenye hali tete namna hii hutakiwi kutoa habari yenye heading ya namna hii, bila kujali ina ukweli ama la.

Na, ashuming kweli hatuna hela, unataka adui sasa atuvamie akijua kuwa hatuna hela? Ningeomba hii mada ifutwe na tuendelee na mijadala mingine, na pia watu wawe waangalifu na watu popular ndani ya forum hii kwa sababu wakati mwingine huwa wanachemsha saaaana ila tunashindwa kuona sababu ya popularity iliyowafunika.
Kwa hili MM ningekuomba usiongee sana hapa, kama una nafasi ongea na hao viongozi na wana siasa ana kwa ana, au hata kwa simu, uwape duku duku lako na si kukaa unamwaga mwaga mambo yako hapa hadharani. Hili swala ni tete na tusilijadili sana hapa, tuviachieni vyombo vinavyohusika vitali-handle. This case is a unique one and very different fron RICHMOND, KAGODA or whichever. Tuliache tusikae tunapayuka payuka hapa. Mwenye hoja, akaongee na viongozi wetu wapo watamsikiliza, na siyo ku-publicize, tuna jeopardize usalama wa nchi yetu na tukiendelea hivi ipo siku itakuja kutugharimu, japo siyo sasa!

Waandishi wengine wavumilieni bure tu maana wanaandika kwa kutaka sifa.
Miaka ya Mwalimu wakati kuna suala tete mobilisation ya kitaifa alikuwa anaandika mwenyewe tahriri ya habari ili jamii tuwe na msimamo mmoja.

Sasa hili la Mwanakijiji kutaka kuonekana kupinga kila kitu kinamwonesha in a different light.
Aidha ni mwoga, au ni fifth columnist au analipwa kufanya hivyo.
Kwa vyovyote vile hali ya kiuchumi ya Tanzania leo ni much better off kuliko 1978, na vile vile kama vita itazuka, wapenda nchi wataenda mbele.

Makala kama hizi za Mwanakijiji kwa kweli zinaonyesha mtu mwenye akili inayomfaa yeye mwenyewe na hali ikiwa mbaya zaidi mpakani, itachukuliwa kuwa inamsaidia adui.
 
Uanajeshi wako una walakini. Amiri Jeshi Mkuu wako ni Sitta? Ni Membe? Ni Lowasa? Unapokea amri kutoka kwa yeyote tu!

Nashukuru,lakni wakati ukifika kila ulio mtaja hapo juu ndio utajua nafasi yake,ukishajua nafasi zao ndio uje uniulize tena ni Nani Amiri Jeshi Mkuu.SISI NI WATU WA VITENDO KWA MASLAHI YA NCHI NA WATU WAKE BILA KUJALI KUNA WANANCHI WAJINGA NA MTAILA KAMA WEWE
 
Sahihi sana mze mwanavillage,ila apo pa kusema wanaume wote 18+ twende vitani,ween4 hatupo tayari na hatutaki kabsaa uo upuuzi,hawakuona umuhim wetu kabla af leo kwenye kifo ndo wanatuweka mbelembele! Maisha ya kitz hayatufanyi tupate uchungu wa kufia nchi. Kama jeshi lisipotosha wapeleke watoto wao ili wakapiganie maslahi na miradi ya baba zao,akina sie hapana kwa kweli.
 
Waandishi wengine wavumilieni bure tu maana wanaandika kwa kutaka sifa.
Miaka ya Mwalimu wakati kuna suala tete mobilisation ya kitaifa alikuwa anaandika mwenyewe tahriri ya habari ili jamii tuwe na msimamo mmoja.

Sasa hili la Mwanakijiji kutaka kuonekana kupinga kila kitu kinamwonesha in a different light.
Aidha ni mwoga, au ni fifth columnist au analipwa kufanya hivyo.
Kwa vyovyote vile hali ya kiuchumi ya Tanzania leo ni much better off kuliko 1978, na vile vile kama vita itazuka, wapenda nchi wataenda mbele.

Makala kama hizi za Mwanakijiji kwa kweli zinaonyesha mtu mwenye akili inayomfaa yeye mwenyewe na hali ikiwa mbaya zaidi mpakani, itachukuliwa kuwa inamsaidia adui.

Mkuu,

Mwanakijiji kama hujamstukizia ni jasusi ambaye anachonganisha mada ili apate kujua reaction yenu ikoje. Na nazidi kujidhihirisha nachokisema kwa makala yake hii na nyengine aliyoiweka leo asubuhi. Kwanini mada zake mara nyingi ni controversial aiming at getting attention. Mfano hii inashangaza analalamika hatuko tayari kwenda kwenye vita wakati nikimuuliza JE WAMALAWI WAKIGOMA KUTUPA ENEO LETU TUWAAMBIE HAYA ASANTE TUNAWASHUKURU NA TUNA MBEYA MNAWEZA KUCHUKUA NA PIA RUKWA. HUO UTAKUWA UPUMBAVU WA HALI YA JUU!!!!!
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom