Swali la kizushi kwa Dr Slaa, Mbowe, Mnyika, Mkumbo na Wanachadema

Hoja ya CHADEMA iko wazi kuwa chama kimoja hakiwezi kujifanya popo.........wanahitaji kuchagua moja katika ushirikiano na vyama vya siasa. Aidha kuwa kwenye serikali au la, that's simple. Sasa CHADEMA wakiwa serikali halafu wakataka kuwa kwenye kambi ya upinzani kwa upande wa pili wa JMT itakuwa ni unafiki kama wanavyotaka CUF kuwa.

Usisahau pia kuwa mambo ya Zanzibar hayatenganishwi na mambo ya bara kwa kisiasa. Kumbuka Raisi mstaafu BW Mkapa alisha wahi kumteua R. Hamad wa CUF kuwa mbunge wa bunge la JMT, pia Raisi JM Kikwete alisha wahi kumteua mh. Jussa kuwa mbunge wa bunge hilo hilo la JMT na yote haya yalifanyika kwa sababu ya miafaka yao ya Zanzibar. Sasa inakuwaje leo CUF wawe serikalini Zanzibar lakini wajifanye hawako serikali (ushirikiano ) na CCM???????????
CUF waache unafiki, waendelee na CCM au wajitoe wakae na vyama vingine

Hayo maelezo yanajibu swali gani kwenye kati ya haya?

"1.Kutokana na tamko lenu kuhusu KUB kuwa hamtawashirikisha CUF kwa kuwa imo ndani ya Serikali ya kitaifa je mtawashirikiasha UDP na NCCR - Mageuzi? na kama hamtawashirikisha ni kwanini?

2.Ninavyoona hamuwatendei haki Wazanzibari ambao miongoni mwao wapo wanaCDM kwa maana Serikali ya umoja wa kitaifa wao waliupigia kura za maoni na kura hizo ndizo zilizopelekea kubadilishwa katiba na kusomeka kama ilivyo sasa.

a) Je kwa katiba iliyopo Zanzibar ikitokea one day YES kwa CDM wakashinda wao na kufuatiwa na chama kingine cha pili mtaunda serikali ya zanzibar peke yenu?

b)Je ikitokea siku moja mkashika nafasi ya pili Zanzibar na katiba inasema kuna Serikali ya kitaifa mtakubali ku join hands na walioshinda ili kuwatumikia wananchi?"
 
Maswali mepesi stahili yake ni majibu mepesi.
Sasa kama hutaki majibu uliyopewa hapo basi ni dhahiri kwamba ulikuwa na maswali mkono mmoja huku ukiwa na majibu mkono wa pili.
Sasa endelea kusubiri majibu unayotaka ama vinginevyo ujijibu mwenyewe kwa kuwa tayari unayo majibu ya maswali yako. Na pengine watakuja kuomba kwako ushauri jinsi ya kupenetrate zanzibar na kuangaza miaka 30 ijayo kama unavyshauri.

Sasa mwita unataka mtoto akizaliwa tu ale mihogo na miwa? simpaka aote meno? wewe ulitaka CDM izuke tu vuuuuuuuuu ichukue zanzibar? Ndugu yangu Mwita hata Roma haikujengwa siku moja. Ni jukumu la kila mwanamapinduzi wa kweli kuijenga CDM ya miaka ijayo kwa kizazi kijacho.

Shukrani sana kwa majibu yako mapesi wewe ni grit sinka
 
Nimefurahi na majibu yako na nimefurahi zaidi kusikia upo Raskazoni si vibaya kama tutaonana Inn by the sae au Raskazone Beach Club nikupanue mawazo.

Hoja yako namba mbili ni hoja dhaifu sana na inaonyesha uchu na njaa ya uongozi. Hizo ni siasa za marekani Tanzania ikiwa na mahusiano na Afghan mnakula kichapo! Ni siasa dhaifu na zinakubalika na wenye mtindio peke yao.

Kuhusu Muungano sina uhakika kama watu hawautaki muungano ila tutobolee siri kama unazo za chini ya kapeti ndani ya CDM wanalizungumziaje? Usikhofu as jina lako halina uhalisia tofauti na mie.

Sukrana Sana kweli wewe ni griti sinka

Nimeona umetumia hilo neno zaidi ya mara tatu hivi. Hii inaonesha jinsi gani unajiona kuwa wewe ni mjuaji wa kila kitu na kila anaekuwa tofaut na wewe ni Griti sinka .lol...nyani haoni.....
 
Nenda zako hatuko hapa kusoma uzushi bali muelekeo wa Tanzania tunayoitaka.
Mkuu,
Mleta mada kaja na masuali mazuri tu na yanahitaji majibu kwa mwenye majibu.

Hebu ifafanue hii Tanzania ambayo wewe na CHADEMA munayoitaka!
Kumbuka Tan(ganyika)Zan(zibar)ia = Tanzania.
Haya fikiria halafu njoo na jibu muafaka.
 
Naomba nikujibu kwa ufupi, waliopiga kura ya maoni ni CUF au wanzibari? je mnajua kuwa CCM walikuwa hawalitaki hili?na hadi leo wapo wahafidhina wasiotaka kutoa ushirikiano. Ikiwa siasa ni kuwatumikia watu kwanini tusiwatumikie kwa pamoja? ili kama lawama ziwe zetu sote!

Mie siamini kwa kuhodhi madaraka kama wanavyofanya sasa CDM kwenye KUB.

Mbona cuf wamehodhi madaraka Visiwani kwa kushirikiana na CCM tu na hatujasikia cdm wakilalamika? Kwani visiwani hamna vyama vingine zaidi ya CCM na CUF?
 
Heshima zenu waheshimiwa ndugu Dr Slaa, Mbowe, Mnyika na Mkumbo, Najua nyie ni wana JF mpo katika hii himaya ya kina invisible na uwepo wenu hapa jamvini umeleta tija kubwa kwa kutujuza mambo mbalimbali ya kimapinduzi na kisiasa.

Sina uhakika kama wote mpo jamvini lakini nina uhakika kuwa Dr Slaa, Mnyika na Mkumbo tunao humu jamvini kwa maana nimeona post zao nyingi tu.


Nisiwachoshe na maelezo naomba niulize maswali mawili la pili likiwa na sehemu aa na be.

1.Kutokana na tamko lenu kuhusu KUB kuwa hamtawashirikisha CUF kwa kuwa imo ndani ya Serikali ya kitaifa je mtawashirikiasha UDP na NCCR - Mageuzi? na kama hamtawashirikisha ni kwanini?

2.Ninavyoona hamuwatendei haki Wazanzibari ambao miongoni mwao wapo wanaCDM kwa maana Serikali ya umoja wa kitaifa wao waliupigia kura za maoni na kura hizo ndizo zilizopelekea kubadilishwa katiba na kusomeka kama ilivyo sasa.

a) Je kwa katiba iliyopo Zanzibar ikitokea one day YES kwa CDM wakashinda wao na kufuatiwa na chama kingine cha pili mtaunda serikali ya zanzibar peke yenu?

b)Je ikitokea siku moja mkashika nafasi ya pili Zanzibar na katiba inasema kuna Serikali ya kitaifa mtakubali ku join hands na walioshinda ili kuwatumikia wananchi?

Nina maswali mengi lakini hayo ni yamsingi mengine ya nyongeza yatakuja baada ya kujibiwa hayo maswali.

Naomba kuwakisha na kutoa shukrani zangu za awali kwa majibu yenu mazuri na yenye kunifanya niwe huru na haya maswali yanayoniumiza kichwa tangu mlipotoa tamko kuhusu kuwashirikisha CUF na vyama vingine kwenye KUB.

Mohammed H. Shossi

Safarini Ngamiani,

CDM wanachoogopa ni hila za CCM zilizojificha kupitia CUF! Na CUF kama inapenda kuungana na CDM kwa nini hawakuwapigia wagombea wake wa uspika na unaibu spika kura na badala yake waliwapigia wapenzi wao CCM? Unakumbuka mambo ya uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijijini jinsi CUF walivyofanya hila mpaka mgombea wa CDM Shitambala akaenguliwa? Finally, hivi CDM imevunja kanuni ipi au Sheria ipi kwa kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni mpaka CUF iwakoromee kiasi hicho?
 
Nimeona umetumia hilo neno zaidi ya mara tatu hivi. Hii inaonesha jinsi gani unajiona kuwa wewe ni mjuaji wa kila kitu na kila anaekuwa tofaut na wewe ni Griti sinka .lol...nyani haoni.....

habari yako mkuu umeshatengeneza mabomu mangapi mpaka sasa? unajua kuna kutofautiana na mtu na kuna mtu kutodiscuss points utakuta tunazungumzia mbaazi mtu abarukia kusifia ngogwe.....

Issue ni katiba ya znz ilivyorekebishwa kwa maoni ya wananchi yaani wazanzibari na kuweza kuandikwa kuwa kutakuwa na serikali ya umoja ya kitaifa itakayojumuisha vyama vyote vyeneye uwakilishi. Leo hii CDM ikipata hata kiti kimoja itaingia sasa kwakua sera yao wao hawataki ushirikiano itakuwaje? si watakuwa wamevunja katiba?

Sasa swali kama hilo mtu anakutolea stori lipumba sijui alimwambia slaa, mtatiro akamjibu cheyo siyu nccr walimtukana nani soma swali jibu hoja!
 
CDM wanachoogopa ni hila za CCM zilizojificha kupitia CUF! Na CUF kama inapenda kuungana na CDM kwa nini hawakuwapigia wagombea wake wa uspika na unaibu spika kura na badala yake waliwapigia wapenzi wao CCM? Unakumbuka mambo ya uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijijini jinsi CUF walivyofanya hila mpaka mgombea wa CDM Shitambala akaenguliwa? Finally, hivi CDM imevunja kanuni ipi au Sheria ipi kwa kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni mpaka CUF iwakoromee kiasi hicho?

Please pitia tena maswali yangu halafu uniambie maelezo yako yanajibu kifungu kipi...............

1.Kutokana na tamko lenu kuhusu KUB kuwa hamtawashirikisha CUF kwa kuwa imo ndani ya Serikali ya kitaifa je mtawashirikiasha UDP na NCCR - Mageuzi? na kama hamtawashirikisha ni kwanini?

2.Ninavyoona hamuwatendei haki Wazanzibari ambao miongoni mwao wapo wanaCDM kwa maana Serikali ya umoja wa kitaifa wao waliupigia kura za maoni na kura hizo ndizo zilizopelekea kubadilishwa katiba na kusomeka kama ilivyo sasa.

a) Je kwa katiba iliyopo Zanzibar ikitokea one day YES kwa CDM wakashinda wao na kufuatiwa na chama kingine cha pili mtaunda serikali ya zanzibar peke yenu?

b)Je ikitokea siku moja mkashika nafasi ya pili Zanzibar na katiba inasema kuna Serikali ya kitaifa mtakubali ku join hands na walioshinda ili kuwatumikia wananchi?
 
Heshima zenu waheshimiwa ndugu Dr Slaa, Mbowe, Mnyika na Mkumbo, Najua nyie ni wana JF mpo katika hii himaya ya kina invisible na uwepo wenu hapa jamvini umeleta tija kubwa kwa kutujuza mambo mbalimbali ya kimapinduzi na kisiasa.

Sina uhakika kama wote mpo jamvini lakini nina uhakika kuwa Dr Slaa, Mnyika na Mkumbo tunao humu jamvini kwa maana nimeona post zao nyingi tu.


Nisiwachoshe na maelezo naomba niulize maswali mawili la pili likiwa na sehemu aa na be.

1.Kutokana na tamko lenu kuhusu KUB kuwa hamtawashirikisha CUF kwa kuwa imo ndani ya Serikali ya kitaifa je mtawashirikiasha UDP na NCCR - Mageuzi? na kama hamtawashirikisha ni kwanini?

2.Ninavyoona hamuwatendei haki Wazanzibari ambao miongoni mwao wapo wanaCDM kwa maana Serikali ya umoja wa kitaifa wao waliupigia kura za maoni na kura hizo ndizo zilizopelekea kubadilishwa katiba na kusomeka kama ilivyo sasa.

a) Je kwa katiba iliyopo Zanzibar ikitokea one day YES kwa CDM wakashinda wao na kufuatiwa na chama kingine cha pili mtaunda serikali ya zanzibar peke yenu?

b)Je ikitokea siku moja mkashika nafasi ya pili Zanzibar na katiba inasema kuna Serikali ya kitaifa mtakubali ku join hands na walioshinda ili kuwatumikia wananchi?

Nina maswali mengi lakini hayo ni yamsingi mengine ya nyongeza yatakuja baada ya kujibiwa hayo maswali.

Naomba kuwakisha na kutoa shukrani zangu za awali kwa majibu yenu mazuri na yenye kunifanya niwe huru na haya maswali yanayoniumiza kichwa tangu mlipotoa tamko kuhusu kuwashirikisha CUF na vyama vingine kwenye KUB.

Mohammed H. Shossi

Safarini Ngamiani,

Na wewe nijibu maswali haya:

1. Cuf wameunda "serikali ya umoja wa kitaifa" kwa kushirikiana na ccm huko zanzibar, je wameshirikisha vyama vingine zaidi ya wao na ccm? Au ndio vyama pekee vilivyoko huko? Na kama hawajashirikisha, ni kwa nini? Utasema katiba. Je wakati inaundwa/kufanyiwa marekebisho hiyo katiba hawakujua kuwa kuna vyama vingine vya siasa ambavyo vinastahili kuwepo kwenye "serikali ya umoja wa kitaifa"?

2. Kwenye chaguzi za spika, naibu spika, wabunge wa east africa na sadc; cuf kwa makusudi mazima walishirikiana na kuchaguana na ccm tena kwa mapatano eti nafasi hii mpeni huyu wa ccm na ile mpeni yule wa cuf. Hakuna mbunge hata mmoja wa cuf aliyepigia kura chadema kwenye chaguzi hizo alkadhalika kwenye chaguzi za mameya, hapakuwa na ushirikiano hapo. Je itawezekanaje cuf hao hao sasa washirikiane na chadema ambao mwanzo waliona hawafai (na ni watu wale wale), waliwatuhumu na kuwabeza na bado wanaendelea kuwabeza?

3. Kwa kutowashirikisha cuf au vyama vingine vya upinzani, chadema inavunja sheria/kanuni gani?

4. Kama hawatakuwa kwenye hiyo kambi, wabunge wa cuf au vyama vingine vya upinzani hawataweza kutekeleza yale waliyowaahidi wapiga kura wao? Je wakati wanaomba kura waliweka sharti la kutekeleza ahadi zao kupitia "KUB"?

Nina maswali mengi lakini kwanza nijibu hayo machache kabla sijaongeza mengine.

Ndimi, Mkeshaji
Nikiwa safarini kuelekea hapahapa.
 
Mbona cuf wamehodhi madaraka Visiwani kwa kushirikiana na CCM tu na hatujasikia cdm wakilalamika? Kwani visiwani hamna vyama vingine zaidi ya CCM na CUF?

Kule zanzibar kulifanyika kura za maoni hazikupigwa na CCM na CUF bali na wananchi yaani wazanzibari kupendekeza kuwe na serikali ya umoja wa kitaifa kutokana na historia ya visiwa hivyo mtakumbuka kuna wakati watu walikuwa hawazikani.

Basi kura nyingi zikawa kuwe na serikali ya umoja wa kitaifa utakaoshirikisha vyama vyote vyenye uwakilishi kwenye baraza hawajasema CCM na CUF tu na sio vyama vingine, yaani leo hii hata demokrasia makini ikipata uwakilishi wanaingia kwnye serikali ya kitaifa.

Tusifanye siasa kuwa chuki hamjamuana mwenyekiti wetu leo anatamabasamu na kushake hand na Rais?
 
Mbona cuf wamehodhi madaraka Visiwani kwa kushirikiana na CCM tu na hatujasikia cdm wakilalamika? Kwani visiwani hamna vyama vingine zaidi ya CCM na CUF?

Mkuu,
Chama kinachopata kuanzia jumla ya kura 5% ndio kinapata ushiriki wa kuunda serikali huko Zanzibar. Kwa bahati mbaya au kutokuwa na mikakkati imara vyama vyengine,ikiwemo CDM havikupata hiyo asilimia na hivyo kukosa haki ya ushiriki kuunda serikali. Sio kwamba CCM au CUF wana kauli juu ya hilo. Ni katiba ndiyo inayoelekeza hivyo.
 
Na wewe nijibu maswali haya:

1. Cuf wameunda "serikali ya umoja wa kitaifa" kwa kushirikiana na ccm huko zanzibar, je wameshirikisha vyama vingine zaidi ya wao na ccm? Au ndio vyama pekee vilivyoko huko? Na kama hawajashirikisha, ni kwa nini? Utasema katiba. Je wakati inaundwa/kufanyiwa marekebisho hiyo katiba hawakujua kuwa kuna vyama vingine vya siasa ambavyo vinastahili kuwepo kwenye "serikali ya umoja wa kitaifa"?

2. Kwenye chaguzi za spika, naibu spika, wabunge wa east africa na sadc; cuf kwa makusudi mazima walishirikiana na kuchaguana na ccm tena kwa mapatano eti nafasi hii mpeni huyu wa ccm na ile mpeni yule wa cuf. Hakuna mbunge hata mmoja wa cuf aliyepigia kura chadema kwenye chaguzi hizo alkadhalika kwenye chaguzi za mameya, hapakuwa na ushirikiano hapo. Je itawezekanaje cuf hao hao sasa washirikiane na chadema ambao mwanzo waliona hawafai (na ni watu wale wale), waliwatuhumu na kuwabeza na bado wanaendelea kuwabeza?

3. Kwa kutowashirikisha cuf au vyama vingine vya upinzani, chadema inavunja sheria/kanuni gani?

4. Kama hawatakuwa kwenye hiyo kambi, wabunge wa cuf au vyama vingine vya upinzani hawataweza kutekeleza yale waliyowaahidi wapiga kura wao? Je wakati wanaomba kura waliweka sharti la kutekeleza ahadi zao kupitia "KUB"?

Nina maswali mengi lakini kwanza nijibu hayo machache kabla sijaongeza mengine.

Ndimi, Mkeshaji
Nikiwa safarini kuelekea hapahapa.


Nadhani kunahitajika nguvu kubwa sana kufahamisha watu nadharia ndogo kwenye hiyo katiba haya majibu nimemjibu mwezako yatakusaidia na wewe inaonyesha mnaongea vitu msivyovifaham ndio mnapoenda kombo.

Kule zanzibar kulifanyika kura za maoni hazikupigwa na CCM na CUF bali na wananchi yaani wazanzibari kupendekeza kuwe na serikali ya umoja wa kitaifa kutokana na historia ya visiwa hivyo mtakumbuka kuna wakati watu walikuwa hawazikani.

Basi kura nyingi zikawa kuwe na serikali ya umoja wa kitaifa utakaoshirikisha vyama vyote vyenye uwakilishi kwenye baraza hawajasema CCM na CUF tu na sio vyama vingine, yaani leo hii hata demokrasia makini ikipata uwakilishi wanaingia kwnye serikali ya kitaifa.

Tusifanye siasa kuwa chuki hamjamuana mwenyekiti wetu leo anatamabasamu na kushake hand na Rais?
 
habari yako mkuu umeshatengeneza mabomu mangapi mpaka sasa? unajua kuna kutofautiana na mtu na kuna mtu kutodiscuss points utakuta tunazungumzia mbaazi mtu abarukia kusifia ngogwe.....

Issue ni katiba ya znz ilivyorekebishwa kwa maoni ya wananchi yaani wazanzibari na kuweza kuandikwa kuwa kutakuwa na serikali ya umoja ya kitaifa itakayojumuisha vyama vyote vyeneye uwakilishi. Leo hii CDM ikipata hata kiti kimoja itaingia sasa kwakua sera yao wao hawataki ushirikiano itakuwaje? si watakuwa wamevunja katiba?

Sasa swali kama hilo mtu anakutolea stori lipumba sijui alimwambia slaa, mtatiro akamjibu cheyo siyu nccr walimtukana nani soma swali jibu hoja!

Laiti kama cdm wangekuwa na hata kiti kimoja Visiwani kisha wakakubali kuingia kwenye hiyo SUK na ingetokea huku bara kuna chama kingine say TLP kina uwezo wa kuunda kambi peke yake au hata kwa kushirikisha vyama vingine nje ya cdm basi ningeshauri cdm wasingie kabisa kwenye hiyo kambi maana wanachoongea cdm na ccm huko nyuma ya pazia kinaweza kuja kuwatafuna hata hao wa kwenye KU. Kumbuka lengo la CCM siku zote ni kuhakikisha ama upinzani unakufa kabisa au unakuwepo wa kiubabaishaji.

CCM wapo tayari hata kuwapa watu wanaotoka upinzani vyeo ili kudhoofisha upinzani. Sote tunajua mambo Msabah,Guninita,Leonard Gama,Tambwe n.k...lazima tujue CCM hawataki upinzani TZ. Hata CUF wasipoangalia wanaweza kuja kuwa CCM kamili achana na sasa wanaitwa CCM B.

Lakini haya yote yasingekuwepo kama CUF wangekubali wazo la CDM kuungana nao toka mwanzo bila kuleta masharti. Ama kweli wahenga walisema majuto ni mjukuu!

Mabomu nayauza Tahrir Squre mkuu. Unahitaji?
 
Naomba nikujibu kwa ufupi, waliopiga kura ya maoni ni CUF au wanzibari? je mnajua kuwa CCM walikuwa hawalitaki hili?na hadi leo wapo wahafidhina wasiotaka kutoa ushirikiano. Ikiwa siasa ni kuwatumikia watu kwanini tusiwatumikie kwa pamoja? ili kama lawama ziwe zetu sote!

Mie siamini kwa kuhodhi madaraka kama wanavyofanya sasa CDM kwenye KUB.
tunataka kila mmoja aongoze dola kivyake ili tuwapime nani hodari?kwa kuihofia CUF CCM waliingiza kwenye utawala. CUF wanapenda siasa za kihistoria kikoloni badala ya siasa leo ya Chadema. (ya ukoloni yameisha tunataka ya kileo jamani)
 
Nimekuwa nina shaka kuwa malengo na nguvu kubwa ni kanda ya ziwa, shinyanga na tabora,arusha,mbeya na kilimanjaro sehemu zenye population kubwa na sehemu watu wanaosifika kwa ukabila. Tuombee hisia zangu ziwe si kweli kama kweli basi tutakuja mtafuta mchawi one day.

Mo pole na safari!
Kaka mie sio mwanachama wa CDM ila nina mahaba nacho, at least for now.
- Sidhani kama kumchagua Wenje (anatokea mara) kuwa mbunge nyamagana (wasukuma wengi) ni ukabila.
- Sugu Mr Two sio mnyakyusa ila kapewa ubunge Mbeya
- Halima Mdee (kilimanjaro) ila ni mbunge Kawe
- Mnyika mbunge ubungo nasikia ni msukuma
- Mrema (Kilimanjaro) mbunge Arusha kamshinda Muarusha (Ms Buriani)

Kwingine kote walikoshinda CDM ni majimbo (18) ambayo wao ni wenyeji wa huko kama ambavyo CCM au CUF walivyosimamisha wagombea wanaotoka maeneo hayo.

Ingekuwa kanda ya ziwa wana ukabila/ukanda kama unavyotaka tuamini basi Bwana Mapesa angekuwa rais wa nchi hii. Ushindi wa Mkapa (toka Mtwara) kwa term zote mbili ulichangiwa na kura nyingi toka Kanda ya Ziwa.

Ingekuwa bungeni ningekuomba ufute usemi wako maana wewe si wa siasa hizo za ukabila na udini.

Huwa nachelea kufikiria juu ya ukabila na kudhani kwamba jambo hili limetokana na ukabila.
 
hivi kweli unategemea kiongozi yeyote wa CHADEMA ajibu swali la "kizushi"? uko serious kweli?
 
Nadhani kunahitajika nguvu kubwa sana kufahamisha watu nadharia ndogo kwenye hiyo katiba haya majibu nimemjibu mwezako yatakusaidia na wewe inaonyesha mnaongea vitu msivyovifaham ndio mnapoenda kombo.

Kule zanzibar kulifanyika kura za maoni hazikupigwa na CCM na CUF bali na wananchi yaani wazanzibari kupendekeza kuwe na serikali ya umoja wa kitaifa kutokana na historia ya visiwa hivyo mtakumbuka kuna wakati watu walikuwa hawazikani.

Basi kura nyingi zikawa kuwe na serikali ya umoja wa kitaifa utakaoshirikisha vyama vyote vyenye uwakilishi kwenye baraza hawajasema CCM na CUF tu na sio vyama vingine, yaani leo hii hata demokrasia makini ikipata uwakilishi wanaingia kwnye serikali ya kitaifa.

Tusifanye siasa kuwa chuki hamjamuana mwenyekiti wetu leo anatamabasamu na kushake hand na Rais?


quote_icon.png
Originally Posted by Mkeshaji
Na wewe nijibu maswali haya:

1. Cuf wameunda "serikali ya umoja wa kitaifa" kwa kushirikiana na ccm huko zanzibar, je wameshirikisha vyama vingine zaidi ya wao na ccm? Au ndio vyama pekee vilivyoko huko? Na kama hawajashirikisha, ni kwa nini? Utasema katiba. Je wakati inaundwa/kufanyiwa marekebisho hiyo katiba hawakujua kuwa kuna vyama vingine vya siasa ambavyo vinastahili kuwepo kwenye "serikali ya umoja wa kitaifa"?

2. Kwenye chaguzi za spika, naibu spika, wabunge wa east africa na sadc; cuf kwa makusudi mazima walishirikiana na kuchaguana na ccm tena kwa mapatano eti nafasi hii mpeni huyu wa ccm na ile mpeni yule wa cuf. Hakuna mbunge hata mmoja wa cuf aliyepigia kura chadema kwenye chaguzi hizo alkadhalika kwenye chaguzi za mameya, hapakuwa na ushirikiano hapo. Je itawezekanaje cuf hao hao sasa washirikiane na chadema ambao mwanzo waliona hawafai (na ni watu wale wale), waliwatuhumu na kuwabeza na bado wanaendelea kuwabeza?

3. Kwa kutowashirikisha cuf au vyama vingine vya upinzani, chadema inavunja sheria/kanuni gani?

4. Kama hawatakuwa kwenye hiyo kambi, wabunge wa cuf au vyama vingine vya upinzani hawataweza kutekeleza yale waliyowaahidi wapiga kura wao? Je wakati wanaomba kura waliweka sharti la kutekeleza ahadi zao kupitia "KUB"?

Nina maswali mengi lakini kwanza nijibu hayo machache kabla sijaongeza mengine.

Ndimi, Mkeshaji
Nikiwa safarini kuelekea hapahapa.[/QUOTE]

Umejibu swali la kwanza, nijibu na hayo yaliyosalia!
 
Mkuu,
Mleta mada kaja na masuali mazuri tu na yanahitaji majibu kwa mwenye majibu.

Hebu ifafanue hii Tanzania ambayo wewe na CHADEMA munayoitaka!
Kumbuka Tan(ganyika)Zan(zibar)ia = Tanzania.
Haya fikiria halafu njoo na jibu muafaka.

Kwa nini CUF inalazimisha ndoa na mume ambaye hawajakubaliana naye?
 
Mkuu,
Chama kinachopata kuanzia jumla ya kura 5% ndio kinapata ushiriki wa kuunda serikali huko Zanzibar. Kwa bahati mbaya au kutokuwa na mikakkati imara vyama vyengine,ikiwemo CDM havikupata hiyo asilimia na hivyo kukosa haki ya ushiriki kuunda serikali. Sio kwamba CCM au CUF wana kauli juu ya hilo. Ni katiba ndiyo inayoelekeza hivyo.

Tumlaumu nani kwa CDM kupata kura chini ya 5%? tuilaumu CUF na MTATIRO? Sometime common sense is common chama lazima kiwe na oparations kule kanda ya ziwa walifanya oparation sangara kwanini zanziba wasifanye oparation papa? Sote tunajua matunda ya oparation sangara kwenye mikoa ya kanda ya ziwa nina wasiwasi CDM wanaangalia sehemu yenye population kubwa zanzibar wapiga ni wachache pengine ni kama wa majimbo matatu bara ni mawazo yangu tu.
 
Back
Top Bottom