sWALI:KWA wanaume na Wanawake.

Ni kutojiamini na kuwa na mawazo potofu kuwa hawapendezi na rangi waliyo nayo...ambayo ni ujinga
 
Ulimbukeni unawasumbua na kuona weupe ni uzuri mwisho wa siku
hawathubutu kupita kwenye jua wanakuwa na mabakamabaka kama batiki
 
napenda mdada natural colour banaa, kama na black ni black beauty na kama ni brown skin iwewee hiyo hiyo si mrembo ana rangi nne duh
 
labda tujadili maana ya rangi nyeupe na nyeusi; tafsiri zitatupa majibu ya kwa nn watu wanatumia hivyo vipodozi!!
 
wale wanaotumia madawa na cream za kujichubua inamaanisha WANAUKANA UAFRICA?

Urembo mkuu, acha watu wapendeze! sio waafrika wote weusi na sio weusi wote ni waafrika. Mimi nadhani mtu afanye kitu roho inapenda yakimrudi shauri yake!:yield:
 
Back
Top Bottom