Watu8
Platinum Member
- Feb 19, 2010
- 70,955
- 93,932
Leo ni siku ya mapumziko ya mwisho wa wiki na nimejipumzisha kitandani kwenye hiki kibanda changu cha kupanga.
Mkononi nimeshika kijarida cha Sani na nafuatilia visa na vioja vilivyochorwa kwa mtindo wa vikaragosi na kuchagwizwa na maneno.
Ghafla nje ya chumba nilichopo ninasikia mwanamke akiporomosha matusi ya nguoni, nami nashusha kijarida chini ili nipate kusikia ni zogo gani linaloendelea(umbea suna huku uswahilini kwetu).
"We mwanaizaya hebu kuja hapa, hivi wewe nilikuzaa au nilikujamba?
Hebu nieleze mwana wewe usiye na haya, kwa nini umekula nyama zote kwenye sufuria?
Baba yako mwenyewe kutwa anazurura tu huko mtaani kama gari la taka na wala hanijali.
Mbwa mkubwa we kasoro mlio, na ukome kabisa kufunuafunua masufuria bila kuniambia.
Haya hebu nitokee hapa kabla sijakutukana...fyoooooooo(msonyo kama ule wa Ndoa ndoana kwenye Orijino Komedi)."
Huyo alikuwa ni Mama Wawili akimchachafya mwanae Kibakuli, na hiyo si mara ya kwanza kufanya hivyo kwa mwanae.
Sasa hapa nauliza swali kwa wamama, hivi ni kwa nini huwa mnaporomosha matusi mazito mazito kwa wanenu wa kuwazaa???
Hakuna namna nyingine ya kuwakanya wanenu hadi mtoe single na kuwashikia vipaza kama hivyo??
Karibu kujadili...
Copy to: Nivea, Lisa, King'asti, AshaDii, MwanajamiiOne, afrodenzi, Kongosho, BADILI TABIA, Paloma, mwaJ, Swts, Madame B, MadameX, Mamndenyi, Preta, marejesho, snowhite, Angel Msoffe, sweetlady, FirstLady1, FirstLady, Remmy, Zion Daughter, Kipipi, Roulette, Smile, Asnam, Binti.com, lara 1, Mrembo by Nature, Raiza, cacico, gfsonwin, Jeska, Lusile
Mkononi nimeshika kijarida cha Sani na nafuatilia visa na vioja vilivyochorwa kwa mtindo wa vikaragosi na kuchagwizwa na maneno.
Ghafla nje ya chumba nilichopo ninasikia mwanamke akiporomosha matusi ya nguoni, nami nashusha kijarida chini ili nipate kusikia ni zogo gani linaloendelea(umbea suna huku uswahilini kwetu).
"We mwanaizaya hebu kuja hapa, hivi wewe nilikuzaa au nilikujamba?
Hebu nieleze mwana wewe usiye na haya, kwa nini umekula nyama zote kwenye sufuria?
Baba yako mwenyewe kutwa anazurura tu huko mtaani kama gari la taka na wala hanijali.
Mbwa mkubwa we kasoro mlio, na ukome kabisa kufunuafunua masufuria bila kuniambia.
Haya hebu nitokee hapa kabla sijakutukana...fyoooooooo(msonyo kama ule wa Ndoa ndoana kwenye Orijino Komedi)."
Huyo alikuwa ni Mama Wawili akimchachafya mwanae Kibakuli, na hiyo si mara ya kwanza kufanya hivyo kwa mwanae.
Sasa hapa nauliza swali kwa wamama, hivi ni kwa nini huwa mnaporomosha matusi mazito mazito kwa wanenu wa kuwazaa???
Hakuna namna nyingine ya kuwakanya wanenu hadi mtoe single na kuwashikia vipaza kama hivyo??
Karibu kujadili...
Copy to: Nivea, Lisa, King'asti, AshaDii, MwanajamiiOne, afrodenzi, Kongosho, BADILI TABIA, Paloma, mwaJ, Swts, Madame B, MadameX, Mamndenyi, Preta, marejesho, snowhite, Angel Msoffe, sweetlady, FirstLady1, FirstLady, Remmy, Zion Daughter, Kipipi, Roulette, Smile, Asnam, Binti.com, lara 1, Mrembo by Nature, Raiza, cacico, gfsonwin, Jeska, Lusile