Swali kwa kina dada, Tunavumilia ili iweje?

Endelea kuvumilia na usichoke utapata thawabu mbinguni, tena mbinguni unajilimbikizia mema usichokoze banaa


ENhee ASANTE BABA......
Binadamu tunaifahamu na kuishika sana mistari mitakatifu ya kwenye,
vitabu vitakatifu, lakin je TUNAITEKELEZA KWA VITENDO??......

THE FINEST je wewe ni miongoni mwa hao WAVUMILIVU WENYE KUTEGEMEA,
KUPATA THAWABU???................................lol
 
Nimekumbuka wimbo wa pwani,
.....'usinitumie vibaya mtoto wa mwenzio wapo walionianza na wapo watakanimaliza"....

Jamani lakini nako kubadilisha sana mahusiano kama kiti cha daladala siyo vizuri hata kidogo......jamani msiache "kupambana"......lol

Kusema pambana ni rahisi sana, na hasa yanapokuwa kwa mwenzio,
manake kupambana kwingine ni kujitafutia R I P mapema....lol

My dear mpaka unampisha apite aendage zake umeshapambana vya kutosha pamoja na kumueleza mara nyingi kwamba my mwarobaini, hivi na hivi mboni sivyo? mwingine anaweza kukusikiliza na kutoa maoni kwamba basi na iwe hivi na hata wewe ni hivi na hivi.

Lakini mwingine kila umwambiapo ndio kwanzaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa anaona unampigia kelele, sa huyo wa nini jama! si apitege tu? Huko aendako ataenda kutana na kiboko yake akija kukumbuka ashachelewa. Au inawezekana ana wake aliepangiwa ambae wewe unazoona kero kwa mwenzio ni faraja kwani binadamu tumetofautiana.

so unampisha ukiwa na imani hata ipite miaka mingapi utashushiwa yule ambae Mungu alimuumba kwa ajili yako atavumilia madhaifu yako na wewe utavumilia yake. Amen lol

NENDAAAAAAAAAAAAAAAAA, KWENDAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA! HATA KAMA ZAMANI NILIKUPENDA
(YA NINI MALUMBANO BANA?)



If you love something, set it free. If it comes back, it was, and always will be yours. If it never returns, it was never yours to begin with
 
Tatizo ni mlio sensitive kushauri mtakavyokua wanyonge yakiwafika...well...tukubaliane kwamba Mapenzi ni bahati nasibu simply coz whom atakuja kuishi nawe hukudream kua naye..kwa phenomena hiyo hiyo tukubaliane kua unaweza kuibuka na kimeo au bahati ikawa upande wako!

Kuibuka na kimeo ni matakwa ya mtu mwenyewe kukubali hicho kimeo, unaweza kukataa au kukubali maana ni maisha yako.
 
Huyo dada ni mjinga (samahani kama ni nimetumia lugha nzito. Hivi anahitaji mtu kumwambia kuwa huyo jamaa anamtumia tu, tena kama taili la spea?

watu wengine bwana (awe KE au ME) nadhani wana matatizo ya akili....


Nimemchukia sana huyu binti...Kwani asipokuwa na mwanamume ndo atakuwa ame..R.I.P??


Nimechoka mwenzeni na hawa watoto... Mzee DC!!

Ndio shida ya wadada wengi, wanaona maisha bila mwanaume hayawezekani ndio maana wanasettle na vimeo
 
My dear mpaka unampisha apite aendage zake umeshapambana vya kutosha pamoja na kumueleza mara nyingi kwamba my mwarobaini, hivi na hivi mboni sivyo? mwingine anaweza kukusikiliza na kutoa maoni kwamba basi na iwe hivi na hata wewe ni hivi na hivi.

Lakini mwingine kila umwambiapo ndio kwanzaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa anaona unampigia kelele, sa huyo wa nini jama! si apitege tu? Huko aendako ataenda kutana na kiboko yake akija kukumbuka ashachelewa. Au inawezekana ana wake aliepangiwa ambae wewe unazoona kero kwa mwenzio ni faraja kwani binadamu tumetofautiana.

so unampisha ukiwa na imani hata ipite miaka mingapi utashushiwa yule ambae Mungu alimuumba kwa ajili yako atavumilia madhaifu yako na wewe utavumilia yake. Amen lol

NENDAAAAAAAAAAAAAAAAA, KWENDAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA! HATA KAMA ZAMANI NILIPENDA
(YA NINI MALUMBANO BANA?)



AMEN Mpendwa ubarikiwe sana....lol

Nahisi pia ulikapigia kura hako kawimbo kipindi cha KILI AWARDS......lol
 
Ndio shida ya wadada wengi, wanaona maisha bila mwanaume hayawezekani ndio maana wanasettle na vimeo


Aaah inaelekea haujawahi kupenda wewe....lol
Siku ukipenda hicho kimeo chako utakiona Malaika 100%.......lol,

Haya bwana hongera kama macho yako yanaona kwenye mapenzi,
masikio yako kama yanasikia kwenye mapenzi.........lol hongera sana.....
 
Aaah inaelekea haujawahi kupenda wewe....lol
Siku ukipenda hicho kimeo chako utakiona Malaika 100%.......lol,

Haya bwana hongera kama macho yako yanaona kwenye mapenzi,
masikio yako kama yanasikia kwenye mapenzi.........lol hongera sana.....

Nnunu mpenzi mi nashangazwa na hili! mara ya kwanza umempenda mtu, ukamkabidhi kichwa, kiwiliwili mpaka unyayo, (moyo na nafsi ndani yake) yaani ulimpenda haswaaaaaaaaaaa akakutenda. Ukaumiaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa maumivu yakaisha,

Wa pili atakuja atakutenda utaumia kama wa mwanzo? si unaanza kuzoea maumivu jama au,

wa tatu na kuendelea utaniambia bado unapenda kiasi cha kuumia mpaka ushindwe kufanya shughuli zako kama yule wa kwanza? kha! Mimi nilishawahi umizwa mara moja tu hiyo ilikuwa kubwa kuliko, jama toka hapo anaenipenda na kudhani ataniumiza huwa namuonea huruma yeye kwani niko kimachale zaidi, ukianza tu mi namalizia sirembi kabisa, kwani nilishawahi remba nikaona madhara yake.
 
Love is blind. Kwa hiyo sisi kama third part ndio tunaona yoote hayo. Mwenzenu anaona she is a luckiest woman in this world. Na kama mdada/mkaka amependa na bado ana huwezo wa kuona vizuri ubaya wa mpenzi wake basi hapo inawezekana bado hajakolezwa na penzi. Penzi likiisha ndio mtu anaanza kuona ubaya woote na kujishangaa. Hata sisi twaweza sema tuna wapenzi perfect kumbe bado tuko blind na watu hawatuambii kwani it is none of their business.
 
Nnunu mpenzi mi nashangazwa na hili! mara ya kwanza umempenda mtu, ukamkabidhi kichwa, kiwiliwili mpaka unyayo, (moyo na nafsi ndani yake) yaani ulimpenda haswaaaaaaaaaaa akakutenda. Ukaumiaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa maumivu yakaisha,

Wa pili atakuja atakutenda utaumia kama wa mwanzo? si unaanza kuzoea maumivu jama au,

wa tatu na kuendelea utaniambia bado unapenda kiasi cha kuumia mpaka ushindwe kufanya shughuli zako kama yule wa kwanza? kha! Mimi nilishawahi umizwa mara moja tu hiyo ilikuwa kubwa kuliko, jama toka hapo anaenipenda na kudhani ataniumiza huwa namuonea huruma yeye kwani niko kimachale zaidi, ukianza tu mi namalizia sirembi kabisa, kwani nilishawahi remba nikaona madhara yake.

Wish i could have your guts my dia.
 
Aaah inaelekea haujawahi kupenda wewe....lol
Siku ukipenda hicho kimeo chako utakiona Malaika 100%.......lol,

Haya bwana hongera kama macho yako yanaona kwenye mapenzi,
masikio yako kama yanasikia kwenye mapenzi.........lol hongera sana.....

Hapana, wanawake wanaosettle na vimeo wana upendo wa kijinga na ni waoga wa kuanza upya maisha wakidhani hawatapata mtu ambaye atawapenda kwa dhati.
 
Nimekua nikijiuliza sana kuhusu mahusiano.

1. Dada ana mpenzi wana miaka,sio mume wala mwanaume hana mpango wa kuoa,
wanafanya kazi mikoa tofauti, ajabu mwanaume anampa mwanamke masharti ya kufika kwa mwanaume.
Dada akienda lazima atoe taarifa kabla na hata ukitoa taarifa sio kwamba lazima atakuruhusu, anaweza kusema usije nina wageni wa ofisini. Dada akienda wageni hakuna na ananuniwa
inabidi aondoke tu. Akirudi kwake mwanaume ndio analeta mapenzi na dada anapata amani kua alimkosea laaziz,hivi huyu mwanamke hapa huwa anang'ang'ania nini?
Kama hamjaoana hakujali, ndani ya ndoa si itakua balaa?

2. wapenzi wqanaishi mikoa tofauti, mwanaume aakienda mkoa anaoishi mpenziwe hamjulishi, dada anaambiwa na wanaomjua huyu kaka kuwa tumemuona,kaka akiulizwa anajibu nipo ila nina mambo mengi nitakutafuta. Kaka anamaliza kilichomleta hadi anaondaoka bila kumtafuta mpenzi wake,bibie akipiga simu kumuulizia kaka anajibu nimeondoka ilikua ghafla!!
Dada anaandaa safari kwenda kwa kijana na zawadi kafungasha, wakiwa kwa mwanaume mapenzi kunoga lakini kaka akienda mkoa anaoishi mdada anajificha.
Mdada anavumilia eti kweli kazi nyingi,jamani kweli au ndio mapenzi upofu?

3. Utakuta dada ana mpenzi ambaye siyo mume, siyo mchumba wala siyo baba mtoto.
Mwanaume ana visa na mbaya zaidi ni mpigaji hadi dada tunakupeleka hospitali lakini ukipona umerudi na style ya maisha ni ile ile kupigana.
Hivi hapa kinachomfanya dada huyu kuvumilia mateso na aibu hii ni nini? Na anavumilia ili aolewe au ndio kupenda?

Kama kweli mapenzi Upofu mbona visa tunavyotendwa tunaviona, TUNALALAMIKA,tunalia tunafuta machozi halafu bado tunajipa moyo, Hivi huwa nini kinatufanya tuendelee kuvumilia?

Da Pretty,

Afadhali umesema! Suala hili lilikuwa linanikera MNO!

Mie ni MKAKA, ila nawashangaa hawa akinadada! Tena utakuta dada mwenyewe ni mrembo wa nguvu, ameumbika kila idara. Anafuatwa na wanaume wengi, tena wengi wako tayari hata kumuoa, lakini yeye anang'ang'ana na JITU liso haya, lisojua utu, lenye ukware kila kona, liso heshima, linalodhani kuwapiga wanawake ndio UANAUME! Uanaume gani huo, zaidi ya kuwa MWOGA tu?"

Kama wamjua huyo dada, mwambie AMPOTEZEE huyo kaka. Wako wanaume wazuri, wapole, wenye kazi zao, wenye kipato chao, wenye nia njema, waoaji, si wachezeaji kama huyo mkware. Mwisho atakuja kumwingiza kwenye gridi ya taifa yakawa ya miwaya, kubaki kilo mbili!

Mie simo! Ila namhurumia sana huyo dada. Tatizo lake HAJIAMINI! Nyie, mtakosa KUJIAMINI mpaka lini?

./Mwana wa Haki
 
jamani huwa inatokea, la ni fundisho kubwa, sana, ila atakapograduate hio course dada yako, ndio atakuwa MWANAMKE halisi, na si msichana tena.
Mwenzio mie niliwahi kuwa na shoga lakini enzi za shule, alikuwa haelewi somo masikini, hata ukimuambia nini, alikuwa akiamini kila anachoambiwa nayule kaka.
Lakini ilifikika siku ya siku, akasema BASI, baada ya pale, yule kaka ndio ilikuwa kazi kufuata mrembo mpole aliekuwa anaongoza darasa lao, lakini dada huyo alikuwa ameshafuzu somo la mapenzi, hakuwa tena limbukeni, wala machozi hatukuona tena, alianza maisha mapya.
Yule kaka bado anaendelea na uplayboy, na kudai kuwa tumempokonye kitumbua chake kwa umbeya.
Ila kwa huyo dada yako, bado hajapona ulimbukeni, endeleeni kumpa maarifa mpaka ajikomboe.
hapa duniani kuna wanaume ambao wanapenda kuwa na wasichana ambao wanawaabudu tu, bila mapenzi yoyote, ni kazi yetu wasichana kuhakikisha tunawakwepa wote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom