Eliphaz the Temanite
JF-Expert Member
- Jan 19, 2010
- 3,018
- 1,147
Mustakabari wa Nchi yetu unachukua mwelekeo ambao si tu unatishia kuipeleka nchi katika mikono ya watu wachache lakini pia tuko katika ukingo au huenda tayari tuna kuwa remote controlled na watu hawa wenye pesa zao(Mafisadi).
Tunashuhudia jinsi gani ufisadi ulivyooanza kama kiwingu kidogo na kuendelea kukuwa na kuleta utando mkubwa na giza nene. Angalia serikali na mamalaka yake iliyonayo inavyoshindwa kuchukua hatua dhidi ya watu hawa licha ya ushahidi na vyombo vya habari kupigia kelele!
Wachache wanaopiga kelele uovu huu ndio wamekuwa walengwa wakuu majimboni mwao wakitaka kung'olewa kwa gharama yeyote ile!
Maswali ninayojiuliza kwanini serikali haichukui hatua dhidi ya hawa watu mathalani, ufisadi wa bandarini unaoripotiwa na vyombo vya habari kila kukicha mpaka wafanyabiashara wanahamia Mombasa na kuikosesha serikali mapato kiasi hiki?
Wakati haya yote yakitokea ninajaribu kuwaza mustakabari wa nchi hii punde wingu hili litakapofunika na kusababisha giza totoro?
Watanzania tufanye nini kuubadili mwelekeo huu ambao nguvu yake imefikia hatua ya kuishinda hata serikali?
Tunashuhudia jinsi gani ufisadi ulivyooanza kama kiwingu kidogo na kuendelea kukuwa na kuleta utando mkubwa na giza nene. Angalia serikali na mamalaka yake iliyonayo inavyoshindwa kuchukua hatua dhidi ya watu hawa licha ya ushahidi na vyombo vya habari kupigia kelele!
Wachache wanaopiga kelele uovu huu ndio wamekuwa walengwa wakuu majimboni mwao wakitaka kung'olewa kwa gharama yeyote ile!
Maswali ninayojiuliza kwanini serikali haichukui hatua dhidi ya hawa watu mathalani, ufisadi wa bandarini unaoripotiwa na vyombo vya habari kila kukicha mpaka wafanyabiashara wanahamia Mombasa na kuikosesha serikali mapato kiasi hiki?
Wakati haya yote yakitokea ninajaribu kuwaza mustakabari wa nchi hii punde wingu hili litakapofunika na kusababisha giza totoro?
Watanzania tufanye nini kuubadili mwelekeo huu ambao nguvu yake imefikia hatua ya kuishinda hata serikali?