Swali kwa ASP Msangi........

Bisek

Member
Apr 2, 2012
77
10
Tumeshuhudia mateso makali na ya kinyama aliyofanyiwa Dr Ulimboka, alitekwa akapigwa kwanza ndani ya gari na baadaye katika Msitu wa Pande, ambako ndiko alikokutwa asubuhi akiwa hoi bin taaban. Madaktari wenzake wanasema kavunjwa mbavu, mikono na taya. Pia kang’olewa meno mawili ya mbele na kunyofolewa kucha.

Sasa viongozi wanasema hawahusiki na tukio hilo lakini “waathirika” wanasema wanamjua mhusika. Hakuna anayemtaja mbele za watu mhusika huyo ni nani, lakini kwenye vijiwe, kila mtu anataja kuwa serikali inahusika na kwamba wahusika ni Kijitonyama.

Ukiuliza Kijitonyama ni nani, wanasema ni wenyewe hao hao serikali. Kiongozi wa nchi kasema serikali haihusiki lakini yaelekea raia hawamwamini na hawaiamini serikali kuwa haihusiki. Lakini mng’oaji meno, mvunjaji mbavu, mikono na mataya atakuwa nani na kwa nini?

Na kwa nini mtu mwenyewe anayevunjwa mikono, mbavu na taya ni yule tu mwenye ugomvi na serikali? Kama ni kweli waliompiga Dk. Ulimboka, wakamvunja taya, mikono, mbavu na wakamnyofoa kucha walikuwa wakimhoji eti “nani wanakutumia kuongoza migomo,” je, ni nani hao wapigaji?


Source: ************************** wavuti - wavuti
 
hivi na mimi naomba kuuliza je Polisi wamefikia wapi katika kuwashika wahusika au watuhumiwa kwa kuanzia na yule ofisa aliye kuwa ana ongea na Dr Ulimboka na Dr Deo siku ya tukio, halafu kuwashika watu aliokuwa anawasiliana nao huyo ofisa kwa kutumia call log? au hatuhabarishwi hizo habari kwa kuwa wahusika ni wao wenyewe? kwani ingekuwa sio wenyewe mida hii tungeisha tolewa Picha za Ofisa wa ikulu feki, na hao watuhumiwa wenzake.
 
Binafsi nahofia pale wezi wa kuku na wale wanaokata nyavu za madirisha usiku watakapoonyeshwa kuwa ndio wahusika wa huu mkasa !!!
 
Tumeshuhudia mateso makali na ya kinyama aliyofanyiwa Dr Ulimboka, alitekwa akapigwa kwanza ndani ya gari na baadaye katika Msitu wa Pande, ambako ndiko alikokutwa asubuhi akiwa hoi bin taaban. Madaktari wenzake wanasema kavunjwa mbavu, mikono na taya. Pia kang’olewa meno mawili ya mbele na kunyofolewa kucha.

Sasa viongozi wanasema hawahusiki na tukio hilo lakini “waathirika” wanasema wanamjua mhusika. Hakuna anayemtaja mbele za watu mhusika huyo ni nani, lakini kwenye vijiwe, kila mtu anataja kuwa serikali inahusika na kwamba wahusika ni Kijitonyama.

Ukiuliza Kijitonyama ni nani, wanasema ni wenyewe hao hao serikali. Kiongozi wa nchi kasema serikali haihusiki lakini yaelekea raia hawamwamini na hawaiamini serikali kuwa haihusiki. Lakini mng’oaji meno, mvunjaji mbavu, mikono na mataya atakuwa nani na kwa nini?

Na kwa nini mtu mwenyewe anayevunjwa mikono, mbavu na taya ni yule tu mwenye ugomvi na serikali? Kama ni kweli waliompiga Dk. Ulimboka, wakamvunja taya, mikono, mbavu na wakamnyofoa kucha walikuwa wakimhoji eti “nani wanakutumia kuongoza migomo,” je, ni nani hao wapigaji?



Source: ************************** wavuti - wavuti


Aulizwe pia kama kile kikosi chake cha kuiba kwenye malori ya Mizigo "SHUSHA SHUSHA" kama bado kipo na kimeshamuungizia Shs ngapi hadi sasa?
 
Ulichomuuliza Ahmed Msangi ACP ni kipi? Anyaway hata hivo mie nimekuwa nikijiuliza baada ya Dr Deo (achana na Abeid) kuona mwenzie Dr Ulimboka kachukuliwa mzobe mzobe katika hali ya shari,,as we're told alichukua hatua gani tokea hiyo saa 3 usiku hadi alipokuja okotwa asbh?
 
Ulichomuuliza Ahmed Msangi ACP ni kipi? Anyaway hata hivo mie nimekuwa nikijiuliza baada ya Dr Deo (achana na Abeid) kuona mwenzie Dr Ulimboka kachukuliwa mzobe mzobe katika hali ya shari,,as we're told alichukua hatua gani tokea hiyo saa 3 usiku hadi alipokuja okotwa asbh?

Hivi wewe ndio unaingia huku mara ya kwanza au ndio unasoma hii taarifa kwa mara ya kwanza? Deo kazungumza mara nyingi kwenye vyombo vy habari kuwa alienda polisi muda ule ule na wakamtafuta vituo vingi vya polisi bila mafanikio mpaka walivyopigiwa simu asubuhi kweli unashangaza.
 
sasa hapo ndo umemuuliza ACP Msangi au!?!?!?

Hivi baba mwenye familia akimchapa mwanae afu mwanae akamshtaki baba yake kwa mama alafu baba aliyetoa kipigo aseme anaunda kamati yeye akiwa mwenyekiti wa hiyo kamati wachunguze kwanini mtoto alipigwa kweli huyo atapata haki kweli
 
Hivi baba mwenye familia akimchapa mwanae afu mwanae akamshtaki baba yake kwa mama alafu baba aliyetoa kipigo aseme anaunda kamati yeye akiwa mwenyekiti wa hiyo kamati wachunguze kwanini mtoto alipigwa kweli huyo atapata haki kweli
Negative
 
Ulichomuuliza Ahmed Msangi ACP ni kipi? Anyaway hata hivo mie nimekuwa nikijiuliza baada ya Dr Deo (achana na Abeid) kuona mwenzie Dr Ulimboka kachukuliwa mzobe mzobe katika hali ya shari,,as we're told alichukua hatua gani tokea hiyo saa 3 usiku hadi alipokuja okotwa asbh?

Dr. Deo alienda police kutoa taarifa usiku ule ule ila jeshi la police halikumpa ushirikiano kama ungesikiliza mahojiano kati ya Dr. Deo kwenye clouds ndio ungejua kwa asilimia 100 police wanahusika...
 
Back
Top Bottom