Swali gumu hili hapa!

Msongoru

JF-Expert Member
Apr 16, 2008
306
24
Mambo vipi wana mahusiano?

Kuna swali moja gumu kweli nimekutana nalo. Jama ana mpenzi ambaye amebakwa na baba yake kwa miaka miatano mfululizo! Demu alikuwa hajarevil kwa jamaa kwa muda mrefu ila alikuwa ana kama jinamizi hivi kila akikumbuka, jamaa kambembeleza amwambie shida yake demu akamwambia: "Nikikuambia bado utanipenda?" Jamaa akajibu kama kawa kwamba mimi na wewe hakuna wa kututenganisha! DEMU AKAMAWBIA NIAPIE! Jamaa kaapa kwa lugha na kwa miungu yote anyoijua. Ndipo demu kamfunulia! " Tangu nikiwa na umri wa miaka 14 baba alikuwa akinibaka, alinitisha kwamba siku nikimwambia mama tu ataniuwa. Ni mpaka nilipofikisha umri wa miaka 19 yaani mwaka jana na nadhani amehamia kwa mdogo wangu ingawa sina uhakika"

Any way, it is a long story, jamaa kaja kuniomba ushauri....Vipi amwache wakati keshaapa?
 
Tena tafadhali mwambie huyo jamaa yako asitake kumuumiza huyo msichana kwani anamhitaji tena sana baada ya kumpa siri hii nzito .. reaction yake inamatter so much now more than ever

amezee infact azidishe upendo na uelewa kwake
 
Mi ushauri wangu ni kwamba huyo jamaa aichukue uamuzi wa kumuacha kwani kitendo cha huyo dada kumwambia siri nzito hivyo inamaanisha kwamba amemuanini sana...! Tena hichi ndio kipindi amabcho huyo dada anamuhitaji sana huyo mpenzi wake kwani ni mtu wa pekee aliyeweza kumshirikisha kwenye siri hii kubwa na ya pekee...!

Anachoweza kufanya ni kuwa nae zaidi na kwa ukaribu na ikibidi washirikiane ili waweze kumwambia mama yake au ikibidi wampeleke huyo baba polisi kwani hio ni INCEST na ni kinyume cha sheria...! Tena hio ni kubaka kabisa...! Huyo mzee naweza akapigwa jela maisha yote...!
 
Huyo jamaa yako ni HOVYO kabisa, utafikiriaje kufanya uamuzi kama huo wa kumuacha mtu? kani alipenda abakwe? Kitendo cha jinamizi ni tosha kuonyesha jinsi alivyoumia kisaikolojia ni mateso makubwa ambayo kabla ya yote angefikiria kumsaidia ili aondokane nayo.

Sasa angekuwa ameoa mwanamke bikira siku moja akaingiliwa na majambazi, one of the damage ni kubakwa kwa m ke wake huyo angefanyaje?

my quick reply
 
....No need kumuacha provided kama kabla ya kumuweka ndani walicheki afya zao na wakaonekana wako safi life goes on....afterall kama alibakwa kwa miaka yote hiyo mali si iko vizuri tu ampe mapenzi kumtuliza na hilo jinamizi...
 
as long as walipima ngoma n they r both safe..n hana ujauzito wala mtoto wa bamkwe wake then asifikirie wala kuwazia kumuacha huyo mwanamama ila tu ajitahidi kumpa support ya kila aina vinginevyo kusema ukweli atamuumiza kupita maelezo huyo bibie n can lead to a more serious disaster....

pia nawapa pole wahusika!

tatu je wat wil b next to huyo mbakaji?je ashitakiwe ama?
 
There is something I call the secrets of your life,this is the one.Siri hizi ukiambiwa jua umeaminiwa and in this a negative response might cause death.
 
yeye anaona ugumu gani kuwa naye?
mini sioni tatizo hapo, manake akimuacha huyo atakutana na mwingine aligawa bure kwa miaka kadhaa, akimuacha atakutana na mwingine aligawa kwa kuomba kupata kazi nk.
We all have our skeletons.
kama wanaendana na inavyoonekana wanapendana, basi wapange mkakati wa kusaidiana na pia kama bado dada anapata nightmares watafute ushauri pamoja.
Msichana anaonekana bado ni mstaarabu, wengine wanasubiri baada ya ndoa ndio wanakuambia! Tena wengine wanakuletea namtoto kabisa ndani ya ndoa.
 
Nadhani kubaki nae kwa huruma ni makosa, Anatakiwa abaki nae kwaajili ya kumpenda na kuthamini uaminifu wake, na kutambua strength yake.
 
Du! Jamaa nilimshauri kwanza atulie ili akili yake irudi kwanza maana inaoneka alikuwa anaamini kuwa binti ni bikra nae alihitaji sana kuoa bikra. Ni binti mstaarabu sana ambaye huwezi kudhania amefanyiwa kitendo kama hicho.

Sababu hasa inayo mfanya afikiri kumwacha ni yeye kuhofia kukutwa na jinamizi pia! Anaona huruma lakini anahofia jinamizi. Anahisi itafika wakati babu atakuwa haamki!!!!
 
Du! Jamaa nilimshauri kwanza atulie ili akili yake irudi kwanza maana inaoneka alikuwa anaamini kuwa binti ni bikra nae alihitaji sana kuoa bikra. Ni binti mstaarabu sana ambaye huwezi kudhania amefanyiwa kitendo kama hicho.

Sababu hasa inayo mfanya afikiri kumwacha ni yeye kuhofia kukutwa na jinamizi pia! Anaona huruma lakini anahofia jinamizi. Anahisi itafika wakati babu atakuwa haamki!!!!

ANATAKA BIKIRA YEYE BIKIRA?
kimsingi umuhimu wa ubikira ni uhakikisho wa kuhijeshimu na kujitunza, mengine ni mameno tu ya mtaani.
kuliko abaki nae kwa huruma bora muache.
Hayuko psychologically fit, bora ulivyomwambia asubiri atulie, huku tulioko manungaembe tu.
bora huyo mara elfu.
Halafu mwambia katika mwenzi wa maisha ubikira wa kufungiwa ndani ya geti haina maana, manake wakiolewa tu wanaanza kutembea na madereva na houseboy.
heshima ya mtu anayo rohoni mwake ndio sababu nikakuambia hapo juu, aangalie strength of character ya huyo dada. Ni mstahimilivu.
 
kwa mawazo yangu:
mwambie namuomba asimwache huyo msichana.

1.alipomwambia aliamini hatamwacha
2.sio kosa lake kwani alibakwa
3.katika ulimwengu wa leo wako watu wengi wameoa wake waliobakwa na wala hawajui wewe umekuwa na nafasi ya kujua mwenzi wako kuwa alibakwa hivyo namini utaweza kumtoa katika hilo jinamizi kwa kumuonyesha roho njema na kwamba wanaume wote sio wakatili kama Baba yake.
4.msaidie kisaikologia ili jinamizi limtoke.
5.jishirikisheni katika mambo ya dini, itamsaidia hali hiyo kumtoka.
6.mateso aliyopitia ni makubwa sana na hastahili adhabu yoyote na hasa ya kuachwa na msiri wake.
naamini wawili hawa watakuja kuwa na maisha mazuri sana.
kipekee namtakia kila la kheri katika mahusiano yao na naomba sana asimwache.najua hakutegemea kusikia kitu kama hicho lakini ndio dunia ya sasa.wasichana wengi sana wanabakwa na ndugu zao,wanaobakwa na Baba ni wachache ila Binamu na ndugu wengine ni wengi sana.
tuzidi kumuomba Mungu ubakaji upungue kama sio kuisha
 
Mambo vipi wana mahusiano?

Kuna swali moja gumu kweli nimekutana nalo. Jama ana mpenzi ambaye amebakwa na baba yake kwa miaka miatano mfululizo! Demu alikuwa hajarevil kwa jamaa kwa muda mrefu ila alikuwa ana kama jinamizi hivi kila akikumbuka, jamaa kambembeleza amwambie shida yake demu akamwambia: "Nikikuambia bado utanipenda?" Jamaa akajibu kama kawa kwamba mimi na wewe hakuna wa kututenganisha! DEMU AKAMAWBIA NIAPIE! Jamaa kaapa kwa lugha na kwa miungu yote anyoijua. Ndipo demu kamfunulia! " Tangu nikiwa na umri wa miaka 14 baba alikuwa akinibaka, alinitisha kwamba siku nikimwambia mama tu ataniuwa. Ni mpaka nilipofikisha umri wa miaka 19 yaani mwaka jana na nadhani amehamia kwa mdogo wangu ingawa sina uhakika"

Any way, it is a long story, jamaa kaja kuniomba ushauri....Vipi amwache wakati keshaapa?
NO ASIMWACHE.
Wote kwa sasa wanasuffer hiyo the so called Nightmare.Imetoka kwa binti imehamia kwa Ndugu yetu.
What 2 do?:
Wote watafute Counsellor, wapo waliospecialize kwenye matatizo mazito kama hayo.Hili ni suala la kitaalamu.Ni taaluma ya watu.Si suala la wao wawili tu kupeana moyo na kufarijiana. WANATAKIWA WAENDE ZAIDI YA HAPO.
NI TATIZO LA AFYA YA AKILI.
Na kwa bahati mbaya NDUGU YETU HUYO AMESHAAMBUKIZWA.

BAADA YA TIBA,YAFUATAYO YANAWEZA KUFANYIKA KWA UMAKINI NA UHAKIKA ZAIDI:
1.HATUA ZA KUCHUKUA KUHUSU HUYO BABA.

2.KUJUA NI KWA JINSI GANI WATAMSAIDIA HUYO MDOGO MTU WA HUYO DADA.AMBAYE ANAHISI BABA YAKE AMEHAMIA HUKO.
WAPE POLE.
NAWATAKIA TIBA NJEMA NA MUAFAKA.
 
Du! Jamaa nilimshauri kwanza atulie ili akili yake irudi kwanza maana inaoneka alikuwa anaamini kuwa binti ni bikra nae alihitaji sana kuoa bikra. Ni binti mstaarabu sana ambaye huwezi kudhania amefanyiwa kitendo kama hicho.

Sababu hasa inayo mfanya afikiri kumwacha ni yeye kuhofia kukutwa na jinamizi pia! Anaona huruma lakini anahofia jinamizi. Anahisi itafika wakati babu atakuwa haamki!!!!

Anahofia jinamizi gani litakalomfata yeye? watu wanoa watu walioachika au hata waliofiwa hawafatwi na majinamizi itakuwa yeye ambaye anaelewa kabisa kwamba huyo binti alikuwa abused for all those years? wanaume wengine sometimes siwaelewi, huyo huyo atakutana na mwingine keshamegwa hadi kachoka na atamdangaya yeye ni ni wa pili tu ataamini.

The girl is innocent, kajaribu kutoa kitu kinachomuumiza kabisa kwake akijua anamuamini, pls mshauri mwenzio asimtose huyo msichana, italeta madhara makubwa coz ataweza kuwachukia men for life au hata kujidhuru kwa kuona hathaminiki tena.
Kitu cha msingi huyo jamaa awe nguzo ya kumuongoza huyo dada hadi wamwambie mama mtu na pia waweke mtego ili huyo baba akamatwe ikiwa anamfanyia pia mdogo wake kama alivyosema anasuspect ili ushahidi wa kumshtaki uwepo, wasipotibu haya maradhi mzee ataharibu watoto wake wote na kama kuna wa kiume pia unaweza kuta anamlamba pia, it has to stop, wakiendelea kuficha siri watavuna mabua.
Na huyo jamaa anayejifanya lengo lake ni kuoa bikra na ndicho kigezo anachotumia kutaka kumtosa huyo binti, je yeye ni bikra pia? au ye keshaharibu sana sasa anataka pure.
thanks
 
Last edited:
ANATAKA BIKIRA YEYE BIKIRA?
kimsingi umuhimu wa ubikira ni uhakikisho wa kuhijeshimu na kujitunza, mengine ni mameno tu ya mtaani.
kuliko abaki nae kwa huruma bora muache.
Hayuko psychologically fit, bora ulivyomwambia asubiri atulie, huku tulioko manungaembe tu.
bora huyo mara elfu.
Halafu mwambia katika mwenzi wa maisha ubikira wa kufungiwa ndani ya geti haina maana, manake wakiolewa tu wanaanza kutembea na madereva na houseboy.
heshima ya mtu anayo rohoni mwake ndio sababu nikakuambia hapo juu, aangalie strength of character ya huyo dada. Ni mstahimilivu.

Kwa kuongezea tu hapo kwa Haika,
Bikira siku hizi zipo hata za artificial, sasa chaguo ni lake.
 
mambo ambayo siombei nikutane nayo ndio haya......mdingi kam mega demu wangu miaka 5 tena nahisi ndio aleimtoa bikira.....alafu sasa dingi siku akitaka kukumbushia?.......naomba iwe hadithi tu na sio kweli
 
Huyo dada anaonaekana ana busara sana. Na pili anampenda huya jamaa yake. Asidhubutu kumwacha. Ninachoshauri, kama nilivyoelewa inawezekana baba yake amehamia kwa mdogo wake. Ninachoshauri ufanyike mtego ili kama namwingilia mtoto wake tene akamatwe apelekwe kwenye vyombo vya sheria.
 
Haraka sana amripoti huyu mzee Polisi ili kumuokoa mdogo wake na madhila ya huyo mzee. Pili asimuache kwani bint hakupenda yaliyomkuta
 
kwanza nampa pole sana huyo mrembo!katika maisha kila mtu ana matatizi aliyokumbana nayo na hayo ndio yanayoweka historia ya mtu.Amebeba siri hiyo kifuani kwa muda wa miaka mitano,ni kwamba alikosa pa kutulia mzigo huo mzito,watu wengi duniani tunaamini MAMA hana mpinzani ndio chombo cha kutupia mabaya na machungu yote,lakini mrembo huyu kwake imekuwa tofauti inawezekana aliona ataharibu ndoa ya wazazi wake au yeye akaonekana mbaya ndani ya familia,sasa amepata mtu anayemuamini kuliko mama yake mzazi kwa nini umuache?!Huyu binti amekuona kama mkombozi katika tatizo lililomuumiza kwa miaka mitano,MPENDE KWA MOYO WAKO WOTE NA KWA NGUVU ZAKO ZOTE,usifanye huruma bali onyesha UPENDO na hilo jinamizi litatoweka.Ushauri wangu tafuteni njia ya kumsaidia mdogo wake,njia ambayo haitaleta madhara makubwa kwa familia hasa kwa mama yao!mimi binafsi nampenda mama yangu na siko tayari kufanya kitu ambach kitamuumiza moyo wake kwasababu nina amini MAMA amebeba mengi machungu ambayo huwa hawapendi kushirikisha watoto wao kwa hofu ya kuwumiza.Kijana imani aliyokuonyesha huyo binti ni kubwa sana nakusihi mtunzie siri hiyo nae atapata faraja ya moyo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom