Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Swahiba mwingine wa Zitto ajitoa Chadema
Na Tumsifu Sanga
SWAHIBA mwingine wa Zitto Kabwe, ambaye naibu katibu mkuu wa Chadema, ametangaza kujitoa kwenye chama hicho na kujiunga ma chama cha Sauti ya Umma (SAU).
Swahiba huyo, Toni Kamukanda anakuwa mtu wa tatu kujiengua kwenye chama hicho ambacho kinaonekana kuendelea kujijenga kisiasa, baada ya watendaji wawili wa ofisi ya makao makuu, David Kafulila na Danda Juju kujiengua baada ya kutimuliwa kazini.
Kamkanda anasadikiwa kuwa miongoni mwa wanachama waliokuwa wakiendesha kampeni kabambe kuhakikisha kuwa Zitto anatwaa nafasi ya uenyekiti wa Chadema katika uchaguzi mkuu uliopita, kabla ya wazee kuingilia kati na kumshauri mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kumwachia mwenyekiti wake, Freeman Mbowe awe mgombea pekee.
Kamkanda, ambaye alikuwa mwenyekiti wa vijana mkoani Dar es salaam, alisema ameamua kuondoka ndani ya chama hicho kutokana na ubinafsi na ukabila uliokithiri kwa viongozi wa juu.
âBaada ya kubainika kuwa mimi Kafulila na Danda tuko katika mashambulizi ya kampeni ya kuhakikisha Zitto anakuwa mwenyekiti, ilianza mikakati ya kimya kimya kutufukuzisha uanachama lakini ilishindikana,â alisema Kamganda.
Kamganda aliongeza kuwa ndio maana kuna baadhi ya watu walifukuzwa uanachama kabla ya sisi kuchukua uamuzi wa kuondoka Chadema.
âKama unakumbuka ndugu mwandishi kabla sisi hatujaondoka Chadema, kuna watu walivuliwa uanachama, ilikuwa tuvuliwe pamoja nao lakini kuna mtu wa karibu na Mbowe alimwambia hawa vijana waache wakae na baada ya hapo ikaanza fitina mpaka tulipoamua wenyewe kwa ridhaa yetu kuondoka,â alisema Kamganda.
Kamganda alisema uendeshaji wa chama hicho haufanyiki kwa misngi ya kiuongozi kutokana na maamuzi ya utendaji kufanywa na mtu mmoja hali ambayo inaashiria kuwa chama hicho kinaendeshwa kikabila na ubinafsi.
Chadema imekuwa ikitetereka tangu kipindi cha maandalizi ya uchaguzi mkuu baada ya Zitto kutangaza nia yake ya kugombea uenyekiti na hivyo kusababisha wasiwasi mkubwa miongoni mwa viongozi. Lakini wazee na waasisi wa chama hicho waliingilia kati na kukinusuru chama.
Hata hivyo chaguzi za viongozi wa mikoa na jumuiya za Chadema zilikumbwa na matatizo mbalimbali yaliyoashiria kuwepo kwa makundi ambayo yalishaanza kukomaa ndani ya chama.
Mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi, Kafulila, ambaye alikuwa ofisa habari wa Chadema, alitimuliwa kazini kwa madai ya kuvujisha siri za chama. Alitimuliwa sambamba na Danda, ambaye alikuwa akishughulikiwa masuala ya Bunge. Wawili hao walitimuliwa na mkuu wao kiutendaji, Dk Willibrod Slaa, ambaye anaongoza sekretarieti.
SWAHIBA mwingine wa Zitto Kabwe, ambaye naibu katibu mkuu wa Chadema, ametangaza kujitoa kwenye chama hicho na kujiunga ma chama cha Sauti ya Umma (SAU).
Swahiba huyo, Toni Kamukanda anakuwa mtu wa tatu kujiengua kwenye chama hicho ambacho kinaonekana kuendelea kujijenga kisiasa, baada ya watendaji wawili wa ofisi ya makao makuu, David Kafulila na Danda Juju kujiengua baada ya kutimuliwa kazini.
Kamkanda anasadikiwa kuwa miongoni mwa wanachama waliokuwa wakiendesha kampeni kabambe kuhakikisha kuwa Zitto anatwaa nafasi ya uenyekiti wa Chadema katika uchaguzi mkuu uliopita, kabla ya wazee kuingilia kati na kumshauri mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kumwachia mwenyekiti wake, Freeman Mbowe awe mgombea pekee.
Kamkanda, ambaye alikuwa mwenyekiti wa vijana mkoani Dar es salaam, alisema ameamua kuondoka ndani ya chama hicho kutokana na ubinafsi na ukabila uliokithiri kwa viongozi wa juu.
âBaada ya kubainika kuwa mimi Kafulila na Danda tuko katika mashambulizi ya kampeni ya kuhakikisha Zitto anakuwa mwenyekiti, ilianza mikakati ya kimya kimya kutufukuzisha uanachama lakini ilishindikana,â alisema Kamganda.
Kamganda aliongeza kuwa ndio maana kuna baadhi ya watu walifukuzwa uanachama kabla ya sisi kuchukua uamuzi wa kuondoka Chadema.
âKama unakumbuka ndugu mwandishi kabla sisi hatujaondoka Chadema, kuna watu walivuliwa uanachama, ilikuwa tuvuliwe pamoja nao lakini kuna mtu wa karibu na Mbowe alimwambia hawa vijana waache wakae na baada ya hapo ikaanza fitina mpaka tulipoamua wenyewe kwa ridhaa yetu kuondoka,â alisema Kamganda.
Kamganda alisema uendeshaji wa chama hicho haufanyiki kwa misngi ya kiuongozi kutokana na maamuzi ya utendaji kufanywa na mtu mmoja hali ambayo inaashiria kuwa chama hicho kinaendeshwa kikabila na ubinafsi.
Chadema imekuwa ikitetereka tangu kipindi cha maandalizi ya uchaguzi mkuu baada ya Zitto kutangaza nia yake ya kugombea uenyekiti na hivyo kusababisha wasiwasi mkubwa miongoni mwa viongozi. Lakini wazee na waasisi wa chama hicho waliingilia kati na kukinusuru chama.
Hata hivyo chaguzi za viongozi wa mikoa na jumuiya za Chadema zilikumbwa na matatizo mbalimbali yaliyoashiria kuwepo kwa makundi ambayo yalishaanza kukomaa ndani ya chama.
Mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi, Kafulila, ambaye alikuwa ofisa habari wa Chadema, alitimuliwa kazini kwa madai ya kuvujisha siri za chama. Alitimuliwa sambamba na Danda, ambaye alikuwa akishughulikiwa masuala ya Bunge. Wawili hao walitimuliwa na mkuu wao kiutendaji, Dk Willibrod Slaa, ambaye anaongoza sekretarieti.