Suzuki Grand Vitara ya 2001(2000cc 16v)

Hebrew

JF-Expert Member
Jul 3, 2008
559
167
Make:Suzuki
Model: Grand Vitara or ESCUDO
Year: 2001
Engine size: 1998cc, 16v
Fuel: Petrol
Transmission: Manual
Door: 5
Mileage: 83,000 Miles
Bei: 18M

Hii gari imetoka UK na nipo kwenye njia za kuitoa.

Kila kitu kinafanya kazi kama kinavyotakiwa. Nimeongeza rear metal bumper nyuma, bull bar ya mbele na spotlights.
Nimendesha RAV4 (Manual na Auto) na kwa mtazamo wangu Grand Vitara ni nzuri sana kwenye barabara mbaya - 4WD yake ina nguvu kuishinda Rav4 na ni ngumu zaidi ila kwenye barabara nzuri Rav4 inaongoza. Kwa wale wa mikoani hii inafaa sana.

Kutokana na kodi kuwa kubwa - TRA etc, naanza na bei hiYo hapo juu. Ni PM kama upo serious -

SPECS:

ABS, Adjustable seats, Adjustable steering column/wheel, Air conditioning, Alloy wheels, Anti theft system, Body kit, CD, Child locks, Cloth upholstery, Colour coding - Body, Colour coding - Interior, Driver airbag, Electric mirrors, Electric windows, Head restraints, Folding rear seats, Limited slip differential, Locking wheel nuts, Lumbar support, Immobiliser, Metallic paintwork, Part Service History, Passenger airbag, Power assisted steering, Radio, Roof rails, Radio/CD, Rear headrests, Sunblind, Audio remote control, Body coloured bumpers, Front electric windows, Front head restraints, Height adjustable drivers seat, Rear wiper, Remote central locking, Alarm, Rear electric windows.
 

Attachments

  • grand1.jpg
    grand1.jpg
    45.9 KB · Views: 131
  • grand2.jpg
    grand2.jpg
    55.4 KB · Views: 129
  • grand4.jpg
    grand4.jpg
    30.5 KB · Views: 100
  • Grand.jpg
    Grand.jpg
    59.1 KB · Views: 95
Gari imetoka.
Wakuu hii bei ipo juu au?

Bei haiko Juu mkuu, Nimecheki kodi ya hiyo gari tu ni 10,998,223.... Tuseme aliinunua #1,000 (pounds) akasafirisha mpaka port kwa 200 (pounds), akaipandisha melini kwa 850 (1000+200+850=2050)
Sasa 2050*2540=5,207,000....
5,207,000+10,998,223=16,205,223 Hiyo ni gharama ya CIF na Kodi.... Haya amelipa shipping line na port charges... Say laki 3 tu...inakuja 16.5, kamlipa clearing agent laki2 16.7m.... So roughly anategemea profit kidogo... kwahiyo kwa 18m na ukizingatia katumia muda zaidi ya mwezi kuitafuta (kuna mtu amepiga simu, na kaenda kuiangalia-hapo lazima phone top up na usafiri ulitumika...) na mpaka kuifikisha hapa... lazima hiyo bei iwe very reasonable...
NB: My Assumptions are based on FOB price of 1000 remember... anaweza kuwa amenunua zaidi ya hapo...

Ningekuwa mimi ningekomaa na 19... 18 naona ndogo sana... Investment ya almost 17m ikileta 1m kwa mwezi ni hasara tupu...
 
Bei haiko Juu mkuu, Nimecheki kodi ya hiyo gari tu ni 10,998,223.... Tuseme aliinunua #1,000 (pounds) akasafirisha mpaka port kwa 200 (pounds), akaipandisha melini kwa 850 (1000+200+850=2050)
Sasa 2050*2540=5,207,000....
5,207,000+10,998,223=16,205,223 Hiyo ni gharama ya CIF na Kodi.... Haya amelipa shipping line na port charges... Say laki 3 tu...inakuja 16.5, kamlipa clearing agent laki2 16.7m.... So roughly anategemea profit kidogo... kwahiyo kwa 18m na ukizingatia katumia muda zaidi ya mwezi kuitafuta (kuna mtu amepiga simu, na kaenda kuiangalia-hapo lazima phone top up na usafiri ulitumika...) na mpaka kuifikisha hapa... lazima hiyo bei iwe very reasonable...
NB: My Assumptions are based on FOB price of 1000 remember... anaweza kuwa amenunua zaidi ya hapo...

Ningekuwa mimi ningekomaa na 19... 18 naona ndogo sana... Investment ya almost 17m ikileta 1m kwa mwezi ni hasara tupu...

Hem na miimi nishushie bei ya TOYOTA VISTA ya acha ile family size no no ile sedan!
 
Bei haiko Juu mkuu, Nimecheki kodi ya hiyo gari tu ni 10,998,223.... Tuseme aliinunua #1,000 (pounds) akasafirisha mpaka port kwa 200 (pounds), akaipandisha melini kwa 850 (1000+200+850=2050)
Sasa 2050*2540=5,207,000....
5,207,000+10,998,223=16,205,223 Hiyo ni gharama ya CIF na Kodi.... Haya amelipa shipping line na port charges... Say laki 3 tu...inakuja 16.5, kamlipa clearing agent laki2 16.7m.... So roughly anategemea profit kidogo... kwahiyo kwa 18m na ukizingatia katumia muda zaidi ya mwezi kuitafuta (kuna mtu amepiga simu, na kaenda kuiangalia-hapo lazima phone top up na usafiri ulitumika...) na mpaka kuifikisha hapa... lazima hiyo bei iwe very reasonable...
NB: My Assumptions are based on FOB price of 1000 remember... anaweza kuwa amenunua zaidi ya hapo...

Ningekuwa mimi ningekomaa na 19... 18 naona ndogo sana... Investment ya almost 17m ikileta 1m kwa mwezi ni hasara tupu...


Mkuu nashukuru kwa hili. Kwa kweli ushuru ulikuwa mkubwa sana ni nearly 90% ya bei yao/customs value + CIF not FOB. Tunalipa Insurance 1.5% ya bei yao + Freight - hivyo 15M hailipili kabisa COURTESY - itakuwa kama nimekupa zawadi na pesa juu!!

19 - 20M naona ndio bei zake
 
Hem na miimi nishushie bei ya TOYOTA VISTA ya acha ile family size no no ile sedan!

Dah Mkuu sasa Kila mtu nikianza kumshushia bei za kodi hapa.... si kila mtu atanipm nimpe bei atakazo lipa... Halaf nikikosea akaenda TRA wakamwambia bei nyingine, Ntakuwa nabeba mzigo wa lawama za bure...
Ngoja tu nikueleze ni jinsi gani unaweza kuzipata na kukokotoa mwenyewe, ili kila asiyefahamu ajue...
Unatakiwa kuingia kwenye website ya TRA, kisha kwenye homepage katikati ya hiyo page kuna links mbili
Ziimeandikwa

*Download Retail Selling Price(RSP) List
*Download Valuation Calculator For Used Motor Vehicles

Download hizo mbili kwenye computer yako, kisha fungua hiyo ya Retail Selling Price.... Tafuta Aina ya gari unayotaka... Copy Bei yake (Retail Selling Price) kulingana na mwaka iliyotengenezwa...(hapa kuna tofauti kidogo, sio kila gari imekuwa listed na mwaka wake wa kutengenezwa)
Ukishacopy au kuandika pembeni bei ya mauzo, then fungua hiyo link ya pili ya Valuation Calculator For used Motor vehicles, Juu kabisa kuna Exchange rate mf: 1580, Ibadili iwe ya siku hiyo kama unaijua... kama huijui weka tu 1600.... Kisha angalia jedwali la kwanza kushoto limeandikwa depreciation for direct imports, then ukishajua gari unayoagiza ina depreciate asilimia ngapi.. Nenda chini kwenye majendwali mengine (yanajieleza vizuri tu na mifano wameweka) halafu ingiza ile bei uliyocopy kutoka kwenye lile file la kwanza ulilodownload na kujua retail selling price, kisha ingiza depreciation percentage (mf 50%), halafu bonyeza enter, Kikokotoo kitafanya kazi na kukwambia total Taxes in Tsh... Hapo utakuwa umejua ni kiasi gani utatakiwa kulipa, hata kama kitazidi au kupungua haitokuwa kwa tofauti kubwa sana....
Then kuna gharama ya clearing agent.... roughly ni Laki Mbili, sijui kama kuna cheaper than that...Pia kuna gharama ya shipping line na port charges hizi sio kubwa sana kwa magari madogo hazifiki dola 300 kwa usoefu wangu...(NB: Kama Halina Storage Bill)
Hapo nadhani umeelewa... Kama hujaelewa... Kwenye ile website ya TRA kuna maelezo mazuri sana ya jinsi ya kucalculate bei ya kodi na tozo mbali mbali za kuingizia vitu nchini... Ukipitia hapo utaelewa...

Nadhani nimejaribu kutoa maelezo ya kutosha kidogo...
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom