Susy kafiwa na Dada yake leo asubuhi

Pole Suzy,
RIP dada yetu.
Mungu awape Faraja KUU!!!
 
pole sana susy!
Sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea.
M mungu akupe wepesi katika kipindi hiki kigumu na pia ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Ameen.
 
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na awape nguvu na faraja wafiwa katika kipindi hiki kigumu kwao~AMEN...Pole sana Susy.
966.jpg
 
Zawadi tuliyopewa hatimaye hatunayo tena. Muumba atupapo zawadi hii huwa ni vigumu sana kujua ni lini ataichukua. Ni kwa style gani hakika hatujui.

Da Susy na familia nzima Mungu awape ujasiri wa kuvumilia msiba huu. Hakika tuko pamoja katika wakati mgumu. Ingawa hatuko karibu nanyi kwa sasa amini kuwa tuko nawe kiroho.

Raha ya milele umpe ee Bwana...na Mwanga wa milele umwangazie,,,, apumzike kwa amani. Amina

@Dena tafadhali tuPM ili tujue utaratibu mzima.
 
Pole sana Dada Susy....mungu awape faraja wote walifikwa na msiba...mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema popeni. Amen
 
Nimepokea taarifa leo asubuhi kuwa member mwenzetu Susy amefiwa na Dada yake aliyekuwa akiishi Gongo la mboto.

Msiba huo umetokana na madhara ya mabomu yaliyotokea gongo la mboto.

Taarifa za msiba ulipo nitawafahamisha hapo baadae.

Bwana alitoa Bawana ametwaa jina la bwana lihimidiwe.

DA
Pole saana Suzy, bali wewe ni mama wanguvu vumilia na Mungu akutie nguvu ili uweze kuvuka kipindi hiki cha majonzi.
Dena tafadhari endelea kutupa taarifa.Poleni kwa familia yote!!!!!
 
Ni Kipindi kigumu,
Ni ngumu kuikubali hali hii,
JIpe Moyo ya kuwa Mungu amemchukua Mja wake,
Na amini kuwa aendako kuna uzima wa milele,
Ametutangulia, sote tutakwenda huko.
Pole kwa kuondokewa na mpendwa wako.
 
Nimepokea taarifa leo asubuhi kuwa member mwenzetu Susy amefiwa na Dada yake aliyekuwa akiishi Gongo la mboto.

Msiba huo umetokana na madhara ya mabomu yaliyotokea gongo la mboto.

Taarifa za msiba ulipo nitawafahamisha hapo baadae.

Bwana alitoa Bawana ametwaa jina la bwana lihimidiwe.

DA
Pole sana suzy mungu akupe nguvu
 
Back
Top Bottom