Sura mbili za MP. Lolensia Bukwimba

Tusker Bariiiidi

JF-Expert Member
Jul 3, 2007
5,520
2,091
Nimekuwa nikifuatilia uchaguzi mdogo wa Busanda,ambapo mgombea wa CCM Bi.Lolensia Bukwimba alishinda,kwa mtazamo wangu nilimuona Mh.Bukwimba kama dada,mama yeyote sehemu za mashambani au vijijini,mfano Wigi lake alilosuka! lakini baada ya kushinda Weeeeeeeeeeeeeee... amebadilika sana utadhani sio yeye... Anapiga viwalo acha,Nwele utadhani sio yule aliyesujudu Busanda! !! Swali ni jee??? alikuwa anawadanganya wananchi wa Busanda au ilikuwaje....naambatanisha na picha ya kwanza na kesho ya sasa....
 
Lete na picha inayo onyesha alivyo badilika mkuu. Tuta linganishaje wakati tunaona tu upande mmoja? Au una assume wote wameona hayo mabadiliko yake?
 
hata kama amebadilika ....nadhani inaweza kuwa ni mkakati wa kikampeni tu, ambao wagombea wote huwa na mikakati yao.

wagombea wanachokisema kwenye kampeni na wanachikitenda ni tofauti kabisa haiwi kitu ...itakuwa nywele?
 
Nilimshuhudia huyu mama kwenye kampeni, she is trully and genuine humble na down to earth maana pia nimemshuhudia Bungeni Dodoma baada ya kuapishwa, hana makuu kabisa, bado ni mama wa kijijini tuu ndani ya mavazi ya mjini. Nadhani hata kugombea enda ikawa alishinikizwa ili kumzibia nafasi yule aliyemfuatia kwa hana uwezo mzuri wa kujieleza jukwaani japo kujieleza vizuri sio kipimo cha utendaji mzuri. Namsubiri kwa hamu mchango wake kwa kwanza atakapochangia hoja ndipo nitathibitisha sasa amebadilika na kuchangamka.
Kama wasipomsaidia huyu mama kutekeza zile ahadi za Busanda za maji, umeme na barabara, 2010, CCM ni kwaheri Busanda.
 
Kweli sana CCM wanatakiwa wajipange vizuri kumsaidiaa huyu mama wakati huu akiwa mgni na muda ukiwa umekwisha....na kila mbunge akiwa "mbogo" kujilinda ulaji wake...asipoangalia hii vita ya wabunge na mawaziri kuhusu upendeleoo atajikuta hakuna hata moja walioahidi wana busanda likawekwa hata kwenye ramani sio kutekelezwa....halafu waje tena watumie nguvu nyiiingiii 2010......kazi kwao na Biharamulo ............
 
Kweli amebadilika mimi nilimuona kwenye Itv , bonge la suti hizo nywele sijui zimefanyaje anapiga pamba za maana,
Lakini si unajua lazima acope na wenzake kule mjengoni. au alipewa hela za kuanzia maisha ya ubunge kwa kweli sasa hivi amependeza sana.
 
Nilimshuhudia huyu mama kwenye kampeni, she is trully and genuine humble na down to earth maana pia nimemshuhudia Bungeni Dodoma baada ya kuapishwa, hana makuu kabisa, bado ni mama wa kijijini tuu ndani ya mavazi ya mjini. Nadhani hata kugombea enda ikawa alishinikizwa ili kumzibia nafasi yule aliyemfuatia kwa hana uwezo mzuri wa kujieleza jukwaani japo kujieleza vizuri sio kipimo cha utendaji mzuri. Namsubiri kwa hamu mchango wake kwa kwanza atakapochangia hoja ndipo nitathibitisha sasa amebadilika na kuchangamka.
Kama wasipomsaidia huyu mama kutekeza zile ahadi za Busanda za maji, umeme na barabara, 2010, CCM ni kwaheri Busanda.
Pasco,

Unafikiri CCM watatekeleza hizo hizo ahadi? Mwaka 2010 wataenda na uongo mwingine. Wao wanakuweka madarakani, kinachofuata kichwani mwako.

Hawa wagombea ubunge karibu wote si wanaishi mijini? Wanaenda tu huko vijijini kuwadanganya wananchi ili wawape kura ya kula, kisha hujirudia maskani kwao mjini mpaka uchaguzi mwingine ukikaribia.
 
Inawezekana mzee wa vitu bariiidi sijakupata! Sasa unataka huyu Mh. aingie bungeni na gumboots? Vinginevyo naona huyu mama kwa swala la physical appearance yuko sawa kabisa kwa maana kwamba akiwa mjini basi atavaa kimjini mjini bush atavaa kibush bush kuendana na mazingira ya huko....ndivyo wote tufanyavyo!

Suala upole au kutoweza kujieleza etc kwa upande wa siasa inaweza kuwatatizo kidogo.....lakini kama ni mtendaji mzuri basi watu wake atawakosha kwa hilo! Ila kama uwezo wa kujieleza ni mdogo na pia utendaji kazi ni mdogo as well...hali yake takuwa mbaya sana!
 
Anacjhotakiwa ni kuhakikisha anawatumikia wananchi kama alivyowaahidi. Vyovyote atakavyovaa, kama atashindwa kuwatumikia wananchi, atahukumiwa kwa matendo yake
 
Busanda wasahau, CCM ni wazuri sana katika kupanga mipango na sababu za kushindwa kuitekeleza pia... Kigumu Chama Cha Majambawazi!!!! lol
 
Kwa mtazamo wangu nadhani aliwataka wapiga kura wake haswa wanawake wamuone kama wao,lakini kumbe sivyo na kama wachangiaji wengine walivyosema kwa kipindi cha lala salama Vigogo wengi (Wabunge na Mawaziri) wanapigana vikumbo kuelekea kufanya Final touches majimboni kwao sijui kama 2010 atakuwa ameweka Umeme tu achilia barabara...
Picha zaidi hizo... (samahani kwa hiyo ya chini iliyotoka katika Daily News la jana tar.16/06/2009 ilibidi niliipige picha)HII HASWA NDIO ILINISTUA...
 
Ndo wanavyo anza ufisadi hivyo hivyo wanabadilika.
Huyu baada ya Bunge mwakani utaona mambo yake yatakuwa mswano kabisa.
 
naona alienda kupiga shopping ya kufa mtu,ila asipotimiza ahadi kule busanda 2010 ASAHAU MAANA KILA MTU ATAKUWA BUSY NA JIMBO LAKE,asitegemee kuwaona kuna malecela,magufuli na wengineo wengi
 
Jamani tusilaumu vitu visivyo na miguu wala kichwa....ni nani bado anafanana na mwaka Juzi...sisi wengine tulikuwa tunavaa Raizon, Zile suti za Nguabi, masuluali ya Buga Nguva...hata nikiangalia picha zangu za zamani naishia kucheka. Nalamba Jeans, raba na matishirt siku zingine na masuti ya kufa mtu lakini nabaki Masa yule yule. Muacheni mama yuko kwenye evolution .....
 
Nimekuwa nikifuatilia uchaguzi mdogo wa Busanda,ambapo mgombea wa CCM Bi.Lolensia Bukwimba alishinda,kwa mtazamo wangu nilimuona Mh.Bukwimba kama dada,mama yeyote sehemu za mashambani au vijijini,mfano Wigi lake alilosuka! lakini baada ya kushinda Weeeeeeeeeeeeeee... amebadilika sana utadhani sio yeye... Anapiga viwalo acha,Nwele utadhani sio yule aliyesujudu Busanda! !! Swali ni jee??? alikuwa anawadanganya wananchi wa Busanda au ilikuwaje....naambatanisha na picha ya kwanza na kesho ya sasa....

Siasa ni pamoja na kujua ku address audience kwa njia zote; body na talken language. Sioni kosa lake hapo zaidi ananifanya niamini kuwa anajua anachokifanya na hiyo pia ni indicator ya uelewa katika mambo. Kama anajua avae nini kwa wakati gani atajua afanye nini kwa wakati gani jimboni kwake. Acha waseme mama we chapa mzigo "greater is he that is in you than those who are in the world"; u r the winner they are the loosers; they shall come to you in one way but would run away through seven ways; no weapon fassioned against you shall prosper. These are your weapons for success next year as the fear of who has made you be so is the beggining of wisdom so with the same fear serve the people of Busanda and success is guranteed. You can do all things through him that strengthens you it does not matter how they see or take you! The race is not for those who are strong and through your weakness the glory of who is in you shall be revealed. Huo ni mchango wangu kwako kama mwanamke na kama ndugu yo even though I am politically your opponent.
 
Siko mbali na Offish kuhusu busanda itakuwa kama afadhali ya Jana. kwani wameingizwa choo cha kike kwani mimi ninavyosoma habari za kwake du!!! naomba kabisa kusema tuangalie kama ametekeleza ahadi zake basi atakuwa amebadilika sana lakini mmmmmmHHHH!!! haya mawazo yangu si vyema ukayafuata sana kwani mimi nimetokea kwenda BUsanda na sehemu nyingine za majimboni na kukaa vikao vizito na waheshimiwa but nimeona walivyokuwa wanafanya. kwani mtu anaishi dar anagombea ubunge kijijini (jimboni) kisha uishi mjini why? unampa KULA na sio KURA. kwani ungempa kura usingempigia mtu kama huyu wewe umempa KULA ndio maana amepata sasa anakwenda mjini kupumzika.
Tuweni makini sasa kwani mimi naudhuria vikao vingi sana chama kikuu sasa
kuleni sahani moja AHADI ATEKELEZE
 
Hapa ndipo mlipotufikisha , tunajadili mavazi ya umjini na ushamba! kweli standards zinashuka jf sasa....
 
Hapa ndipo mlipotufikisha , tunajadili mavazi ya umjini na ushamba! kweli standards zinashuka jf sasa....
unakosea....there must be something fishy here. total make over and hiding her true identity...why?
 
unakosea....there must be something fishy here. total make over and hiding her true identity...why?

U mean amefanya plastic surgery? au aliegombea sie alieshinda?

JF is bigger than those cheap politics mate!
 
Ndo wanavyo anza ufisadi hivyo hivyo wanabadilika.
Huyu baada ya Bunge mwakani utaona mambo yake yatakuwa mswano kabisa.

Bro Fidel,

Unategemea mtu asibadilike kwa mshahara wa Tshs 12,000,000 kwa mwezi kweli....! hata kama afya ilikuwa mgogoro vipi utabadilika kwa kunawili zaidi wakuu si lazima mtu awe fisadi!

Wakuu ...hiyo kny bold nimeitoa kule kny thread ya Zitto kung'atuka...

Wengine ni mazoea tu kwamba unaachaje ulaji? Yaani unaacha mshahara wa 12m kwa mwezi Zitto?
 
Back
Top Bottom