Sumaye: CCM kaa chonjo

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Waziri mkuu mstaafu na mjumbe wa Kamati Kuu Chadema Fredrick Sumaye ameitaka CCM kukaa chonjo kwani Chadema imedhamiria kutwaa dola mwaka 2020 na haitishwi na porojo za chama hicho hicho kinachoonyesha wazi kufilisika.

Sumaye amesema anayo kazi moja tu ya kukitumikia Chadema na kukieneza kuanzia vitongojini na wala hashtushwi na watu wanaomsakama kwani wanaonyesha hofu kubwa waliyo nayo kwake.

Sumaye alizungumza kwa kifupi sana wakati anaingia ndani ya kikao cha Kamati Kuu Chadema kutokana na swali aliloulizwa na mwandishi kuhusu jina lake kuwa kama agenda kwenye mkutano mkuu wa CCM leo.

Jina la Sumaye lilitawala ndani ya mkutano mkuu huo ambaye alitajwa sana kwa kejeli na viongozi kadhaa waliopata nafasi ya kuzungumza ndani ya mkutano huo.

Hiyo ni kuashiria Waziri mkuu huyo mstaafu ni kati ya watu wanaoitia kiwewe CCM.
 
By the way, ahsante Molemo kwa.kumjibia Wa Mchangani. Swali langu kwako, je ulifanikiwa kumtekodi wakati akitoa ufafanuzi huo?
 
Kutoka Waziri Mkuu wa Tanzania mpaka kugombea Umwenyekiti wa Chama Kanda halafu bado anaiambia CCM ikae chonjo kwa sababu yeye ni mgombea wa Uenyekiti wa Kanda.

Sumaye wa leo anayegombania cheo na Kubenea ndiye anayeiambia CCM ikae chonjo. This is fun to say the least.

Bora hata Mbowe akisema CCM ikae chonjo unaweza kumsikiliza kwa makini kwa sababu hajawahi kuwa serikalini.

Kikwete amempiga vijembe kweli kweli na vijembe vimemfanya atoke ndani ya pango na kuanza kupiga kelele.
 
Kutoka Waziri Mkuu wa Tanzania mpaka kugombea Umwenyekiti wa Chama Kanda halafu bado anaiambia CCM ikae chonjo kwa sababu yeye ni mgombea wa Uenyekiti wa Kanda. This is fun to say the least.

Bora hata Mbowe akisema CCM akae chonjo unaweza kumsikiliza kwa makini kwa sababu hajawahi kuwa serikalini.
Wewe shoga tulia uone moto wa sumaye!Kwanini atajwe Sana kwenye kikao chenu cha ukoo
Kikwete amempiga vijembe kweli kweli na vijembe vimemfanya atoke ndani ya pango na kuanza kupiga kelele.
 


Ifikapo 2020.

Wengi wata relax, wakidhani kama nguvu ya 2015 haikufua dafu, nini ya 2020!

Kitakachotokea watabaki mdomo wazi
 
Waziri mkuu mstaafu na mjumbe wa Kamati Kuu Chadema Fredrick Sumaye ameitaka CCM kukaa chonjo kwani Chadema imedhamiria kutwaa dola mwaka 2020 na haitishwi na porojo za chama hicho hicho kinachoonyesha wazi kufilisika.

Sumaye amesema anayo kazi moja tu ya kukitumikia Chadema na kukieneza kuanzia vitongojini na wala hashtushwi na watu wanaomsakama kwani wanaonyesha hofu kubwa waliyo nayo kwake.

Sumaye alizungumza kwa kifupi sana wakati anaingia ndani ya kikao cha Kamati Kuu Chadema kutokana na swali aliloulizwa na mwandishi kuhusu jina lake kuwa kama agenda kwenye mkutano mkuu wa CCM leo.

Jina la Sumaye lilitawala ndani ya mkutano mkuu huo ambaye alitajwa sana kwa kejeli na viongozi kadhaa waliopata nafasi ya kuzungumza ndani ya mkutano huo.

Hiyo ni kuashiria Waziri mkuu huyo mstaafu ni kati ya watu wanaoitia kiwewe CCM.

Ameshapitishwa kugombea uenyekiti wa kibaha..?!!
 
Back
Top Bottom