Waziri mkuu mstaafu na mjumbe wa Kamati Kuu Chadema Fredrick Sumaye ameitaka CCM kukaa chonjo kwani Chadema imedhamiria kutwaa dola mwaka 2020 na haitishwi na porojo za chama hicho hicho kinachoonyesha wazi kufilisika.
Sumaye amesema anayo kazi moja tu ya kukitumikia Chadema na kukieneza kuanzia vitongojini na wala hashtushwi na watu wanaomsakama kwani wanaonyesha hofu kubwa waliyo nayo kwake.
Sumaye alizungumza kwa kifupi sana wakati anaingia ndani ya kikao cha Kamati Kuu Chadema kutokana na swali aliloulizwa na mwandishi kuhusu jina lake kuwa kama agenda kwenye mkutano mkuu wa CCM leo.
Jina la Sumaye lilitawala ndani ya mkutano mkuu huo ambaye alitajwa sana kwa kejeli na viongozi kadhaa waliopata nafasi ya kuzungumza ndani ya mkutano huo.
Hiyo ni kuashiria Waziri mkuu huyo mstaafu ni kati ya watu wanaoitia kiwewe CCM.
Sumaye amesema anayo kazi moja tu ya kukitumikia Chadema na kukieneza kuanzia vitongojini na wala hashtushwi na watu wanaomsakama kwani wanaonyesha hofu kubwa waliyo nayo kwake.
Sumaye alizungumza kwa kifupi sana wakati anaingia ndani ya kikao cha Kamati Kuu Chadema kutokana na swali aliloulizwa na mwandishi kuhusu jina lake kuwa kama agenda kwenye mkutano mkuu wa CCM leo.
Jina la Sumaye lilitawala ndani ya mkutano mkuu huo ambaye alitajwa sana kwa kejeli na viongozi kadhaa waliopata nafasi ya kuzungumza ndani ya mkutano huo.
Hiyo ni kuashiria Waziri mkuu huyo mstaafu ni kati ya watu wanaoitia kiwewe CCM.