Giro
JF-Expert Member
- Feb 9, 2009
- 359
- 22
Daily News; Tuesday,March 03, 2009 @20:14
Hatma ya nauli ya mabasi kushuka inatarajiwa kufahamika baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kukamilisha mchakato wa kukokotoa hesabu. Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israel Sekirasa, alisema jana kuwa bado wanamalizia mchakato huo na siku yoyote wiki hii watatoa majibu juu ya mapendekezo ya Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo, kutaka nauli ishuke kwa asilimia 25 baada ya bei ya mafuta kushuka.
Katika kikao cha wadau wa usafiri kilichofanyika Januari 26 mwaka huu, mamlaka hiyo iliahidi kutoa majibu baada ya wiki mbili, kutokana na maoni ya wadau kuhusu mapendekezo hayo. Wakati huohuo, Sekirasa alisema vitendo vya uvamizi wa meli katika Bahari ya Hindi vinaongezeka kila mwaka, hivyo kutishia uchumi kwa meli za kimataifa kuogopa kutumia bandari za nchini kwa kuhofia usalama
Hatma ya nauli ya mabasi kushuka inatarajiwa kufahamika baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kukamilisha mchakato wa kukokotoa hesabu. Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israel Sekirasa, alisema jana kuwa bado wanamalizia mchakato huo na siku yoyote wiki hii watatoa majibu juu ya mapendekezo ya Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo, kutaka nauli ishuke kwa asilimia 25 baada ya bei ya mafuta kushuka.
Katika kikao cha wadau wa usafiri kilichofanyika Januari 26 mwaka huu, mamlaka hiyo iliahidi kutoa majibu baada ya wiki mbili, kutokana na maoni ya wadau kuhusu mapendekezo hayo. Wakati huohuo, Sekirasa alisema vitendo vya uvamizi wa meli katika Bahari ya Hindi vinaongezeka kila mwaka, hivyo kutishia uchumi kwa meli za kimataifa kuogopa kutumia bandari za nchini kwa kuhofia usalama