SUMATRA kutangaza nauli wiki hii

Giro

JF-Expert Member
Feb 9, 2009
359
22
Daily News; Tuesday,March 03, 2009 @20:14

Hatma ya nauli ya mabasi kushuka inatarajiwa kufahamika baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kukamilisha mchakato wa kukokotoa hesabu. Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israel Sekirasa, alisema jana kuwa bado wanamalizia mchakato huo na siku yoyote wiki hii watatoa majibu juu ya mapendekezo ya Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo, kutaka nauli ishuke kwa asilimia 25 baada ya bei ya mafuta kushuka.

Katika kikao cha wadau wa usafiri kilichofanyika Januari 26 mwaka huu, mamlaka hiyo iliahidi kutoa majibu baada ya wiki mbili, kutokana na maoni ya wadau kuhusu mapendekezo hayo. Wakati huohuo, Sekirasa alisema vitendo vya uvamizi wa meli katika Bahari ya Hindi vinaongezeka kila mwaka, hivyo kutishia uchumi kwa meli za kimataifa kuogopa kutumia bandari za nchini kwa kuhofia usalama
 
Daily News; Tuesday,March 03, 2009 @20:14

Hatma ya nauli ya mabasi kushuka inatarajiwa kufahamika baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kukamilisha mchakato wa kukokotoa hesabu. Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Israel Sekirasa, alisema jana kuwa bado wanamalizia mchakato huo na siku yoyote wiki hii watatoa majibu juu ya mapendekezo ya Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo, kutaka nauli ishuke kwa asilimia 25 baada ya bei ya mafuta kushuka.

Katika kikao cha wadau wa usafiri kilichofanyika Januari 26 mwaka huu, mamlaka hiyo iliahidi kutoa majibu baada ya wiki mbili, kutokana na maoni ya wadau kuhusu mapendekezo hayo. Wakati huohuo, Sekirasa alisema vitendo vya uvamizi wa meli katika Bahari ya Hindi vinaongezeka kila mwaka, hivyo kutishia uchumi kwa meli za kimataifa kuogopa kutumia bandari za nchini kwa kuhofia usalama

Yeah, hope it takes into account the increment rate when oil prices rose and the actual situation now for is ought to be a to way traffic here
 
Back
Top Bottom