SUGU vs MWANA FA

that was then this is now, mambo ya mechange na zile style haziwezi fanya kazi sasa si hapa bongo tu mpaka mbele huko
 
Wajua mziki inabidi ukupe ujumbe huku ukikuburudisha, kama msanii hakuweza fanya hilo basi ni wazi kuwa utakuboa na hutausikiliza tena. Ni infact ni wazi mashairi ya FA yatakufanya uwaze zaidi kuliko mashairi ya sugu. Sugu namkubari kama mwanaharakati na mwasisi wa mziki wa Hip Hop lakini niki compare miziki yake na FA, kwangu sugu miziki yake ni low.
Hip Hop ya mwaka 1990 ni tofauti na ya leo ukiimba style ile ya miaka ile ni wachache watakusikiliza mziki unabadilika na kumbuka mziki unaimbia watu wasikilize so ukiimba kitu ambacho ni wachache watakao sikiliza sidhani kama ina make sense

Sasa kama hiphop ya 90s ni tofauti na hii ya leo kwa nini unafananisha Sugu na FA. Fact ni kwamba wakati ngoma za Sugu zina hit kwenye AM na later katika FM station chache mwama FA alikuwa afahamiki kabisa!! Kwa mantiki hiyo ni makosa sana kumfananisha Sugu na FA na hakuna Logic katika similarity hii!!

Vilevile wakati mwana FA anafikiri kuingia katika siasa sugu amesha practice politics, kwa hiyo kila kitu yeye ndio anaanza wengine wanafuata, hiyo ni fact ya pili.

Bottomline ni kuwa huwezi kufananisha Sugu na FA kwa lolote kuanzia muziki, maisha, misimamo na harakati!!

Hayo mambo mengine kusema kuwa mziki lazima uburudike ni kudhihirisha kuwa wanaopenda miziki ya watu aina ya FA ni wale waliozoea kuwa brainwashed, i mean ni sawa na walevi!!
 
wabongo wakimpenda mtu hata mambo yaliyo wazi hawataki kukubari ili mradi basi tu emotions zina tu drive zaidi ya reality
 
unajua watu walioanza kuujua mziki miaka ya jk hawawezi kumfahamu sugu. Ndo maana wanataka kumlinganisha na mwana FA. Unakumbuka enzi za niko mikononi mwa polisi? Wanataka kutuambia ujinga wa fa wa bado niponipo ni sawa na mashairi ya sugu enzi hizo? Huwezi kushangaa kwani hata watoto wasiomfahamu zidane wataanza kumlinganisha na cristiano.

Ni sawa na kumfananisha J. K. Nyerere na Mrisho J. K.

Kisa wote wamekuwa maraisi na wote majina yao yana alphabet J. K:majani7:
 
Hao ndio wakali Don Town ukweli wote wanaujuwa, hata kipindi kile kwenda Mantoni ilikuwa ni maujiko uliza ni msanii gani mwenye wa kwanza kula pipa kwenda viwanja?

Leo nimemsoma mtoto wa Magomeni na nimemuelewa!!
 
ni dhambi kumfananisha baba na mtoto jamani hata kama mtoto anaakili kuliko baba.Nilitegemea mwanafa apambanishwe na watu kama JMO,FID Q,n.k
 
Sugu hana chochote cha kumlinganisha na mwana FA,kuuliza swali bungeni mpaka aandikiwe kwenye karatasi na kina mnyika ndo anajibu, hana lolote sema watanzania wamechoka wanachagua tu ili mradi awe mpinzani,mwana FA huwez kumlinganisha na huyu mshamba

Dume jike wewe
 
Sugu ni Mbunge anayepata Mshahara wa shilling million 7 kwa mwezi plus marupurupu kibao, wewe ndio unataka kumlinganisha na huyu Njiti MwanaFa!!??
Watu wengine bwana,sijui inakuaje wako humu.nimaneno ya kuongea mtu mzima.eti njiti,unajua maana yake lakin?
 
FA alishasema wananidiss ila mioyo yao inajua, FA kimuziki yuko juu sana zaid ya sugu.. FA kakuza kiswahili kwa kiasi fulani maneno kibao yanatumika leo mlianza kuyasikia kwa mistari yake. Okoa nguvu na muda muite B.
 
Namkubali SUGU kwa kuwa hana woga kwenye mistari yake ,haogopi kuongea ukweli kwenye mambo ambayo ni vigumu kwa msanii kuyazungumzia track kama Miaka chini ya 18,Mikononi mwa Polisi hadi leo ziko tight.FA anajua kucheza na lugha hicho ndio kitu ambacho kinambeba sana na nyimbo zake nyingi zimebase kwenye mapenzi na jamaa ni mwoga nakumbuka aliandika kuwa anajitoa kura za Kili Music mwaka uluiofuatia akashiriki na jamaa wakampa tuzo kumfariji
 
FA alishasema wananidiss ila mioyo yao inajua, FA kimuziki yuko juu sana zaid ya sugu.. FA kakuza kiswahili kwa kiasi fulani maneno kibao yanatumika leo mlianza kuyasikia kwa mistari yake. Okoa nguvu na muda muite B.

m/kt nikumbushe ni maneno gani yameanza kuonekana kwa sababu ya fa.
 
Hapa tutasugar-coat ila ukweli FA yupo juu kimziki..........mengine majaliwa.
 
Embu acheni ushamba sugu minyimbo yake ni kujisifia tumi ananiboa kuwahi kutoka kisanii si ndio mkali kiivyo kutangulia si kufika kitu mwanafa
 
Back
Top Bottom