Suala ya Pensheni laibuka Bungeni, Lissu na Zitto watoa hoja, Mhagama ataka lijadiliwe kikamati

Lapigwa dana dana na mwenyekiti wa Bunge hadi saa saba mchana wakutane kikamati na watoa hoja waje na data za kueleweka juu ya kipi wananchi wanakilalamikia.

Wabunge wa CCM wamzomea Lissu kwa hoja ilipitishwa tayari na bunge

aliyetoa hoja hii anaitwa Jafu
 
Mh. Lugola leo amewasuta na kuwaonyesha wabunge kuwa ni wanafiki kwa kitendo chao cha kupitisha sheria ya mpya ya mifuko ya jamii na leo kuonekana kuunga mkono hoja ya mh. Lusinde alietaka bunge lijadili kwa dharura kanuni hiyo ili ibadilishwe.

Baada ya mh. Lusinde kutoa hoja hiyo wabunge wengi waliiunga mkono kanakwamba sio wao waliipitisha sheria hiyo inayozuia mafao ya kujitoa mpaka mtu afikishe angalau miaka 55. Kweli hatuna bunge makini ila tuna bunge la ndio hata kwa mambo ambayo ni wazi si ya kupitisha kabisa.

Hivi sheria hii inatofauti gani na zile za kikoloni? Hivi kweli hawa ni wabunge kwa ajili ya kutete mwananchi au ni wabunge kwa ajili ya kutetea serikali? Hili bunge bora livunjwe kwani ni mzigo na ni janga la kitaifa.

Mh. Lugola aliomba muongozo na alipopewa nafasi aliwasuta wabunge na kusema bunge haliko makini. Mimi naungana na huyu mh. kwani ni wabunge hawahawa ndio walipitisha sheria hii mwezi Aprill mwaka huu ila baada ya kuona umma umekuja juu sasa wanajidai kutetea wananchi.

Mtu mnafiki ni hatari kuliko hata ukoma.
 
Hakuna cha maoni ni hivi sisi wafanyakazi hatuitaki hiyo sheria kandamizi ikibidi tutalala mabarabarani kuipinga hiyo sheria
 
sheria kandamizi hii....ifutwe la sivyo wafanyakazi wachukue ushauri wa civil rights activist.....Martin Luther Jr ambaye alisema watu wana wajibu wa kugomea na kutozifuata sheria kandamizi....
 
Kama hapo saa saba itabaki hivyo walivyopitisha mwanzo, basi nasisitiza kuwa na wao Wabunge mafao yao ya baada ya miaka mitano yaingizwe katika mifumo ya mifuko ya PENSHENI ya UZEENI wasilipwe mkupuo!.

kazi ya kamati ya uongozi wa bunge ni kupanga ratiba na uendeshaji wa bunge kwa hiyo hata kama kamati ikiruhusu lijadiliwe si kwamba ndio madiliko yatapitishwa leo. Bunge litaiagiza serikali kuleta mswada wa mabadiliko ya sheria hiyo ili bunge lijadili na kuidhinisha. Na huenda mabadiliko hayo wakayaleta bunge lijalo..
Mkuu asante kwa ufafanuzi, lakini kama hapo saa saba Bunge itaagiza kama ulivyosema tayari haitakuwa kama nilivyosema hapo juu kuwa iwapo itabaki kama walivyoamua hapo awali. Lakini bunge likiona ni sawa mswada uliopitishwa awali uendelee kama sheria halali ndiyo nilichopendekeza hapo juu tukishikie bango!.
 
wabunge wasijaribu kupitisha sheria ya namna hiyo. naumia kodi kubwa then na NSSF wanaitamani! aah hilo haiwezekani. tumeona east africa wakilala barabarani wakidai haki zao za msingi, iweje tukiwa na reference mtuambie nikiwa na nguvu nisitumie mafao yangu baada ya kujitoa mwanachama ili kufanya miradi mingine....! au mnataka nguvu zikishaisha tuje tuandamane kudai haki zetu.
MP you have to swallow this and digest it properly and not to panic otherwise tutawaadhibu kwa kutoa elimu hata kwa wasiolifahamu ni jinsi gani msivyokuwa makini na uchaguzi ujao ni kupigwa chini tu.

nawakilisha

Hapo kwenye red.
Mkuu sio nguvu kuisha ni warithi wako ndo watapata hayo mafao(If at all kweli watapewa) maana life expectancy ya mtanzania ni below 55 years, kwahiyo utakuwa umekufa!!!!!

This country bwana!!!! Aaagh
 
Lakini je, si wanaweza kuamua kusitisha kuanza kutumika kwa hii sheria. Na tunaomba hawa wabunge wawaambie wazi kabisa kuwa wapite kwa wafanya kazi kutaka maoni..

Hawawezi kusitisha kutumika kwa sheria. Hii sheria imeshaanza kufanya kazi tangu July 1, 2012.

Kamati inachoweza kuafnya ni kuiagiza SERIKALI ilete muswaada wa marekebisho wa sheria hiyo katika HATI YA DHARURA.
 
Mh: Jaffu aliomba muongozo wa spika kupitia kwa Jenista Mhagama na kuomba swala la mifuko ya jamii lijadiliwe bungeni kama jambo la dharura kwasababu wananchi wengi wanalalamikia mabadiliko ya sheria ya kupata mafao pale mwanachama atakapo fikia umri wa miaka 55.

Jenista Mhagama akakubaliana nae kisha akamuagiza akapange hoja yake vizuri in details aiwakilishe bungeni saa saba mchana ili ijadiliwe na wabunge.

nimekupa mkuu
 
Unadhani uwepo wao hao wachache unaweza kubadili nini? Ni wakati wa wananchi (hasa wafanyakazi) kujiuliza nini matokeo ya uamuzi wao wa kuipa kura CCM 2010. Majuto mjukuu.

Mkuu mi nilichoshangaa ni kwamba hata michango yao hawakugusia kabisa suala hili. Suala la kujadili halina wingi, kila mtu anaruhusiwa kuchangia. Lakini hata wao hawakuliona kabisa.
 
kuna bunge huko Tanzania au kuna Bange? wapuuz kabisa hao wanajidai kujadili nini sasa kwan walivo pitisha awali walikuwa wamefumba macho?
 
Lakini je, si wanaweza kuamua kusitisha kuanza kutumika kwa hii sheria. Na tunaomba hawa wabunge wawaambie wazi kabisa kuwa wapite kwa wafanya kazi kutaka maoni..

Ndugu yangu mm si mtaalam wa sheria sijui kama sheria inaweza kusitishwa kwa azimio la bunge. Inachotakiwa ni serikali kuleta mabadiliko haraka iwezekanavyo.
 
Mh. Lugola leo amewasuta na kuwaonyesha wabunge kuwa ni wanafiki kwa kitendo chao cha kupitisha sheria ya mpya ya mifuko ya jamii na leo kuonekana kuunga mkono hoja ya Lusinge alietaka bunge lijadili kwa dharura kanuni hiyo ili ibadilishwe.

Baada ya mh. Lusinde kutoa hoja hiyo wabunge wengi waliiunga mkono kanakwamba sio wao waliipitisha sheria hiyo inayozuia mafao ya kujitoa mpaka mtu afikishe angalau miaka 55. Kweli hatuna bunge makini ila tuna bunge la ndio hata kwa mambo ambayo ni wazi si ya kupitisha kabisa.

Hivi sheria hii inatofauti gani na zile za kikoloni? Hivi kweli hawa ni wabunge kwa ajili ya kutete mwananchi au ni wabunge kwa ajili ya kutetea serikali? Hili bunge bora livunjwe kwani ni mzigo na ni janga la kitaifa.

Mh. Lugola aliomba muongozo na alipopewa nafasi aliwasuta wabunge na kusema bunge haliko makini. Mimi naungana na huyu mh. kwani ni wabunge hawahawa ndio walipitisha sheria hii mwezi Aprill mwaka huu ila baada ya kuona umma umekuja juu sasa wanajidai kutetea wananchi.

Mtu mnafiki ni hatari kuliko hata ukoma.

Alichosema Lugola ni sawa. Bunge haliko makini kwenye hilo.
 
Hawawezi kusitisha kutumika kwa sheria. Hii sheria imeshaanza kufanya kazi tangu July 1, 2012.

Kamati inachoweza kuafnya ni kuiagiza SERIKALI ilete muswaada wa marekebisho wa sheria hiyo katika HATI YA DHARURA.

Shukrani kwa clarification.
 
Naipenda nchi yangu Tanzania, ila kwahili la pension sijui, yaani sijui.... Ngoja nisubiri hiyo saa saba
 
Jeni amekubali ijadiliwe kwa vigezo gani, au kwa sababu Jafu ni CCM? Angekuwa wa CDM suala lingekuwa mahakamani au kanuni zingekuwa zimekiukwa!
 
kura zinapigwa kwa mtindo wa ndio au sio,utawalaumu wa kina lissu buree.
serikali imeshindwa kukusanya kodi kufanya shughuli za maendeleo kwa hyo inataka kutumia mifuko kutimiza malengo yake.
tatizo ni kwamba wadau wenyewe ambao ndio wachangiaji wakuu hawajashirikishwa na mbaya wana vyama vyao.
huu ni uonevu hasahasa wale ambao wapo kwenye NGO'S kwasababu mikataba yao ni mifupi sana.
serikali inatakiwa itambue kwamba wengi tunatumia hiyo michango hadi kujisomesha wanatakiwa wajadili na sisi.
nssf,lapf,ppf nk.hawana haki ya kutumia au kufanya maamuzi yeyote bila ya kushirikisha wadau ambao ni wafanyakazi.
huu ni mwanya mwingine kwa waajiri ambao hawana tabia ya kupeleka michango ya watumishi kwasababu morale ya wafanyakazi kufuatilia hadi awe 50s,sasa kampuni ikifa?
life expectancy rate ni below 45!!!!!!another silly decision
 
Back
Top Bottom