Suala ya Pensheni laibuka Bungeni, Lissu na Zitto watoa hoja, Mhagama ataka lijadiliwe kikamati

dosama

JF-Expert Member
Dec 25, 2010
912
957
Lapigwa dana dana na mwenyekiti wa Bunge hadi saa saba mchana wakutane kikamati na watoa hoja waje na data za kueleweka juu ya kipi wananchi wanakilalamikia.

Wabunge wa CCM wamzomea Lissu kwa hoja ilipitishwa tayari na bunge
Mh. Lugola leo amewasuta na kuwaonyesha wabunge kuwa ni wanafiki kwa kitendo chao cha kupitisha sheria ya mpya ya mifuko ya jamii na leo kuonekana kuunga mkono hoja ya Lusinge alietaka bunge lijadili kwa dharura kanuni hiyo ili ibadilishwe.

Baada ya mh. Lusinde kutoa hoja hiyo wabunge wengi waliiunga mkono kanakwamba sio wao waliipitisha sheria hiyo inayozuia mafao ya kujitoa mpaka mtu afikishe angalau miaka 55. Kweli hatuna bunge makini ila tuna bunge la ndio hata kwa mambo ambayo ni wazi si ya kupitisha kabisa.

Hivi sheria hii inatofauti gani na zile za kikoloni? Hivi kweli hawa ni wabunge kwa ajili ya kutete mwananchi au ni wabunge kwa ajili ya kutetea serikali? Hili bunge bora livunjwe kwani ni mzigo na ni janga la kitaifa.

Mh. Lugola aliomba muongozo na alipopewa nafasi aliwasuta wabunge na kusema bunge haliko makini. Mimi naungana na huyu mh. kwani ni wabunge hawahawa ndio walipitisha sheria mwezi Aprill mwaka huu ila baada ya kuona umma umekuja juu sasa wanajidai kutetea wananchi.

Mtu mnafiki ni hatari kuliko hata ukoma.
 
Mh. Jaffu akubaliwa kuleta hoja kuhusu mabadiliko ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii na aiwasilishe leo hii saa saba mchana ijadiliwe bungeni.


Source: Bunge Live
 
Nimemkubali Kangi Lugola kwamba kama bunge linakubali kujadili hoja, basi inamaanisha kua halikua makini mwanzo.
 
Mimi naangalia hapa,halijapigwa danadana, mwenyekiti Jenista Mhagama amekubaliana na hoja ya mheshimiwa suleiman jafu mbunge wa CCM kisarawe, amambiwa awasiliane na wafanyakazi, aandae vema malalamiko juu ya masuala ya pensheni, saa saba na robo awasilishe kwa mwenyekiti, na saasaba hiyo kamati ya uongozi itakutana, na hatimae kupanga kujadiliwa kwa kina. AMEKUBALI LIJADILIWE KWA UDHARURA! SAFI SANAAAA!
 
Mheshimiwa zito aliunga mkono hoja ya mheshimiwa jafu,na akashauri kamati ya uongozi ikutane,imekubaliwa na mwenyekiti.

Mheshimiwa kangi lugola akaomba mwongozo na kusema ni kivipi sheria iliyopitishwa na bunge hilohilo,iletwe tena kujadiliwa bungeni, kwa maana kwamba inaonyesha jinsi gani bunge halikuwa makini katika kupitisha hiyo sheria.

Mwenyekiti wa bunge mhe jenista mhagama amesema sheria zinazopita bungeni sio MSAHAFU,ruksa KUANGALIWA NA KUJADILIWA UPYA KWA MANUFAA YA WANANCHI!
 
Kama lilipitishwa bungeni kuna jinsi waliliskip kwa kutoliona au liliwasilishwa kimazingira ambayo isingekuwa rahisi kugundua impact yake kwa walengwa. Huu mchezo unachezwa sana na si kweli kwamba wabunge akiwemoLugola hawakuwa makini kiasi hicho
 
Nimemkubali Kangi Lugola kwamba kama bunge linakubali kujadili hoja, basi inamaanisha kua halikua makini mwanzo.

Huyu jamaa ni Gamba, lakin ana elements za Ugwanda. Ni mojawapo ya wabunge wachache wa Ccm waliokubali kusaini list ya "Vote of No Confidence" kwa Waziri Mkuu
Huyu jamaa Kichwa sana. CCM wanataka kujipatia umaarufu kuwa wanawajali wafanya kazi wakati wao ndio waliosema ndiooooooo miezi mitatu tu iliyopita kuunga mkono hoja hii..Iweje leo tena wabunge wajifanye hawakushiriki uhuni huu?
 
Yaelekea wabunge huwa wanasinzia tu bungeni. Nimeshangaa eti na wao wanaishangaa hiyo sheria wakati ilipitia hapo bungeni. Kweli hawa jamaa wapo kwa ajili ya matumbo yao tu.
 
Kama hapo saa saba itabaki hivyo walivyopitisha mwanzo, basi nasisitiza kuwa na wao Wabunge mafao yao ya baada ya miaka mitano yaingizwe katika mifumo ya mifuko ya PENSHENI ya UZEENI wasilipwe mkupuo!.
 
Lapigwa dana dana na mwenyekiti wa Bunge hadi saa saba mchana wakutane kikamati na watoa hoja waje na data za kueleweka juu ya kipi wananchi wanakilalamikia.

Wabunge wa CCM wamzomea Lissu kwa hoja ilipitishwa tayari na bunge

wabunge wa CCM hawakumzomea Lissu kwa vile hoja ilipitishwa na bunge! Walichowaza ni kama vile mh Lissu anataka kuiteka hoja yao ambayo imetolewa na mh Jaffo mbunge wa kisarawe.
 
Hebu funguka zaid, kasemaje mpaka kakubaliwa?

Mh: Jaffu aliomba muongozo wa spika kupitia kwa Jenista Mhagama na kuomba swala la mifuko ya jamii lijadiliwe bungeni kama jambo la dharura kwasababu wananchi wengi wanalalamikia mabadiliko ya sheria ya kupata mafao pale mwanachama atakapo fikia umri wa miaka 55.

Jenista Mhagama akakubaliana nae kisha akamuagiza akapange hoja yake vizuri in details aiwakilishe bungeni saa saba mchana ili ijadiliwe na wabunge.
 
Back
Top Bottom