Laptop01
JF-Expert Member
- Nov 29, 2009
- 1,365
- 796
Mzozo kuhusu Suala la Mpaka kati ya Tanzania na Malawi katika Ziwa Nyasa ni miongoni mwa masuala ambayo yanagonga vichwa vya watu, taasisi na tawala mbalimbali duniani kwa sasa. Zaidi ni kati ya Utawala wa Rais JK waTanzania na Utawala wa Rais JB wa Malawi.
Kama ilivyo ada, yawezekana yapo mataifa yanayofurahia mzozo huo ukue na kukomaa mpaka moshi ufuke kwasababu ni muuhimu kwa mauzo ya bidhaa zao ikiwa ni pamoja na silaha zitakazouzwa endapo vita itatokea (Mungu aepushie mbali).
Suala la mpaka huo linasemekana kugusa maagano, mapatano na sheria za kimataifa. Ningependa kusikia Taasisi zetu za masuala ya kisheria (kwa mfano TLS , LHR hata UDSM School of Law na Ile Sehemu ya Masuala ya Uhusiano wa Kimataifa zinatuelimisha kuhusu hili. TAASISI HIZI SIZISIKII WALA SIZIONI KUFANYA HIVYO. Hii siyo vita ya JKpeke yake. Kama suala hili liko chini ya taratibu zilizowazi kuhusu mipaka ya namna hiyo HOFU YETU YA NINI KUELIMISHANA? Au taratibu za uhusiano wa kimataifa zinakataza?
Nilitegemea pia kuwasikia Wasemaji Wakuu Wa Vyama vya Upinzani katika Masuala ya Kimataifa wakitolea maoni na kumpa nguvu Rais kuhusu Suala la Mpaka huu, SIWASIKII WALA SIWAONI KATIKA HILI!
Simaanishi kwamba waliongelee kwa namna ambayo ni yakukuuza mgogoro bali kwa namna itakayoonesha kuwa inapokuja kwenye masuala ya kitaifa, tuko pamoja.
Ni maoni tu.
Kama ilivyo ada, yawezekana yapo mataifa yanayofurahia mzozo huo ukue na kukomaa mpaka moshi ufuke kwasababu ni muuhimu kwa mauzo ya bidhaa zao ikiwa ni pamoja na silaha zitakazouzwa endapo vita itatokea (Mungu aepushie mbali).
Suala la mpaka huo linasemekana kugusa maagano, mapatano na sheria za kimataifa. Ningependa kusikia Taasisi zetu za masuala ya kisheria (kwa mfano TLS , LHR hata UDSM School of Law na Ile Sehemu ya Masuala ya Uhusiano wa Kimataifa zinatuelimisha kuhusu hili. TAASISI HIZI SIZISIKII WALA SIZIONI KUFANYA HIVYO. Hii siyo vita ya JKpeke yake. Kama suala hili liko chini ya taratibu zilizowazi kuhusu mipaka ya namna hiyo HOFU YETU YA NINI KUELIMISHANA? Au taratibu za uhusiano wa kimataifa zinakataza?
Nilitegemea pia kuwasikia Wasemaji Wakuu Wa Vyama vya Upinzani katika Masuala ya Kimataifa wakitolea maoni na kumpa nguvu Rais kuhusu Suala la Mpaka huu, SIWASIKII WALA SIWAONI KATIKA HILI!
Simaanishi kwamba waliongelee kwa namna ambayo ni yakukuuza mgogoro bali kwa namna itakayoonesha kuwa inapokuja kwenye masuala ya kitaifa, tuko pamoja.
Ni maoni tu.