Kuna taarifa nimezipata kutoka kwa mwanahabari mmoja kuwa wahariri walioalikwa kwenye press conference ya mtu aliyejitambulisha kama mmiliki wa Dowans walihongwa Sh. 500,000 kila mmoja ili kuhakikisha wanaipa uzito habari hiyo potofu. Inasemekana mialiko iliratibiwa na mhariri wa gazeti la Tanzania Daima ambaye ni swaiba wa Rostam. Bila shaka kuna wanahabari wengine wana taarifa zaidi kuhusiana na press conference hiyo, na maelezo ya kwa nini mmiliki huyo hakutaka kupigwa picha.